Tuesday, April 10, 2012

ARSENAL YAICHAKACHUA MAN CITY, MAN U YAUA


Muuaji wa Man City Mikel Arteta Kulia

Mkwaju wa mbali wa Mikel Arteta umeipa Arsenal ushindi muhimu na kuiacha Manchester City ikiwa pointi nane nyuma ya Manchester United katika ligi kuu ya England.
Yaya Toure alitoka mapema kutokana na kuumia na nafasi yake kuchukuliwa na David Pizzaro huku Balotelli akitolewa kwa kadi nyekundu.
Mara mbili Robin Van Persie aligonga mwamba huku mkwaju mwingine aliopachika wavuni ukiwa wa kuotea.
Arteta alipata mwanya katika dakika ya 86 kwa kuachia mkwaju umbali wa yadi 25.
Arsenal sasa wamerejea katika nafasi ya tatu, pointi mbili juu ya Tottenham walio nafasi ya nne.
Schioles
PAUL SCHOLES

Shuti kali la Scholes lilihakikisha ushindi wa United
Awali manchester United iliichapa QPR kwa mabao 2-0 kwenye uwanja wa Old Trafford.
Man United sasa imefikisha pointi 79, City ikifuatia na pointi 71 ikiwa imesalia michezo sita kumalizika kwa ligi.

SABABU ZA KIFO CHA STEVEN KANUMBA, RATIBA YA MAZISHI


Marehemu Steven Kanumba

Msanii nyota wa filamu nchini, Steven Kanumba amefariki dunia kutokana na tatizo la mtikisiko wa ubongo linalojulikana kitalaamu kama Brain Concussion, taarifa za kitabibu zimeeleza.
Taarifa hizo za ndani, zilizopatikana jana baada ya jopo la madaktari bingwa watano wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu huyo, zimeeleza kuwa tatizo hilo linaweza kumfanya mtu apoteze maisha mara moja au baada ya siku kadhaa. Mmoja wa madaktari hao ambaye aliomba jina lake lisitajwe gazetini alisema waligundua tatizo hilo baada ya kumfanyia uchunguzi huo kwa zaidi ya saa mbili.

Tulianza kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu kuanzia saa 4:00 asubuhi hadi saa 6:45 mchana na tukagundua kuwa marehemu alifariki kutokana na mtikisiko wa ubongo kwa kitaalamu, Brain Concussion, alisema daktari huyo. Alisema Kanumba alipata mtikisiko wa ubongo ambao husababisha kufeli kwa mfumo wa upumuaji (cardio-respiratory failure) Kilichomuua hasa ni mtikisiko wa ubongo, ambao endapo unatokea katika sehemu ya nyuma ya ubongo (cerebrum), huua kwa haraka alisema daktari huyo na kuongeza kuwa mtikisiko wa ubongo  wa nyuma, husababisha matatizo ya mfumo wa upumuaji na hilo limeonekana katika mwili wake.

Baada ya ubongo wake kutikiswa kwa nguvu, mfumo wa upumuaji ulifeli na ndiyo maana tumekuta kucha za Kanumba zikiwa na rangi ya bluu, huku mapafu yake yakiwa yamevilia damu na kubadilika kuwa kama maini, hizo ndizo dalili za kufeli kwa mfumo wa upumuaji.

Mtu aliyepata mtikisiko wa ubongo huweza kutokwa na mapovu mdomoni na hukoroma kabla ya kukata roho na ndivyo ilivyokuwa kwa Kanumba kabla hajafariki.

Daktari mwingine aliyeshiriki katika uchunguzi huo ambaye pia aliomba jina lake lisitajwe alisema ubongo wa mwigizaji huyo ulikuwa umevimba na kushuka karibu na uti wa mgongo na hivyo kuathiri mfumo wa upumuaji.
Alisema sehemu ya maini na majimaji ya machoni ya marehemu, vimepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ili kubaini endapo kuna sumu au kitu kingine katika mwili huo.

