Friday, May 25, 2012

CHADEMA IKO JUU, CHEZEA MNYIKA WEWE!


John Mnyika,Mbunge wa Ubungo(CHADEMA) aliyeshinda kesi ya uchaguzi.

Kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi jimbo la Ubungo umeunguruma katika mahakama kuu kanda ya Dar es salaam na mbunge wa Jimbo la Ubungo John Mnyika (Chadema) amemshinda tena Hawa Ng'humbi (CCM) baada ya Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam kutoa hukumu kuwa ushindi wa Mbunge Mnyika uliofanyika Oktoba 31, 2010 ulikuwa wa halali.

Kesi hiyo namba 107 ya 2010, ilifunguliwa na aliyekuwa mgombea wa CCM, Hawa Ngh’umbi dhidi ya Mnyika ambaye ni mdaiwa wa pili katika kesi hiyo akitetewa na Wakili Edson Mbogoro.

Mdaiwa wa kwanza katika kesi hiyo iliyoko mbele ya Jaji Upendo Msuya ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na aliyekuwa Msimamizi wa Uchaguzi (RO) katika jimbo hilo, (aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni) ambao walikuwa wakitetewa na Wakili Mkuu wa Serikali (PSA), Justice Mulokozi.

Katika uchaguzi huo, uliofanyika Oktoba 31, 2010, Msimamizi wa Uchaguzi, Raphael Ndunguru alimtangaza Mnyika kuwa mshindi Novemba 2, 2010 baada ya kupata kura 66,742. Ngh’umbi alipata kura 50,544.

Hata hivyo, Ngh'umbi hakuridhishwa na matokeo hayo akaamua kufungua kesi Mahakama Kuu kuyapinga, akimtumia Wakili Issa Maige.

Katika hati yake ya madai na wakati akitoa ushahidi mahakamani, Ngh’umbi na mashahidi wake walidai kuwa kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa taratibu na kisheria katika ujumlishaji wa kura na utangazaji wa matokeo ambao umeathiri matokeo hayo.

Tuesday, May 22, 2012

HAPA NDIPO AMBAPO HAMNA MAANA YA KUVAA (KOFIA)HELMET







HII NDIO MARCEDES MAYBACH YENYE THAMANI YA DOLA MILIONI 1.3


Marcedes Maybach Inavyoonekana kwa mbele


Sehemu ya ndani mbele


Sehemu ya ndani nyuma ambapo unaweza kujiachia kama jamaa anavyopata udambwidambwi


Pale kati ina sehemu ya kuhifadhia glasi na vinywaji vya kila aina ili mradi umatemate uwe unaruhusu tu


Unaweza kujiachia namna hii na kusahau kama kuna siku utaiaga dunia na starehe hizo ukawaaachia wenzio


ACHA NDOTO SASA RUDI KATIKA MAISHA YA UWEZO WAKO ALAAAAAH

Huu ndio saizi yetu..au mnasemaje?

BOBAN AANGUUKA NA KUZIMIA UWANJA WA NDEGE


Mgosi na Boban wakiwa katika msiba mjini Kinshasa

MICHAEL MOMBURI, KINSHASA
KIUNGO wa Simba, Haruna Moshi Boban, ameanguka katika Uwanja wa Ndege wa N`Djili mjini Kinshasa kutokana na mapigo ya moyo kushuka ghafla.

Tukio hilo lilitokea jana Jumatatu wakati Boban akiwa anajiandaa kurudi Dar es Salaam baada ya kuhudhuria mazishi ya Patrick Mafisango aliyefariki Alhamisi iliyopita kwa ajali ya gari iliyotokea jijini Dar es Salaam.

Hali ya Boban ilibadilika ghafla akiwa uwanjani hapo na akashindwa kuona mbele kabla ya kulegea na kuanguka.

Madaktari wa uwanja huo walitumia zaidi ya saa 1:30 kumtibu Boban kabla hajarejea katika hali ya kawaida huku bado akiwa na simanzi kubwa kutokana na kifo cha Mafisango.

"Nilimkumbuka sana Mafisango, wakati nikitafakari, nikaona ninalegea, nikashindwa kuona kitu chochote mbele na nikaanguka," Boban aliliambia Mwanaspoti katika uwanja huo wa ndege wa Kinshasa.

Daktari aliyemuhudumia Boban aliliambia Mwanaspoti kuwa: "Alikuwa na hali mbaya sana, mapigo ya moyo yalikuwa chini, yangeweza kuondoa maisha yake."

Licha ya kupata matibabu hayo, Boban pia alipewa kahawa kwa lengo la kuinua mapigo yake ya moyo.

