Friday, June 17, 2011
NG'OMBE ALIYEKATA KAMBA AZUA KIZAAZAA MTAANI.
Ng'ombe aliyekuwa amefungwa katika nyumba moja nchini Sri lanka , haijulikani ni kwasababu alikuwa na njaa au alikuwa na hasira gani ghafla alikata kamba na kuanza kukimbia mitaani na kusababisha taharuki kwa wapita njia kama inavyoonekana pichani. Haikuweza kufahamika mara moja kama baada ya tukio hilo huyo ng'ombe alikamatwa vipi na je kuna mtu aliyejeruhiwa au kuuwawa.
VITU 10 KWA MWANAMKE VINAVYOMPENDEZA MWANAUME.
Katika historia ya mwanadamu tunaelezwa kuwa mungu baada ya kuumba kila kitu duniani aliamua na kuumba mtu wa kuvitawala vitu hivyo,ndipo akamuumba Adam na baadaye akaona sio vyema Adamu awe peke yake akaamua kumuumba mwenza wake ndipo akamuumba Hawa. Hivyo Adam akiwa ni jinsia ya kiume na Hawa ni jinsia ya kike ,akawaambia wautawale na kuujaza ulimwengu.Wataujazaje ulimwengu? ni kupitia kujamiiana na hatimae wazae watoto nao waje wazaane na kuujaza ulimwengu.
Kutokana na hilo Duniani watuy tumekuwa tukipendana na kila mmoja na vigezo vyake binafsi katika kupenda lakini leo nina vitu ambavyo wanaume wengi huvipenda kwa mwanamke,kama ifuatavyo;
1} UZURI WA ASILI, hivi unajua kama wanawake Marekani wanatumia dola 200 za marekani kwa ajili ya vipodozi? lakini mwisho wa siku wanaume wamekuwa na mapenzi na wanawake wenye uzuri wa asili,wanapenda ngozi safi na ya asili. wengi wanasema wanapenda kumuona mwanamke katika muonekano uleule muda wote iwe anatoka kulala, au kuoga na hata akiwa kazini sura yake na muonekano unakuwa ni wa asili.
2} MUONEKANO WA TUMBO, Wanaume wengi hupenda tumbo la mwanamke ambalo lipo katika mkao mzuri linaonekana kuendana na mwili wa mwanamke."Napenda tumbo lake" anasema Derke mwenye miaka 30, "Ni la duara" aliendelea, napenda anavyolimaintain na ni laini.
3} UCHANGAMFU, Wanaume wengi wanapenda wanawake wachangamfu,wenye matendo ya kuwafurahisha wanapokuwa wawili,ubunifu wa mambo fulanifulani humfanya mwanaume kuvutiwa na mpenzi wake wawapo wawili ikiwa ni pamoja na wakati wa tendo la ndoa au wanapokuwa wanapunga upepo au wamepumzika. "mke wangu anaimba nje ya key kabisa"anasema Ivan,miaka 38. "anapoimba bafuni,inapendeza ingawa sauti inatisha lakini haiachi kunichekesha"aliendelea kusema juu ya mpenzi wake. Vilevile kucheza wakati mnaposikiliza muziki ni njia mojawapo ambacho mwanaume atapenda amuone mpenzi wake akijaribu kufanya hivyo sio lazima awe anajua sana.
4} NYWELE, Muonekano wa nywele huwavutia sana wanaume,pale ambapo mwanamke anatunza nywele zake na kuwa na muonekano mzuri iwe ni za asili au zilizowekwa dawa au za bandia ili mradi ziendane na jinsi alivyo ambapo zitamfanya apendeze. "Mke wangu ana nywele ndefu sana akiingia bafuni inamchukua masaa mawili kila siku kwa ajili ya nywele tu,ni kitu kizuri" anasema Steve miaka 30.
5} KOPE, "Napenda macho yake"anasema Trevor miaka 46. "wakati mwingine anaponiangalia nikimtazama macho na jinsi kope zilivyo huwa vinanifanya nitamani tuende kitandani moja kwa moja" aliongezea. "macho yake ni moja ya vitu vinavyonivutia kwake,yananifanya niwe na hisia za moja kwa moja kwake"alimalizia.
"Mpenzi wake ana kope za ajabu,ningependa niwe na msichana kama yeye" alisema Vik miaka 26 rafiki yake Seth.
