Thursday, July 26, 2012

VIWANJA VITAKAVYOCHIMBIKA OLYMPIC 2012



Aquatics Centre
Olympic Park, Eneo hili linajumuisha viwanja vitakavyotumika katika mashindano ya Olympiki 2012 jijini London nchini Uingereza. Olympic Park inajumuisha Aquatics Centre,Basketball Arena,BMX Track,Copper Box,Olympic Stadium,Riverbank Arena,Velodrome na WaterPolo Arena.

OLYMPIC STADIUM

Olympic Stadium una uwezo wa kuchukua watazamaji 60,000 wakiwa wamekaa. Ulikamilika Machi 2011 na mpaka sasa Mashindano 42 yameshafanyika uwanjani hapo.

AQUATICS CENTRE
Aquatics Centre
Uwanja huu wa ndani una uwezo wa kuingiza watazamaji 17,500 ambao ulimalizika kujengwa julai 2011. Michezo ni pamoja na Kuogelea,Kuzamia.

BASKETBALL ARENA



Basketball Arena una uwezo wa kuingiza watazamaji 12,000 wakiwa wamekaa na unatumika kwa michezo ya Mpira wa kikapu(Basketball) na mpira wa mikono(Handball)

COPPER BOX



Copper Box una uwezo wa kumeza watazamaji 7,000 na michezo inayohusika humo ni Mpira wa mikono(Handball) na Modern Pentathlon


WATER POLO ARENA


Water Polo Arena una pakia watazamaji 5,000 mchezo ni mmoja tu wa Water Polo


BMX TRACK


Khalen Young - LOCOG Test Events for London 2012 - BMX UCI World Cup
Khalen Young - LOCOG Test Events for London 2012 - BMX UCI World Cup

BMX Track inakusanya watazamaji 6,000 na mchezo ni wa Kukimbiza baiskeli aina ya BMX


RIVERBANK ARENA



Riverbank Arena una uwezo wa kuwakalisha chini watazamaji 16,000 na mchezo ni Mpira wa magongo(Hockey)


RICOH ARENA




Ricoh Arena ni uwanja wa Coventry City ya jijini London, uwanja una uwezo wa kukusanya watazamaji 32,609 wakiwa wameweka makalio chini, mchezo ni mpira wa miguu pekee.


VELODROME



Veldrome unaingiza watazamaji 15,000 mchezo ni Baiskeli


EARLS COURT


Earls Court wanaingia watazamaji 16,000 mchezo ni Volleyball


ETON DORNEY


The Australian Ladies & Mens Coxed Eights squad practise during rowing training at Eton Dorney on July 24, 2012 in London, England.
Eton Dorney watazamaji 20,000 wanaweza kuangalia michezo ya Rowing na Canoe sprint.


EXCEL



Excel ni uwanja wa ndani wenye uwezo wa kuingiza watazamaji 10,000, michezo ni Ngumi(Boxing),Kunyanyua vitu vizito(Weightlifting),Table Tennis,Fencing,Judo,Taekwondo,wrestling(Mieleka)


GREENWHICH PARK


Katika viwanja hivi watazamaji zaidi ya 23,000 wanaweza kushuhudia mbio za farasi na michezo mingine


HADLEIGH FARM




Hadleigh farm watazamaji wapatao 20,00 wanaweza kushuhudia michezo ya baiskeli


HAMPDEN PARK


Hampden Park uwanja huu unauwezo wa kuingiza watazamaji 52,063 wakiwa wamekaa kushuhudia mchezo wa soka

VIGOGO WAGAWANA VIWANJA DAR,WALALAHOI WACHINJIWA BAHARINI

MANISPAA ya Temeke imetoa orodha ya majina ya wananchi waliopewa viwanja katika manispaa hiyo, ambayo inaonyesha kuwamo kwa vigogo wanaojumuisha mawaziri, wabunge, watendaji wakuu wa Serikali pamoja na baadhi ya watoto wa vigogo hao.Katika orodha hiyo, jumla ya watu 1,800 walipatiwa viwanja hivyo, huku majina hayo ya vigogo yakiwa ni zaidi ya 50, ambao baadhi wamejiandikisha wenyewe, wengine wake zao, ndugu na watoto wao.
Orodha ya Vigogo hao iliyobandikwa katika ofisi za manispaa ya Temeke gazeti la Mwananchi 25 Julai 2012 limeyanyaka kama ifuatavyo;

Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama; Naibu Spika, Job Ndugai; Waziri wa Mawasiliano, Sanyansi na Teknolojia, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima.

