Friday, May 11, 2012
Thursday, May 10, 2012
OBAMA APITISHA USHOGA MAREKANI
Ndoa ya jinsia moja ya kiume
Rais Barack Obama amesema kwamba watu wa jinsia moja wawe na haki ya kuoana.
Bwana Obama amesema daima amekuwa mgumu kukubali kwamba wanaume na wanawake wenye uhusiano wa mapenzi ya jinsia moja nchini Marekani watendewe haki na jamii kwa kutambua uhusiano huo, lakini amekuwa akipitia kile anachokiita mabadiliko ya kimtazamo kuhusu suala la ndoa za jinsia moja.
Ndoa ya jinsia moja ya kike
Kwa kauli hii Obama anakuwa rais wa kwanza wa Marekani kuunga mkono ndoa za jinsia moja, suala ambalo limeleta mgawanyiko miongoni mwa raia wa Marekani. Kumekuwa na maoni tofauti miongoni mwa Wamarekani kuhusu kuunga mkono ndoa za aina hii.
Jamaa kaopoa kifaa anaona utaaaaaaaaaaaaamu
Rais Obama anasema amejadili suala hilo na familia, marafiki na majirani kwa muda mrefu na kutilia maanani wafanyakazi wenzake na askari ambao wamejikita katika uhusiano wa mapenzi ya jinsia moja.
Mapenzi ya jinsia moja yakiwa yamekolea ..wanaona utaaaaaaaaaaaaaaaaaaaamu
Hatimaye amekuja na hitimisho kwamba ndoa zilizozoeleka hazikidhi matarajio ya wote.
Mpinzani wake katika uchaguzi wa rais wa mwaka huu, Mitt Romney, wa chama cha Republican amesema bado anabakia kupinga ndoa za watu wa jinsia moja.
Amesema wakati akiunga mkono ndoa ambazo hazijatambuliwa kisheria, kwa maoni yake, suala la ndoa za kawaida ni jambo lingine tofauti na hizo ndoa za jinsia moja.
Kauli ya Bwana Obama, imekuja siku moja baada ya jimbo la North Carolina kupitisha mabadiliko ya katiba ya jimbo hilo, yanayofafanua kuwa ndoa ni muungano tu kati ya mwanaume na mwanamke.
Waandamanaji wakidai ndoa za jinsia moko
Hotuba ya Obama akipitisha ndoa za jinsia moja
Wednesday, May 9, 2012
LIVERPOOL YALIPA KISASI KWA CHELSEA YAIBAMIZA 4-1
Caroll akibinjuka tik-tak mbele ya beki wa Liverpool
Ikiwa ni siku tatu tu baada ya Chelsea kuichapa Liverpool katika fainali ya kombe la FA kwa
Ivanovic aliesimama na Essien alielala wakishuhudia mpira uliopigwa na Suarez na kumgonga Essien ukitumbukia kimiani
magoli 2-1. Hatimaye Liverpool wakiwa katika dimba lao la Nyumbani pale Anfield wamewararua Chelsea kwa kamba 4-1 bila huruma mbele ya mashabiki 40,721 waliohudhuria mtifuano huo.

Luis Suarez akishangilia goli la kwanza la Liverpool
Kiama cha Chelsea kilianza katika dakika ya 18 pale Suarez alipoilamba vyenga ngome ya Chelsea na kuingia na mpira mpaka kwenye eneo la hatari pembeni ya uwanja alipoingiza kati mpira kwa ufundi na ukamgonga Essien na kutumbukia kambani na kuandika bao la kuongoza kwa Liverpool.
Caroll na Henderson wakishangilia kamba ya pili iliyotupiwa na J Henderson
Iliwachukua dakika 24 Liverpool kuendeleza kipigo pale J Henderson alipotupia kambani goli la pili kwa Liverpool na kuwaacha Chelsea wakiwa hawaamini kimbunga kinachowanyemelea.
Mara nyingine tena D Agger katika dakika ya 27 alitupia kambani bao la tatu ambalo kwa kiasi kikubwa liliwanyong'onyesha Chelsea kama sio kuwazorotesha na mbwembwe zote za Ubingwa wa FA zikawatokea puani.
J Hernandes waoooooooooooooooooooo
Mungu sio Athumani mnamo dakika ya 49 mchezaji mwenye juhudi na bidii na ubishi wa kiafrika ingawa ni mbrazili Ramires aliipatia Chelsea bao la kupangusia machozi ya kipigo katika mechi hiyo.

