Wednesday, September 28, 2011

MATOKEO MECHI ZA LIGI YA MABINGWA ULAYA

CSKA MOSCOW 2-3 INTER MILAN

REAL MADRID 3-0 AJAX

   BAYERN MUNICH 2-0 MAN CITY


               TRABZONSPOR 1-1 LILLE

 MAN UNITED 3-3 BASEL

Arsenal,Chelsea kibaruani leo ligi ya mabingwa ulaya

WINGA wa Chelsea, Juan Mata atakutana na rafiki zake wakati atakaporudi kucheza mechi Ligi ya Mabingwa dhidi ya Valencia leo ikiwa ni miezi mwezi moja tangu alipoondoka.

Kocha Andre Villas-Boas alitumia karibu dola 40.4 milioni kumsajili nyota huyo mwenye miaka 23 na tayari ameonyesha uwezo wake kwa kufunga kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi E walioshinda 2-0 dhidi ya Bayer Leverkusen.“Nipo tayari kucheza dhidi yake na wote tunamsubili,” alisema winga Valencia, Pablo Hernandez aliyekuwa wakilala chumba kimoja na Mata.

“Itakuwa ni siku yake nzuri kurudi nyumbani, lakini hatutakuwa na urafiki uwanjani. Tutafanya kila kitu kuhakikisha tunawafunga pamoja na Juan, baada ya hapo tutamtakia mfanikio mema.”

Chelsea wapo ipo kwenye kiwango cha juu baada ya kushinda 4-1 dhidi ya Swansea City pale Jumamosi na kuwafanya wapande hadi nafasi ya tatu katika Ligi Kuu, nyuma kwa pointi tatu kwa vinara Manchester United na Manchester City.Mshambuliaji wa Hispania, Fernando Torres alitolewa nje kwa kadi nyekundu dakika 39 pale Jumamosi, lakini anaonekana kurudi kwenye kiwango chake akiwa ameshafunga mabao mawili katika mechi mbili mfululizo.

Safu ya ushambuliaji wa Chelsea imeimarika na kurejea kwa nyota wa Ivory Coast, Didier Drogba aliyeingia kuingia akitokea benchi na kufunga baada ya wiki nne za kuwa nje kwa sababu ya kuumia.

LONDON, Robin van Persie ameanza kuthibisha kwamba anaweza kuiongoza Arsenal anategemewa kuibeba klabu hiyo leo kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Olympiakos.Van Persie alichukua unahodha huo baada ya Cesc Fabregas kutimikia Barcelona, Robin alifunga mabao mawili waliposhinda 3-0 dhidi ya Bolton Wanderers Jumamosi.

Olympiakos wenyewe wamepoteza mechi tisa walizocheza dhidi ya timu za England kwenye mashindano ya Ulaya, wakiwa wamefungwa mabao 29 na wao kufunga moja tu.

Van Persie, 28, ameshafunga mabao matano msimu huu na Wenger anaamini Mdachi huyo aliyeripotiwa na vyombo vya habari vya England, Jumatatu hataki kuharakisha kuongeza mkataba wake wake unamalizika 2013, kuwa kwa sasa amekuwa na anaweza kuongoza kwenye ufungaji na kuwatia moyo wenzake.

“Robin amekuwa kutoka mvulana anayesumbuliwa na presha za jamii wakati anakuja hapa na leo ni mtu mzima,” Wenger aliimbia tovuti ya Arsenal.Hilo alitakuwa vumbi pekee kutimka wiki hii Ulaya mashariki wakati BATE Borisov watakapowakaribisha mabingwa wa Ulaya, Barcelona katika mchezo wa Kundi H hapo leo.

BATE walitoka sare1-1 na Belshina Bobruisk pale Ijumaa, Barca walituma salamu kwa kuisambaratisha Atletico Madrid 5-0 Jumamosi huku mchezaji bora wa Dunia, Lionel Messi alifunga mabao matatu peke yake.

KIKOSI KITAKACHOKABILIANA NA MORROCCO HIKI HAPA


Tanzania imetangaza kikosi kitakachopambana na Morrocco katika michuano ya kufuzu kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwakani.
Taarifa iliyotolewa na chama cha soka cha Tanzania TFF imesema Taifa Stars ambayo inafundishwa na kocha Jan Poulsen itaondoka Oktoba 6 kwenda Morrocco, na kujitupa uwanjani Oktoba 9 mjini Marrakech kupambana na timu ya taifa ya Morrocco.

