John Mnyika,Mbunge wa Ubungo(CHADEMA) aliyeshinda kesi ya uchaguzi.
Kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi jimbo la Ubungo umeunguruma katika mahakama kuu kanda ya Dar es salaam na mbunge wa Jimbo la Ubungo John Mnyika (Chadema) amemshinda tena Hawa Ng'humbi (CCM) baada ya Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam kutoa hukumu kuwa ushindi wa Mbunge Mnyika uliofanyika Oktoba 31, 2010 ulikuwa wa halali. Kesi hiyo namba 107 ya 2010, ilifunguliwa na aliyekuwa mgombea wa CCM, Hawa Ngh’umbi dhidi ya Mnyika ambaye ni mdaiwa wa pili katika kesi hiyo akitetewa na Wakili Edson Mbogoro.
Mdaiwa wa kwanza katika kesi hiyo iliyoko mbele ya Jaji Upendo Msuya ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na aliyekuwa Msimamizi wa Uchaguzi (RO) katika jimbo hilo, (aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni) ambao walikuwa wakitetewa na Wakili Mkuu wa Serikali (PSA), Justice Mulokozi.
Katika uchaguzi huo, uliofanyika Oktoba 31, 2010, Msimamizi wa Uchaguzi, Raphael Ndunguru alimtangaza Mnyika kuwa mshindi Novemba 2, 2010 baada ya kupata kura 66,742. Ngh’umbi alipata kura 50,544.
Hata hivyo, Ngh'umbi hakuridhishwa na matokeo hayo akaamua kufungua kesi Mahakama Kuu kuyapinga, akimtumia Wakili Issa Maige.
Katika hati yake ya madai na wakati akitoa ushahidi mahakamani, Ngh’umbi na mashahidi wake walidai kuwa kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa taratibu na kisheria katika ujumlishaji wa kura na utangazaji wa matokeo ambao umeathiri matokeo hayo.
MICHAEL MOMBURI, KINSHASA KIUNGO wa Simba, Haruna Moshi Boban, ameanguka katika Uwanja wa Ndege wa N`Djili mjini Kinshasa kutokana na mapigo ya moyo kushuka ghafla.
Tukio hilo lilitokea jana Jumatatu wakati Boban akiwa anajiandaa kurudi Dar es Salaam baada ya kuhudhuria mazishi ya Patrick Mafisango aliyefariki Alhamisi iliyopita kwa ajali ya gari iliyotokea jijini Dar es Salaam.
Hali ya Boban ilibadilika ghafla akiwa uwanjani hapo na akashindwa kuona mbele kabla ya kulegea na kuanguka.
Madaktari wa uwanja huo walitumia zaidi ya saa 1:30 kumtibu Boban kabla hajarejea katika hali ya kawaida huku bado akiwa na simanzi kubwa kutokana na kifo cha Mafisango.
"Nilimkumbuka sana Mafisango, wakati nikitafakari, nikaona ninalegea, nikashindwa kuona kitu chochote mbele na nikaanguka," Boban aliliambia Mwanaspoti katika uwanja huo wa ndege wa Kinshasa.
Daktari aliyemuhudumia Boban aliliambia Mwanaspoti kuwa: "Alikuwa na hali mbaya sana, mapigo ya moyo yalikuwa chini, yangeweza kuondoa maisha yake."
Licha ya kupata matibabu hayo, Boban pia alipewa kahawa kwa lengo la kuinua mapigo yake ya moyo.
Boban ambaye alikuwa rafiki mkubwa wa Mafisango ikiwa ni pamoja na kulala chumba kimoja wanapokuwa kambini Simba, aliwakilisha wachezaji wengine wa klabu hiyo katika msiba huo mjini Kinshasa.
Mwili wa Mafisango aliyekuwa akicheza nafasi ya kiungo enzi za uhai wake, ulizikwa katika makaburi ya Kinkole nje kidogo ya Kinshasa juzi Jumapili kuhitimisha safari yake ya miaka 32 ya uhai wake duniani.
