Thursday, November 3, 2011

Wimbo wa leo, Moyo wa Subira-LINEX

Man U, Man C, Real, Bayern, Ajax, Zafanya kweli ligi ya mabingwa ulaya

Yaya Toure akishangilia goli.

Wakati Man United wakisumbuliwa na na Otelul Galati, mahasimu wao Man City walikuwa wakiwafunza mpira Villareal nyumbani kwaoUhispania.

Yaya Toure aliipatia Manchester City magoli mawili na kuiongezea matumaini ya kusonga mbele katika michuano hiyo ya klabu bingwa bara Ulaya.

Ingawa Man City walikuwa wanacheza kama watu walio uwanjani kwao wakifanya mazoezi ,lakini walitoka uwanjani wakiwa na hofu baada ya mchezaji wao matata David Silva kuondoka uwanjani akiwa na maumivu mgongoni.

Olympique Lyon 0-2 Real Madrid

Cristiano Ronaldo alifunga mabao mawili na kuipatia Real Madrid ushindi wa mabao mawili na wenyeji wao Olympique Lyon ya Ufaransa sufuri.

Ajax Amsterdam 4-0 Dynamo Zagreb.

Nayo Ajax Amsterdam iliwachapa wageni wao Dynamo Zagreb 4-0 .

Hivyo Real Madrid wanaongoza kundi D na pointi 12 wakifuatwa na Ajax Amsterdam na alama 7.

Bayern Munich 3-2 Napoli.

Bayern Munich waliwafunga wageni wao Napoli ya Italy 3-2.

Kwa ushindi huo Bayern iko kileleni mwa kundi A na pointi 10 wakifuatwa na Manchester City na pointi 7. Villarreal ni ya mwisho.

Manchester United waliwafunga Otelul Galati mbili sufuri lakini walitolewa jasho na timu hiyo ya Rumania.
Antonio Valencia aifungia Man U bao la kwanza
Wakati Antonio Valencia alipoifungia Man U bao la kwanza katika dakika ya nane , mashabiki wa mashetani wekundi walikuwa na matumaini makubwa kuwa timu ya Otelul ingelibebeshwa gunia la mabao. kumbe sivyo!
Baada ya bao lao la kwanza, vijana Sir Alex Ferguson ambao walikuwa wanacheza nyumbani Old Traford hawakuwa na mchezo wa kuvutia.
Ni baadae sana katika dakika ya 87 ambapo Wayne Rooney aliifungia Manchester United bao la pili.
Hii ilikuwa ni mara yakwanza kwa Man U kucheza katika uwanja wao wa nyumbani tangu walipopigwa 6-1 na jirani zao Man City.
Tangu kipigo hicho Manchester United hawaja weza kutulia na kuonyesha mchezo wa kuvutia. Hata hivyo la muhimu nikuwa Jumatano usiku waliifunga Otelul Galati, 2-0 na kuzoa pointi tatu.
Baada ya matokeo ya mechi hizo Manchester sasa wanaongoza kundi C na point nane sawa na Benfica ya Ureno lakini kwa wingi wa magoli.

Wednesday, November 2, 2011

SANAA YA LEO PENSELI NA KAMERA

See more HOT pictures

http://groups.yahoo.com/group/babes_in_blue/

http://groups.yahoo.com/group/babes_in_blue/

http://groups.yahoo.com/group/babes_in_blue/

JUDGE Vs CHILD (Kichekesho)

http://www.feedthechildren.org/images/abc/pages/abc_about_faqs/child-tears.jpg
Judge to child: Do you want to live with your mother?
Child: No
Judge: Why?
Child: She beats me.
Judge: Okay, so you want to live with dad?
Child: No
Judge: Why not?
Child: He beats me too.
Judge: So who do you want to live with?
Child: TAIFA STARS.
Judge: WHY??
Child: They never beat anyone!

JINSI AMBAVYO NYOKA ANAANDALIWA TAYARI KWA KULIWA



Dried gallbladder of snakes are used like immunomodulator, the medicine reinforcing immune system; encapsulated snake oil is a natural product containing collagen - good for CVD prevention; powder made of snake genitals is a secret of men's sexual drive.
There is one more thing - you may try to drink fresh snake blood and eat its still warm heart. It's believed that drinking blood of a creature with perfect immune system makes your own immune system much stronger - that's the reason why people drink blood of crocodiles and snakes. Heart is eaten to obtain the power of the animal that was killed.
First of all Siamese cobra must be chosen.
 
It is let our from the cage and it crawls right at your feet, it seems the cobra needs just a second to get to you and make a deadly bite, but it's known that snakes don't attack first.
 
Kwanza nyoka hukamatwa na kuminywa shingoni.
 
Then its body is cleaned.
 
Shallow notch and the snake's heart is taken out
 
Blood is drained into a glass
 
When the heart is extracted it still beats for some time...
 

Blood is diluted with whiskey and tossed off.

The heart is cut for two persons. It's eaten and washed down with alcohol


The cooked meat of the cobra looks like this.

Snake liver tastes like beef liver, there is no much meat but it tastes rather well.

TUZO ZA MWANANDINGA BORA WA DUNIA BARCELONA YATOA 8

Wayne Rooney ni mchezaji pekee wa Uingereza aliyeingia katika mchujo wa wachezaji watakaowania tuzo ya Fifa ya mwanakandanda bora wa mwaka ijulikanayo Ballon d'Or.

