Thursday, February 2, 2012
SIMBA YAENDELEZA DOZI YAIKANDAMIZA JKT OLJORO 2-0
Uhuru Selemani wa Simba akifanya vitu vyake
JKT Oljoro jana walishindwa kwenda sambamba na kasi ya Simba waliocheza pungufu sehemu kubwa ya mchezo na kukubali kipigo cha mabao 2-0, shukrani kwa mabao ya kipindi cha pili ya mshambualiaji, Emmanuel Okwi yaliyoihakikishia Wekundu hao wa Msimbazi pointi zote tatu.
Katika mechi hiyo iliyochangamshwa na ushindani mkubwa toka timu zote mbili kwenye Uwanja wa Taifa, ilishuhudia kiungo wa Simba Haruna Moshi 'Boban' akionyeshwa kadi nyekundu isiyo na onyo baada ya kumrushia teke la makusudi mchezaji wa Oljoro, Omary Mtaki dakika ya 42.
Mwamuzi Isiaka Shirikisho wa Tanga, ambaye alionekana kushindwa kwenda sawa na kasi ya mchezo, pia aliwalima kadi za njano Omary Khasim wa JKT kwa kumchezea vibaya Haruna Moshi, kisha Kelvin Yondani na Jonas Gerald wa Simba kwa kuwachezea vibaya Kalege Mgunda na Nyambele.
Ushindi huo umeifanya Simba kuendelea kubaki kileleni mwa msimamo kwa kufikisha pointi 34, tatu mbele ya mahasimu wao Yanga watakaoshuka dimbani mwishoni mwa wiki hii.
Katika mechi hiyo ambayo Simba walitumia zaidi viungo kufanya mashambulizi, JKT Oljoro waliofungwa 2-0 mzunguko wa kwanza, itabidi wajilaumu kwa kushindwa kutumia ya fursa ya wapinzani wao kucheza pungufu kupata ushindi.
Kocha wa Oljoro, Ally Kidy mara baada ya mchezo alikiri kuzidiwa na Simba, lakini akawalaumu wachezaji wake kushindwa kutumia vizuri nafasi nyingi za kufunga walizopata na pia kutumia mwanya wa Simba kucheza pungufu.
Simba walitawala dakika 20 za mwanzo wa mchezo na kukosa mabao kadhaa, huku Oljoro wakirejea mchezo dakika 10 za mwisho za kipindi hicho baada ya awali kufunikwa sehemu ya kiungo.
Mabadiliko yaliyofanywa na Simba kumtoa Gervais Kago na kuingia mshambualiaji wa kimataifa kutoka Uganda, Okwi katika kipindi cha pili ndiyo yaliyoipa ushindi timu hiyo.
Okwi, ambaye pengo la kutokuwapo kwake katika mchezo wa kwanza lilionekana wazi, alitumia dakika 15 tangu aingie uwanjani kuipeleka Simba mbele kwa bao zuri akimalizia pasi ya Uhuru Selemani.
Dakika nne baada ya bao hilo, Oljoro walikuja juu na kufanya shambulizi la nguvu ambalo nusura lizae bao la kusawazisha kufuatia piga nikupige kabla ya mabeki wa Simba kuokoa hatari.
Mchezaji Bakari Kigodeko wa Oljoro hatasahau nafasi ya wazi kufunga akiwa amebaki na nyavu na kisha kupiga mpira nje katika dakika ya 71.
Walikuwa Simba waliotawala mchezo bila kuonekana kama walikuwa pungufu uwanjani na kujipatia bao la pili dakika saba kabla ya filimbi ya mwisho baada ya Okwi kuinasa pasi ya Mafisango na kufunga bao hilo.
Kocha wa Simba Cirkovic Milovan aliwapongeza wachezaji wake kwa kuonyesha mchezo mzuri na kushinda mchezo huo pamoja na kwamba walicheza pungufu. "Matokeo mazuri kwetu, ni ishara ya kuwa tayari kwa ajili ya mechi dhidi ya Kiyovu ya Rwanda," alisema.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo iliyopigwa Mbagala, nje kidogo ya jiji kwenye Uwanja wa Azam, Chamazi kati ya African Lyon iliichapa Polisi Dodoma mabao 2-0.Mechi hiyo ilishuhudia timu zote zikishambuliana kwa zamu kipindi cha kwanza, huku Lyon wakionekana kufika zaidi langoni mwa wapinzani wao.