Baba mzazi azungumza Baba mzazi wa mwigizaji huyo, Charles Musekwa Kanumba alisema kwamba alipata taarifa za kifo cha mwanawe Jumamosi saa 10:00 alfajiri baada ya kupigiwa simu na dada wa marehemu, Sara Kanumba.  Sara aliniuliza: Una taarifa yoyote kuhusu mwanao Kanumba? Nikamjibu kuwa sina taarifa yoyote, ndipo aliponieleza habari za kifo hicho. Aliniambia Kanumba hatupo naye tena amefariki kwa kuanguka, amekorofishana na mpenzi wake.  alisema taarifa hizo zilimsababisha aishiwe nguvu kwa kuwa kilikuwa kifo cha ghafla Basi kuanzia hapo, nilianza kupigiwa simu za kupewa pole, ndipo nilipoamini kumbe mwanangu amefariki.

Akizungumzia kuchelewa kufika msibani, alisema kumetokana na tatizo la mawasiliano. Awali, alikuwa amepanga mtoto wake Kanumba akazikiwe Mwanza kwa babu yake ndiyo maana hakufika mapema msibani.  Nilikuwa nimepanga apitishwe hapa kwangu Shinyanga aagwe, halafu tumpeleke Mwanza kwa babu yake kumzika huko lakini alipokuja mama yake alinishauri kuwa huko kutakuwa na nafasi ndogo kwa sababu watu ni wengi pia alikuwa na marafiki wengi, wengine wa kutoka nje ya nchi kwa hiyo alinishawishi na tukakubaliana kumzika Dar es Salaam, alisema.

Pia alikanusha uvumi kuwa hajafika msibani kwa kuwa walikuwa na ugomvi na marehemu akisema walishamaliza tofauti zao. Alisema anatarajia kufika leo usiku tayari kushiriki mazishi hayo.

Wabunge  kilio Jana, baadhi ya wabunge waliofika nyumbani kwa marehemu Kanumba waliangua vilio wakati walipotoa salamu zao za rambirambi.
Mbunge wa Viti Maalumu, Martha Mlata hakuzungumza na badala yake aliimba kipande cha wimbo uliozungumzia kifo na maneno ya wimbo huo yalionekana kuwagusa wafiwa na kusababisha vilio kuanza upya huku baadhi wakipoteza fahamu.
Mbunge mwingine, Neema Mwinyimgaya aliongeza majonzi masibani hapo alipounganisha msiba huo na wa mama yake Mama yangu amefariki miezi mitatu iliyopita, huko uliko mama, nakuomba umpokee kijana mwenzetu,รข€ alisema mbunge huyo na kushindwa kuendelea.

Wabunge wengine waliohudhuria msiba huo ni Ismail Aden Rage (Tabora Mjini), Aboud Juma (Kibaha Vijijini), Mussa Azan Zungu (Ilala), Abbas Mtemvu (Temeke), Peter Serukamba (Kigoma Mjini) na Ritha Kabati (Viti Maalumu).
 Kova na mchango wa Kanumba Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema anakumbuka mchango wa Kanumba katika kuzuia uhalifu jijini.

Tulishirikiana naye pamoja na wasanii wengine kuandaa bonanza maalumu ambalo lilidhamiria kukabiliana na uhalifu hapa jijini na kwa kweli mchakato ule ulifanikiwa kwani uhalifu ulipungua kwa kiasi kikubwa alisema Kova.
Kifo chake kimekuwa cha ghafla mno na nafikiri kujiweka tayari (kiimani) ni jambo ambalo kila mmoja anatakiwa kuwa makini nalo katika maisha yake, alisema Kova.

Ratiba ya mazishi2:30 - Msafara kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili kupitia Barabara ya Umoja wa Mataifa na Ali     Hassan Mwinyi hadi Viwanja vya Leaders Club.
3:30 - Misa ya kumuombea na salamu mbalimbali.
6:00 - Kuaga
9:00 - Kuelekea Makaburi ya Kinondoni kupitia Barabara ya Tunisia

Thursday, April 5, 2012

CHELSEA YAIFUATA BARCELONA NUSU FAINALI KLABU BINGWA BARANI ULAYA

Blue is the colour: Chelsea will play Barcelona in the semi-finals of the Champions League
Wachezaji wa Chelsea wakishangilia goli la penati alilofunga Lampard

