Monday, January 21, 2013

SIMBA YATAKATA OMAN YAIBANJUA AHLI-SIDAB,NYOSSO APATA TIMU OMAN

Mabingwa wa soka Tanzania bara, Simba s.c "wekundu wa msimbazi" wamepata ushindi wao wa kwanza nchini Oman baada ya kuiadabisha Ahli Sidab kwa mabao 2-1 katika mchezo wa kirafiki uliochezwa Oman ambako Simba wamepiga kambi kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Tanzania bara.

Viungo Kigi Makassy na Amri Kihemba walikuwa mashujaa kwa upande wa Simba baada ya kutupia kambani mabao katika kila kipindi cha mchezo huu.
Makassy alitupia kambani bao la kwanza dakika 21 kabla ya kutolewa nje baada ya kuumia na nafasi yake kuchukuliwa na Amri Kiemba ambaye aliingia na kutupia kambani bao la pili na la ushindi katika dakika ya 68.

Wakati huohuo, baada ya kumrudisha kundini beki Juma Nyosso wiki iliyopita, uongozi wa Simba sasa upo mbioni kumuuza beki Juma Nyoso nchini Oman.
Simba kwa sasa ipo kambini Oman na viongozi wake wapo kwenye mazungumzo na wakala Said Ally aliyeonyesha nia ya kumtafutia timu Nyoso.

Nimeshazungumza na Simba na kila kitu kinaenda sawa, tukifikia mwafaka nitaweka wazi ni timu gani atachezea na kiasi ambacho atauzwa, alisema wakala huyo.

Simba wiki iliyopita walimaliza tofauti zao na Nyoso aliyedaiwa kushuka kiwango na kumlazimisha kuchezea timu B, jambo lililopingwa vikali na beki huyo.


Juma Nyosso

MATOKEO KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA 2013

Kombe la Mataifa ya Afrika |MATOKEO


20 January
Mali1 - 0Niger
S Keita (83)
Nelson Mandela Bay Stadium Attendance (20000)
20 January
Ghana2 - 2Congo DR
E Agyemang-Badu (39)
K Asamoah (48)
TM Mputu (52)
D Mbokani (pen 68)
Nelson Mandela Bay Stadium Attendance (7000)
19 January
Angola0 - 0  Morocco
National Stadium Attendance (25000)
19 January
South Africa 0 - 0  Cape Verde Islands
National Stadium Attendance (50000)

TOTTENHAM YAIDAI MAN U "CHENJI" DAKIKA YA 90

Washikilia usukani wa ligi kuu ya England, Manchester United imeambulia pointi moja baada ya kutoka sare ya bao 1-1 na Tottenham.

Mshambuliaji Robin Van Persie aliiwezesha timu yake ya Manchester United kuongoza kipindi cha kwanza baada ya kufunga bao katika dakika ya 25.

Van Persie alipata goli hilo akiunganisha kwa kichwa krosi ya Tom Cleverly baada ya Welbeck kufanya kazi nzuri.

Man United wakiamini kuwa tayari wamepata ushindi katika mechi hiyo,Tottenham waliendelea kudai Chenji kwa kulisakama lango la Man United na  katika dakika ya 90 ya mtanange huo Climp Dempsey aliwanyanyua mashabiki wa Tottenham waliofurika katika dimba la White Hart Lane.Mpambano huo ulishuhudiwa na mashabiki wapatao 35,956

Matokeo hayo bado yanaiacha Manchester United kuendelea kushika usukani wa ligi hiyo ikiwa na pointi 56, huku ikifuatiwa na Manchester City yenye pointi 51.

Tottenham iko katika nafasi ya nne ikiwa na pointi 41, pointi nne nyuma ya Chelsea yenye pointi 45, ikikakalia nafasi ya tatu ya ligi kuu ya England.

Timu zote nne mpaka sasa zimeshacheza mechi 23.

Van Persie akipiga kichwa kilichoelekea moja kwa moja wavuni

Robin Van Persie akishangilia goli

Mshikemshike



Dempsey akishangilia goli baada ya kubadili matokeo katika dakika ya 90
Tottenham 1-1 Man U

ARSENAL YAZAMA DARAJANI

Chelsea imeweza kupata pointi tatu muhimu katika kinyang'anyiro cha ligi kuu ya Soka England baada ya kuipasua Arsenal magoli 2-1 katika uwanja wa Stanford Bridge.

Juan Mata alitupia bao la kwanza la Chelsea kabla ya Frank Lampard kuhitimisha machungu ya mashabiki wa Arsenal kwa kufunga bao la pili kupitia mkwaju wa penalti.

Hata hivyo Arsenal kupitia kwa mshambuliaji wake Theo Walcott aliweza kufunga bao zuri, akiwazidi maarifa walinzi wa Chelsea pamoja na mlinda mlango mahiri Peter Cech.

Kipindi cha Arsenal ilizidi kuibana Chelsea ambapo ilipata kona tisa dhidi ya tatu za Chelsea. Hata hivyo mechi hiyo ilimalizika kwa Chelsea kuibuka na ushindi huo wa magoli mawili kwa moja.