6} MIGUU, Miguu ya mwanamke haijalishi mnene, mwembamba,mfupi au mrefu ili mradi iwe na mwonekano mzuri, "Miguu yake ni laini,napenda vile inavosisimua na wakati anapovaa viatu virefu hakika hunitia wazimu" alisema James 26,alipomuongelea mpenzi wake Sarah.
"mimi binafsi ni mzaifu nionapo miguu,hivyo anapoipitisha katikati yangu huwa siwezi kujizuia,nae anafahamu hilo" alisema David 43. "Napenda miguu ya mwanamke lakini sijui kwanini,miguu ya wanawake ni ya kifahari ambayo sisi hatuna,ninapenda kitu tofauti ndio maana kwanini napenda matiti kwasababu mimi sina" alisema Nate 32.
7} STAILI YAKO, Wanaume huvutiwa na vile mwanamke anavyojua kupangilia viwalo,jinsi ya kujua ni ni cha kuvaa na kwa wakati gani hakika huwavutia wanaume hasa pale mwanamke anapotoka bomba. Lazima ujue ukivaa nini inakufit na kukutoa chicha,pia ujue jinsi ya kupangilia vitu yaani kuanzia viatu,nguo,mikoba,hereni,bangili na hata cheni.
8} MANUKATO, "Sifahamu anawezaje,lakini muda wote ananukia vizuri" alisema Brent 29."Hata kama anatoka kuoga" alisema. "Napenda kumnusa maeneo haya",anasema Damien 35 huku akionesha sehemu za shingoni kwa mpenzi wake. Kuna wanaume wengine wanadiriki kusema huwa hawafikirii mwanamke atavaa nini zaidi ya kufikiria jinsi atakavyonukia.
9} KUSEMA UNACHOTAKA, Katika mapenzi kila mtu ana uhuru wa kusema ni nini anataka mpenzi wake amfanyie na kipi asifanye,ingawaje wanawake wengi hawalifahamu hili kwani imefikia wanachagua vitu vya kuomba na vingine kuona sio haki yao,mfano tendo la ndoa wanawake wengi husubiri mpaka mwanaume aanze kusema yeye kimya. pia wakati wa tendo miguno ya mwanamke na maelekezo ya wapi pa ku kita na wapi pa kupekecha mwanamke anaposema mwanaume hufurahia tendo na kumfanya kumpenda zaidi mwanamke.
10} KAZI YAKO, Mwanamke anaewajibika humvutia mwanaume. wanaume wengi wanasema wanapenda kuwaona wanawake wao wakiwa sehemu zao za kazi wakiwajibika." Anafanya kazi katika shule ya awali,napenda ninapomuona akifundisha na kucheza na watoto" anasema Garisson 42. "mke wangu ni Profesa wa masuala ya wanawake,napenda kumuona akifundisha wanawake wenzake kupata kazi na kupigania haki zao"anasema Samuel 49.
Kutokana na hilo Duniani watuy tumekuwa tukipendana na kila mmoja na vigezo vyake binafsi katika kupenda lakini leo nina vitu ambavyo wanaume wengi huvipenda kwa mwanamke,kama ifuatavyo;
1} UZURI WA ASILI, hivi unajua kama wanawake Marekani wanatumia dola 200 za marekani kwa ajili ya vipodozi? lakini mwisho wa siku wanaume wamekuwa na mapenzi na wanawake wenye uzuri wa asili,wanapenda ngozi safi na ya asili. wengi wanasema wanapenda kumuona mwanamke katika muonekano uleule muda wote iwe anatoka kulala, au kuoga na hata akiwa kazini sura yake na muonekano unakuwa ni wa asili.
2} MUONEKANO WA TUMBO, Wanaume wengi hupenda tumbo la mwanamke ambalo lipo katika mkao mzuri linaonekana kuendana na mwili wa mwanamke."Napenda tumbo lake" anasema Derke mwenye miaka 30, "Ni la duara" aliendelea, napenda anavyolimaintain na ni laini.
3} UCHANGAMFU, Wanaume wengi wanapenda wanawake wachangamfu,wenye matendo ya kuwafurahisha wanapokuwa wawili,ubunifu wa mambo fulanifulani humfanya mwanaume kuvutiwa na mpenzi wake wawapo wawili ikiwa ni pamoja na wakati wa tendo la ndoa au wanapokuwa wanapunga upepo au wamepumzika. "mke wangu anaimba nje ya key kabisa"anasema Ivan,miaka 38. "anapoimba bafuni,inapendeza ingawa sauti inatisha lakini haiachi kunichekesha"aliendelea kusema juu ya mpenzi wake. Vilevile kucheza wakati mnaposikiliza muziki ni njia mojawapo ambacho mwanaume atapenda amuone mpenzi wake akijaribu kufanya hivyo sio lazima awe anajua sana.