Kikosi hicho cha wachezaji 23 ni:

Makipa:


Shabani Dihile  (JKT Ruvu Stars)
Juma Kaseja  (Simba)
Shabani Kado   (Yanga)


Mabeki:


Shadrack Nsajigwa (Yanga)
Erasto Nyoni (Azam)
Idrissa Rajab (Sofapaka, Kenya)
Amir Maftah (Simba)
Aggrey Morris (Azam)
Juma Nyoso (Simba)
Victor Costa (Simba)


Viungo:


Henry Joseph (Kongsvinger IL, Norway)
Nurdin Bakari (Yanga)
Shabani Nditi (Mtibwa Sugar)
Jabir Aziz (Azam)
Nizar Khalfan (Vancouver Whitecaps, Canada)
Mrisho Ngassa (Azam)
Ramadhan Chombo (Azam)


Washambuliaji:


Abdi Kassim (DT Long An, Vietnam
Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC)
Dan Mrwanda (DT Long An, Vietnam)
Athuman Machupa (Vasalund IF, Sweden)
John Bocco (Azam)
Hussein Javu (Mtibwa Sugar)


Tanzania iko kundi D, pamoja na Algeria, Jamhuri ya Afrika ya Kati na Morrocco.

Tanzania ina pointi 5 baada ya michezo mitano na kushinda mmoja, sawa na Algeria. Morrocco na Jamhuri ya Afrika ya Kati zinaongoza kundi hilo zikiwa na pointi 8.

Tuesday, September 27, 2011

Oljoro yawachakaza walioidindia Simba yawalamba Toto 2-0

JKT Oljoro iliyopanda daraja msimu huu imetafuna mfupa uliowashinda Simba baada ya kuinyuka Toto African mabao 2-0 kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Pia jana Azam F.C ilishindwa kuendeleza kazi yake ya ushindi baada ya kulazimishwa suluhu na Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi wakati kwenye uwanja wa Chamazi, JKT Ruvu vilevile waligawana pointi na Villa Squad.

Timu za Kanda ya Ziwa zilijijengea jina wiki iliyopita baada ya kutibua rekodi ya Simba, ambapo Kagera Sugar ilitoka sare ya 1-1 na na timu hiyo halafu Toto African ikatoka nayo sare ya 3-3 na vinara hao wa ligi, lakini mambo yamekuwa tofauti baada ya timu hizo mbili zote kupokea kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa vijana wa Arusha.

Iliwachukua dakika sita Oljoro JKT kupata bao la kuongoza kupitia Sunday Mussa aliyepokea pasi nzuri kutoka kwa Paul Nonga na kupiga shuti lililojaa wavuni.

Wakati Toto wakiwa hawaamini kinachotokea Oljoro waliandika bao la pili dakika ya 18 kupitia Amir Hamadi akiunganisha kwa kichwa krosi nzuri ya Nonga iliyomshinda kipa wa Toto, Mustapha Mabrouk aliyekuwa ametoka nje kidodo ya goli lake.

Mzuka wa mechi dhidi ya Simba haukuwa kwa Toto kwani nyota wao Mnigeria Darlington Enyima alikosa bao dakika 38 baada ya kupiga shuti nje akiwa yeye na kipa wa Oljoro.

Katika dakika ya 43 Castol Mumbala alitoa pasi mbaya kwa kipa wake ambaye alishindwa kutuliza mpira huo kwa mguu na kuamua kuudaka hivyo mwamuzi kumzawadia kadi ya njano Mustapha Mabrouk kwa kitendo hicho.

Kwa ushindi waliopata Oljoro wanasogea hadi nafasi ya tatu wakiwa na pointi 13 katika michezo nane, lakini ndoto ya timu ya Azam ya kuisogelea Simba kileleni ilififia baada ya kulazimishwa suluhu na Ruvu Shooting katika mechi ya ligi.

Mshambuliaji John Boko wa Azam alikosa bao katika dakika ya 32 baada ya kushindwa kumalizia kwa umakini krosi ya Ibrahim Mwaipopo.

Shooting walijibu mapigo kupitia Abdallah Juma aliyekosa bao katika dakika ya 62 baada ya kuwatoka mabeki wa Azam na kupiga shuti lililopanguliwa na kipa Mwadini Ally na kutoka nje.