Huu ni ushindi wa kwanza kwa Chelsea katika uwanja wake mwaka huu 2013 kati ya mechi nne ilizocheza uwanjani hapo Stanford Bridge.

Wachezaji wa Chelsea wakishangilia goli la kwanza

Torres akijaribu kuwatoka mabeki wa Arsenal

Lampard akipiga penati kuandika bao la pili

Walcott akitupia kambani goli la Arsenal

Walcott akishangilia goli na mchezaji mwenzake Jack Wilshere
Chelsea 2-1 Arsenal

Friday, January 18, 2013

VIWANJA VITAKAVYOWAKUTANISHA WABABE WA SOKA KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA


NATIONAL STADIUM
National Stadium

 
FACTS
Uwanja: National Stadium
Jiji: Johannesburg
Umejengwa: 1987
Matengenezo: Major upgrade
Umemalizika: 2009
Watazamaji: 94 700



MOSES MABHIDA STADIUM

Moses Mabhiba Stadium


FACTS
Jina: Moses Mabhida Stadium
Jiji: Durban
Matengenezo: Mpya
Umemalizika: 2009
Watazamaji: 70, 000 (wamepunguzwa mpaka 54, 000)



NELSON MANDELA BAY

Nelson Mandela Bay Stadium

Nelson Mandela Bay Stadium
Jina: Port Elizabeth
Jiji: Nelson Mandela Bay/Port Elizabeth
Matengenezo: mpya
Kumalizika:
2009
Watazamaji: 48, 000

MBOMBELA STADIUM

Mbombela Stadium


Jina: Mbombela
Jiji: Nelspruit
Matengenezo: mpya
Umemalizika: 2009
Watazamaji: 46, 000 (wamepunguzwa mpaka 41, 000)

ROYAL BAFOKENG STADIUM

Royal Bafokeng Stadium

Royal Bafokeng
Jina: Royal Bafokeng
Jiji: Rustenburg
Umejengwa: 1999
Matengenezo: marekebisho madogo
Umemalizika: 2010
Watazamaji: 42, 000

RATIBA KAMILI KOMBE LA MATAIFA YA AFRICA (AFCON 2013)

KOMBE LA MATAIFA YA AFRICA | RATIBA


Majira yote CAT (TZ, GMT+3)

Saturday 19 January 2013
1 South Africa v Cape Verde Islands National Stadium 19:00
2 Angola v Morocco National Stadium 22:00

Sunday 20 January 2013
3 Ghana v Congo DR Nelson Mandela Bay Stadium 18:00
4 Mali v Niger Nelson Mandela Bay Stadium 21:00

Monday 21 January 2013
5 Zambia v Ethiopia Mbombela Stadium 18:00
6 Nigeria v Burkina Faso Mbombela Stadium 21:00

Tuesday 22 January 2013
7 Ivory Coast v Togo Royal Bafokeng Stadium 18:00
8 Tunisia v Algeria Royal Bafokeng Stadium 21:00

Wednesday 23 January 2013
9 South Africa v Angola Moses Mabhida Stadium 18:00
10 Morocco v Cape Verde Islands Moses Mabhida Stadium 21:00

Thursday 24 January 2013
11 Ghana v Mali Nelson Mandela Bay Stadium 18:00
12 Niger v Congo DR Nelson Mandela Bay Stadium 21:00

Friday 25 January 2013
13 Zambia v Nigeria Mbombela Stadium 18:00
14 Burkina Faso v Ethiopia Mbombela Stadium 21:00

Saturday 26 January 2013
15 Ivory Coast v Tunisia Royal Bafokeng Stadium 18:00
16 Algeria v Togo Royal Bafokeng Stadium 21:00

Sunday 27 January 2013
17 Morocco v South Africa Moses Mabhida Stadium 20:00
18 Cape Verde Islands v Angola Nelson Mandela Bay Stadium 20:00

Monday 28 January 2013
20 Congo DR v Mali Moses Mabhida Stadium 20:00
19 Niger v Ghana Nelson Mandela Bay Stadium 20:00

Tuesday 29 January 2013
22 Ethiopia v Nigeria Royal Bafokeng Stadium 20:00
21 Burkina Faso v Zambia Mbombela Stadium 20:00

Wednesday 30 January 2013
23 Algeria v Ivory Coast Royal Bafokeng Stadium 20:00
24 Togo v Tunisia Mbombela Stadium 20:00

Saturday 02 February 2013
26 Winner Group B v Runner-up Gp A Nelson Mandela Bay Stadium 18:00
25 Winner Group A v Runner-up Gp B Moses Mabhida Stadium 21:30

Sunday 03 February 2013
28 Winner Group D v Runner-up Gp C Royal Bafokeng Stadium 18:00
27 Winner Group C v Runner-up Gp D Mbombela Stadium 21:30

Wednesday 06 February 2013
30 Winner Q/F 3 v Winner Q/F 2 Mbombela Stadium 18:00
29 Winner Q/F 1 v Winner Q/F 4 Moses Mabhida Stadium 21:30

Saturday 09 February 2013
31 Loser SF1 v Loser SF2 Nelson Mandela Bay Stadium 21:00

Sunday 10 February 2013
32 Winner SF1 v Winner SF2 National Stadium 21:00

Thursday, January 17, 2013

MAN U,ARSENAL ZATAKATA KOMBE LA FA

Vigogo wa ligi kuu ya Uingereza Man United na Arsenal jana zimefanikiwa kupenya raundi ya nne ya Kombe la FA baada ya kupata ushindi katika mechi zao za jana Arsenal ikiizabua timu iliyoonesha upinzani mzuri kuanzia mechi ya awali ya Swansea kwa goli 1-0 huku wenzao Man United wakiichabanga Westham kwa bao 1-0.