Boban ambaye alikuwa rafiki mkubwa wa Mafisango ikiwa ni pamoja na kulala chumba kimoja wanapokuwa kambini Simba, aliwakilisha wachezaji wengine wa klabu hiyo katika msiba huo mjini Kinshasa.

Mwili wa Mafisango aliyekuwa akicheza nafasi ya kiungo enzi za uhai wake, ulizikwa katika makaburi ya Kinkole nje kidogo ya Kinshasa juzi Jumapili kuhitimisha safari yake ya miaka 32 ya uhai wake duniani.

MILOVAN ALAMBA DUME SIMBA SPORTS CLUB


Kocha Milovan(Kushoto) na mwenyekiti wa Simba(Kulia)Rage

Timu ya Simba Sport Club ambao ni mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara wamemuongezea mkataba kocha wao Milovan Cirkovic kwa miaka miwili zaidi na kumfanya kocha huyo kuwa na uhakika na "umatemate" zaidibaada ya ule waliokuwa wamempa mwanzo wa miezi sita kumalizika.
Mkataba uliomalizika wa Milovan ni baada ya kurithi mikoba ya Mganda Moses Basena, akitangaza kumuongezea mkataba huo kocha Milovan, Makamu mwenyekiti wa Simba Godfrey Nyange Kaburu amesema" Kipimo cha mafanikio ya kocha ni mataji na soka safi,kitu ambacho sisi kama viongozi wa Simba tumekishuhudia chini ya Profesa Milovan,sasa hatuoni kwanini tusimuongezee mkataba."
Kaburu aliongeza kuwa sababu nyingine ni mipango mizuri aliyonayo Milovan kwa soka la Vijana wa Simba, ni kitu ambacho hakipingiki katika ligi iliyokwisha tumeshuhudia Vijana wa Simba wakipata nafasi ya kucheza na dhahiri wameonesha uwezo wao,mfano mzuri Jonas Mkude,Singano na wengine yote hayo ni mafanikio ya kocha Milovan kuwapa nafasi Vijana kuonesha "udambwidambwi" wao.

NADAL BINGWA ITALIAN OPEN AMCHAPA DJOKOVIC


Rafael Nadal (Kushoto) akiwa amebeba kombe la Ubingwa wa Italian Open baada ya kumshinda Djokovic(Kulia)

Rafael Nadal, mchezaji wa Uhispania, alifanikiwa kumshinda mchezaji bora zaidi duniani wa kiume, Novak Djokovic katika mashindano ya Italia Open, na kupata ubingwa wake wa sita katika mashindano hayo ya Italia.

Nadal alipata ushindi wa 7-5 6-3 katika fainali hiyo ambayo ilichezwa Jumatatu baada ya kuahirishwa siku ya Jumapili kutokana na mvua kunyesha mno mjini Roma.

Ushindi huo umemweka Nadal katika nafasi ya pili katika orodha ya wachezaji bora zaidi katika mashindano ya wanaume duniani.


Pamoja na hali ya hewa kuwa si shwari lakini wapenzi wa mchezo wa Tennis waliendelea kufuatilia mtifuano huo kati ya Nadal an Djokovic

Kabla ya mashindano ya Jumatatu, Djokovic, raia wa Serbia, amekuwa akimshinda Nadal mfululizo katika mashindano saba yaliyopita, kabla ya kuanza kuibuka tena kama mshindi katika fainali ya Monte Carlo Masters mwezi uliopita.
Sasa Nadal amemshinda katika fainali mbili za mwisho walizokutana.

Nadal alisema: "Mawazo ya ushindi yalinijia wakati muwafaka, kwani kumshinda Novak, unahitaji kuwa katika hali yako bora zaidi ya uchezaji, kwani yeye hukusukuma hadi mjwisho katika pambano lote.

"Nadhani kiakili nilikuwa katika hali thabiti kila wakati muhimu nilipohitajika kuwa hivyo."
Nadal Vs Djokovic

Monday, May 21, 2012

CHELSEA YATWAA NDOO YA LIGI YA MABINGWA WA ULAYA


Wachezaji wa Chelsea wakiwa na mwali wa ligi ya mabingwa ulaya

Meneja wa mda wa Chelsea Roberto di Matteo alipoingia mkutano wa wandishi wa habari kwa mazungumzo ya baada ya mechi saa saba na robo usiku wa manane, akijivunia rekodi kubwa kwa meneja yeyote wa muda kuwahi kushinda, machungu ya Chelsea daima kukosa Kombe la Ligi ya mabingwa tayari yalikua yamefutwa kwa dawa nyepesi kutamka, Ushindi.
Didier Drogba alipojipanga, bila pupa,wasiwasi wala hofu na kuupiga mpira ule kumpita golikipa wa Bayern, Manuel Neuer, mwenye sifa ya kuzuia mikwaju ya penati na kuthibitisha ushindi wa 4-3 kupitia matuta, miaka mingi ya kosa kosa iliwatoka wachezaji wote,wafanyakazi na viongozi wa Chelsea.