Wakicheza kwa kushambuliana, Semy Kessy aliifungia Lyon bao la kwanza dakika ya 30 kwa shuti kali lililomshinda kipa wa Polisi, Gerald Mwingira baada ya awali kuwalamba chenga mabeki wa timu hiyo.Lyon walijihakikishia pointi tatu ushindi kwa kufunga bao la pili kupitia Sunday Juma baada ya kushirikiana vizuri na Samuel Ngasa katika dakika ya 76.
Mwenyeji Guinea atupwa nje kombe la mataifa ya Afrika,Botswana nayo yaangukia pua
Ghana ilijitengea nafasi yake katika robo fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, baada ya kutoka sare 1-1 na Guinea katika uwanja wa Franceville.
Ghana wametinga fainali baada ya kuongoza kundi D
Abdoul Razzagui Camara hata hivyo alisawazisha bao hilo mwishoni mwa kipindi cha kwanza.
Guinea walijitahidi kupata bao la ushindi, lakini hawakufanikiwa.Ushindi wa Mali wa magoli 2-1 dhidi ya Botswana ulimaanisha Guinea wanaondoka pasipo kucheza robo fainali.
Ghana vs Guinea
Botswana ilikuwa ya kwanza kufunga kupitia Mogakolodi Ngele, bao la ufundi mkubwa, na ambalo kipa Oumar Sissoka hakujui ni nini kimepita hadi wavuni.
Garra Dembele aliweza kuisawazishia Mali, kabla kiungo cha kati Seydou Keita kumaliza kazi kwa bao la ushindi.
Ushindi huo ulimaanisha kwamba Mali ilimaliza katika nafasi ya pili katika kundi D, nyuma ya Ghana.
Timu zitapumzika siku mbili, kabla mapambano mawili ya kwanza ya robo fainali kuchezwa siku ya Jumamosi.
Mali vs Botswana
74 WAFARIKI UWANJANI KATIKA VURUGU ZA SOKA MISRI
Moto ukiwaka uwanjani
Watu 74 wamefariki kufuatia ghasia kati ya mashabiki wa timu mbili katika mji wa Port Said, nchini Misri.
Taarifa hizo ni kwa mujibu wa televisheni ya taifa.
Mashabiki wakiwa wamevamia uwanja katika vurugu hizo
Watu hao walikiufa baada ya mashabiki kuanza kuingia uwanjani, baada ya mechi kati ya vilabu viwili vikuu vinavyoongoza ligi nchini humo, Masry na Al-Ahly, siku ya Jumatano.
Inahofiwa kwamba idadi ya vifo huenda ikaongezeka, kwani zaidi ya watu 156 wamejeruhiwa.
Huu ndio msiba mkubwa zaidi nchini Misri kuwahi kutokea katika uwanja wa kandanda, alielezea naibu waziri wa afya nchini Misri.
“Huu ni msiba wa kusikitisha mno”, alisema Hesham Sheiha kupitia matangazo ya televisheni.
Kati ya waliokufa ni pamoja na maafisa wa usalama.
Wachezaji wakikimbia kunusuru maisha yao
Mwandishi wa BBC anaelezea kwamba ukosefu wa usalama mkali ambao hudumishwa kwa kawaida huenda ikawa ni jambo ambalo lilichangia kutokea ghasia hizo.
Polisi nchini Misri wametulia mno tangu kufanyika maandamano yaliyomtoa Rais Hosni Mubarak madarakani.
Kimenukaaaaaa
Katika mechi hiyo ya Jumatano, timu ya Port Said, Masry, ilipata ushindi wa magoli 3-1.
Walioshuhudia walielezea kwamba kulikuwa na hali ya wasiwasi muda wote wa mechi hiyo, tangu shabiki mmoja wa Al-Ahly alipoinua bango ambalo inadaiwa lilikuwa linawatukana mashabiki wa timu ya nyumbani.
Katika mitandao ya jamii, licha ya kutokuwepo ushahidi, uvumi umekuwa ukienea kwamba maafisa wa usalama walikuwa wanapanga njama ya kupambana na mashabiki wa Al-Ahly.
Maafisa wachache wa polisi walijitahidi kuwapa ulinzi wachezaji, lakini hawakufanikiwa kabisa.
Sehemu moja ya uwanja ilichomwa moto.
Maafisa wanaohusika wameelezea kwamba vifo vingi vilitokana na watu kupata majeraha makubwa ya kichwa kwa kupigwa au kukatwa, na wengine kuzimia hadi kufa wakati wa mkanyagano.
Ndege za helikopta zilitumwa hadi Port Said kuwasafirisha hadi hospitali mashabiki waliojeruhiwa.
Maiti zilizopoteza maisha papohapo
"Huu si mpira. Hivi ni vita na watu wanakufa mbele yetu", alisema mchezaji wa Al-Ahly, Mohamed Abo Treika.
