Monday, February 6, 2012

GHANA yawasambaratisha waarabu yaifuata MALI nusu fainali

Wachezaji wa Ghana
Ghana "Black Stars"

Andrew Ayew,Johnson Ayew na wachezaji wengine wakishangilia goli lililopeleka msiba Tunisia

Ghana siku ya Jumapili ilifuzu kuingia nusu fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa kuishinda Tunisia magoli 2-1, katika muda wa ziada.
Kipindi cha kawaida cha dakika 90 kilipokwisha, timu hizo zilikuwa sare ya 1-1.
Nahodha wa Black Stars ya Ghana, John Mensah, alifunga bao la kwanza katika mechi hiyo, katika dakika ya tisa, kabla Sabeur Khalifa kuisawazishia Tunisia kabla ya kipindi cha kwanza kumalizika.
Bao la ushindi la Ghana lilifungwa na Andre 'Dede' Ayew.
Ghana 2-1 Tunisia

Katika historia ya mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, Tunisia haijawahi kuishinda Ghana.
Black Stars sasa wana matumaini ya kuendelea katika mashindano hayo na kupata ubingwa baada ya subira ya miaka 30, na watakutana na Zambia katika nusu fainali itakayochezwa uwanja wa Bata, siku ya Jumatano, tarehe 8 Februari, na ikiwa ni nusu fainali ya kwanza.
Mali na Ivory Coast nao watapambana katika nusu fainali ya pili siku ya Jumatano, katika uwanja wa Libreville.
Mali vs Gabon

Mali ilifuzu kuingia nusu fainali baada ya kuwashinda wenyeji Gabon 5-4 katika kupiga mikwaju ya penalti, baada ya mechi kumalizika kwa sare ya 1-1, na mabao kukosekana hata katika muda wa ziada.
Bao la Eric Mouloungui lilikuwa limewatia matumaini wenyeji Gabon, ambao mwaka huu wamekuwa wakishirikiana na Equatorial Guinea kuandaa mashindano ya mwaka huu.
Lakini kutangulia sio kufika, na Tidiane Diabate aliweza kuisawazishia Mali, zikiwa zimesalia dakika tano tu kabla ya mechi kumalizika.
Kwa kushindwa kufungana katika muda wa ziada, ilikuwa ni pigo kubwa wakati wa mikwaju ya penalti, Pierre-Emerick Aubameyang aliposhindwa kuifungia Gabon bao.
Gabon hawajawahi kufuzu kufika nusu fainali za mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika.
Idhaa ya Kiswahili ya BBC, ikishirikiana na redio washirika, itakutangazia nusu fainali kati ya Mali na Ivory Coast kutoka mjini Libreville, Gabon, katika matangazo maalum ya Ulimwengu wa Soka.
Charles Hilary vile vile atakutangazia mechi ya fainali ya mashindano hayo.

WEBB aibeba Man United kutoa sare na Chelsea

Howard Webb refa alieibeba Man United

Meneja wa Chelsea, Andre Villas-Boas, amelalamika kuhusiana na uamuzi wa Howard Webb, baada ya timu yake ambayo ilikuwa ikiongoza magoli 3-0, hatimaye ilipotoka sare ya magoli 3-3 na Manchester United katika mechi ya Jumapili.
Chelsea, ikichezea uwanja wa nyumbani wa Stamford Bridge, ilionekana kuelekea kupata ushindi, lakini kufuatia uamuzi wa refa Webb, Wayne Rooney aliweza kufunga magoli mawili ya penalti, na mchezo kubadilika.
Chelsea 3-3 Man United

Sare hiyo imeiwezesha Manchester United kupunguza tofauti kati yake na majirani Manchester City, na ambao wanaongoza ligi, kuwa pointi mbili tu kati yao.
"Penalti ya kwanza ilikuwa ni wazi, na hakuna la kusema, lakini ya pili, ni ya kutiliwa shaka kabisa", alielezea Villas-Boas.
"Sijui kama Howard Webb alikuwa katika nafasi muwafaka ya kuweza kuona vyema na kufanya uamuzi, lakini ni jambo la kutoridhisha kwa yeye kutoa penalti hiyo", alilalamika meneja wa Chelsea.
Villas-Boas aliongezea: "Sijui kama Howard alikuwa analipizia jambo fulani ambalo hakulifanya katika nusu ya kwanza, lakini uamuzi wake haukufaa".
Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson alisisitiza kwamba penalti zote mbili zilikuwa halali, na akielezea kwamba hata walistahili penalti zaidi, baada ya Gary Cahill kugongana na Danny Wellbeck katika kipindi cha kwanza.
"Tungeliweza kupata jumla ya nafasi nne za penalti", alisema.
Katika mchezo wa awali wa Jumapili, Papiss Demba Cisse, aliyesajiliwa na Newcastle, na akicheza mechi yake ya kwanza, aliweza kuifungia timu yake bao, na wakapata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Aston Villa.
Newcastle sasa imo katika nafasi ya tano katika ligi kuu ya Premier kufuatia ushindi huo.
Cisse alisajiliwa kwa pauni milioni 10.
Mapema mwenzake kutoka Senegal, Demba Ba, alikuwa ameiwezesha timu yake kupata bao la kwanza katika mechi hiyo, lakini Robbie Kean akaisawazishia Villa.

