Saturday, June 16, 2012

MWANAMAMA FATOU ARITHI MIKOBA YA OCAMPO MAHAKAMA YA KIMATAIFA YA UHALIFU WA KIVITA


Bi Fatou Bensouda

Luis Moreno Ocampo(kushoto) mwendesha mashtaka anaemaliza muda wake na Bi Fatou Bensouda (kulia)

Mwendesha Mashtaka Mkuu mpya wa Mahakama ya Kimataifa ya kukabiliana na Uhalifu wa Kivita ameapishwa mjini Hague hii leo.

Bi Fatou Bensouda, aliyekuwa Waziri wa Haki nchini Gambia,ndiye Mwafrika na pia mwanamke wa kwanza kushikilia wadhifa huo wa kuendesha mashtaka ya uhalifu wa kivita.
Mtihani wa kwanza kwa mwanamama Fatou ni kumleta Hague mtoto wa aliyekuwa kiongozi wa Libya, Kanali Muamar Gaddafi, Saif al-Islam Gadaffi, ambaye ameshtakiwa kwa makosa dhidi ya binadamu na wakati huohuo kuongoza mashtaka yanayomkabili aliyekuwa kiongozi wa Ivory Coast, Laurant Gbagbo.


Bi Bensouda akila kiapo kuitumikia mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita

Fatou Bensouda amechukua nafasi ya Luis Moreno Ocampo"Jembe", ambaye ameongoza mahakama hiyo kwa zaidi ya mwongo mmoja.

Kesi ya rais wa zamani wa Liberia, Charles Taylor, ilisikilizwa na mahakama ya Umoja wa mataifa inayosikiliza kesi za waliohusika na vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini
Sierra Leone.


Bi Bensouda amekuwa akifanya kazi kama naibu wa Luis Moreno-Ocampo anayemaliza muda wake katika mahakama ya ICC huko The Hague.

Mwandishi wa BBC anasema kuwa licha ya kwamba Bi Bensouda sio mgeni kwa mambo ya Hague, uteuzi wake unakuja wakati mfumo wa sheria ya kimataifa unahojiwa sana.

Pia anachukua jukumu hilo wakati kuna mtafaruku katika mahakama hiyo huku maafisa wanne wa mahakama hiyo wakiwa wanazuiliwa nchini Libya.

Mwandishi wa BBC anasema kuwa Bi Bensouda anasifika kwa kuwa mtulivu kitu ambacho huenda kimemsaidia katika kazi yake.
Ikizingatiwa kuwa washukiwa wengi ambao kesi zao ziko katika mahakama ya ICC ni waafrika na hili limekosolewa huku ofisi ya mwendesha mashtaka mkuu  ikisadikiwa kuwalenga zaidi waafrika.


Bi Bensouda akifuatilia jambo mahakamani huko The Hague

Bi Bensouda katika "swagga"

Inatarajiwa kwamba kwa kuwa Bi Bensouda mwenyewe ni Mwafrika tena wakili, huenda akasaidiwa na hili kunyamazisha wakosoaji wake, kulingana na wadadisi wa mambo.

Mwezi Machi mbabe wa kivita kutoka DRC, Thomas Lubanga alipokea hukumu ya kwanza ya kesi yake ikiwa hukumu ya kwanza kuwahi kutolewa na mahakama hiyo tangu kuundwa kwake miaka kumi iliyopita.

Kikosi cha viongozi wa mashtaka wanataka Lubanga atundikwe miaka 30 jela kwa makosa ya kutumia watoto kama wanajeshi wakati wa vita mashariki mwa DRC  kati ya mwaka 2002 na 2003.

Friday, June 15, 2012

EURO 2012 MPAKA SASA MAGOLI 38 KAMBANI

Uefa Euro 2012 | GOAL SCORERS


Player Team Goals
Alan Dzagoev Russia 3
Mario Gomez Germany 3
Andriy Shevchenko Ukraine 2
Fernando Torres Spain 2
Francesc Fabregas Spain 2
Mario Mandzukic Croatia 2
Nicklas Bendtner Denmark 2
Vaclav Pilar Czech Republic 2
Andrea Pirlo Italy 1
Antonio Di Natale Italy 1
David Silva Spain 1
Dimitris Salpingidis Greece 1
Helder Postiga Portugal 1
Jakub Blaszczykowski Poland 1
Joleon Lescott England 1
Kleper Pepe Portugal 1
Michael Krohn-Delhi Denmark 1
Nikica Jelavic Croatia 1
Petr Jiracek Czech Republic 1
Robert Lewandowski Poland 1
Robin van Persie Netherlands 1
Roman Pavlyuchenko Russia 1
Roman Shirokov Russia 1
Samir Nasri France 1
Sean St. Ledger Ireland 1
Total 38