4} NYWELE, Muonekano wa nywele huwavutia sana wanaume,pale ambapo mwanamke anatunza nywele zake na kuwa na muonekano mzuri iwe ni za asili au zilizowekwa dawa au za bandia ili mradi ziendane na jinsi alivyo ambapo zitamfanya apendeze. "Mke wangu ana nywele ndefu sana akiingia bafuni inamchukua masaa mawili kila siku kwa ajili ya nywele tu,ni kitu kizuri" anasema Steve miaka 30.
5} KOPE, "Napenda macho yake"anasema Trevor miaka 46. "wakati mwingine anaponiangalia nikimtazama macho na jinsi kope zilivyo huwa vinanifanya nitamani tuende kitandani moja kwa moja" aliongezea. "macho yake ni moja ya vitu vinavyonivutia kwake,yananifanya niwe na hisia za moja kwa moja kwake"alimalizia.
"Mpenzi wake ana kope za ajabu,ningependa niwe na msichana kama yeye" alisema Vik miaka 26 rafiki yake Seth.
6} MIGUU, Miguu ya mwanamke haijalishi mnene, mwembamba,mfupi au mrefu ili mradi iwe na mwonekano mzuri, "Miguu yake ni laini,napenda vile inavosisimua na wakati anapovaa viatu virefu hakika hunitia wazimu" alisema James 26,alipomuongelea mpenzi wake Sarah.
"mimi binafsi ni mzaifu nionapo miguu,hivyo anapoipitisha katikati yangu huwa siwezi kujizuia,nae anafahamu hilo" alisema David 43. "Napenda miguu ya mwanamke lakini sijui kwanini,miguu ya wanawake ni ya kifahari ambayo sisi hatuna,ninapenda kitu tofauti ndio maana kwanini napenda matiti kwasababu mimi sina" alisema Nate 32.
7} STAILI YAKO, Wanaume huvutiwa na vile mwanamke anavyojua kupangilia viwalo,jinsi ya kujua ni ni cha kuvaa na kwa wakati gani hakika huwavutia wanaume hasa pale mwanamke anapotoka bomba. Lazima ujue ukivaa nini inakufit na kukutoa chicha,pia ujue jinsi ya kupangilia vitu yaani kuanzia viatu,nguo,mikoba,hereni,bangili na hata cheni.
8} MANUKATO, "Sifahamu anawezaje,lakini muda wote ananukia vizuri" alisema Brent 29."Hata kama anatoka kuoga" alisema. "Napenda kumnusa maeneo haya",anasema Damien 35 huku akionesha sehemu za shingoni kwa mpenzi wake. Kuna wanaume wengine wanadiriki kusema huwa hawafikirii mwanamke atavaa nini zaidi ya kufikiria jinsi atakavyonukia.
9} KUSEMA UNACHOTAKA, Katika mapenzi kila mtu ana uhuru wa kusema ni nini anataka mpenzi wake amfanyie na kipi asifanye,ingawaje wanawake wengi hawalifahamu hili kwani imefikia wanachagua vitu vya kuomba na vingine kuona sio haki yao,mfano tendo la ndoa wanawake wengi husubiri mpaka mwanaume aanze kusema yeye kimya. pia wakati wa tendo miguno ya mwanamke na maelekezo ya wapi pa ku kita na wapi pa kupekecha mwanamke anaposema mwanaume hufurahia tendo na kumfanya kumpenda zaidi mwanamke.
10} KAZI YAKO, Mwanamke anaewajibika humvutia mwanaume. wanaume wengi wanasema wanapenda kuwaona wanawake wao wakiwa sehemu zao za kazi wakiwajibika." Anafanya kazi katika shule ya awali,napenda ninapomuona akifundisha na kucheza na watoto" anasema Garisson 42. "mke wangu ni Profesa wa masuala ya wanawake,napenda kumuona akifundisha wanawake wenzake kupata kazi na kupigania haki zao"anasema Samuel 49.
ASHUSHWA KWENYE NDEGE KWA KUVAA MLEGEZO.