Friday, February 3, 2012

How to Plan For Valentine's Day

Happy Valentines Day
Valentine's Day is a festival that cheers love and romance. Valentine's Day is an occasion to openly express love to your beloved and what better way to do so than by means of flowers! Every year lovers use flowers as the medium to convey their feelings for their Valentine. Of all the flowers used on a Valentine's Day most commonly used Valentine's Day flower is the red Rose as this flower is traditionally recognized as the symbol of love and passion. A single perfect red rose clubbed with Baby's Breath flower is considered to a red rose by the florists and is the most sought after Valentine's Day flowers.


One of the most popular way of celebrating this festival is to go for a date with your sweetheart. Those in love start thinking about unique Valentine's Day gifts ideas days in advance to ensure a romantic and memorable time with their beloved. On the other hand, the singles who haven't got a date start registering themselves for various online and offline dating services so that they do not miss out on the fun the couples enjoy on a Valentine's Day. In case you are looking for perfect Valentine's Day gifts idea, here are some tips to inspire the creativity cells in your brain and heart !!

Other flowers that are popular on the occasion of Valentine's Day include tulips, daffodils and irises. Many people also prefer a mixed flower bouquet on Valentine's Day, as it looks colourful and attractive. Most lovers try and avoid silk or artificial flowers as nothing matches the beauty and aroma of fresh flowers. Besides it is said that fresh flowers represent the genuine feelings of love towards the recipient. No, wonder florists across the world do a roaring business on Valentine's Day.

Another unique custom of Feast of Lupercalia was the pairing of young boys and girls who otherwise lived a strictly separated lives. During the evening, all the young marriageable girls used to place a chit of their name in a big urn. Each young man used to draw out a name of a girl from the urn and became paired with that girl for the rest of the year. Quite often, the paired couple would fall in love and marry.

Best Valentine Gifts to Make the Day Special















Valentines Day is dedicated to the celebration of love and is characterized by beautiful Valentine gifts. The most popular symbols like heart-shaped curios, doves and the figure of the winged cupid are popular as valentine gifts for the loved one. There are other all time favorite valentine gifts like Chocolates, confectionary, red roses and perfumes. Well thought out gifts offer an exhilarating gifting experience. Yes, innovative gifts that speak more than a hundred words make great valentine gifts. Choosing to shop online also lets you send valentine gifts to India or any other destination in a hassle free manner.

Valentines Day is round the corner, and the event calls for celebration with innovative
Valentine roses. Valentines day gifts make the day all the more special. It is a great way of celebrating togetherness and showing your loved ones how much they mean to you. The Valentine gifts catalog at online and physical gift stores are profuse with innovative Valentines day gifts ideas to liven up the day. There are many Valentine day gifts that are integral to this special day. Valentine Chocolates are amongst the best loved presents and they come in beautiful heart shaped moulds. Valentine cakes, flowers, perfume and Valentine soft toys are amongst the contemporary Valentine gifts. You may have loved ones living in different parts of the world. There are many ways to send valentine gifts to India or abroad and online marts have emerged as a good option.

Valentine soft toys:Soft toys have a unique quality to make your loved one feel special. Yes, they make ideal Valentine gifts for women and are a great way to express true love. A cuddly teddy bear with a valentine outline, mushy message or a simple red rose makes a very good gift. Valentine soft toys may also include valentine figurines, the beautiful white dove or the universal symbol of love the cupid. The valentine soft toys are profuse at online marts and one must be careful in choosing them right. The Valentine soft toys must ideally convey the same message of sentiment that one feels for the beloved. Online marts that have the option to customize these cuddly
Valentine day flowers are a good option. Besides, if you wish to send valentine gifts to India online marts offer good discounts and a wide catalog to choose from. Choose any of the Valentine soft toys and personalize them with suitable messages to convey your message of love this Valentines Day.

Valentine Chocolates:

Valentine chocolates are closely associated with celebrations as chocolates are a hot favorite amongst youngsters. The gifting culture is predominant amongst the younger generation and Valentine chocolates in different moulds make great Valentine gifts. Made to order chocolates are a favorite amongst revelers. Certain online marts cater to the rising need of made-to-order or personalized chocolates especially as Valentines Day gifts ideas. They are a great option if you wish to send valentine gifts to India.

The festival dedicated to people in love is much awaited. As shops spruce up with great gifts and greeting cards, take a look at the exclusive product display at online marts. The great discounts and innovative Valentine gifts will entice you to come back for more.