Chelsea imetinga katika hatua ya nusu fainali ya klabu bingwa barani ulaya baada ya kuichapa Benfica ya ureno kwa mabao 2-1 na kuipa ushindi wa jumla wa mabao 3-1 baada ya kushinda pia katika mchezo wa kwanza kwa bao 1-0.
Katika mchezo huo ambao ulikuwa mkali lakini Chelsea ikionekana dhaifu mbele ya Benfica ilifanikiwa kupata bao la kuongoza katika dakika ya 21 kwa njia ya penati baada ya Ashley Cole aliyekuwa akielekea kumsabahi golikipa wa Benfica kuchezewa vibaya katika eneo la hatari,penati hiyo ikitupiwa kambani na Lampard.
Dakika ya 40 Benfica walinyong'onyeshwa baada ya beki wake kutolewa kwa kadi nyekundu baada ya kupewa kadi ya njano ikiwa ni ya pili na hivyo kutolewa nje.
Benfica kama hawakuwa pungufu vile waliendelea kuwanyanyasa Chelsea na kujipatia bao la kusawazisha katika dakika ya 85 kupitia mshambuliaji wake Jarvia Garcia.
Raul Meireles alieingia kipindi cha pili alihitimisha shughuli katika dakika ya 90 kwa kuachia shuti kali la mbali na kufunga goli zuri katika mchezo huo.
Spot on: Frank Lampard was the match-winner with a penalty in the first half
Lampard akipiga penati iliyoiandikia Chelsea goli la kwanza

Dynamite: Raul Meireles settled the tie beyond all doubt with a thunderous strike into the top corner
Meireles akipigilia msumari wa pili

Dynamite: Raul Meireles settled the tie beyond all doubt with a thunderous strike into the top corner
Mfungaji wa goli la pili Raul Meireles akiwasherehesha mashabiki wa Chelsea

Benfica's Javi Garcia (L) Scores
Javi Garcia akifunga goli maridadi kwa kichwa na kuisawazishia Benfica


Torres alicontrol mpira mbele ya beki wa Benfica

Wednesday, April 4, 2012

Bob Junior-Nichum

MKE WA MAJID MICHEL AMEIONA HII? MAJID NA MERCY JOHNSON

Woow ninatamani na mimi niwe mcheza filamu kwa sababu hiyo ya kubambiabambia mademu wakali,aaah....Hii tasnia inavutia sana!Tukirudi katika mada najiuliza mke wa Majid Michel yuko wapi aione hii ili Majid atakaporudi amzabe vibao,Mercy Johnson ana umbo la kuvutia kimahaba lenye kuweza kusimamisha turubai muda wowote na hiyo ndio utajua kwanini Majid anastahili kupigwa na mkewe.
Pamoja na hayo ni filamu lakini ukaribu huu unaweza kumfanya mke wa Majid akajikalia nyumbani akiwaza huku michozi ikimtiririka mithili ya chemchem ya Udzungwa, pia najiuliza Mercy ameolewa? vp mumewe au mchumba wake anapoyaona haya? Tazama mwenyewe sitaki ushahidi mie........

Mercy Johnson And Majid Michel
Mercy Johnson na Majid Michel

Mercy Johnson And Majid Michel

Mercy Johnson And Majid Michel

Mercy Johnson And Majid Michel
Mercy Johnson na Majid katika pozi tofauti nadhani umejionea mwenyewe kama mmojawapo mpenzi wake anaangalia mara kwa mara anaweza kupatwa na preshaaaa!!!!