MSIMAMO WA MAKUNDI MPAKA SASA EURO 2012

Uefa Euro 2012 | LOGS

Group A

Pos Team P W D L GF GA GD Pts
1 Russia 2 1 1 0 5 2 3 4
2 Czech Republic 2 1 0 1 3 5 -2 3
3 Poland 2 0 2 0 2 2 0 2
4 Greece 2 0 1 1 2 3 -1 1

Group B

Pos Team P W D L GF GA GD Pts
1 Germany 2 2 0 0 3 1 2 6
2 Portugal 2 1 0 1 3 3 0 3
3 Denmark 2 1 0 1 3 3 0 3
4 Netherlands 2 0 0 2 1 3 -2 0

Group C

Pos Team P W D L GF GA GD Pts
1 Spain 2 1 1 0 5 1 4 4
2 Croatia 2 1 1 0 4 2 2 4
3 Italy 2 0 2 0 2 2 0 2
4 Ireland 2 0 0 2 1 7 -6 0

Group D

Pos Team P W D L GF GA GD Pts
1 Ukraine 1 1 0 0 2 1 1 3
2 England 1 0 1 0 1 1 0 1
3 France 1 0 1 0 1 1 0 1
4 Sweden 1 0 0 1 1 2 -1 0

EURO 2012 SPAIN YAISUKUMA IRELAND NJE YA MICHUANO YAICHAKAZA 4-0



Torres (juu)akiachia  nduki iliyojaa moja kwa moja wavuni na kuvungua ukurasa wa mabao (chini) akishangilia.

Fernando Torres alifanikiwa kutupia kambani magoli mawili katika mechi ambayo Uhispania kwa urahisi ilifanikiwa kuilazimisha Jamhuri ya Ireland kukusanya virago na kuondoka katika mashindano ya Euro 2012.

Mkwaju wa Torres uliopigwa kwa kasi ya kutakata kutoka yadi kumi ulianzisha mfululizo wa magoli, mara tu baada ya bao hilo la kwanza kuingia wavuni katika dakika ya nne ya mchezo.

Mara tu baada ya kipindi cha pili, David Silva aliongezea bao la pili katika dakika ya 49.

Torres alifanikiwa kutupia bao lake la pili katika mechi hiyo katika dakika ya 70, huku mchezaji wa akiba Cesc Fabregas naye alitupia kambani bao la nne kwa nduki kali iliyokaribia kuchana nyavu za goli katika ya 83. Shukrani za pekee zimuendee mlinda mlango wa Ireland Shay Given kwa kuokoa michomo mingi ya Wahispania na hivyo kupunguza kapu la magoli.

Matokeo hayo yameiwezesha Uhispania kuipita Croatia na kuongoza kundi C.
Uhispania sasa itakutana na Croatia siku ya Jumatatu, mechi ambayo inatazamiwa kuwa ngumu.



Fabregas (juu)akitupia kambani goli la nne kwa shuti kali (chini) akishangilia.

Mchezo wa Jamhuri ya Ireland bila shaka ulikuwa na dosari nyingi, na katika mashindano yao makubwa baada ya kipindi cha miaka kumi, wamefungwa magoli mengi kirahisi.

Katika kila mechi waliocheza ya Euro 2012, katika kila nusu ya mchezo ilipoanza, walifungwa bao chini ya dakika nne za mwanzo, hii ikiwa ni pamoja na katika mechi walioshindwa na Croatia magoli 3-1.


Mashabiki wa Ireland ambao kwa kiasi kikubwa walionesha uzalendo kwa kushangilia mwanzo mwisho bila kujali kichapo walichokishuhudia kutoka kwa Uhispania..WaTanzania tuigeni uzalendo huu pindi timu zetu zinapocheza

Kabla ya mechi hiyo, Jamhuri ya Ireland ilikuwa haijawahi kupokea kichapo cha zaidi ya magoli matatu katika mashindano makubwa.
Lakini hayo sasa yametokea, wakifungwa magoli mengi mara mbili katika kipindi cha siku tano.