Thursday, February 2, 2012

VALENCIA 1-1 BARCELONA

SIMBA YAENDELEZA DOZI YAIKANDAMIZA JKT OLJORO 2-0
















Uhuru Selemani wa Simba akifanya vitu vyake

JKT Oljoro jana walishindwa kwenda sambamba na kasi ya Simba waliocheza pungufu sehemu kubwa ya mchezo na kukubali kipigo cha mabao 2-0, shukrani kwa mabao ya kipindi cha pili ya mshambualiaji, Emmanuel Okwi yaliyoihakikishia Wekundu hao wa Msimbazi pointi zote tatu.
Katika mechi hiyo iliyochangamshwa na ushindani mkubwa toka timu zote mbili kwenye Uwanja wa Taifa, ilishuhudia kiungo wa Simba Haruna Moshi 'Boban' akionyeshwa kadi nyekundu isiyo na onyo baada ya kumrushia teke la makusudi mchezaji wa Oljoro, Omary Mtaki dakika ya 42.
Mwamuzi Isiaka Shirikisho wa Tanga, ambaye alionekana kushindwa kwenda sawa na kasi ya mchezo, pia aliwalima kadi za njano Omary Khasim wa JKT kwa kumchezea vibaya Haruna Moshi, kisha Kelvin Yondani na Jonas Gerald wa Simba kwa kuwachezea vibaya Kalege Mgunda na Nyambele.
Ushindi huo umeifanya Simba kuendelea kubaki kileleni mwa msimamo kwa kufikisha pointi 34, tatu mbele ya mahasimu wao Yanga watakaoshuka dimbani mwishoni mwa wiki hii.
Katika mechi hiyo ambayo Simba walitumia zaidi viungo kufanya mashambulizi, JKT Oljoro waliofungwa 2-0 mzunguko wa kwanza, itabidi wajilaumu kwa kushindwa kutumia ya fursa ya wapinzani wao kucheza pungufu kupata ushindi.
Kocha wa Oljoro, Ally Kidy mara baada ya mchezo alikiri kuzidiwa na Simba, lakini akawalaumu wachezaji wake kushindwa kutumia vizuri nafasi nyingi za kufunga walizopata na pia kutumia mwanya wa Simba kucheza pungufu.
Simba walitawala dakika 20 za mwanzo wa mchezo na kukosa mabao kadhaa, huku Oljoro wakirejea mchezo dakika 10 za mwisho za kipindi hicho baada ya awali kufunikwa sehemu ya kiungo.
Mabadiliko yaliyofanywa na Simba kumtoa Gervais Kago na kuingia mshambualiaji wa kimataifa kutoka Uganda, Okwi katika kipindi cha pili ndiyo yaliyoipa ushindi timu hiyo.

Okwi, ambaye pengo la kutokuwapo kwake katika mchezo wa kwanza lilionekana wazi, alitumia dakika 15 tangu aingie uwanjani kuipeleka Simba mbele kwa bao zuri akimalizia pasi ya Uhuru Selemani.
Dakika nne baada ya bao hilo, Oljoro walikuja juu na kufanya shambulizi la nguvu ambalo nusura lizae bao la kusawazisha kufuatia piga nikupige kabla ya mabeki wa Simba kuokoa hatari.
Mchezaji Bakari Kigodeko wa Oljoro hatasahau nafasi ya wazi kufunga akiwa amebaki na nyavu na kisha kupiga mpira nje katika dakika ya 71.
Walikuwa Simba waliotawala mchezo bila kuonekana kama walikuwa pungufu uwanjani na kujipatia bao la pili dakika saba kabla ya filimbi ya mwisho baada ya Okwi kuinasa pasi ya Mafisango na kufunga bao hilo.
Kocha wa Simba Cirkovic Milovan aliwapongeza wachezaji wake kwa kuonyesha mchezo mzuri na kushinda mchezo huo pamoja na kwamba walicheza pungufu. "Matokeo mazuri kwetu, ni ishara ya kuwa tayari kwa ajili ya mechi dhidi ya Kiyovu ya Rwanda," alisema.

Katika mechi nyingine ya ligi hiyo iliyopigwa Mbagala, nje kidogo ya jiji kwenye Uwanja wa Azam, Chamazi kati ya African Lyon iliichapa Polisi Dodoma mabao 2-0.Mechi hiyo ilishuhudia timu zote zikishambuliana kwa zamu kipindi cha kwanza, huku Lyon wakionekana kufika zaidi langoni mwa wapinzani wao.
Wakicheza kwa kushambuliana, Semy Kessy aliifungia Lyon bao la kwanza dakika ya 30 kwa shuti kali lililomshinda kipa wa Polisi, Gerald Mwingira baada ya awali kuwalamba chenga mabeki wa timu hiyo.Lyon walijihakikishia pointi tatu ushindi kwa kufunga bao la pili kupitia Sunday Juma baada ya kushirikiana vizuri na Samuel Ngasa katika dakika ya 76.