Marman
"Siku ya jumatano muda wa saa tatu asubuhi polisi wa San Francisco walipokea simu kuwa nje ya geti la shirika la ndege la marekani kuna mtu amevaa hovyohovyo" alisema Sgt Michael Rodriguez. Wafanyakazi wa uwanja wa ndege walimuona kabla Marman hajapanda ndege 488,walipomuona amevaa suruali chini ya matako lakini juu ya magoti walimtaka kupandisha suruali yake lakini Marman alikaidi amri hiyo na kuendelea na safari ya kuingia ndani ya ndege,ndipo wafanyakazi hao walipoamua kupiga simu polisi na polisi walipofika uwanjani hapo walimkuta Marman ameshaingia ndani ya ndege na amekaa raha mustarehe. Askari walipomuamuru kushuka aliwajibu itanichukua dakika 15 mpaka 20 kushuka ndipo askari walipomkamata kwa kosa hilo,na kuachiwa siku ya alhamisi kwa dhamana ya dola 11,000 za kimarekani.
Mama wa Marman alipohojiwa alisema mwanae alikuwa na hali mbaya kihisia kwani alitoka kuhudhuria mazishi ya rafiki yake ambaye ni mwanafunzi mwenzake siku ya jumanne baada ya kuuwawa. Lakini wamarekani wengi wamejitokeza kulalamikia swala hilo na kusema lina uhusiano na ubaguzi wa rangi kwani Marman alivaa jinsi ambayo ilikuwa haimkeri mtu moja kwa moja.
Thursday, June 16, 2011
SIKU YA MTOTO WA AFRIKA.
Leo ni maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika, Siku hii barani Afrika inaadhimishwa huku kukiwa na changamoto nyingi zinazoikabili jamii nzima ya Afrika kuhusiana na malezi ya watoto. Watoto Afrika wanakabiliwa na changamoto za maisha duni ya jamii kubwa barani Afrika ambapo katika nchi nyingi za kiafrika inaaminika kuwa familia nyingi zinaishi maisha ya taabu ambapo matumizi ya familia kwa siku yanasadikika kuwa ni chini ya dola moja ya kimarekani. Kutokana na jamii kubwa kuwa na maisha ya hali ya chini inapelekea malezi ya watoto nayo kuwa duni,watoto wanakosa haki za msingi kutokana na familia zao ama wazazi kutokuwa na uwezo wa kuwatekelezea haki hizo ambazo ni pamoja na haki ya kusoma, chakula, malazi,michezo na haki nyinginezo.
Siku hadi siku wimbi la watoto wa mitaani limezidi kuongezeka kutokana na ukweli kuwa maisha yanazidi kupanda kadri siku zinavyozidi kwenda na familia nyingi kujikuta kusambaratika kutokana na kutokuwa na uwezo wa kukaa pamoja na kupata mahitaji ya kila siku.
Leo ikiwa ni siku ya mtoto wa Afrika hatuna budi kutafuta mbinu za kukabiliana na matatizo yanayowakabili watoto, tuangalie ni jinsi gani tunaweza kuboresha mazingira yao ya kusomea yaani shule, pia tuweze kuangalia jinsi gani tutawatoa watoto waliopo mitaani ambapo hapa Tanzania inasadikika watoto wa mitaani ni wengi sana hasa katika mikoa ya Dar es salaam, Dodoma,Mbeya,Singida na Kilimanjaro. Viwanja vya kuchezea watoto visimilikiwe na watu kwani kufanya hivyo ni kuwanyima haki yao ya msingi, Kwa pamoja tuwe na wito unapomuona mtoto a mwenzio basi umuone na kumthamini kama mtoto wako wa kumzaa hapo ndio tunaweza kuwalea na kuwatunza katika maadili yaliyo mazuri.
Watoto wana haki ya kucheza.
Watoto wana haki ya kupata elimu.
Siku hadi siku wimbi la watoto wa mitaani limezidi kuongezeka kutokana na ukweli kuwa maisha yanazidi kupanda kadri siku zinavyozidi kwenda na familia nyingi kujikuta kusambaratika kutokana na kutokuwa na uwezo wa kukaa pamoja na kupata mahitaji ya kila siku.
Watoto wana haki ya kupata chakula bora.
Leo ikiwa ni siku ya mtoto wa Afrika hatuna budi kutafuta mbinu za kukabiliana na matatizo yanayowakabili watoto, tuangalie ni jinsi gani tunaweza kuboresha mazingira yao ya kusomea yaani shule, pia tuweze kuangalia jinsi gani tutawatoa watoto waliopo mitaani ambapo hapa Tanzania inasadikika watoto wa mitaani ni wengi sana hasa katika mikoa ya Dar es salaam, Dodoma,Mbeya,Singida na Kilimanjaro. Viwanja vya kuchezea watoto visimilikiwe na watu kwani kufanya hivyo ni kuwanyima haki yao ya msingi, Kwa pamoja tuwe na wito unapomuona mtoto a mwenzio basi umuone na kumthamini kama mtoto wako wa kumzaa hapo ndio tunaweza kuwalea na kuwatunza katika maadili yaliyo mazuri.
