Thursday, August 18, 2011

TAZAMA VIDEO JINSI BARCA ILIVYOICHARAZA REAL MADRID


Iniesta akitia nyavuni bao la kwanza




Messi akitia kwenye kamba goli la pili


Benzema akiisawazishia Real goli la pili


Ronaldo akipachika bao la kwanza kwa Real Madrid


Marcello amchezea vibaya Fabregas



SIMBA YAILIZA YANGA 2 KWA BUYU

Sunzu akishangilia baada ya kutia kambani goli la pili

SIMBA, Simba ndio ulikuwa wimbo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam baada vijana hao wa mtaa wa Msimbazi kulipinza kisasi kwa ukifunga Yanga mabao 2-0 kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii.

Simba waliofungwa kwenye Kombe la Kagame na Ngao ya Jamii mwaka jana vijana hao wa Mganda Moses Basena walizinduka na kupata mabao ya mapema kupitia kiungo Haruna Moshi 'Boban' dakika 15 na penalti ya Felix Sunzu dakika 38.

Simba iliyoanza kwa kasi mchezo huo ilifanikiwa kupata bao la kuongoza kupitia kwa Moshi 'Boban' aliyemalizia vizuri krosi ya kutoka upande wa kushoto iliyopigwa na mshambuliaji wa kimataifa wa Sunzu aliyekuwa na ushirikiano mkubwa na Emmanuel Okwi.

Mshambuliaji Sunzu alifungia Simba bao la pili kwa mkwaju wa penalti baada ya Nadir Haroub kumchezea vibaya Moshi 'Boban', kwenye eneo la hatari dakika 35. Sunzu alilazimika kuonyesha ueledi wake pale alipotakiwa kurudia penalti hiyo baada ya mwamuzi Israel Mjuni kusema Kado alitokea kabla ya kupigwa kwa penalti ya kwanza pamoja na kuwa alikuwa amefunga.

Kocha Moses Basena aliyeonekana kujifunza kwa makosa alitumia mfumo wa 4:2:3:1 na kutoa nafasi kubwa kwa Okwi, Haruna na Sunzu kutawala sehemu kubwa ya kiungo tofauti na ilivyokuwa kwenye fainali ya Kombe la Kagame.

Okwi alifanya atakalo mbele ya mabeki wa Yanga walionekana kuwa kama watu waliozidiwa na mazoezi na kukosa unyumbulifu mchezoni, huku safu ya ulinzi wa Simba chini ya mkongwe Victor Costa aliweza kuwapoteza mchezoni kabisa mshambuliaji Keneth Asamoah na Jerry Tegete.

Kiungo Haruna Niyonzima alijitahidi kuonyesha uwezo mkubwa wa kutawala mpira na kujaribu kutafuta goli kwenye mechi yake ya kwanza ya watani wa jadi, lakini alikosa msahada kutoka kwa wenzake.

Simba ilianza mashambulizi kwa kasi na dakika kwanza Okwi alikosa bao baada ya shuti lake kumgonga Haroub na kupaa juu ya goli.

Okwi alipoteza nafasi nyingine dakika 8 baada ya kuwalamba chenga mabeki wa Yanga, lakini aliugonga mpira mbele zaidi na kipa Shaaban Kado akauwahi.

Beki wa Yanga, Chacha Marwa, nahodha Shadrack Nsajigwa alipewa kadi ya njano kwa kumchezea vibaya Okwi. Naye Juma Nyoso wa Simba alipewa kadi ya njano kwa kumchezea vibaya Asamoah.

Haruna Niyonzima alipiga shuti la umbali wa mita 25 baada ya kumchungulia Juma Kaseja kwa bahati mpira huo ulipaa juu ya goli.

Kipindi cha pili Yanga iliamka baada ya kuingia Hamisi Kiiza na Rashid Gumbo lakini walishindwa kuipenya ngome ya Simba.

