Huo unakuwa mchezo wa kwanza kwa Newcastle kupoteza msimu huu.
Monday, November 21, 2011
MAN CITY YAPAA,ARSENAL YAPETA
Manchester City ilipata mabao mawili kwa njia ya mikwaju ya penati wakati walipopata ushindi murua wa mabao 3-1 dhidi ya Newcastle.
Mlinzi Ryan Taylor aliunawa mpira eneo la hatari na kusababisha Manchester City kupata bao lao la kwanza kwa mkwaju wa penalti uliojazwa kimiani na Mario Balotelli. Sergio Aguero baadae akatengeneza pasi murua kwa mlinzi Micah Richards aliyemaliza kazi kwa kufunga bao la pili.
Richards aliangushwa na Hatem Ben Arfa ndani ya eneo la hatari na kusababisha Manchester City wapate bao la tatu na penalti hiyo ilifungwa na Aguero.
Hata hivyo wakijitahidi dakika za mwisho Newcastle walifanikiwa kupata bao la kufutia machozi lililopachikwa na Dan Gosling baada ya kuuwahi mpira ambao ulipigwa na Demba Ba na kumgonga mlinda mlango Joe Hart.
Bao la dakika za mwisho lililofungwa na Leighton Baines kwa mkwaju wa penalti, liliipatia Everton ushindi wake wa pili wa ligi nyumbani msimu huu baada ya kuilaza Wolves mabao 2-1.
Stephen Hunt ndiye alikuwa wa kwanza kuipatia Wolves bao la kuongoza kwa mkwaju wa penalti baada ya kiungo Marouane Fellaini kumchezea rafu David Edwards ndani ya eneo la hatari.
Phil Jagielka aliisawazishia Everton baada ya kuunganisha kwa kichwa mpira wa free-kick uliochongwa na Baines kutokea upande wa kushoto.
Alikuwa Baines aliyeipatia bao la ushindi Everton zikiwa zimesalia dakika saba kabla mchezo kumalizika kwa mkwaju wa penalti baada ya Stephen Ward kumsukuma Louis Saha ndani ya sanduku.
Queens Park Rangers ikiwa imeanza kufungwa na Stoke, ilibadilika na kuweza kushinda kwa mabao 3-2 ambapo walisawazisha kwa bao la Heidar Helguson.
Stoke wakicheza uwanja wa nyumbani walipata bao la kuongoza lililowekwa wavuni na Jon Walters aliyeachia mkwaju mkali wa pembeni, kabla ya Helguson kusawazisha kwa kichwa akiwa hajakabwa na mchezaji yeyote.
Luke Young aliipatia QPR bao la pili kabla ya Helguson kuongeza la tatu kwa mkwaju wa karibu na lango.
Ryan Shawcross alifanikiwa kuipatia Stoke bao la pili naye kwa mkwaju wa karibu, lakini dakika nazo zilikuwa zimewatupa mkono na QPR ndio waliondoka na washindi.
Shane Long amerejea kwa kishindo katika klabu yake ya West Brom na kuinyanyua timu yake hadi nafasi ya 10 na kuzidi kuiongezea matatizo Bolton baada ya kufunga bao la pili la ushindi.
Mshambuliaji huyo alifunga bao lake la nne kwa msimu huu wa ligi katika dakika ya 56 ikiwa ni wiki nne tu tangu alipoumia goti.
West Brom ndio walikuwa wa kwanza kupata bao lililopachikwa na Jerome Thomas alipotegua mtego wa kuotea na akamzunguka mlinda mlango Jussi Jaaskelainen.
Ivan Klasnic alisawazisha dakika chache baadae kwa mkwaju wa penalti baada ya Fabrice Muamba kufanyiwa rafu, lakini hadi mwisho West Brom 2 Bolton 1.
Yakubu alikuwa shujaa wa Blackburn baada ya kufunga bao la kusawazisha kwa mkwaju wa penalti katika dakika ya 99 na kuipatia timu yake iliyokuwa ikicheza pungufu ya mchezaji mmoja sare ya mabao 3-3 dhidi ya Wigan.
Mshambuliaji huyo alisawazisha baada ya Wigan kuwa mbele kwa mabao 3-2.
Robin van Persie alikuwa mwiba wa kuotea mbali baada ya kuipatia timu yake ya Arsenal mabao 2-1 dhidi ya Norwich na timu hiyo kupata ushindi wake wa 10 kati ya mechi 12.
Van Persie akicheza kwa kiwango cha juu msimu huu, kwa mara nyingine alisaidia Arsenal kuweza kuamka na kuvuna pointi tatu ugenini.
Alipata bao lake la kwanza baada ya kuunganisha pasi ya pembeni kutoka kwa Theo Walcott na bao lake la pili lilitokana na pasi maridadi ya Alex Song.