Arsenal waliizabua Swansea kwa bao 1-0 katika dimba lao la Emirates mpambano ukishuhudiwa na watazamaji wapatao 58,359. Umati huo ulishuhudia mpambano mkali ambao ulitawaliwa zaidi na timu ya Arsenal huku wakikosa magoli mengi katika mpambano huo. Baada ya kosakosa nyingi katika dakika ya 85 wakati jua likielekea magharibi ya roho sio mwingine bali ni kipenzi cha waingereza Jack Wilshere aliewainua vitini mashabiki wa Arsenal kwa kutupia kambani goli pekee na la ushindi kwa mkwaju mkali uliomshinda Vorm mlinda mlango wa Swansea.
Mpaka mwamuzi wa mchezo huo Clattenburg anapuliza kipyenga cha mwisho matokeo yalikuwa Arsenal 1-0 Swansea. Kwa matokeo hayo Arsenal wameitupa nje ya kombe la FA timu ngumu ya Swansea na kupenya raundi ya nne.

Wilshere akifumua nduki iliyotinga moja kwa moja kambani kuandika bao la Arsenal


Wilshere akilipuka kwa furaha baada ya kufunga goli dhidi ya Swansea

Patashika langoni mwa Swansea

Vikosi vilikuwa;

Arsenal

  • 01 Szczesny
  • 03 Sagna
  • 04 Mertesacker
  • 05 Vermaelen
  • 28 Gibbs
  • 02 Diaby (Ramsey - 82' )
  • 10 Wilshere
  • 14 Walcott
  • 19 Cazorla
  • 22 Coquelin
  • 12 Giroud

Substitutes

  • 24 Mannone
  • 11 Santos
  • 25 Jenkinson
  • 15 Oxlade-Chamberlain
  • 16 Ramsey
  • 23 Arshavin
  • 09 Podolski

Swansea City

  • 01 Vorm
  • 02 Bartley
  • 04 Chico
  • 21 Tiendalli
  • 07 Britton
  • 12 Dyer
  • 15 Routledge
  • 20 De Guzman (Ki Sung-Yeung - 60' )
  • 26 Agustien (Pablo - 59' )
  • 29 Richards
  • 10 Graham (Michu - 71' )

Substitutes

  • 25 Tremmel
  • 16 Monk
  • 33 Davies
  • 09 Michu
  • 11 Pablo
  • 24 Ki Sung-Yeung
  • 17 Shechter

Man United nao walifanikiwa kuivurumisha nje ya kombe la FA timu ya Westham baada ya kuibanjua kwa goli 1-0 katika dimba la Old Trafford huku mtanange huo ukihudhuriwa na mashabiki wapatao 71,081.  Alikuwa ni Wayne Rooney akiripoti rasmi baada ya kuwa nje ya dimba kwa wiki nne alipotupia kamabni bao la pekee na la ushindi katika dakika ya 8 tu ya mchezo baada ya kupata pande murua kutoka kwa Chicharito.


Rooney akifunga goli dhidi ya Westham

Rooney akipiga penati ambayo iliota mbawa

Carrick akijaribu kuwatoka mabeki wa Westham

Manchester United

  • 13 Lindegaard
  • 02 Rafael
  • 04 Jones
  • 12 Smalling
  • 28 Buttner
  • 07 Valencia
  • 08 Anderson (Carrick - 67' )
  • 11 Giggs
  • 17 Nani (Scholes - 77' Booked )
  • 10 Rooney
  • 14 Hernandez

Substitutes

  • 40 Amos
  • 05 Ferdinand
  • 16 Carrick
  • 22 Scholes
  • 26 Kagawa
  • 19 Welbeck
  • 20 Van Persie

West Ham United

  • 22 Jaaskelainen
  • 02 Reid
  • 05 Tomkins
  • 27 Spence Booked
  • 33 Potts
  • 14 Taylor
  • 21 Diame (Collison - 65' )
  • 23 Diarra
  • 32 O'Neil
  • 09 Cole (Nolan - 65' Booked )
  • 12 Vaz Te (Lee - 78' )

Substitutes

  • 30 Spiegel
  • 20 Demel
  • 04 Nolan
  • 07 Jarvis
  • 10 Collison
  • 43 Lletget
  • 47 Lee
ARSENAL 1-0 SWANSEA

MAN U 1-0 WESTHAM U