Oscar akishangilia goli pamoja na wenzake Ramires na David Luiz
Mabingwa watetezi wa klabu bingwa barani Ulaya, Chelsea ya
Uingereza, wakiwa katika dimba la nyumbani la Stamford Bridge, walishindwa
kuifunga Juventus ya Italia katika pambano la Jumatano usiku.
Nyota wa Chelsea alikuwa ni mchezaji Oscar kutoka Brazil, ambaye alifanikiwa
kutumbukiza magoli mawili kambani katika kipindi cha kwanza; dakika ya 31 na
33.
Bao la pili liliingia kupitia mkwaju wa mbali, na ambalo lilimuacha kipa wa
Juventus, Gianluigi Buffon akiwa amezubaa. Oscar alisajiliwa na Chelsea hivi
majuzi. Hata hivyo Juventus, mabingwa wa Italia, na ambao hawakushindwa katika mechi
42 za Serie A huko nyumbani, walijikakamua na hatimaye kusawazisha na
kujinyakulia pointi moja. Arturo Vidal aliwafungia bao kabla ya kipindi cha kwanza kumalizika, na
baadaye mchezaji wa zamu, Fabio Quagliarella, zikiwa zimesalia dakika tisa mechi
kumalizika, alithibitisha Juventus ilikuwa na nia ya kuondoka na angalau pointi
moja.
Oscar akifunga goli katika mechi dhidi ya Juventus Oscar akimdhibiti mkongwe Andre Pirlo Oscar akitupia Kamba ya pili
Wachezaji wa Juventus wakishangilia goli la kusawazisha Torres akiwa chini ya ulinzi mkali
Kazi kweli kweli ..Lampard amekamwata Kati ya mechi nane za Jumatano, Manchester United pia ilikuwa uwanjani kupambana na Galatasaray, na vijana wa Sir Alex Ferguson wakichezea nyumbani, mechi ya kundi G, walipata ushindi wa bao 1-0. Michael Carrick aliandikisha bao hilo mapema, dakika ya 7.
Klabu hiyo ya Uturuki itadhaniwa na wengi kwamba ilinyimwa nafasi ya kusawazisha, kwa mwamuzi kuwapa penalti, baada ya Nemanja Vidic kumchezea vibaya Umut Bulup. Picha zikionesha jinsi Carrick alivyomtesa mlinda mlango wa Galatasaray na kutia mpira kambani. Wachezaji wa Man U wakimpongeza Carrick
Crater is 12 miles (19 km) across and covers 102 square miles (264 sq km)
Rises over 2,000 feet above the caldera floor
Home to over 30,000 animals including the rare black rhino
Ngorongoro Crater is the world's largest unbroken caldera. Often referred to as "Africa's Garden of Eden," the crater is home to over 30,000 animals including elephants, lions, cheetahs, wildebeests, buffaloes, and the rare black rhinos. View Wildlife of Ngorongoro Crater to learn more about the wildlife and View Birds of Ngorongoro Crater to discover some of the many species that are found in the area. Ngorongoro Crater was created from a volcano that exploded creating the caldera wilderness haven. The crater is 12 miles (19 km) across and consumes 102 square miles (264 sq km) of wilderness. The rim of the crater rises just over 2,000 feet (610 m) above the caldera floor reaching an elevation of 7,500 feet (2,286 m).
Arsenal imeanza vyema michuano ya ligi ya mabingwa hatua ya makundi baada ya kuichabanga Montpellier kwa magoli 2-1 nyumbani kwao katika dimba la La Mosson.
Wenyeji ndio walikuwa wa kwanza kuzifumania nyavu za wageni kwa bao maridadi la mkwaju wa penati iliyopigwa na Belhanda katika dakika ya 8 ya mchezo.
Watoto wa London,Arsenal "The Gunners" waliibuka kama mbogo aliejeruhiwa na kusawazisha goli katika dakika ya 15 likitupiwa kambani na Lucas Podolski.
Mtanange uliendelea huku kila timu ikisaka bao la ushindi na kuthibitisha hilo karata zilichezeka vizuri upande wa Arsenal na katika dakika ya 17 Gervinho aliwainua vitini mashabiki wa Arsenal kwa kutupia kambani goli la pili.