Barcelona imeingiza wachezaji wanane katika orodha ya mchujo huo, akiwemo Lionel Messi, ambaye ndiye mshindi wa tuzo hiyo kwa mizimu miwili iliyopita.
Nani (Man Utd), Luis Suarez (Liverpool) na Sergio Aguero (Man City) ni wachezaji wengine wanaocheza soka England waliomo katika mchujo huo.
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger anaungana na Sir Alex Ferguson na meneja wa Chelsea Andre Villas-Boas katika orodha ya mameneja wanaowania tuzo kwa eneo lao la mameneja. Uamuzi utatolewa tarehe 9 mwezi wa Januari.
Rooney msimu wa ligi wa 2011 aliisaidia sana klabu yake ya Manchester United kuweka rekodi ya kunyakua taji la ligi la soka la England kwa mara ya 19 na kufika fainali ya Ligi ya Ubingwa wa Ulaya.
Mabingwa wa kandanda wa Ulaya klabu ya Barcelona imetawala orodha hiyo ya Fifa kwa kuingiza wachezaji wanane, ambapo Cesc Fabregas, aliyekuwemo kwa muda fulani katika kikosi cha Arsenal mwaka 2011, yumo katika orodha hiyo pamoja na Messi.
Real Madrid imeingiza wachezaji watano, akiwemo mshambuliaji wa zamani wa Manchester United Cristiano Ronaldo na kiungo wa zamani wa Liverpool Xabi Alonso.
Orodha hiyo itachujwa tarehe 5 mwezi wa Desemba na kubakisha majina ya matatu kwa kila nyanja.
Wachezaji walioteuliwa kuwania tuzo ya Fifa na nchi zao katika mabano:



 Eric Abidal (Ufaransa),



Sergio Aguero (Argentina),



Karim Benzema (Ufaransa),


Iker Casillas (Hispania),


Cristiano Ronaldo (Ureno),

 
Dani Alves (Brazil),


Samuel Eto'o (Cameroon),


Cesc Fabregas (Hispania),


Diego Forlan (Uruguay),


Andres Iniesta (Hispania),


Lionel Messi (Argentina),

Thomas Muller (Ujerumani),


Nani (Ureno),


Neymar (Brazil),


Mesut Ozil (Ujerumani),


Gerard Pique (Hispania),


Wayne Rooney (England),


Bastian Schweinsteiger (Ujerumani),


Wesley Sneijder (Uholanzi),


Luis Suarez (Uruguay),


David Villa (Hispania),


Xabi Alonso (Hispania),


Xavi (Hispania).
Mameneja walioteuliwa kuwania tuzo hiyo na nchi pamoja na vilabu vyao:
Vicente Del Bosque (Hispania na timu ya taifa ya Hispania), Sir Alex Ferguson (Scotland/Manchester United), Rudi Garcia (Ufaransa/Lille), Pep Guardiola (Hispania/Barcelona), Jurgen Klopp (Ujerumani/Borussia Dortmund), Joachim Loew (Ujerumani na timu ya taifa ya Ujerumani), Jose Mourinho (Ureno/Real Madrid), Oscar Tabarez (Uruguay/Na timu ya taifa ya Ujerumani), Andre Villas-Boas (Ureno/Porto, Chelsea), Arsene Wenger (Ufaransa/Arsenal).

Barcelona yaua 4 Arsenal Yalazimishwa suluhu na Marseille

Licha ya kucheza nyumbani, timu ya Arsenal wameshindwa kuifunga timu ya Olympic Marseille ya Ufaransa ilikujihakikishia tiketi katika hatua ya 16 bora ya ligi ya mabingwa.
Hatua ya Mkufunzi Arsene Wenger kumuacha njee ya kikosi chake nahodha Robin van Persie kulionekana kuwapunguzia miamba ya Arsenal motisha.

Washambulizi wa Arsenal hawakuonekana kwamba ni tishio katika ngome ya wageni wao Marseille katika mechi hiyo.

Badala yake ni Olympic Marseille ndio waliokuwa mwiba katika ngome ya Arsenal huku Jordan na Andre Ayew wakikosa nafasi kadhaa za kuiadhibu Arsenal nyumbani kwao Emirates.

Licha ya sare hiyo Arsenal bado inaongoza kundi F wakiwa na alama nane . Olympic Marseille ni ya pili na alama saba.

Barcelona 4 - 0 Viktoria Plzen


Kwengineko mabingwa watetezi Barcelona ya Uhispania waliwatwanga Viktoria Plzen ya Jamhuri ya Ucheki kwa magoli 4-0.

Mchezaji bora duniani Lionel Messi aliwaonyesha kivumbi wenyeji wao kwa kufunga mabao matatu. Cesc Farbregas aliipatia Barca bao la tatu katika dakika ya 72.

Hii ni mara ya 14 kwa Lionel Messi kufunga mabao matatu katika mechi moja tangu aanze kuichezee Barcelona .

Kwa ushindi huo Barcelona inakuwa timu ya kwanza kujikatia tiketi ya kuingia katika hatua ya 16 bora ambayo ni mechi za muondoano.