BARCELONA NI NOMAA, YAITUPA AC MILAN NJE NA KUTINGA NUSU FAINALI KLABU BINGWA ULAYA

Soccer - Barcelona v AC Milan Champions League - Quarter Finals - Second Leg - Nou Camp
Andre Iniesta(8) akitupia kambani msumari wa tatu na wa ushindi

Barcelona ya Uhispania imefanikiwa kuingia hatua nzuri katika michuano ya klabu bingwa ya ulaya baada ya kuichapa AC Milan ya Italia kwa magoli 3-1 katika uwanja wake wa nyumbani wa Nou Camp.
Barcelona waliokuwa wakishambulia tangu mwanzoni mwa kipindi iliwachukua dakika 11 pale Leonel Messi alipoangushwa katika eneo la hatari na bila ajizi refa wa mchezo huo aliamuru ipigwe penati, Leonel Messi alitupia penati hiyo kimiani na kuwafanya Barca kuongoz kwa goli moja.
Goli hilo liliwapa ari na kuwanyong'onyesha AC Milan kabla ya kuwarudisha katika mchezo ikiwa ni dakika ya 32 pale mshambuliaji Machachari mbrazil Robinho kufanya kazi ya ziada na kumpatia pasi murua Ibrahimovic nae bila ajizi akamchomekea pande la mwisho Antonio Nocerino akiwa katika nafasi nzuri nae akatupia kambani kuisawazishia AC Milan na kufanya magoli kuwa ni 1-1.
Ilionekana kama AC Milan wamerudi mchezoni kwa kucheza kwa kasi huku Barcelona wakicheza mchezo wao wa kawaida wa pasi nyingi na fupifupi. Kwa mara nyingine tena Barcelona walipata penati nyingine baada ya Nesta kumdandia mtu wakati kona inachongwa kuelekezwa langoni mwa AC Milan.
Dakika ya 53 Andre Iniesta alitupia kambani goli la tatu na kuwakata kabisa maini na kuwafanya AC Milan kuondokana na ndoto za kutinga nusu fainali za klabu bingwa ulaya. Mpaka mpira unakwisha matokeo yalikuwa Barcelona 3-1 AC Milan na hivyo Barcelona kusonga nusu fainali kwa jumla ya mabao 3-1 ikumbukwe mechi ya kwanza iliyochezwa huko Italia timu hizo zilitoshana nguvu.
Tazama picha za matukio katika mechi hiyo
Soccer - Barcelona v AC Milan Champions League - Quarter Finals - Second Leg - Nou Camp
Messi akikatiza katika msitu wachezaji wa AC Milan Mexes,Nesta na Nocerino

Soccer - Barcelona v AC Milan Champions League - Quarter Finals - Second Leg - Nou Camp
Dan Alves akiwa chini na golikipa wa AC Milan Abbiati huku Nesta akiwatazama katika purukushani hiyo

Soccer - Barcelona v AC Milan Champions League - Quarter Finals - Second Leg - Nou Camp
Fabregas akipimana ubavu na Ambrosini

Soccer - Barcelona v AC Milan Champions League - Quarter Finals - Second Leg - Nou Camp
Mtu tatu Mexes,Nesta na Nocerino zikimuandama Leonel Messi

Soccer - Barcelona v AC Milan Champions League - Quarter Finals - Second Leg - Nou Camp
Cuenca akikosa goli la wazi mbele ya Kipa wa AC Milan


Soccer - Barcelona v AC Milan Champions League - Quarter Finals - Second Leg - Nou Camp
Wachezaji wa AC Milan wakishangilia baada ya Nocerino kutupia goli la kusawazisha

Soccer - Barcelona v AC Milan Champions League - Quarter Finals - Second Leg - Nou Camp
Messi akifunga penati huku golikipa Abbiati akichumpa bila mafanikio


Soccer - Barcelona v AC Milan Champions League - Quarter Finals - Second Leg - Nou Camp
Shangwe na chereko baada ya Messi kutupia kambani kwa penati


Soccer - Barcelona v AC Milan Champions League - Quarter Finals - Second Leg - Nou Camp
Alves akimtuliza mizuka Robinho....take it esy meeeeeen!!!

Soccer - Barcelona v AC Milan Champions League - Quarter Finals - Second Leg - Nou Camp
Valdes akidaka mpira kichwani mwa Ibrahimovic

Soccer - Barcelona v AC Milan Champions League - Quarter Finals - Second Leg - Nou Camp
Kocha wa AC Milan Allegri akitoa maelekezo ambayo yaligonga mwamba kwa kuchapwa 3-1

Eto'o aipotezea Barcelona