Fundi XAVI akifanya mamboz katika mtanange huo

Dogo hapa huendi kokote!!... Silva akidhibitiwa na walinzi wa Ireland

Kwa Uhispania ambayo ilitoka sare ya 1-1 iipocheza na Italia katika mechi yao ya kwanza, hili ni onyo muhimu kwa wapinzani, kuonyesha kwamba nchi hiyo ina nia ya kuandikisha historia kwa kuwa mabingwa katika mashindano makubwa.

Ujumbe umewasilishwa kikamilifu chini ya saa 24 tangu Ujerumani nayo ilipoonyesha uhodari wake kwa kuilaza Uholanzi magoli 2-1.
SPAIN  4-0  REPUBLIC OF IRELAND

Thursday, June 14, 2012

10 Things Your Interviewer Won't Tell You


Wondering what's running through your interviewer's mind? Here are 10 things your interviewer might be thinking--but probably won't tell you:

1. You showed up too early. Many interviewers are annoyed when candidates show up more than five or 10 minutes early, since they may feel obligated to interrupt what they're doing and go out to greet the person. Some feel guilty leaving someone sitting in their reception area that long. Aim to walk in five minutes early, but no more than that.

2. We're judging how you're dressed and groomed. In most industries, a professional appearance still matters. You don't need to wear expensive clothes, but showing up in a casual outfit or clothes that don't fit properly, having unkempt hair, or inappropriately flashy makeup can harm your chances.

3. We don't want you to try to sell us. It's a turn-off when a candidate seems overly focused on closing the deal, rather than on figuring out if the job is the right fit. No hiring manager wants to think she's being aggressively sold; we want the best person for the job, not the pushiest spiel.

4. Little things count. Candidates often act as if only "official" contacts, like interviews and formal writing samples, count, but hiring managers are watching everything, including things like how quickly you respond to requests for writing samples and references, whether your email confirming the time of the interview is sloppily written, and how you treat the receptionist.

5. We might act like we don't mind you bad mouthing a former employer, but we do. We'll let you talk on once you start, but internally we're noting that you're willing to trash-talk people who have employed you in the past and are wondering if you'll do that to us too. What's more, we're wondering about the other side of the story--whether you're hard to get along with, or a troublemaker, or impossible to please.

6. You might be talking too much. Your answers to your interviewer's questions should be direct and to-the-point. Rambling and unnecessary tangents raise doubts about your ability to organize your thoughts and convey needed information quickly. If you're tempted to go on longer than two minutes, instead ask, "Does that give you what you're looking for, or would you like me to go more in depth about this?" If the interviewer wants more, she'll say so.

7. Fit really, really matters, so we think a lot about your personality. You might have all the qualifications an employer is looking for, but still not get hired because your working style would clash with the people with whom you'd be working. Remember, it's not just a question of whether you have the skills to do the job; it's also a question of fit for this particular position, with this particular boss, in this particular culture, and in this particular company.

8. We want you to talk about salary first for the exact reason you fear. Salary conversations are nerve-wracking for job seekers because they know that they risk low-balling themselves by naming a number first. And that's exactly why interviewers push candidates to throw out a number first. In an ideal world, employers would simply let candidates know the range they intend to pay, but in reality, plenty take advantage of the power disparity by making candidates talk about money first.

9. We're going to ask other people what they think of you. We're going to ask anyone who came in contact with you for their impressions--from the receptionist to the guy who you met for two minutes in the hallway.

10. We like thank-you notes, but not for the reason you think. Post-interview thank-you notes aren't just about thanking the interviewer for her time; the ones that are done well build on the conversation and reiterate your enthusiasm for the job.

EURO 2012 GOMEZ APELEKA KILIO UHOLANZI IKILALA DORO MBELE YA UJERUMANI


Pepe akishangilia baada ya kuipatia Ureno kamba ya kwanza


Ureno imeiadhibu Denmark 3-2 katika mtanange wa kundi B katika michuano ya Euro 2012.
Ushindi wa Ureno wa 3-2 dhidi ya Denmark katika michuano wa Euro 2012 unaweka matumaini ya nchi hiyo kuendelea hadi robo fainali.
Bao lililonusuru matumaini hayo lilitiwa kimyani na Silvestre Varela aliyeletwa kipindi cha pili aliyefunga bao na kufuta bao la Nicklas Bendtner la kusawazisha mapema katika kipindi cha pili.