Mshambuliaji John Boko alifunga bao katika mechi hiyo, lakini mwamuzi alilikataa hivyo kocha wa Azam, Stewart Hall alilalamikia bao hilo, lakini mwamuzi alisema mfungaji ameotea na kuahidi kupeleka picha ya video ya tukio hilo TFF kama uthibitisho.

Katika mechi hiyo wahudumu wa huduma ya kwanza wa Redcross walikuwa hawajavaa sare zao za kazi walipokuwa wakiingia uwanjani kuwahudumia wachezaji katika mechi hiyo ya Azam dhidi ya Ruvu Shooting.

Pia mashabiki waliojitokeza kwenye uwanja wa Mabatini kushuhudia pambano hilo walilalamikia uchache wa tiketi uliowafanya washindwe kuingia uwanjani hapo ili kushuhudia mchezo huo.

Akizungumza baada ya mechi hiyo kumalizika kocha wa Shooting, Boniface Mkwasa alisema mchezo ulikuwa mgumu, lakini amewasifu wachezaji wake kwa kucheza kwa moyo na kupata matokeo hayo mazuri na sasa wanajipanga kuikabili Mtibwa Sugar.

Wakati Mkwasa akisifu kiwango cha wachezaji wake hali ilikuwa tofauti kwenye Uwanja wa Chamazi kwani kocha wa JKT Ruvu, Charles Kilinda aliwalaumu wachezaji wake kwa kushindwa kucheza kama kawaida yao na kusababisha timu hiyo kupoteza pointi kwenye mchezo huo.

"Sijawahi kuona timu yangu ikicheza mpira mbovu kama waliocheza leo tangu nilipoanza kuifundisha miaka minne iliyopita,"alisema Kilinda.

Kilinda aliongeza labda wamechoka kwa sababu wapo wachezaji wachache kwenye kikosi chake kwa sababu wengine wamekwenda kwenye kozi za kijeshi.

Hata hivyo timu ya JKT Ruvu watajilaumu wenyewe kwa kupoteza nafasi nyingi za kufunga kupitia washambuliaji wake Hussein Bunu, Rajab Chau na Emmanuel Linjechele katika dakika ya 20, 32, 38 na 40 kwa mashuti yao kutoka nje.

JKT Ruvu wanaosifika kwa kucheza soka ya pasi nyingi na kuvutia walishindwa kuonyesha mchezo wao huo mbele ya Villa Squad na kushuhudia timu hizo zikienda mapumziko zikiwa hazijafungana.

Ruvu walimtoa Alhaji Zege na kumwingiza Haruna Adolf wakati Villa walimpumzisha Mohamed Kijuso na nafasi yake kuchukuliwa na Allu Bilal.

Katika mchezo huo makipa wa timu zote mbili Mohamed Bambino wa Villa Squad na Hamis Nyangalio wa JKT Ruvu walifanya kazi kubwa kulinda magoli yao.

SIMBA, MTIBWA ZAINGIZA Sh 74 mil

Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Mtibwa Sugar iliyochezwa Septemba 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh 74,345,000.

Watazamaji waliokata tiketi kushuhudia mechi hiyo walikuwa 13,285 ambapo kiingilio kilikuwa sh 5,000 kwa viti vya bluu na kijani, sh 7,000 rangi ya chungwa, sh 15,000 kwa VIP C na B na sh 20,000 kwa VIP A.

Eneo lililoingiza watazamaji wengi ni kwenye viti vya bluu na kijani ambapo waliingia mashabiki 11,798 wakati eneo lililoingiza watazamaji wachache ni la VIP A ambapo waliingia mashabiki 58.

Baada ya kuondoa gharama za awali za mchezo ambazo ni sh 11,637,000 na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambayo ni sh 11,340,762.70 kila timu ilipata
sh 15,410,171.19.
Mgawo mwingine ulikwenda kwa gharama za mchezo (sh 5,136,723.73), uwanja (sh 5,136,723.73), TFF (sh 5,136,723.73), Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu- FDF (sh 2,568,361.86), Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam- DRFA (sh 2,054,689.49) na Baraza la Michezo la Taifa- BMT (sh 513,672.37).

Monday, September 26, 2011

WATU MAARUFU WENYE MAHUSIANO WANAWAKE WAFUPI NA WANAUME MIRABA MINNE

WILL & JADA   photo | Jada Pinkett Smith, Will Smith
Will Smith(6'2") na mkewe Jada Pinkett Smith (5') hii inaonesha suala la urefu haliathiri mapenzi ya kweli.