Kwa upande wa Makatibu Wakuu wa Wizara wapo, Dk Florence Turuka (Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia), Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Ramadhan Kijjah; Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Omary Chambo na Dk Idris Rashid ambaye ni Gavana wa Zamani wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Pia wamo Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk Didas Masaburi, Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Slaa; Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu Dar es Salaam, Suleinan Kova.

Wengine ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), Haruna Masebu; Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh na Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili(MNH),Marina Njelekela.

Kwa upande wa wabunge wamo Dk Augustine Mrema (Vunjo - TLP), Mbunge wa Ludewa (CCM), Deo Filikunjombe; Mbunge wa Kibaha Mjini (CCM), Sylvester Koka; Mbunge wa Kinondoni (CCM), Idd Azzan; Mbunge wa Moshi Vijijini (CCM), Dk Cyril Chami na Mbunge wa Singida Kusini (CCM), Mohamed Misanga.
Wengine ni Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila; Mbunge wa Igunga (CCM), Dk Peter Kafumu na Mbunge wa Bukene (CCM), Seleman Zedi.

Wabunge wa Viti Maalumu (Chadema), Maulida Komu na Suzan Lyimo, Viti Maalumu CCM, Dk Mary Mwanjelwa na Zakhia Meghji ambaye ni mbunge wa kuteuliwa.

Orodha hiyo pia inaonyesha majina ya ukoo yanayofanana na majina ya baadhi ya viongozi ambao ni Miraji Kikwete, Khalfan Kikwete, Juanita Mramba, Suzan Mkapa, Zainab Mkomwa, George Rupia, Maimuna Mfutakamba, Mary Membe, Pharles Ngeleja, Judith Kahama na Wilfred Mwanri.

Mkurugenzi apepesa macho na kung'ata maneno ashindwa kutoa maelezo yaliyonyooka
Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Magreth Nyalile alipoulizwa kuhusu orodha hiyo alisema kuwa, majina hayo hajayaona na kwamba waliobandika wamefanya uamuzi huo bila ya yeye kuupitia.

Majina yenyewe sijayaona, hivyo basi siwezi kujua ni kina nani waliopewa viwanja hivyo, kwa sababu wako zaidi ya 1,000, jambo ambalo litakuwa vigumu kwangu kubaini tatizo hilo,” alisema Nyalile.

Aliongeza kuwa, kutokana na hali hiyo hawezi kusema lolote kwa sababu yuko nje ya ofisi kwa ajili ya shughuli nyingine za ujenzi wa taifa.

Hata hivyo, Nyalile alisema mchakato wa ugawaji wa viwanja hivyo ulifuata taratibu za kisheria na kwamba hakuna mtu au kiongozi yeyote aliyependelewa, jambo ambalo linaweza kusababisha mgongano wa hapa na pale.

Nyalile alisema kuwa kama kuna viongozi walipewa kwa njia zisizo sahihi, au kwa rushwa wakati wa uwasilishaji wa majina hayo, walipaswa kutoa taarifa kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.

Wednesday, July 25, 2012

WANAOONGOZA KWA KUTIKISA NYAVU KATIKA MICHUANO YA KAGAME 2012


Etikiama Taddy, Mshambuliaji wa AS Vita anaongoza mpaka sasa kwa kutikisa nyavu katika michuano ya Kagame ana mabao 6

ORODHA KAMILI YA WALIOTIKISA NYAVU MPAKA SASA

Taddy Etikiama (AS Vita)       6

Said Bahanuzi (Yanga SC)    5

Hamisi Kiiza (Yanga SC)       4

John Bocco (Azam FC)         4

Suleiman Ndikumana (APR) 3

Abdallah Juma (Simba SC)   2

Leonel St Preus (APR)         2           
 
Didier Kavumbagu (Atletico) 2

Feni Ali (URA)                       2

Robert Ssentongo (URA)      2

MRISHO NGASSA ANATAKA KURUDI YANGA, AIFANYIA AZAM MGOMO BARIDI


Mrisho Ngassa akiwa katika Benchi la Azam katika mechi ya robo fainali kombe la Kagame kati ya Azam na Simba

KOCHA wa Azam FC, Muingereza Stewart Hall amesema hamtumii Mrisho Khalfan Ngassa kwa sasa, kwa sababu haonyeshi dalili za kutaka kucheza.

“Hana jitihada zozote, hajitumi, hana hamu ya kucheza, siwezi kumchezesha,”alisema Stewart mapema tu, kabla ya mechi ya Robo Fainali dhidi ya Simba SC, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Pamoja na kucheza bila Ngassa, Azam imeshinda 3-1 na kuingia Nusu Fainali, ambako itamenyana na AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Kuna tetesi kwamba, Ngassa yupo kwenye mgomo baridi kushinikiza uhamisho wa kurejea Yanga, lakini habari ambazo  zimepatikana kutoka ndani ya Azam, zinasema kwamba, klabu hiyo itaendelea kuishi naye hivyo hivyo ‘kimakunyanzi’ hadi amalize mkataba wake msimu ujao.

