Friday, September 21, 2012

TBL YAZIKABIDHI SIMBA NA YANGA NDINGA ZAO


Basi walilokabidhiwa mabingwa wa ligi kuu ya Tanzania bara Simba Sports Club.


Basi walilokabidhiwa Dar Young Africans (YANGA)

Thursday, September 20, 2012

CHELSEA YAGAWANA POINTI NA JUVENTUS, MAN U YAIBURUZA GALATASARAY

Oscar akishangilia goli pamoja na wenzake Ramires na David Luiz
 
Mabingwa watetezi wa klabu bingwa barani Ulaya, Chelsea ya Uingereza, wakiwa katika dimba la nyumbani la Stamford Bridge, walishindwa kuifunga Juventus ya Italia katika pambano la Jumatano usiku.

Nyota wa Chelsea alikuwa ni mchezaji Oscar kutoka Brazil, ambaye alifanikiwa kutumbukiza magoli mawili kambani katika kipindi cha kwanza; dakika ya 31 na 33.
Bao la pili liliingia kupitia mkwaju wa mbali, na ambalo lilimuacha kipa wa Juventus, Gianluigi Buffon akiwa amezubaa.
Oscar alisajiliwa na Chelsea hivi majuzi.


Hata hivyo Juventus, mabingwa wa Italia, na ambao hawakushindwa katika mechi 42 za Serie A huko nyumbani, walijikakamua na hatimaye kusawazisha na kujinyakulia pointi moja.

Arturo Vidal aliwafungia bao kabla ya kipindi cha kwanza kumalizika, na baadaye mchezaji wa zamu, Fabio Quagliarella, zikiwa zimesalia dakika tisa mechi kumalizika, alithibitisha Juventus ilikuwa na nia ya kuondoka na angalau pointi moja.


Oscar akifunga goli katika mechi dhidi ya Juventus


Oscar akimdhibiti mkongwe Andre Pirlo


Oscar akitupia Kamba ya pili


Wachezaji wa Juventus wakishangilia goli la kusawazisha


Torres akiwa chini ya ulinzi mkali


Kazi kweli kweli ..Lampard amekamwata

Kati ya mechi nane za Jumatano, Manchester United pia ilikuwa uwanjani kupambana na Galatasaray, na vijana wa Sir Alex Ferguson wakichezea nyumbani, mechi ya kundi G, walipata ushindi wa bao 1-0.
Michael Carrick aliandikisha bao hilo mapema, dakika ya 7.

Klabu hiyo ya Uturuki itadhaniwa na wengi kwamba ilinyimwa nafasi ya kusawazisha, kwa mwamuzi kuwapa penalti, baada ya Nemanja Vidic kumchezea vibaya Umut Bulup.



Picha zikionesha jinsi Carrick alivyomtesa mlinda mlango wa Galatasaray na kutia mpira kambani.

Wachezaji wa Man U wakimpongeza Carrick

Wednesday, September 19, 2012

NGORONGORO CRATER "AFRICA'S GARDEN OF EDEN"

QUICK FACTS ABOUT NGORONGORO CRATER
  • Largest unbroken caldera in the world
  • Also referred to as "Africa's Garden of Eden"
  • Crater is 12 miles (19 km) across and covers 102 square miles (264 sq km)
  • Rises over 2,000 feet above the caldera floor
  • Home to over 30,000 animals including the rare black rhino


  • Ngorongoro Crater is the world's largest unbroken caldera. Often referred to as "Africa's Garden of Eden," the crater is home to over 30,000 animals including elephants, lions, cheetahs, wildebeests, buffaloes, and the rare black rhinos. View Wildlife of Ngorongoro Crater to learn more about the wildlife and View Birds of Ngorongoro Crater to discover some of the many species that are found in the area.
    Ngorongoro Crater was created from a volcano that exploded creating the caldera wilderness haven. The crater is 12 miles (19 km) across and consumes 102 square miles (264 sq km) of wilderness. The rim of the crater rises just over 2,000 feet (610 m) above the caldera floor reaching an elevation of 7,500 feet (2,286 m).






    OMMY DIMPLES- Baadae


    ARSENAL YAIADHIBU MONTPELLIER

    Arsenal imeanza vyema michuano ya ligi ya mabingwa hatua ya makundi baada ya kuichabanga Montpellier kwa magoli 2-1 nyumbani kwao katika dimba la La Mosson.

    Wenyeji ndio walikuwa wa kwanza kuzifumania nyavu za wageni kwa bao maridadi la mkwaju wa penati iliyopigwa na Belhanda katika dakika ya 8 ya mchezo.
    Watoto wa London,Arsenal "The Gunners" waliibuka kama mbogo aliejeruhiwa na kusawazisha goli katika dakika ya 15 likitupiwa kambani na Lucas Podolski.

    Mtanange uliendelea huku kila timu ikisaka bao la ushindi na kuthibitisha hilo karata zilichezeka vizuri upande wa Arsenal na katika dakika ya 17 Gervinho aliwainua vitini mashabiki wa Arsenal kwa kutupia kambani goli la pili.