Mpaka mapumziko ngoma ilinoga kwa Arsenal kuwa mbele kwa kamba 2 kwa 1 ya Montpellier.Kipindi cha pili hakikuwa na mabadiliko ya matokeo ya mchezo huo uliohudhuriwa na mashabiki wapatao 30,000 katika dimba hilo la Montpellier, na mpaka kipyenga cha mwamuzi kinaenda hewani matokeo yalikuwa Montpellier 1-2 Arsenal. Podolski akitupia kambani goli la kusawazisha Podolski akishangilia goli la kwanza Hapa huendi kokote we mirasta!!! Gibbs akijaribu kupiga majaro langoni mwa Montpellier
Gervinho akitupia kambani goli la pili Gervinho akishangilia goli
Vicent Company akijaribu kumzuia Christian Ronaldo asilete maafa
Kamba ya Cristiano Ronaldo katika dakika ya mwisho ya mchezo
iliiwezesha klabu ya Real Madrid kuibangua Manchester City magoli 3-2
walipowakaribisha katika uwanja wao wa Bernabeu nchini Uhispania, mechi ya klabu
bingwa barani Ulaya.
Kipa Joe Hart alikuwa mwiba kwa Real Madrid na aliiwezesha Man City kuendelea vyema bila
kufungana mabao katika mechi ya Jumanne usiku, hadi Edin Dzeko alipowashangaza
wenyeji kwa kupata bao katika kipindi cha pili.
Marcelo alisawazisha, kupitia mpira ambao ulimgusa mchezaji wa City kabla ya
kubadilisha mwendo, lakini City wakafanikiwa kuendelea tena kuongoza baada ya
mkwaju wa free-kick kutoka kwa Aleksandar Kolarov, wakati mpira moja
kwa moja ulielekea hadi wavuni. Kisha Karim Benzema aliweza kusawazisha,
kabla ya Ronaldo kuandikisha bao la tatu na la ushindi katika mechi hiyo, na
matokeo yakawa 3-2.
Kati ya mechi nyingine za klabu bingwa barani Ulaya ilikuwa ni pamoja na
mchezo wa Arsenal, ambayo ilianza kampeni yake ya 15 ya mashindano hayo kwa
kuwashinda wageni katika michuano hiyo, Montpellier ya Ufaransa. Timu ya Arsene Wenger ililemewa ugenini baada ya dakika tisa, wakati nahodha
Thomas Vermaelen aliposababisha penalti,ambayo ilifungwa na Belhanda, lakini
kutokana na magoli mawili ya Arsenal kupatikana kwa haraka katika kipindi cha
kwanza, kutoka kwa Lukas Podolski na Gervinho, hali ya mchezo ilibadilika, na
Arsenal ikapata ushindi wa magoli 2-1. Ushindi huo unamaanisha Arsenal na Schalke ya Ujerumani ndio vilabu ambavyo
vinaongoza katika kundi B. Shughuli pevu...Khedira na Kolarov Yaya Toure akipasua mawimbi huku Essien akimfuatilia kwa karibu zaidi Tevez chini ya ulinzi mkali Edwin Dzeko akishangilia bao la pili Mourinho na Ronaldo wakishangilia goli la tatu na la ushindi lililofungwa na Christiano Ronaldo kwa staili ya kufanana. Ndio mpira kaka "FAIR PLAY" Mancini na Mourinho wakisalimiana kabla ya mpambano kuanza
Ujenzi wa Daraja la Kigamboni ukiendelea, na pichani ni daraja la muda Ujenzi wa Daraja la Kigamboni jijini Dar es Salaam, umeanza kwa kishindo na jana Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli alitembelea eneo hilo na kuwahimiza makandarasi kukamilisha kazi hiyo kwa muda uliopangwa.
Daraja hilo linalojengwa na Serikali kwa kushirikiana na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), linatarajiwa kukamilika katika kipindi cha miaka mitatu huku likigharimu Sh214 bilioni.
Ujenzi wa daraja hilo unafanywa na Kampuni ya China Railways Construction na China Major Bridge Engineering Company, zote za nchini China.
Akizungumza na makandarasi hao, Waziri Magufuli aliwataka waongeze kasi ya ujenzi na kuahidi kwamba Serikali itatoa ushirikiano wa hali na mali ili kukamilisha kazi hiyo.
"Nataka niwahakikishie kwamba Serikali itaendelea kuwa bega kwa bega nanyi. Lakini najua nyie ni wachapa kazi, mnaweza kufanya kazi usiku na mchana na kufanya ujenzi uchukue miezi 30 badala ya 36 ya sasa," alisema Dk Magufuli. Wajomba kazini Waziri wa Ujenzi Dkt John Magufuli sambamba na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam wakiangalia vifaa vya kampuni inayotengeneza daraja linalounganisha Kigamboni na Kurasini.