KOMBE LA KAGAME, MNYAMA ALAMBA LAMBALAMBA YENYE SUMU KALI UWANJA WA TAIFA


Wachezaji wa Azam wakishangilia bao lililotupiwa na John Bocco "Adebayor/Boko Haramu" aliekaa chini.

Vilabu vya Azam na Vita vimefanikiwa kuingia nusu fainali ya michuano ya soka ya Cecafa.

John Bocco alikuwa shujaa pale timu yake ya Azam ya Tanzania, ilipofanikiwa kuingia nusu fainali ya mashindano ya klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati baada ya kuwafunga mabingwa wa Tanzania, Simba, mabao 3-1.

Katika mechi hiyo ya robo fainali iliyochezwa Jumanne mjini Dar es Salaam, Bocco alitupiamo kambanio mabao yote dakika ya 17, 46 na 73, wakati bao la kufutia machozi la Simba likitupiwa na Shomari Kapombe dakika ya 53.

Timu hiyo sasa itapambana na Vita Club ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo kwenye nusu fainali itakayochezwa Alhamisi.

Vita Club walifuzu baada ya kushinda kwa mambao 2-1 dhidi ya Atletico ya Burundi kwenye mechi nyingine iliyochezwa Jumanne. Mabao ya Vita yalifungwa na Taddy Etekiama na Basilua Makola wakati bao la Atletico lilifungwa na Pierre Kwizera.

Matokeo hayo yamekuwa ya kushangaza hasa ikizingatiwa kuwa Simba ni timu kongwe ambayo imeshinda kombe hili la ukanda mara sita.

Nayo Azam, iliyoanzishwa mwaka 2007, haya ni mashindano yao ya kwanza kimataifa tangu timu ianzishwe na ilipata tiketi ya kushiriki baada ya kumaliza ligi msimu uliopita ikiwa nafasi ya pili.

Mafanikio ya Azam yanakuja baada ya kusajili wachezaji kutoka Ivory Coast na Kenya na kumwajiri kocha kutoka Uingereza.

Mechi zote za nusu fainali zitachezwa Alhamisi kufuatia kuondoshwa Simba kwenye mashindano.

Timu nyingine zitakazokutana kwenye hatua hiyo ni bingwa mtetezi Yanga ya Tanzania na APR ya Rwanda.

Fainali itachezwa Jumamosi na bingwa atapewa zawadi ya dola 30,000 na mshindi wa pili 20,000, na atakayemaliza katika nafasi ya tatu ataondoka na kitita cha dola 10,000.

Katika mchezo wa huo, kikosi cha Azam kilikuwa; Deo Munishi, Ibrahim Shikanda, Erasto Nyoni, Said Mourad, Aggrey Morris, Kipre Michael Balou/Ramadhan Chombo, Kipre Herman Tcheche/George Odhiambo ‘Blackberry’, Salum Abubakar, John Bocco, Ibrahim Mwaipopo na Khamis Mcha ‘Vialli’/Jabir Aziz.

Simba SC; Juma Kaseja, Haruna Shamte, Shomary Kapombe, Lino Masombo, Juma Nyosso, Mussa Mudde, Uhuru Suleiman/Kiggi Makassy, Mwinyi Kazimoto, Felix Sunzu, Haruna Moshi na Jonas Mkude/Amri Kiemba.

Mrisho Ngassa akiwa ubaoni


Kocha wa Simba Milovan Cirkovic akiwa amelowana kwa kichapo.


Kocha wa Yanga Tom Saintfiet ,Felix Minziro naMfaume athumani wakifuatilia mtanange kati ya Simba na Azam


Benchi la Simba haliamini kilichotokea katika mechi yao dhidi ya Azam

Mashabiki wa Azam F.C


Mashabiki wa Simba S.C


John Bocco "Boko Haramu" akijaribu kuiponyoka ngome ya Simba


Felix Sunzu akiwa amerudi nyuma kusaidia kuokoa jahazi wakati mpira wa kona ukielekezwa lango la Simba


Kipre Cheche wa Azam akitiririka kuelekea kumsalimu Juma Kaseja


John Bocco "Boko Haram" akishangilia bao la pili


John Bocco 'Boko Haram" na Abubakar Saalum 'Sure Boy' wakishangilia kwa mtindo wa aina yake.

Nazi hii ilivunjwa na kamati ya ufundi ya Simba S.C lakini haikufua dafu!