Kocha Milovan(Kushoto) na mwenyekiti wa Simba(Kulia)Rage
Timu ya Simba Sport Club ambao ni mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara wamemuongezea mkataba kocha wao Milovan Cirkovic kwa miaka miwili zaidi na kumfanya kocha huyo kuwa na uhakika na "umatemate" zaidibaada ya ule waliokuwa wamempa mwanzo wa miezi sita kumalizika. Mkataba uliomalizika wa Milovan ni baada ya kurithi mikoba ya Mganda Moses Basena, akitangaza kumuongezea mkataba huo kocha Milovan, Makamu mwenyekiti wa Simba Godfrey Nyange Kaburu amesema" Kipimo cha mafanikio ya kocha ni mataji na soka safi,kitu ambacho sisi kama viongozi wa Simba tumekishuhudia chini ya Profesa Milovan,sasa hatuoni kwanini tusimuongezee mkataba." Kaburu aliongeza kuwa sababu nyingine ni mipango mizuri aliyonayo Milovan kwa soka la Vijana wa Simba, ni kitu ambacho hakipingiki katika ligi iliyokwisha tumeshuhudia Vijana wa Simba wakipata nafasi ya kucheza na dhahiri wameonesha uwezo wao,mfano mzuri Jonas Mkude,Singano na wengine yote hayo ni mafanikio ya kocha Milovan kuwapa nafasi Vijana kuonesha "udambwidambwi" wao.
Rafael Nadal (Kushoto) akiwa amebeba kombe la Ubingwa wa Italian Open baada ya kumshinda Djokovic(Kulia)
Rafael Nadal, mchezaji wa Uhispania, alifanikiwa kumshinda
mchezaji bora zaidi duniani wa kiume, Novak Djokovic katika mashindano ya Italia
Open, na kupata ubingwa wake wa sita katika mashindano hayo ya Italia. Nadal alipata ushindi wa 7-5 6-3 katika fainali hiyo ambayo ilichezwa
Jumatatu baada ya kuahirishwa siku ya Jumapili kutokana na mvua kunyesha mno
mjini Roma.
Ushindi huo umemweka Nadal katika nafasi ya pili katika orodha ya wachezaji
bora zaidi katika mashindano ya wanaume duniani.
Pamoja na hali ya hewa kuwa si shwari lakini wapenzi wa mchezo wa Tennis waliendelea kufuatilia mtifuano huo kati ya Nadal an Djokovic
Kabla ya mashindano ya Jumatatu, Djokovic, raia wa Serbia, amekuwa akimshinda
Nadal mfululizo katika mashindano saba yaliyopita, kabla ya kuanza kuibuka tena
kama mshindi katika fainali ya Monte Carlo Masters mwezi uliopita. Sasa Nadal amemshinda katika fainali mbili za mwisho walizokutana. Nadal alisema: "Mawazo ya ushindi yalinijia wakati muwafaka, kwani kumshinda
Novak, unahitaji kuwa katika hali yako bora zaidi ya uchezaji, kwani yeye
hukusukuma hadi mjwisho katika pambano lote. "Nadhani kiakili nilikuwa katika hali thabiti kila wakati muhimu
nilipohitajika kuwa hivyo."
Wachezaji wa Chelsea wakiwa na mwali wa ligi ya mabingwa ulaya
Meneja wa mda wa Chelsea Roberto di Matteo alipoingia mkutano wa wandishi wa
habari kwa mazungumzo ya baada ya mechi saa saba na robo usiku wa manane,
akijivunia rekodi kubwa kwa meneja yeyote wa muda kuwahi kushinda, machungu ya
Chelsea daima kukosa Kombe la Ligi ya mabingwa tayari yalikua yamefutwa kwa dawa
nyepesi kutamka, Ushindi. Didier Drogba alipojipanga, bila pupa,wasiwasi wala hofu na kuupiga mpira ule
kumpita golikipa wa Bayern, Manuel Neuer, mwenye sifa ya kuzuia mikwaju ya
penati na kuthibitisha ushindi wa 4-3 kupitia matuta, miaka mingi ya kosa kosa
iliwatoka wachezaji wote,wafanyakazi na viongozi wa Chelsea.