Yanga waliendeleza sera yao ya kugomea jezi za wadhamini wa ligi Vodacom zenye nembo nyekundu kwa kuvaaa jezi za mdhamini wao TBL tofauti na Simba wenyewe walivaa zile walizopewa na Vodacom

Vikosi Yanga;
Shaaban Kado, Shadrack Nsajigwa, Oscar Joshua, Nadir Haroub, Chacha Marwa, Juma Seif, Godfey Taita, Haruna Niyonzima, Keneth Asamoah/ Gumbo, Jerry Tegete, Kigi Makasi/ Kiiza.
Simba: Juma Kaseja, Said Nasoro, Amir Maftah, Juma Nyoso, Victor Costa, Partick Mafisango, Salum Machaku/ Kiemba, Jerry Santo, Felix Sunzu, Haruna Moshi/ Gervais Kago, Emmanuel Okwi/ Kapombe

UFISADI INDIA MARUFUKU WANANCHI WAANDAMANA

Maelfu ya raia India wamejitokeza mitaani kumunga mkono mwanaharakati wa kupinga ufisadi Anna Hazare.
manmohan singh na anna hazare
Maelfu ya watu nchini India wamekerwa na viwango vya ufisadi
Awali wafuasi wa Bw Hazare walikusanyika nje ya jela mmoja mjini Delhi ambako amekuwa akizuiliwa tangu jumanne.
Bw Hazare amegoma kuondoka katika jela hilo hadi serikali ya India itakapo mruhusu kutekeleza mpango wake kususia kula chakula hadharani.
Mwanaharakati huyo anahurumiwa na wengi nchini India na tayari maandamano ya kumuunga mkono yanazidi kuvutia idadi kubwa ya watu kote nchini humo.
Bw Hazare anashinikiza kufanyika kwa mageuzi katika sheria za kupambana na rushwa na alikuwa amepanga kuanza kukesha bila chakula ili kushinikiza hilo lifanyike.
Watu wengi wanaomuunga mkono wamejitokeza na mabango huku wakikemea serikali wakitaka aachiwe huru.
Raia hao wa India wanasema lazima serikali ichukue hatua za kukabili ufisadi uliokithiri nchini humo.
Hata hivyo waziri mkuu wa India Manmohan Singh amemkosoa mwanaharakati huyo akisema, ingawa nia yake ni nzuri anatumia dhana potufu kulazimisha bunge lifuate matakwa yake.
Mshirika wa karibu wa Bw Hazare amesema kuwa sasa amekubali kuondoka jela baada ya polisi kuridhia kuwa anaweza kufanya mgomo huo wa kususia chakula kwa siku kumi na tano kwenye bustani mmoja mjini Delhi.
Bw Hazare na wafuasi wake 1,200 walitiwa nguvuni na polisi wakiwa kwenye bustani ya JP park saa chache kabla waanza kusisia chakula.
Mwezi April, Bw Hazare alivunja mgomo wake wa kususia chakula baada ya siku nne pale serikali ilikubali kuwa anaweza kuhusika kuandaa mswada wa kupambana na ufisadi nchini humo ambapo kutakuwa ofisi maalum ya kuchunguza wanasiasa na watumishi wa serikali wanashukiwa kuhusika na ufisadi.
Mwanaharakati huyo mwenye miaka 74, hata hivyo anapinga mswada uliowasilishwa bungeni kwa kuwa waziri mkuu na majaji hawata chunguzwa.

Wednesday, August 17, 2011

Man City to Complete Deal Worth £57.3m to Sign Arsenal Star Samir Nasri Within 48 Hours



Samir Nasri has confirmed he is close to following Cesc Fabregas out of Arsenal and claimed he will do so with a sense of ‘anger and bitterness’.
A day after accusing fans of being disrespectful on Twitter, Nasri left a message for Facebook followers to reinforce his feelings.
‘It’s nearly done,’ said the France midfielder in reference to a proposed £23million transfer to Manchester City.