    Mpaka mapumziko ngoma ilinoga kwa Arsenal kuwa mbele kwa kamba 2 kwa 1 ya Montpellier.Kipindi cha pili hakikuwa na mabadiliko ya matokeo ya mchezo huo uliohudhuriwa na mashabiki wapatao 30,000 katika dimba hilo la Montpellier, na mpaka kipyenga cha mwamuzi kinaenda hewani matokeo yalikuwa Montpellier 1-2 Arsenal.

    Podolski akitupia kambani goli la kusawazisha



    Podolski akishangilia goli la kwanza

    Hapa huendi kokote we mirasta!!!

    Gibbs akijaribu kupiga majaro langoni mwa Montpellier


    Gervinho akitupia kambani goli la pili

    Gervinho - Montpellier Herault SC v Arsenal FC - UEFA Champions League
    Gervinho akishangilia goli

    Montpellier 1-2 Arsenal

    REAL MADRID YAICHAPA MAN CITY KWA TAABU

    Vicent Company akijaribu kumzuia Christian Ronaldo asilete maafa
     
    Kamba ya  Cristiano Ronaldo katika dakika ya mwisho ya mchezo iliiwezesha klabu ya Real Madrid kuibangua Manchester City magoli 3-2 walipowakaribisha katika uwanja wao wa Bernabeu nchini Uhispania, mechi ya klabu bingwa barani Ulaya.

    Kipa Joe Hart alikuwa mwiba kwa Real Madrid na aliiwezesha Man City kuendelea vyema bila kufungana mabao katika mechi ya Jumanne usiku, hadi Edin Dzeko alipowashangaza wenyeji kwa kupata bao katika kipindi cha pili.

    Marcelo alisawazisha, kupitia mpira ambao ulimgusa mchezaji wa City kabla ya kubadilisha mwendo, lakini City wakafanikiwa kuendelea tena kuongoza baada ya mkwaju wa free-kick kutoka kwa Aleksandar Kolarov, wakati mpira moja kwa moja ulielekea hadi wavuni.
    Kisha Karim Benzema aliweza kusawazisha, kabla ya Ronaldo kuandikisha bao la tatu na la ushindi katika mechi hiyo, na matokeo yakawa 3-2.

    Kati ya mechi nyingine za klabu bingwa barani Ulaya ilikuwa ni pamoja na mchezo wa Arsenal, ambayo ilianza kampeni yake ya 15 ya mashindano hayo kwa kuwashinda wageni katika michuano hiyo, Montpellier ya Ufaransa.

    Timu ya Arsene Wenger ililemewa ugenini baada ya dakika tisa, wakati nahodha Thomas Vermaelen aliposababisha penalti,ambayo ilifungwa na Belhanda, lakini kutokana na magoli mawili ya Arsenal kupatikana kwa haraka katika kipindi cha kwanza, kutoka kwa Lukas Podolski na Gervinho, hali ya mchezo ilibadilika, na Arsenal ikapata ushindi wa magoli 2-1.

    Ushindi huo unamaanisha Arsenal na Schalke ya Ujerumani ndio vilabu ambavyo vinaongoza katika kundi B.

    Shughuli pevu...Khedira na Kolarov

    Yaya Toure akipasua mawimbi huku Essien akimfuatilia kwa karibu zaidi


    Tevez chini ya ulinzi mkali


    Edwin Dzeko akishangilia bao la pili



    Mourinho na Ronaldo wakishangilia goli la tatu na la ushindi lililofungwa na Christiano Ronaldo kwa staili ya kufanana.


    Ndio mpira kaka "FAIR PLAY" Mancini na Mourinho wakisalimiana kabla ya mpambano kuanza

    REAL MADRID 3-2 MAN CITY

    Tuesday, September 18, 2012

    DARAJA LA KIGAMBONI KAZI IMEANZA





















    Ujenzi wa Daraja la Kigamboni ukiendelea, na pichani ni daraja la muda

    Ujenzi wa Daraja la Kigamboni jijini Dar es Salaam, umeanza kwa kishindo na jana Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli alitembelea eneo hilo na kuwahimiza makandarasi kukamilisha kazi hiyo kwa muda uliopangwa.

    Daraja hilo linalojengwa na Serikali kwa kushirikiana na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), linatarajiwa kukamilika katika kipindi cha miaka mitatu huku likigharimu Sh214 bilioni.

    Ujenzi wa daraja hilo unafanywa na Kampuni ya China Railways Construction na China Major Bridge Engineering Company, zote za nchini China.

    Akizungumza na makandarasi hao, Waziri Magufuli aliwataka waongeze kasi ya ujenzi na kuahidi kwamba Serikali itatoa ushirikiano wa hali na mali ili kukamilisha kazi hiyo.

    "Nataka niwahakikishie kwamba Serikali itaendelea kuwa bega kwa bega nanyi. Lakini najua nyie ni wachapa kazi, mnaweza kufanya kazi usiku na mchana na kufanya ujenzi uchukue miezi 30 badala ya 36 ya sasa," alisema Dk Magufuli.


    Wajomba kazini




    Waziri wa Ujenzi Dkt John Magufuli sambamba na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam wakiangalia vifaa vya kampuni inayotengeneza daraja linalounganisha Kigamboni na Kurasini.