Manager Roberto Di Matteo of Chelsea speaks to the media during a press conference at Chelsea Training Ground on May 15, 2012 in Cobham, England.
Kocha wa Muda wa Chelsea Robert Di Matteo aliyeipa ubingwa wa barani ulaya Chelsea na kuweka rekodi ya kocha wa muda mwenye mafanikio zaidi
Hili lilifuatiwa na Drogba kuvua shati lake na kulipeperusha juu ya kichwa chake kuonyesha furaha ya ushindi baada ya kukimbia kuzunguka uwanja mzima, huku Fernando Torres na David Luiz wakipanda juu ya besera la goli kuonyesha furaha yao. Wakati huo Mmiliki wa klabu hio Abramovich mwenyewe akiruka na kupiga makofi huku akiimba ikidhihirisha sura isiyoonekana kwa kawaida kwa mtu msiri asiyeonyesha hisia zake.


Drogba akishangilia baada ya kutupia kambani penati ya mwisho iliyoipa ubingwa Chelsea

Ikiwa mkwaju huo ulikua wa mwisho kwa mchezaji huyu kutoka Ivory Coast kama mchezaji wa Chelsea, pamoja na bao lake la kusawazisha lile la Thomas Mueller, basi Drogba ataondoka kwa kuweka rekodi yake binafsi.


Drogba akimiliki mpira katika fainali hiyo

Drogba mwenyewe hakuweza kuelezea bayana juu ya majaliwa yake baada ya kukabidhiwa zawadi ya mchezaji bora wa mechi hio ya fainali ya Ligi ya mabingwa barani Ulaya. Punde mkataba wake unafikia mwisho na bado hakuna matumaini ya kama ataongezewa mda.

Hatma ya Meneja wa mda Di Matteo bado haijabainika na mwenyewe alishindwa kusema ni nini alidokezewa na Abramovich walipokumbatiana kwenye ngazi kabla ya sherehe za kukabidhiwa Kombe kwa mara ya kwanza katika historia ya miaka 107 ya klabu hio.
Haikua kazi rahisi kwa Chelsea uwanjani mpira ulipochezwa katika sehemu ya uwanja ya Chelsea lakini hadi mwisho lakini waliepuka uwezekano mkubwa wa kufungwa zaidi ya mabao manne ila kutimiza ndoto ya Abramovich.



Mara pekee kwa klabu hii kushamiri katika mashindano ya Ulaya, ulikua mwaka 1971 kabla ya hata Liverpool kushinda nje ya England, Chelsea ilipoichapa Real Madrid na kujishindia Kombe la Mshindi la mwaka huo wa 1971.

Drogba, aliongoza na kua kinara, na hivyo kuandika jina lake kwa vitendo katika historia. Kipa Petr Cech amepitia kipindi kigumu wakati wa kampeni ya Ligi ya mabingwa wa Ulaya lakini mjini Munich alionyesha ukomavu kwa kuzuia mkwaju wa Arjen Robben katika kipindi cha ziada na wakati wa matuta alizuia mkwaju wa Ivica Olic.
Mwamko wa Chelsea ulianza pale alipotimuliwa Andre Villas Boas kufuatia kipigo cha 3-1 na Napoli na mrithi wake Di Matteo akageuka kua chachu ya ufanisi kwa kusababisha ushindi wa Kombe la FA na mechi kadhaa za Ligi kuu ya Premiership.


Matokeo ya Napoli yakageuka kuipendelea Chelsea na baada ya hapo kuichabanga Benfica kujishindia fursa ya kukutana na Barcelona ambayo waliweza kuishinda kwa hatua zote mbili,nyumbani na ugenini licha ya kusukumwa kwa dakika nyingi.


Sifa kubwa anastahili Roberto Di Matteo aliyechimba ndani ya bongo za wachezaji aliyewafahamu na kuamini kua wana uwezo wa kushiriki na kucheza soka kwa kiwango cha juu na kushinda.

Bila shaka wadadisi watakosoa mbinu zilizotumiwa dhidi ya Barcelona na huko Munich lakini jibu la Di Matteo ni moja tu angalia rekodi ya mwaka 2012, Mabingwa wa Ulaya ni Chelsea.

Uwanja wa Allianz Arena ambapo kipute cha fainali ya ligi ya mabingwa kilipigwa na Chelsea
kuibuka kidedea


MIPIGO YA PENATI