Kocha wa Muda wa Chelsea Robert Di Matteo aliyeipa ubingwa wa barani ulaya Chelsea na kuweka rekodi ya kocha wa muda mwenye mafanikio zaidi
Hili lilifuatiwa na Drogba kuvua shati lake na kulipeperusha juu ya kichwa
chake kuonyesha furaha ya ushindi baada ya kukimbia kuzunguka uwanja mzima, huku
Fernando Torres na David Luiz wakipanda juu ya besera la goli kuonyesha furaha
yao. Wakati huo Mmiliki wa klabu hio Abramovich mwenyewe akiruka na kupiga
makofi huku akiimba ikidhihirisha sura isiyoonekana kwa kawaida kwa mtu msiri
asiyeonyesha hisia zake.
Drogba akishangilia baada ya kutupia kambani penati ya mwisho iliyoipa ubingwa Chelsea
Ikiwa mkwaju huo ulikua wa mwisho kwa mchezaji huyu kutoka Ivory Coast kama
mchezaji wa Chelsea, pamoja na bao lake la kusawazisha lile la Thomas Mueller,
basi Drogba ataondoka kwa kuweka rekodi yake binafsi. Drogba akimiliki mpira katika fainali hiyo
Drogba mwenyewe hakuweza kuelezea bayana juu ya majaliwa yake baada ya
kukabidhiwa zawadi ya mchezaji bora wa mechi hio ya fainali ya Ligi ya mabingwa
barani Ulaya. Punde mkataba wake unafikia mwisho na bado hakuna matumaini ya
kama ataongezewa mda. Hatma ya Meneja wa mda Di Matteo bado haijabainika na mwenyewe alishindwa
kusema ni nini alidokezewa na Abramovich walipokumbatiana kwenye ngazi kabla ya
sherehe za kukabidhiwa Kombe kwa mara ya kwanza katika historia ya miaka 107 ya
klabu hio. Haikua kazi rahisi kwa Chelsea uwanjani mpira ulipochezwa katika sehemu ya
uwanja ya Chelsea lakini hadi mwisho lakini waliepuka uwezekano mkubwa wa
kufungwa zaidi ya mabao manne ila kutimiza ndoto ya
Abramovich. Mara pekee kwa klabu hii kushamiri katika mashindano ya Ulaya, ulikua mwaka
1971 kabla ya hata Liverpool kushinda nje ya England, Chelsea ilipoichapa Real
Madrid na kujishindia Kombe la Mshindi la mwaka huo wa 1971. Drogba, aliongoza na kua kinara, na hivyo kuandika jina lake kwa vitendo
katika historia. Kipa Petr Cech amepitia kipindi kigumu wakati wa kampeni ya
Ligi ya mabingwa wa Ulaya lakini mjini Munich alionyesha ukomavu kwa kuzuia
mkwaju wa Arjen Robben katika kipindi cha ziada na wakati wa matuta alizuia
mkwaju wa Ivica Olic. Mwamko wa Chelsea ulianza pale alipotimuliwa Andre Villas
Boas kufuatia kipigo cha 3-1 na Napoli na mrithi wake Di
Matteo akageuka kua chachu ya ufanisi kwa kusababisha ushindi wa Kombe
la FA na mechi kadhaa za Ligi kuu ya Premiership. Matokeo ya Napoli yakageuka kuipendelea Chelsea na baada ya hapo kuichabanga
Benfica kujishindia fursa ya kukutana na Barcelona ambayo waliweza kuishinda kwa
hatua zote mbili,nyumbani na ugenini licha ya kusukumwa kwa dakika nyingi. Sifa kubwa anastahili Roberto Di Matteo aliyechimba ndani ya bongo za
wachezaji aliyewafahamu na kuamini kua wana uwezo wa kushiriki na kucheza soka
kwa kiwango cha juu na kushinda. Bila shaka wadadisi watakosoa mbinu zilizotumiwa dhidi ya Barcelona na huko
Munich lakini jibu la Di Matteo ni moja tu angalia rekodi ya mwaka 2012,
Mabingwa wa Ulaya ni Chelsea. Uwanja wa Allianz Arena ambapo kipute cha fainali ya ligi ya mabingwa kilipigwa na Chelsea kuibuka kidedea