Watoto wana haki ya kucheza.
Watoto wana haki ya kulala mahala safi na salama.
BAMBO APATA AJALI YA PIKIPIKI AVUNJIKA MGUU.
Wasanii wakimuangalia Bambo kitandani kwa huzuni.
Dereva wa pikipiki iliyokodiwa na Bambo akiwa hoi hospitalini.
Wednesday, June 15, 2011
UANGALIAJI WA TV HUUMIZA AFYA YAKO.
Wale wanaopenda kukaa na kuangalia Luninga(TV) muda wote ambao kwa kitaalamu tunawaita "Couch Potatoes" mpo katika hatari ya kupata madhara katika afya zenu kwa kutazama luninga kwa masaa mawili au zaidi ambapo utafiti umeonesha kuna hatari ya kupata Type 2 diabetes,Cardiovascular disease na vifo vya mapema kutokana na hayo madhara na inaripotiwa na jarida ya chama cha madawa cha Marekani (J.A.M.A).
Uangaliaji wa luninga unahusishwa na kutokuwa na mpangilio mzuri katika ulaji wa chakula, kuongezeka kwa uzito, athari za kisukari,magonjwa ya moyo na maisha mafupi. Utafiti umeonesha pia kutolala kwa usahihi pia kunasababishwa na uangaliaji wa luninga ambapo kwa kawaida mtu anatakiwa alale masaa saba mpaka nane. Kwa haya yote hatupaswi kulaumu luninga kwani sisi ndio tunaoiwasha na kushika remote na kukaa masaa yote kwenye kochi.Angalia tabia ya kuangalia luninga inavyoweza kuhatarisha afya yako:
1} TYPE 2 DIABETES; zaidi ya wamarekani milioni 26 wana kisukari kwa hili wana hatari kubwa ya kupata magonjwa ya moyo na kiharusi.Type 2 diabetes husababishwa na uzito kupita kiasi,maisha ya sedentary (sedentary lifestyle),mlo usiokamili, Ili kuepukana na hili punguza uzito na fanya mazoezi kwani kunasaidia insulin kufanya kazi ambayo ndio sababu kubwa ya kisukari.
2} CARDIOVASCULAR DISEASE (CVD). Hii inahusisha ugonjwa wa moyo,mapigo ya moyo kwenda mbio(high blood pressure),maumivu ya kifua,kiharusi na moyo kushindwa kufanya kazi. utafiti unaonesha madhara haya huwapata wanaoangalia TV kwa masaa 2 kwa siku, mwanga wa TV unaowaingia watoto unapunguza njia machoni mwao na siku za usoni wanaweza kupatwa na CVD.
Njia ya kujikinga ni kufanya mazoezi kwa nusu saa kwa siku tano au zaidi kwa wiki, kupima blood pressure na cholestrol mara kwa mara.
3}ALL CAUSE MORTALITY. Utafiti wa (J.A.M.A) umeonesha uangaliaji wa TV kwa masaa zaidi ya matatu kwa siku kunapelekea kuwa na mazoea na TV yaani "couch potato" Njia ya kuepuka hili ni ni kama zile za kujikinga na kisukari na CVD.
4}SLEEP DEPRIVATION. Kiafya tunahitaji masaa 7-8 ya kulala kila siku lakini watu wengi hawayapati ipasavyo, utafiti unaonesha uangaliaji wa TV karibu na kitanda ni wa kulaumu. Utafiti umeonesha kuwa mwanga wakati wa usiku ikiwamo wa TV una hatari ya kusababisha kansa ya maziwa kwa wanawake.
Njia ya kuepuka hili,zima TV kwa saa moja kabla ya kwenda kulala kwasababu mwanga wa TV unaupa ubongo uwezo wa kufanya kazi na hivyo kukufanya iwe ngumu kupata usingizi kwa haraka.
5} NEARSIGHTEDNESS IN KIDS. Hii imeathiri watu zaidi ya bilioni 1.6 duniani kote,idadi ni kubwa zaidi katika nchi ambazo watoto wanaangalia TV na kucheza Computer game badala ya kucheza viwanjani yaani nje.Tokyo na Hongkong 30%-50% ya watoto ni myopic(nearsightedness) na 20% U.S.A. Utafiti wa mwaka 2009 umeonesha watoto wenye athari hii ni wale wanaotumia muda wa saa 4-5 kwa wiki katika TV.