‘I will leave with bitterness and anger in my heart. I am proud for having played with the Gunners.
‘I have been very disappointed by the supporters last weekend. I am still an Arsenal player but I will leave very soon.’
City hope to complete the transfer before the weekend, with Arsenal at home to Liverpool on Saturday lunchtime.
It was during the goalless draw at St James’ Park when visiting Gunners fans reworked their usual celebratory Nasri song to accuse him of being greedy.
The sentiment stems from his refusal to extend a contract at the Emirates which expires next summer.
Arsenal have offered a new deal worth £90,000 a week but City have dwarfed it with a package worth £165,000 a week

SIMBA NA YANGA KUTIFUANA LEO

                                                          



Wapinzani wa jadi katika soka la Tanzania, timu za Simba na Yanga leo zitaingia katika vita nyingine pale zitakaposhuka dimbani kukabiliana katika mechi ya kuwania Ngao ya Jamii itakayofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mpambano huo unaoashiria ufunguzi wa msimu mpya wa Ligi Kuu itakayoanza Jumamosi hii, unatarajiwa kuwa na upinzani mkali huku ukiwa unafanyika takribani siku 36 tu tangu timu hizo zilipokutana katika mechi ya fainali ya michuano ya Kombe la Kombe la Kagame katika mechi iliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa na Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

Ugumu wa mpambano huo unatokana na ukweli kwamba Simba itataka kulipiza kisasi baada ya kufungwa kwa penalti katika mechi ya msimu uliopita ya Ngao ya Jamii wakati Yanga ikitarajia kulinda heshima yake baada ya kufuta uteja wa kufungwa na mpinzani wake kwa takribani miaka nane mfululizo.

Maandalizi.

Timu zote zinaonekana kujiandaa kikamilifu kutokana na kucheza mechi kadhaa za kirafiki za kujipima nguvu na timu za ndani na nje ya nchi.

Wakati Yanga ilisafiri hadi nchini Sudan kucheza na mabingwa wa nchi hiyo timu ya El Hilal, Simba ilijichimbia visiwani Zanzibar kwa takribani wiki mbili, ambapo ilicheza na timu za Polisi Zanzibar na timu ya taifa ya vijana Zanzibar,Karume Boys kabla ya kuhamishia kambi jijini Arusha, ambapo ilialika timu za Victors ya Uganda na AFC Leopards ya Kenya na kucheza nazo mechi za kirafiki.

Makocha:

Kocha wa Yanga, Mganda Sam Timbe amesema ataendeleza rekodi yake kwa kuibuka na ushindi katika mchezo wa leo, ambapo pia aliahidi kuibuka na ushindi kila wakati timu hizo zitakapokutana ili awape raha mashabiki wa klabu yake.

Naye Moses Basena ambaye pia ni raia wa Uganda amewataka mashabiki wa klabu hiyo kutokuwa na wasiwasi akisema amefunga njia zote ambazo wapinzani wanaweza kuchoropoka ili kuepuka kipigo.

Vikosi:

Baadhi ya sura zilizokuwapo wakati wa michuano ya Kagame hazitarajiwi kuonekana dimbani leo kwa upande wa Simba, sura hizo ni pamoja na mshambuliaji Mussa Mgosi aliyeuzwa katika timu ya DC Motema Pembe ya DR Congo, Mohammed Idd Banka aliyesitishiwa mkataba pamoja pia Mwinyi Kazimoto na Ulimboka Mwakingwe ambao ni majeruhi wakati Yanga inatarajiwa kumkosa kiungo mkabaji Nurdin Bakari.

Wachezaji wanaotarajia kuanza kwa upande wa kikosi cha Simba ni pamoja na
kipa Juma Kaseja, Said Nassoro' Chollo', Amir Maftah, Obadia Mangusa, Juma Nyosso, Jerry Santo, Uhuru Suleiman, Patrick Mafisango, Felix Sunzu, Haruna Moshi 'Boban' na Emmanuel Okwi.
Wakati kikosi cha Yanga kinatarajiwa kuwa; Yaw Berko, Shadrack Nsajigwa, Oscar Joshua,Nadir Haroub 'Cannavaro',Chacha Marwa, Juma Seif kijiko, Godfrey Taita, Haruna Niyonzima, Kenneth Asamoah, Jerry Tegete na Kigi Makasi.
Waamuzi
Idd Mbaga, Israel Mjuni, Hamis Chang'waru.

Ulinzi:
Mkurugenzi wa Kampuni ya mafuta ya Big Bon waliyonunua mechi hiyo, Ahmed Baashwani mbali ya kusema watatumiachombo maalumu kuwabaini watu watakaoghushi tiketi, pia alisema vyombo vya usalama vitakuwa imara kudhibiti vurugu huku akiwataka mashabiki kukaa katika majukwaa kulingana na maelekezo ya tiketi zao.