Mbunge wa Port Said, Albadry Farghali, aliwalaumu maafisa wa usalama.
"Walikuwa wapi haya yote yakitokea?"
"Watu wa Mubarak bado wako uongozini. Kiongozi wa utawala ameng'atuliwa, lakini watu wake bado wapo madarakani", alielezea kupitia televisheni.
"Usalama uko wapi? Serikali iko wapi?"
Mjini Cairo, mwamuzi alisitisha mechi nyingine, alipoarifiwa juu ya ghasia za Port Said.
Jambo ambalo liliwafanya mashabiki kuchoma moto sehemu fulani za uwanja.
Mechi zote za ligi kuu zimefutiliwa mbali, na bunge jipya la Misri siku ya Alhamisi litakutana katika kikao cha dharura kuujadili msiba huu.
Wednesday, February 1, 2012
Botswana na Mali kufa na kupona leo kombe la mataifa ya Afrika
KOCHA wa Botswana, Stanley Tshosane amesisitiza timu yake haitaibeba Mali watakapokutana leo kwenye mchezo wa mwisho wa Kundi D. Baada ya kuitoa jasho Ghana kabla ya kufungwa bao mmoja, Pundamilia hao kutoka Gaborone walisambaratishwa 6-1 na Guinea katika mchezo wao wa pili.
Botswana walioweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza kufuzu kucheza fainali za mataifa ya Afrika mwaka huu, watasubiri miujiza pekee kuweza kufuzu kuingia robo fainali. Kilichokuwa cha muhimu kwenye mchezo wa leo dhidi ya Mali huu ndio utakaoamua timu mbili za mwisho zitakazofuzu kushiriki nane bora.
Hakutakuwa na kuwabeba. Tulifanya kazi kufika hapa, hivyo Mali nao wanapaswa wafanye kazi kubaki kwenye mashindano, alisisitiza Tshosane, ambaye mkataba wake unamalizika mwezi huu.
Tutacheza kama tulivyopanga. Tutaingia kwenye mchezo huo kwa umakini mkubwa kwa sababu tunataka kuondoka Gabon na ushindi.
Nao mabingwa mara nne wa michuano hiyo Ghana wanaopewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa wa michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, leo wanashuka dimbani kukamilisha mechi za makundi kwa kuumana na Guinea mjini, Franceville.Ghana ambayo inahitaji sare tu kujihakikishia nafasi ya kucheza hatua ya robo fainali, inaongoza Kundi D kwa kuwa na pointi sita kabla ya mechi ya leo.
Iwapo itashinda mechi ya leo itafikisha pointi tisa na hivyo kumaliza kundi lao bila kupoteza mchezo, lakini hata sare tu inaweza kuifanya kubaki kileleni mwa kundi .
Hata hivyo mechi hiyo inatarajiwa kuwa ngumu, kwani Guinea watashuka uwanjani kusaka pointi za kuwawezesha kucheza hatua ya robo.Guinea wanahitaji kushinda au sare iwapo Mali itafungwa na Botswana au timu hizo zikigawana pointi.
Hatua ya robo fainali ya michuano hiyo inatarajiwa kufanyika Jumamosi na Jumapili wiki hii, huku Zambia ikiwavaa Sudan na wenyeji Equatorial Guinea wakiwa na kibarua kizito mbele Ivory Coast.
Simba kuichezesha kwata Oljoro leo?
NYASI za Uwanja wa Taifa ulio kusini mwa jiji la Dar es Salaam leo zitakuwa katika msuguano mkali wakati vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba SC watakapokabiliana uso kwa uso na maafande wa JKT Oljoro.
Mbali ya vita hiyo kati ya Simba na JKT Oljoro inayofananishwa na ile 'takatifu' pia zitashuhudiwa harakati nyingine za ligi hiyo zikiendelea kwenye dimba la Uwanja wa Azam Complex ambapo African Lyon itakuwa ikipepetana na Polisi Dodoma.
Hata hivyo shughuli pevu inaonekana kusalia kwenye Uwanja wa Taifa, ambapo Simba yenye pointi 31 itakuwa inaukabili mtihani wa kusaka pointi tatu kutoka kwa Oljoro ambayo ipo Ligi Kuu kwa mara ya kwanza na ilianza msimu wa kwanza vizuri.
Simba inahitaji zaidi ushindi iwakimbie watani wao wa jadi Yanga waliofungana kwa pointi kileleni huku wakitofautiana kwa mabao ya kufunga na kufungwa.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga timu ya Simba ipo kambini katika hoteli ya Lamada tangu juzi na maamuzi hayo yalitokana na maombi ya wachezaji na benchi la ufundi kwa uongozi wa Simba.