Norwich walikuwa wa kwanza kuistua Arsenal walipofunga bao la kwanza lililofungwa na Steve Morison kutokana na makosa ya mlinzi wa Arsenal Per Mertesacker.
CHELSEA HOI MBELE YA LIVERPOOL,YALALA 2-1 NYUMBANI
Glen Johnson amefanikiwa kuipatia ushindi Liverpool kwa bao la dakika za mwisho wakati Chelsea ilipolala kwa mabao mabao 2-1 katika uwanja wao wa Stamford Bridge.
Steven Gerrad akishangilia bao
Liverpool walikuwa wa kwanza kupata bao katika kipindi cha kwanza lililofungwa na Maxi Rodriguez katika dakika ya 33 baada ya gonga ya hapa na pale ya Craig Bellamy na Luis Suarez.
Daniel Sturridge aliyeingia kipindi cha pili aliisawazishia Chelsea kutokana na juhudi kubwa iliyooneshwa na Florent Malouda katika dakika ya 55.
Branislav Ivanovic nusura aipatie Chelsea bao la pili alipopiga kichwa lakini mpira huo ukaokolewa, lakini alikuwa mlinzi wa upande wa kulia Johnson aliyeihakikishia pointi tatu muhimu Liverpoo kutokana na jitahada zake binafsi alipokokota mpira upande wa kushoto na kuwapita walinzi wa Chelsea kama anafanya mazoezi na kupachika bao safi la pili.
Misri "kimenuka" Zaidi wafariki katika maandamano
Waandamanaji wakiwa wamekusanyika katika uwanja wa Tahrir 18/11/2011
Mamia ya waandamanaji nchini Misri wameivamia tena medani ya Tahrir katika mji mkuu wa Cairo hata baada ya polisi na wanajeshi kutumia nguvu kuwaondoa.
Chini ya muda wa saa moja baada ya kuondolewa Tahrir,waandamanaji walirudi tena mahali hapo huku wakitoa matamshi dhidi ya utawala wa kijeshi wa Misri.
Katika makabiliano hayo mengine ya siku ya Jumapili, watu 11 wameripotiwa kuuwawa.Kutokana na vifo hivyo jumla ya idadi ya watu waliouwawa tangu siku ya Jumamosi imefikia 13.
Kwa mujibu wa madaktari watu wengine wapatao 900 wamejeruhiwa wakiwemo maafisa wa usalama 40.
Awali, waandamanji walilazimika kutoroka baada ya maafisa wa usalama kuwarushia gesi ya kutoa machozi na kisha kuwapiga kwa marungu.
Machafuko mengine pia yalishuhudiwa katika miji mingine ikiwemo , Alexandria, Suez na mji wa Aswan.
Waandamanaji wa chama cha Muslim Brotherhood na vyama vingine vinashiriki katika maandamano hayo
Wandamanaji hao ambao walikuwa wameziba nyuso zao ili gesi ya kutoa machozi isiwadhuru wanalalamika kuwa watawala wa kijeshi walikuwa na njama za kunyakuwa uongozi wa nchi hiyo.
Machafuko hayo yametokea kukiwa kumesalia wiki moja tu kabla ya uchaguzi wa maeneo bunge kuanza ambao utakuwa wa kwanza tangu Rais Hosni Mubarak kupinduliwa mwezi wa Februari.
Mwandishi wa BBC Helena Merriman amesema kuwa hali sio nzuri sana kwa sababu mara kunashuhudiwa hali ya utulivu na baadaye tena hali inabadilika na kuwa ya taharuki na watu kuanza kukimbia.
Katika kipindi cha wiki kadhaa zilizopita makundi wa Kiiislamu pamoja na wakereketwa wengine wamekuwa wakifanya maandamano nchini Misri huku waandamanaji wakidai kuwa kuna njama za kubadilisha katiba ili kuruhusu baraza la kijeshi kuendelea kuwa na uwezo mkubwa.
Friday, November 18, 2011
WAMAREKANI WAANDAMANA KUPINGA TOFAUTI KUBWA KATI YA TAJIRI NA MASIKINI
Waandamanaji wanaopinga tabaka la masikini na matajiri wakiwa katika mtaa mdogo wa Manhattan karibu na soko kuu la hisa "New York stock exchange" katika siku waliyoiita siku ya vitendo wakiwa wameandamana kutoka New york mpaka New York stock exchange
Maelfu ya waandamanaji katika mji wa New York wameendelea na harakati zao wakielekea kuvuka daraja la Brooklyn, kuonyesha ghadhabu zao dhidi ya kuendelea kuwepo matabaka nchini humo.
Waandamanaji wanaadhimisha kuanza kwa kampeni ya kupinga mfumo wa kiuchumi unaosababisha matabaka nchini Marekani ambapo walipiga kambi katika mtaa wa Wall Street kuliko na soko kuu la hisa na taasisi kubwa za kifedha Marekani. Mwezi uliopita, polisi waliwakamata mamia ya waandamaji .