KIM & KRIS   photo | Kim Kardashian, Kris Humphries
Kim Kardashian (5'3") na mumewe Kris (6'9")


SACHA & ISLA   photo | Isla Fisher, Sacha Baron Cohen
Sacha(6'3'') na Isla (5'3'')


SHAQ & NICOLE   photo | Shaquille O'Neal

















Shaq(7'1'') na Nicole(5'2")


REESE & JIM   photo | Jim Toth, Reese Witherspoon
Reese na Jim


DAX & KRISTEN   photo | Dax Shepard, Kristen Bell
Kristen(5'1") na Dax(6'1")


CHRIS & ELSA   photo | Chris Hemsworth, Elsa Pataky
Chris(6'3") na mkewe Elsa (5'4")

SIMBA JUU KWA JUU YATAFUNA MIWA YA MTIBWA, KAGERA SUGAR YATOA DOZI KWA POLISI

















Uhuru Selemani akichanja mbuga

MSHAMBULIAJI Emmanuel Okwi alitia kambani bao pekee na kuipaisha Simba kileleni mwa Ligi Kuu katika mechi dhidi ya Mtibwa Sugar, pia Kagera Sugar imepata ushindi wake wa kwanza msimu huu baada ya kuilaza Polisi Dodoma mabao 2-0.

Simba ambao walishuka kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wakiwa na kumbukumbu ya kulazimishwa sare mara mbili Kanda ya Ziwa iliwachukua dakika 35 kabla ya mashabiki wake kufurahi baada ya Okwi kupokea vizuri pasi ya Uhuru Seleman na kufunga bao hilo kwa shuti kali ambalo limeiwezesha Simba kufikisha pointi 18.

Pamoja na ushindi huo wa bao 1-0 ilioupata Simba, beki wa timu hiyo Victor Costa alikosa mkwaju wa penalti katika dakika ya 90 baada ya mkwaju wake kupanguliwa na kipa wa Mtibwa Sugar, Deogratius Munishi"Dida"

Mabingwa wa mwaka 2000, Mtibwa Sugar walianza mechi kwa kishindo kupitia Masoud Ally aliyepokea pasi ya Thomas Maurice na kupiga shuti kali la umbali wa mita 25, lililopanguliwa na kipa wa Simba, Juma Kaseja.

Simba walijibu mapigo katika dakika ya nane kupitia kwa Uhuru Seleman aliyetokea winga ya kushoto na kutoa pasi kwa Emmanuel Okwi aliyepiga shuti lililopaa juu.

Mtibwa waliendelea kupeleka mashambulizi katika lango la Simba, ambapo walipata faulo ambayo ilipigwa na Masou Ally katika dakika ya11 na mpira uligonga mwamba na mabeki wa Simba waliokoa mpira huo na kuwa kona.

Pia Simba na wenyewe waliendelea kulishambulia lango la Mtibwa ila katika dakika ya 13 Okwi alishindwa kutumia vizuri pasi ya Jerry Santo kufunga bao.

Mechi hiyo pia ilisimama kwa dakika kadhaa baada ya kiungo Zuberi Katwila wa Mtibwa kugongana na Victor Costa wakati wakiwania mpira wa juu na wote wawili walitolewa nje kwa ajili matatibu, lakini walitibiwa na kurudi kuendelea na mchezo.

Lakini hali ya Katwila ilionekana siyo nzuri kwani alikuwa akichechea na aliomba kutoka hivyo kocha wa Mtibwa Sugar, Tom Olaba alilazimika kumtoa Katwila katika dakika ya 22 na kumwingiza Awadhi Juma.

Chipukizi Shomari Kapombe wa Simba katika mechi hiyo alikosa bao dakika ya 28 baada ya shuti lake kumgonga beki wa Mtibwa na kuwa kona ambayo haikuleta madhara.

Kapombe pia alitengeneza pasi nzuri kwa Uhuru aliyemchungulia Okwi ambaye aliutumia vizuri udhaifu wa nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Salum Sued aliyeoneka kushindwa kwenda na kasi ya mchezo kufunga bao la Simba katika dakika ya 35.