Njia ya kujikinga, utumiaji wa saa 2 kwa siku nje hupunguza tatizo hili kwa watoto na tuwashauri kuangalia vitu vilivyo mbali ili kuimarisha uwezo wa macho kuona. michezo ya nje pia huimarisha uzito wa mtoto kulingana na afya yake.
kwa maswali jiffjeff@yahoo.com +255712184598
Uangaliaji wa luninga unahusishwa na kutokuwa na mpangilio mzuri katika ulaji wa chakula, kuongezeka kwa uzito, athari za kisukari,magonjwa ya moyo na maisha mafupi. Utafiti umeonesha pia kutolala kwa usahihi pia kunasababishwa na uangaliaji wa luninga ambapo kwa kawaida mtu anatakiwa alale masaa saba mpaka nane. Kwa haya yote hatupaswi kulaumu luninga kwani sisi ndio tunaoiwasha na kushika remote na kukaa masaa yote kwenye kochi.Angalia tabia ya kuangalia luninga inavyoweza kuhatarisha afya yako:
1} TYPE 2 DIABETES; zaidi ya wamarekani milioni 26 wana kisukari kwa hili wana hatari kubwa ya kupata magonjwa ya moyo na kiharusi.Type 2 diabetes husababishwa na uzito kupita kiasi,maisha ya sedentary (sedentary lifestyle),mlo usiokamili, Ili kuepukana na hili punguza uzito na fanya mazoezi kwani kunasaidia insulin kufanya kazi ambayo ndio sababu kubwa ya kisukari.
2} CARDIOVASCULAR DISEASE (CVD). Hii inahusisha ugonjwa wa moyo,mapigo ya moyo kwenda mbio(high blood pressure),maumivu ya kifua,kiharusi na moyo kushindwa kufanya kazi. utafiti unaonesha madhara haya huwapata wanaoangalia TV kwa masaa 2 kwa siku, mwanga wa TV unaowaingia watoto unapunguza njia machoni mwao na siku za usoni wanaweza kupatwa na CVD.
Njia ya kujikinga ni kufanya mazoezi kwa nusu saa kwa siku tano au zaidi kwa wiki, kupima blood pressure na cholestrol mara kwa mara.
3}ALL CAUSE MORTALITY. Utafiti wa (J.A.M.A) umeonesha uangaliaji wa TV kwa masaa zaidi ya matatu kwa siku kunapelekea kuwa na mazoea na TV yaani "couch potato" Njia ya kuepuka hili ni ni kama zile za kujikinga na kisukari na CVD.
4}SLEEP DEPRIVATION. Kiafya tunahitaji masaa 7-8 ya kulala kila siku lakini watu wengi hawayapati ipasavyo, utafiti unaonesha uangaliaji wa TV karibu na kitanda ni wa kulaumu. Utafiti umeonesha kuwa mwanga wakati wa usiku ikiwamo wa TV una hatari ya kusababisha kansa ya maziwa kwa wanawake.
Njia ya kuepuka hili,zima TV kwa saa moja kabla ya kwenda kulala kwasababu mwanga wa TV unaupa ubongo uwezo wa kufanya kazi na hivyo kukufanya iwe ngumu kupata usingizi kwa haraka.
5} NEARSIGHTEDNESS IN KIDS. Hii imeathiri watu zaidi ya bilioni 1.6 duniani kote,idadi ni kubwa zaidi katika nchi ambazo watoto wanaangalia TV na kucheza Computer game badala ya kucheza viwanjani yaani nje.Tokyo na Hongkong 30%-50% ya watoto ni myopic(nearsightedness) na 20% U.S.A. Utafiti wa mwaka 2009 umeonesha watoto wenye athari hii ni wale wanaotumia muda wa saa 4-5 kwa wiki katika TV.
Njia ya kujikinga, utumiaji wa saa 2 kwa siku nje hupunguza tatizo hili kwa watoto na tuwashauri kuangalia vitu vilivyo mbali ili kuimarisha uwezo wa macho kuona. michezo ya nje pia huimarisha uzito wa mtoto kulingana na afya yake.
kwa maswali jiffjeff@yahoo.com +255712184598
Tuesday, June 14, 2011
Subscribe to:
Posts (Atom)






