Taswira nje ya soko kuu la fedha la Marekani ni raia wenye ghathabu kubwa wakiendelea kukaribia jumba la soko hilo na kulizingira kabisa.Polisi wamekuwa na wakati mgumu kuwazuia kwa kuweka vizuizi nje ya jumba hilo. Baadhi ya waandamanaji wamekamatwa huku kukiwa na makabiliano na ujibizanaji wa maneno makali.
Waandamanaji wakiwa wamebeba bango
Hamasa ya waandamanaji hao ni kufuatia hatua ya polisi kuwafurusha katika eneo walikokita kambi katika bustani ya Zuccotti. Hii imewafanya kushindwa kukesha huko. umati wa watu ambao walikuwa wamekusanyika nje ya Wall Street wameondoka.
Hata hivyo wamepanga kukusanyika tena katika kituo cha treni na jioni watafanya jaribio jingine la kuvuka daraja kuu ya Brooklyne.
Waandamanji hao wanasisitiza kwamba ni haki yao kuandamana.
Thursday, November 17, 2011
Onesho la sanaa ya matikiti maji yafana(Water melon art Festival)
Wengi tunayafahamu matikiti maji ama kwa lugha ya kigeni WATERMELON.
Huko nchini Italia kuna maonesho yanayojulikana kama Watermelon art Festival, ambapo wasanii kutoka sehemu mbalimbali za Italia hukutana huku kila mmoja akiwa na matikiti kadhaa ambayo ametumia usanii wake kuyatia nakshinakshi za aina mbalimbali na kuleta maumbo tofauti yenye kuvutia.Zifuatazo ni baadhi ya picha za maonesho hayo huko Italia.
Huko nchini Italia kuna maonesho yanayojulikana kama Watermelon art Festival, ambapo wasanii kutoka sehemu mbalimbali za Italia hukutana huku kila mmoja akiwa na matikiti kadhaa ambayo ametumia usanii wake kuyatia nakshinakshi za aina mbalimbali na kuleta maumbo tofauti yenye kuvutia.Zifuatazo ni baadhi ya picha za maonesho hayo huko Italia.
Syria "kimenuka" Jumuiya ya nchi za Kiarabu yaipa siku3 kumaliza Mzozo
Mmoja wa majeruhi akipata huduma ya kwanza
Waziri wa Mambo ya nje wa Ufaransa Alain Juppe anatarajiwa kufanya ziara maalum nchini Uturuki, kujadili hatua dhidi ya mzozo unaoendelea nchini Syria.
Jumuiya ya nchi za kiarabu imeipa Syria siku tatu kumaliza tatizo hilo la sivyo itawekewa vikwazo vya kiuchumi.
Mmoja kati ya waandamanaji nchini Syria akiwa amebeba bango"Bashar acha mauaji"
Habari zinasema majeshi yaliyoasi yameendelea kulenga kambi za jeshi linalotii serikali.
Ni miezi minane ambapo waandamanaji wasiokuwa na silaha wamekuwa wakilengwa na wanajeshi watiifu kwa Rais Bashar Assad. Hali imebadilika na majeshi asi yameanza kukabiliana na mahasimu wao.Rais wa Syria Bashar Al-asaad
Duru kwamba majeshi yaliyoasi na chini ya mwavuli Jeshi Huru La Syria yameshambulia vituo kadhaa vya kijeshi mjini Damascus na kuwaua wanajeshi kadhaa wa serikali ya Syria bado hazijathibitishwa. Lakini ikiwa madai haya yana ukweli wowote, basi ni ishara kwamba huenda mzozo wa Syria umechukua mkondo hatari.
Jumuiya ya nchi za kiarabu imeonya kuiwekea Syria vikwazo vya kiuchumi ikiwa serikali ya Rais Assad haitakoma kutumia nguvu dhidi ya waandamanaji na imetaka dhuluma hizo kukomeshwa siku tatu.
Maandamano nchini Syria kupinga utawala wa Bashar
Umati wa waandamanaji nchini Syria
Ututruki pia inatathmini kuiwekea Syria vikwazo. Tayari Marekani na jumuiya ya Ulaya zimeweka vikwazo, japo haijabainika athari za viwazo hivi ni ipi.
Jumuiya ya nchi za Magharibi na mataifa ya magharibi yameanza kutafakari mustakabali wa Syria bila uwongozi wa Bashar Al Asaad.
Waandamanaji nchini Syria
Hata hivyo pande zote ziko maakini kuzuia vita vya wenyewe kwa wenyewe katika nchi hiyo. Hata hivyo ni vigumu kuafikia lengo hilo bila kuwepo ung'anganizi wa madaraka usipokuwa kwa mtutu wa bunduki.
Subscribe to:
Posts (Atom)



