Kikosi cha Simba




Kikosi Cha Azam F.C

Tuesday, July 24, 2012

ROBO FAINALI KAGAME CUP,HATUMWI MTOTO SOKONI SIMBA Vs AZAM


'Mwali" wa Kagame ambapo imefikia hatua ya robo fainali

Mabingwa wa Soka nchini, Simba na mabingwa wa Kombe la Mapinduzi, Azam FC leo zina fursa kupalilia kampeni ya kuongeza mataji kwenye makabati yao zitakapokutana katika mchezo wa robo fainali ya michuano ya Kombe la Kagame kwenye Uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam.
Mbali na mechi hiyo inayotarajia kuwa na ushindani mkubwa, pia kutakuwa na mchezo mwingine wa robo fainali utakaozikitanisha Atletico ya Burundi dhidi ya Vita Club ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Mchezowa Simba na Azam ni kama fainali kwani zimekuwa zikikamiana kila zinapokutana, ambapo mara ya mwisho zilikutana fainali ya Kombe la Urafiki na Simba kushindwa kwa mikwaju ya penalti baada ya sare ya 2-2.
Lakini kabla ya hapo, Simba ilinyukwa mabao 2-0 kwenye michuano ya Kombe la Mpinduzi, kabla ya Wekundu hao wa Msimbazi kulipa kisasi kwa ushindi wa mabao 2-0 katika mechi ya marudiano ya Ligi Kuu.
Mechi ya leo inazikutanisha kwa mara ya nne, ambapo zitakutana tena katika mchezo wa Ngao ya Jamii mwishoni mwa mwezi ujao kama ishara ya mwanzo wa msimu mpya wa Ligi Kuu Bara.
Azam inashiriki michuano ya Kombe la Kagame kwa mara ya kwanza na imepania kutaka kuweka rekodi ya kutwaa taji lingine baada ya lile la Mapinduzi.
Kocha Stewart Hall anajivunia kikosi chake kilichokuwa Kundi C la michuano hiyo pamoja na Mafunzo na Tusker ya Kenya.
Atamtegemea zaidi kipa mpya, Deogratius Munishi 'Dida'  ndiye atakayesimama langoni, huku Waziri Salum akirejea uwanjani kucheza beki wa kushoto na mchezaji bora nchini, Aggrey Morris atasimama katikati akishirikiana na Joseph Owino na Erasto Nyoni akicheza beki wa kulia.
Viungo watatu watakuwa ni Kipre Bolou, Salum Abubakar na Ramadhan Chombo Redondo, wakati mfungaji bora wa klabu John Bocco atasimama katika ushambuliaji akishirikiana na Kipre Tchetche na Mrisho Ngasa.
Kwa upande wa Simba ambayo makali yake katika safu ya ushambuliaji bado hayajaonekana tangu kuondoka kwa Emmanuel Okwi, itaendelea kumtegemea Felix Sunzu kupachika mabao.
Kocha Circovic Milovan, amekiri wazi kukosekana Okwi na kufariki kwa Patrick Mafisango, kumeacha pengo kubwa kwenye kikosi chake.
Simba ilianza vibaya michuano hiyo kwa kunyukwa 2-0 na URA ya Uganda kalba ya kuichapa Ports ya Djibouti mabao 3-1 na kulazimishwa sare ya 1-1 na Vita Club ya Kongo.
Majeruhi Shomari Kapombe na Amir Maftah wanampa presha Milovan na itabidi atumie muungano wa Haruna Shamte na Kiggi Makasi na nafasi ya Okwi akiiziba Abdallah Juma ambaye ni kinda aliyemfunika Felix Sunzu kutokana na kutumia vema nafasi hiyo.
"Kukosekana kwa ubunifu baada ya Okwi kuondoka ni ngumu kwetu, lakini Juma Abdallah anajitahidi kucheza vizuri ingawa bado haijaimudu vizuri.
"Nahitaji harakati mshambuliaji mmoja muhimu, nina uhakika wa asilimia 75 Okwi hawezi kurudi tena Simba," alisema Milovan.
Mechi nyingine itanayotarajia kuwa kali itazikutanisha Atletico na Vita Club ambazo zimeonyesha uwezo na kucheza kwa ufundi tangu kuanza kwa michuano hii.
Atletico imetinga robo fainali bila ya nyavu zake kutikiswa baada ya kuinyuka Yanga mabao 2-0 na kisha kwenda sare ya bila kufungana na APR, kabla ya kuinyuka Wau Salaam ya Sudan ya Kusini mabao 5-0 huku Vita ambayo inashiriki michuano hii kama wageni waalikwa walianza harakati zao kwa kuinyuka Ports ya Djibouti mabao 7-0 na kujikuta ikinyukwa mabao 3-1 na URA ya Uganda na kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Simba mwishoni mwa  wiki.