Varela alieingia kipindi cha pili akishangilia goli la tatu na la ushindi la Ureno baada ya kutupia kambani.

Ureno iliongoza kupitia kipindi cha kwanza kupitia wachezaji wasiotarajiwa ambapo beki Pepe na Helder Postiga waliipatia Ureno mabao ya kuwapa matumaini ya kupiga hatua.

Lakini kukosa fursa kadhaa kwa nyota wao Cristiano Ronaldo kulitishia kuiangusha Ureno na kurejea nyumbani mapema.


Christia Ronaldo akijaribu kumhadaa mlinzi wa Denmark lakini alikosa mabao lukuki katika mechi hiyo

Ushindi huu unaiweka Ureno sambamba na Denmark kwa pointi kutokana na ushindi wa Denmark dhidi ya Uholanzi katika mechi ya ufunguzi kwa pande hizo mbili.

Katika mchezo wa pili siku ya Jumatano, Mario Gomez wa Ujerumani aliwafunza wachezaji wa Uholanzi namna ya kufunga mabao, walipoondoka na ushindi wa magoli 2-1.


Gomez (23) akitupia kambani goli la kwanza la Ujerumani

Hapa hapatoshi!!! Robben akijaribu kufanya udambwidambwi katika mtanange huo

Mshambulizi huyo wa Bayern Munich kwa upesi aliweza kugeuka alipopokea mpira kutoka kwa Bastian Schweinsteiger na kuandikisha bao la kwanza la Ujerumani katika dakika ya 24, na baadaye kuongezea la pili katika dakika ya 38, katika kuhakikisha Uholanzi itaondoka katika michuano ya Euro 2012 mapema.


Robin Van Persie na Van Der Vaart wakishangilia goli la kufutia machozi lililotupiwa kambani na Van Persie

Robin van Persie, ambaye alishindwa kuitumia nafasi nzuri iliyojitokeza na kuiwezesha Uholanzi kuongoza kufunga, hatimaye aliwafungia bao la kujituliza, lakini timu yake ikashindwa kufunga magoli zaidi.
DENMARK  2-3  URENO


UJERUMANI  2-1  UHOLANZI

DI MATTEO NAMBA YA BAHATI YAFYATUKA SASA KOCHA MKUU CHELSEA


Kocha alielamba dume Chelsea Roberto Di Matteo

Chelsea hatimaye imemteua Roberto Di Matteo kama meneja wake wa kudumu kwa kutiliana saini mkataba wa miaka miwili na sasa Di Matteo ana uhakika na umatemate kama kocha mkuu kwa nyundo mbili.
Di Matteo aliwekwa kama kocha wa mda kufuatia kutimuliwa kwa Andre Villas-Boas mnamo mwezi Machi, na akaweza kuiongoza klabu hio akifanikiwa kuifikisha na kushinda fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya na vilevile kombe la FA la England.


Di Matteo kulia akiteta jambo na kocha alietimuliwa Andre Villa Boas, ambae sasa Di Matteo ndie amerithi Mikoba yake.

Meneja huyo aliyekua kiongozi wa MK Dons na pia West Brom, Di Matteo alipoteza mechi tatu tu kati ya mechi 21 alizosimamia, na kutokana na hali hiyo wachezaji wengi wa klabu waliunga mkono ateuliwe kama meneja wa kudumu hususan baada ya kushinda kombe lililoikwepa klabu hio kwa mda mrefu la Mabingwa wa Ulaya.

Di Matteo akiwa ameshikilia ndoo ya Ubingwa wa Ulaya alipoiwezesha Chelsea kulinyakua hivi karibuni baada ya ukata wa kombe hilo kwa muda mrefu na kumhakikishia Di Matteo kuwa na uhakika wa umatemate kwa miaka miwili kama kocha mkuu





Cherekochereko asie na mwana aeleke jiwe Di Matteo juujuu baada ya kutwaa kombe la mabingwa wa Ulaya