Mtifuano kati ya Terry na Suarez
Wakati kila mtu akiamini kichapo kimefikia mwisho, Golikipa wa akiba wa Chelsea alifanya boko la maana pale alipiga mpira katikati ya uwanja ili hali hayupo golini na ndipo kingekewa cha kupata goli kilipomuangukia J Shevley nae bila ajizi akatupia kambani kwa shuti kali katika dakika ya 60 na kuhitimisha dhoruba kali la mabao 4-1 kwa Chelsea toka kwa Liverpool.
Poleni sana fans wa Chelsea msife moyo mnaweza jipoza kwa Bayern Munich haa haaa haaaaaaa!!!
OKWI, BOBAN NA SUNZU KWENYE REKODI ZA C.A.F ,SIMBA YAIFUATA AL AHLY SHANDY
Emmanuel Okwi
Wawakilishi wa Tanzania kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho, Simba wanaondoka leo kwenda Khartoum, Sudan tayari kwa mchezo wa marudiono dhidi ya Al Ahly Shendi, washambuliaji nyota wa Wekundu hao wa Msimbazi, Emmanuel Okwi na Felix Sunzu wameingia kwenye rekodi ya wafungaji bora Afrika katika michuano ya Kombe la Shirikisho la soka Afrika.

Haruna Moshi "BOBAN"
Okwi, raia wa Uganda na Felix Sunzu ambaye ni Mzambia, wote wametajwa kuwa na mabao matatu kila mmoja kwa mujibu wa mtandao wa tensport.com.
Mshambuliaji huyo anayechezea pia Uganda Cranes, alifunga bao moja dhidi ya Entente Sportive de Setif katika mchezo wa kwanza kati ya mawili walioshinda mabao 2-0 Dar es Salaam na moja likifungwa na Haruna Moshi.

Felix Sunzu
Mchezo wa marudiano, Okwi alifunga moja wakati Simba ikilala mabao 3-1. Mshambuliaji huyo alifunga dhidi ya Al Ahly Shendi kati ya mabao matatu huku mengine yakifungwa na Boban na Patrick Mafisango.
Kwa hali hiyo, Boban na Sunzu kila mmoja wana mabao matatu. Sunzu aliyafunga katika mchezo walioshinda mabao 2-1 dhidi ya Kiyovu ya Rwanda na lingine likifungwa na Parick Mafisango.
Mbali na wachezaji hao, wengine wenye mabao matatu ni Komara, Niamba wote wa Leopards ya Congo, Chinyengetere (Hwange ya Zimbabwe, Moco (InterClube (Angola) na Raouf (ENPPI, Misri) na Seri wa Asec Mimosa ya Ivory Coast.
Mpaka sasa Fiston (Lydia Academic, Burundi) na Girma wa St George ya Ethiopia wana mabao manne kila mmoja.
Wakati huo huo, msafara wa Simba unaondoka leo mchana kwenda Sudan kupitia Nairobi, Kenya tayari kwa mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Al Ahly Shandy baada ya kukwama kuondoka kutokana na majambazi kuvunja na kuiba katika ubalozi wa Sudan.
Juzi usiku majambazi walivunja sefu ya kuhifadhia fedha na kuiba zaidi ya dola 40,000 ubalozini hapo pamoja fedha nyingine pamoja na kuiba kompyuta zote zinazotumika kuhifadhia kumbukumbu mbalimbali.
Kutokana na hali hiyo, Simba walikwama kupata viza zao juzi na jana na zinataraji kutolewa leo asubuhi kabla ya kuondoka saa 10:00 kwenda Sudan kupitia Nairobi ikiwa na wachezaji wote wa timu hiyo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile alithibitisha juzi kutokea tukio hilo.
Monday, May 7, 2012
SIMBA YAIRARUA YANGA 5-0, OKWI AINYANYASA BEKI YA YANGA,LOYD NCHUNGA ATOKA ATIMUA MBIO BAADA YA BAO LA TANO, MASHABIKI 3 WAZIMIA UWANJANI
Kioo cha matangazo cha uwanja mkuu wa Taifa kilivyokuwa kikisomeka katika dakika za majeruhi
Lloyd Nchunga jana alishindwa kuvumilia na kuamua kukimbia uwanjani baada ya timu yake kutandikwa bao la nne, wakati Yanga ilipopokea kipigo cha Paka mwizi cha mabao 5-0 kutoka kwa wapinzani wao, Simba.
Mwenyekiti huyo ambaye hivi karibuni alijikuta katika wakati mgumu, baada ya wazee wa klabu yake kutaka kuichukua timu mikononi mwake, alishuhudia mvua ya mabao kutoka kwa mabingwa, Simba, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar na kuzidi kuwa katika hali ngumu zaidi.Katika mchezo huo, Simba walianza kupata bao dakika ya kwanza tu ya mchezo kupitia kwa Emmanuel Okwi aliyeunganisha vizuri pasi ya Felix Sunzu baada ya Nurdin Bakari kupoteza mpira karibu na lango la Yanga.

Nimewanyongaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

Mchezaji aliyei-cost Yanga kuliko mchezaji mwingine yeyote Shadrack Nsajigwa

wa Yanga Papic jukwaani akiAliyekuwa kocha mkuu shuhudia timu hiyo ikinyanyaswa na Simba
Baada ya bao hilo, Yanga walifanya mashambulizi kadhaa katika dakika ya tisa na 11 huku shuti moja lililopigwa na Athuman Idd ‘Chuji’ likigonga mwamba na kurejea dimbani kabla Hamis Kiiza kupiga tena na safari hii mlinda mlango Juma Kaseja akiucheza mpira na baadaye kuokolewa na mabeki wake.
Okwi akishangilia baada ya kuitengeneza Yanga goli la kwanza
Kipindi cha kwanza kiliisha kwa Simba kuendelea kuongoza kwa bao 1-0 lakini kipindi cha pili ndicho kilichopeleka simanzi kubwa Jangwani baada ya kushuhudia kipa Said Mohammed aliyechukua nafasi ya Yaw Berko, akiokota mipira minne langoni mwake.
Aibu ya Yanga ilianzia dakika ya 53, baada ya Felix Sunzu, kupiga penalti kwa ufundi akiandika bao la pili. Penalti hiyo ilitokana na Okwi kuchezewa faulo katika eneo la hatari.
Dakika ya 62, Okwi alifanya tena kazi ya ziada, alipomtoka beki mkongwe, Shadrack Nsajigwa na kufunga bao safi lililowaacha wachezaji wa Yanga wakiwa wameshika viuno kwa huzuni.
Huku Jangwani wakiendelea kujiuliza, Simba walipata penalti nyingine katika dakika ya 66 baada ya Okwi kufanyiwa faulo tena ndani ya eneo la hatari na kipa, Mohammed. Juma Kaseja ndiye aliyepiga penalti hiyo na kuiandikia Simba bao la nne.
Nahodha wa Simba Juma Kaseja Juma akikabidhiwa kombe la ligi kuu ya Tanzania bara
Wachezaji wa Simba wakishangilia na kombe lao
Katika hali ya kushangaza, Simba walipata penalti ya tatu dakika ya 71 iliyotokana na beki, Athuman Idd ‘Chuji’ kumfanyia faulo Okwi ndani ya eneo la hatari. Patrick Mafisango alipiga penalti hiyo na kufikisha bao lake la 11 kwenye Ligi Kuu ya Bara msimu huu.
Katika tukio la kusikitisha, mashabiki wawili wa Yanga walizimia na kubebwa na watu wa Msalaba Mwekundu, baada ya Mafisango kufunga bao la tano huku Kocha Msaidizi wa timu hiyo, Fred Felix Minziro, akigoma kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu mchezo huo.
Naye Kocha Mkuu wa Simba, Milovan Cirkovic, amesema baada ya kufanikiwa kutwaa ubingwa, kwa sasa wanachokiangalia ni kufanya vizuri kwenye michuano ya kimataifa.
Katika mchezo wa mzunguko wa kwanza Yanga ilifanikiwa kuichapa Simba bao 1-0.
Katika matokeo mengine, licha ya Villa Squad kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Mlandizi, Pwani, ilijikuta ikishuka daraja na kuungana na Polisi Dodoma pamoja na Moro United.

Umati uliohudhuria kichapo cha Yanga
Kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, JKT Oljoro ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Polisi, wakati huko Mkwakwani, Tanga, Toto ilipata kipigo kama hicho kutoka kwa Coastal Union na kunusurika kushuka daraja kutokana na kuwa na uwiano mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa licha ya kuwa na pointi 26 sawa na Villa.
Mtibwa Sugar iliendeleza ubabe wake kwa kuifunga Moro United bao 1-0 kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro, Azam ikiishinda Kagera mabao 2-1, Chamazi, Dar na African Lyon ikiibamiza JKT Ruvu mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Manungu, Morogoro
Subscribe to:
Posts (Atom)