VUMBI LAHAMIA NOU CAMP LEO

LEO ni fainali ya Hispania Super Cup, ambapo Barcelona itakuwa ikikabiliana na Real Madrid katika mechi ya pili ya kuwania kombe hilo baada ya timi hizi kukutana kwa mara ya kwanza Jumapili iliyopita kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu na kutoka sare ya 2-2.

Katika mechi ya kwanza iliyozikutanisha Real Madrid na Barcelona ya kuwania Hispania Super Cup siku ya Jumapili, timu ya Real Madrid ilipiga mashuti mengi golini, lakini mabingwa wa Ulaya na mabingwa wa Ligi Kuu ya Hispania wao walipata faida ya magoli mawili ya ugenini.

Timu hizi mbili zimekutana kwa mara ya kwanza katika kuwania Hispania Super Cup, ambapo katika mechi ya leo ya marudiano kwenye uwanja wa Camp Nou, Barcelona inapewa nafasi kubwa ya kutwaa kombe hilo.

Katika mechi ya kwanza kipa wa Real Madrid, Iker Casillas alishindwa kuzuia mipira ya hatari golini mwake kwa sababu mipira miwili ya hatari iliyopigwa golini mwake yote ilitinga nyavuni kati ya mashuti manne waliyopiga Barcelona.

Hivyo uwezo walioonyesha Barcelona ni wazi timu ya Real Madrid iliyo chini ya kocha Jose Mourinho itabidi ibadilishe mikakati yake katika mechi ya leo, lakini tangu Mourinho alipojiunga na Real Madrid ameweza kutoa ushindani mkubwa kwa klabu ya Barcelona tangu 2010.

Real Madrid itaingia leo kwenye Nou Camp ikiwa inajiamini kwamba juhudi zao walizozionyesha katika mechi ya kwanza wataziendeleza katika mechi hii ya leo, Real Madrid katika mechi hiyo ya mwanzo walionekana kuwa imara na hawakusumbuliwa na mfumo wa pasi nyingi wa Barcelona.

Ingawa Karim Benzema hakufunga katika mechi ya kwanza, lakini aliweza kusaidia vizuri Mesut Ozil ambaye alikuwa mchezaji muhimu wa Real Madrid katika mechi hiyo.

Cristiano Ronaldo vilevile alikuwa katika kiwango chake cha kutandaza soka, pia kocha Mourinho alipanga safu imara ya ulinzi hata hivyo Barcelona waliweza kuipenya ngome hiyo na kufunga magoli.

Katika mechi ya kwanza, Barcelona haikumtumia beki wake Carles Puyol na pia katika mechi ya leo beki huyo hatacheza. Kukosekana kwa beki huyo wa kati kulionyesha wazi pengo hilo, ingawa mabeki Javier Mascherano na Eric Abidal walijitahidi sana kucheza katika mechi hiyo.

Swali kubwa linalomkabili kocha Pep Guardiola katika mechi ya leo ni kama atampanga kiungo wake mpya Cesc Fabregas na kama atampanga atamtumia kwa muda gani.

Tangu siku ya Jumatatu Cesc Fabregas alianza kufanya kazi na wachezaji wenzake wa Barcelona hata hivyo mchezaji huyo anayetokea Arsenal ya England kwa muda mrefu sasa amekuwa hachezi mechi za ushindani.

Kocha wa Barcelona, Pep Guardiola anakabiliwa na wachezaji wake mahiri kutokuwa fiti, ambapo katika mechi ya kwanza dhidi ya Real Madrid wachezaji wake Xavi Hernandez, Gerard Pique na Pedro walitokea benchi.

Katika mechi ya leo Je, Barcelona itanufaika na kikosi chake na kutwaa ubingwa wa Hispania Super Cup ? au Real Madrid itaondoka na kombe hilo katika uwanja wa Camp Nou unaomilikiwa na Barcelona?

ARSENAL IPO TAYARI KUMUACHIA EMMANUEL EBOUE KWENDA GALATASARAY YA UTURUKI KWA KITITA CHA PAUNDI ZA UINGEREZA MILIONI 4 IMEELEZWA KUTOKA KLABUNI HPOA JIJINI LONDON UINGEEZA.