Mtibwa walirudi kwa kasi katika kipindi cha pili, ambapo katika dakika ya 47, nusura wasawazishe baada ya krosi ya kiungo Shabaan Nditi kutua kichwani mwa Maurice ambaye alipiga nje.
Katika dakika ya 90, Simba walipata penalti baada ya Haruna Moshi kuangushwa kwenye eneo la hatari na mwamuzi David Paulo kutoka Mtwara kuamuru adhabu hiyo.

Beki wa Simba, Costa alishindwa kutoa zawadi ya bao kwa mtoto wake watatu wa kiume aliyezaliwa juzi baada ya mkwaju wake wa penalti kupanguliwa na kipa wa Mtibwa Sugar, Munishi katika dakika ya 90.

Kocha Olaba wa Mtibwa katika mechi hiyo alimtoa Ally Mohamed na kumwingiza Hussen Javu wakati, Moses Basena wa Simba aliwatoa Uhuru Selemani ,Amri Kiemba na Gervais Kago na kuwaingiza Ulimboka Mwakingwe, Shija Mkina na Haruna Moshi.

Akizungumza baada ya mechi hiyo kumalizika kocha wa Mtibwa, Olaba alisema wachezaji wake hawakucheza vizuri katika kipindi cha kwanza, lakini walibadilika dakika 45 za mwisho.

"Viungo walikosa maelewano katika kipindi cha kwanza, lakini tuliporudi mapumziko walibadilika na kufanya vile tulivyotaka."

KAGERA: Wenyeji Kagera Sugar baada ya kupokea kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Oljoro katikati ya wiki walibadilika jana na kuichakaza Polisi Dodoma mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

Washambuliaji Hussein Sued na Said Dilunga walitia kambani mabao mawili katika kipindi cha kwanza na kurudisha imani ya wanakagera kwa timu yao ambayo imepata ushindi huo kwa mara ya kwanza.

Sued alifunga bao la kwanza kwa mkwaju wa penalti dakika ya kumi baada ya Dilunga kuangushwa kwenye eneo la hatari na beki wa Polisi, Frank Sindato na mwamuzi Amon Paul kutoka mkoani Mara kuamuru penalti.

Wakati maafande hao waliokuwa chini ya kocha msaidizi wakijiuliza nini kinatokea Sued alipitisha krosi nzuri iliyomkuta Dilunga aliyesukuma mpira wavuni na kuwainua mashabiki wa Kagera Sugar waliojitokeza kwenye uwanja huo.

Kagera Sugar iliwapumzisha Malegesi Mwanga, Sunday Frank, Sued na kumwingiza Khamis Ally na Temmy Felix, Ibrahim Mamba, Katika mechi hiyo Polisi iliwapumzisha Raygan Mbuta na Delta Nyamancheja na nafasi zao kuchukuliwa na Ibrahim Masawe na Haruna Hassan.
Pia katika mchezo huo wenyeji walioneka kucheza kwa kujiamini na kuelewana tofauti na ilivyokuwa walipocheza dhidi ya Oljoro.

Ligi hiyo inaendelea leo kwa Azam wanaoshika nafasi ya pili kuwavaa Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Mabatini Mlandizi, wakati Chamazi, JKT Ruvu watakuwa na kibarua kizito mbele ya Villa Squad huku jijini Mwanza Toto African watakuwa wenyeji wa Oljoro JKT kwenye Uwanja wa CCM Kirumba.

Katika hatua nyingine Shirikisho la soka Tanzania limetangaza viingilio vya mchezo kati ya Yanga na Coastal Union kuwa ni sh 3,000 kwa viti vya bluu na kijani, sh 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa VIP C ni sh 7,000, VIP B ni sh 10,000 na VIP A itakuwa sh. 15,000.

VIDEO ZA MATUKIO NA MAGOLI KATIKA MECHI ZA MWISHO WA WIKI LIGI MBALIMBALI DUNIANI

                                                       LIGI KUU UINGEREZA 

                                               Newcastle United 3-1 Blackburn Rovers


Stoke City 1-1 Man United



Wigan Athletic 1-2 Tottenham Hotspurs


Manchester City 2-0 Everton


LIGI KUU UJERUMANI

Bayern Munich 3-0 Bayer Leverkusen


LIGI KUU ITALIA

AC Milan 1-0 Cesena


Bologna 1-3 Inter Milan


LIGI KUU UHOLANZI

PSV Eindhoven 7-1 Roda JC


LIGI KUU UHISPANIA

Real Madrid 6-2 Rayo Vallecano


Barcelona 5-0 Atletico Madrid