Kimsingi mtanange huu unaonekana kuwa mzito kwa Simba hasa kwa kuzingatia wapinzani wao JKT Oljoro walio nafasi ya nne na pointi zao 26 nyuma ya Azam FC inayokamata nafasi ya tatu na pointi zake 29, pia watakuwa wakihaha kusaka pointi tatu kwa lengo la kupunguza pengo kati yake na walio juu.
Ukiondoa nia, sababu na uwezo wa kila timu wakati huu, kumbukumbu ya ushindi wa mabao 2-0 ilioupata Simba ikiwa ugenini katika pambano la mzunguko wa kwanza inaweza kuwa faida nyingine kwa kikosi hicho cha kocha Milovan Cirkovic kuondoka na pointi tatu.
Pia, kurejea kwa mshambuliaji wao Emmanuel Okwi ambaye ilielezwa alikuwa 'amejificha' nyumbani kwao Uganda kunaweza kuongeza morali katika kikosi cha Simba ambacho katika mechi kadhaa zilizopita kilionekana kumtegemea zaidi Felix Sunzu ambaye sasa ni majeruhi ambapo hali hiyo ilisababisha Cirkovic awatumie zaidi viungo wake Haruna Moshi'Boban' na Uhuru Selemani katika kupachika mabao.
Nayo African Lyon ikiwa katika nafasi ya 10 na pointi zake 14 na ambayo hivi karibuni imekumbwa na wasiwasi baada ya Mkurugenzi wake, Rahim Zamunda kutishia kuiondoa kwenye ligi, kocha wake Jumanne Chale ameweka wazi kuwa kikosi chake kitaendelea kupigana hadi tone la mwisho ili kuhakikisha kinaondoka katika hatari ya kushuka daraja na leo kinatarajia kuibuka na ushindi kitakapokwa kikipambana na JKT Ruvu.
"Pamoja na hali ya wasiwasi iliyowakumba wachezaji wangu bado tutaendelea kupambana hadi tone la mwisho, nimewaambia vijana wangu waelekeze akili zao uwanjani kwani ndio kazi yao hivyo sina shaka katika kutekeleza wajibu wao kesho(leo),"alisema Chale.
Kwenye kambi ya kikosi cha Polisi Dodoma kinachokamata nafasi ya 13 mbele ya Villa Squad inayokamata mkia kwa pointi 10 kocha wa timu hiyo, Rashid Chama amesema ushindi walioupata katika mechi yao ya mwisho dhidi ya JKT Ruvu umewaongezea nguvu na sasa watahakikisha wanaitwanga Lyon.
"Sitaki masikhara tena kwa sababu nafasi tuliyopo sio nzuri, tumelitumia dirisha dogo kwa umakini, tuna watu kama Aman George atashirikiana na wengine kuipa timu pointi tatu na hili litathibitika kesho(leo) tutakapowanyuka African Lyon," alisema Chama
Tuesday, January 31, 2012
HOW TO READ BAR CODES
ALWAYS READ THE LABELS ON THE FOODS YOU BUY--NO MATTER WHAT THE FRONT OF THE BOX OR PACKAGE SAYS, TURN IT OVER AND READ THE BACK---CAREFULLY
With all the food and pet products now coming from China, it is best to make sure you read label at the supermarket and especially Walmart (ASDA - US owned) when buying food products.
Many products no longer show where they were made, only give where the distributor is located.
The whole world is concerned about China-made "black hearted goods".
Can you differentiate which one is made in Taiwan or China ?
Can you differentiate which one is made in Taiwan or China ?
The world is also concerned about GM (Genetically Modified) foods; steroid fed animals etc in USA.
How to read Bar Codes .... interesting!
This may be useful to know when grocery shopping, if it's a concern to you.
If the first 3 digits of the barcode are 690 691 or 692, the product is MADE IN CHINA. 471 is Made in Taiwan .
If the first 3 digits of the barcode are 00 - 09 then it's made or sourced in USA
This is our right to know, but the government and related departments never educate the public, therefore we have to RESCUE ourselves.Nowadays, Chinese businessmen know that consumers do not prefer products "MADE IN CHINA", so they don't show from which country it is made.
However, you may now refer to the barcode - remember if the first 3 digits are:
690-692 ... then it is MADE IN CHINA
00 - 09 ... USA & CANADA
30 - 37 FRANCE
40 - 44 GERMANY
471 ... Taiwan
49 ... JAPAN50 ... UK
Subscribe to:
Posts (Atom)