Tuesday, June 26, 2012

STAR WA BONGO MOVIE FLORA MVUNGI KATIKA KASHFA YA UTAPELI WA 200,000/=


Flora Mvungi

Star maarufu katika tasnia ya filamu za kibongo "Bongo Movies" Flora Mvungi ameshutumiwa kupokea mlungula wa kiasi kadhaa unaofikia shilingi za kibongo laki mbili (200,000) kutoka kwa mtayarishaji wa filamu chipukizi aliejulikana kwa jina moja la Othman.

Akielezea mkasa huo wa "kupigwa" Tshs 200,000/= za kibongo na staa wa filamu nchini Mtayarishaji huyo wa filamu a.k.a Producer amesema Alikubaliana na Flora ampatie kiasi hicho ili aweze kushiriki katika filamu anayoiandaa inayoenda kwa jina la MZIWANDA. Othman anasema walipokubaliana alimtumia Flora mkwanja huo kwa njia ya Tigopesa, lakini ilipofika muda wa kuwa mahala pa kutayarisha filamu (Location) Staa huyo hakutokea kwa visingizio lukuki. Lakini Producer huyo akafunguka kuwa safari hii ilikuwa mara ya nne kuzinguliwa na Flora katika maswala mazima ya kufika eneo la tukio maarufu kama Location.

Producer Othman alipokuwa akihojiwa na kituo kimoja maarufu cha redio hapa nchini alifunguka hayo na ndipo mtangazaji wa kipindi hicho alipoamua kuwaunganisha kwa njia ya simu, katika hali ya mshangao staa huyo alikana kumfahamu Producer huyo wa movie za kibongo lakini alikiri kuwa kuna filamu ambayo aliitwa akashiriki lakini kutokana na sababu fulanifulani hakufika na akaahidi aitwe mambo yatakapokuwa tayari.
Utamu ukanoga pale mtangazaji alipomvutia kamba Flora Mvungi na kisha akamuuliza maswali kadhaa halafu akamuweka hewani wapeane makavu na producer, Hali ilikuwa ya majibizano makali Flora akikana kupokea mkwanja hali iliyoonekana kumkera zaidi Producer huyo na akisisitiza kuwa staa huyo asijifanye mjanja kwani yeye ana uthibitisho wa Message alizomtumia pesa ghafla Flora akakata simu nganjaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!! Hali hii iliacha SINTOFAHAMU ikiwa imetanda katika sakata hilo.

DOGO JANJA AFANYA KUFURU MLIMANI CITY, MANUNUZI MIL 2.5


Abdul Aboubakar Chande "Dogo Janja"

Unaweza usiamini na huenda ukahisi labda ni story za town, lakini ukweli ndio huo, Siku chache baada ya kutua Bongo na Pipa (Ndege) akitokea Kilimanjaro na kujiunga na kampuni ya Mtanashati Entertainments ya jijini, nyota wa Bongo Fleva , Abdul Abubakar Chande ‘Dogo Janja’ mwishoni mwa wiki iliyopita alisomea kisomo maalumu cha kuomba Mwenyezi Mungu amnyooshee mambo yake na "umatemate" zaidi pindi atakapoanza kushusha ngoma mpya.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa kisomo hicho kichoshudiwa na Teentz.com, Mkurugenzi wa kampuni hiyo Ostaz Juma na Musoma alisema kuwa wameamua kumfanyia kisomo hicho kwa lengo la kuweka kazi zote za Dogo janja mikononi mwa Mungu kwa kuwa wanaamini wapo watu ambao hawajafurahishwa na mpango mzima wa dogo huyo kurejea Bongo

Katika shopingi hiyo Dogo janja alitumia zaidi ya shilingi Milioni 2.5 za kibongo kununua vitu mbalimbali, kama Seti 5 za viatu, Suti 4, Jeans 10, T shirt 10,miwani 5, simu aina ya BlackBerry, Laptop na vitu vingine kibao .
Huku akionekana mwenye furaha kubwa Dogo Janja aliiambia Teentz.com kuwa amefuahi kwa kiasi kikubwa kwa yale yote ambayo Ostaz Juma na kundi zima la Mtanashati kwa yote wanayomfanyia hivi sasa kwani hatakuwa na malipo mengine zaidi ya kuwafanyia kazi nzuri zenye kiwango.

“Nina furaha sana, hakika namshukuru Ostaz kwa yote anayofanya kwangu sina la kusema zaidi wasubiri ngoma za kweli zitakazokuwa kama shukurani kwao kwa sababu ndiyo kitu pekee ambacho naweza kukifanya kwao” alisema Dogo Janja.


VENUS WILLIAM AONDOLEWA MAPEMA WIMBLEDON


Venus akirudisha mchomo kwa mpinzani wake Elena Vesnina

Bingwa mara tano katika mashindano ya tennis ya Wimbledon, Mmarekani Venus Williams, amesema hana nia ya kuachana na mchezo huo baada ya kuondolewa katika siku ya kwanza ya mashindano ya mwaka 2012 ya Wimbledon, katika raundi ya kwanza, alipopokea kipigo kitakatifu kutoka kwa mchezaji Mrusi, Elena Vesnina.
Venus, mwenye umri wa miaka 32, na anayeugua ugonjwa unaofahamika kama Sjogren's Syndrome, alishindwa 6-1 6-3 siku ya Jumatatu.
Mpinzani wake Vesnina amepangwa katika nafasi ya 79 katika orodha ya wachezaji bora zaidi wa tennis wa kike ulimwenguni.

Kiboko ya Venus Williams,Elena Vesnina akipeleka mchomo kwa Venus

"Haiwezekani nipumzike tu na kukata tamaa," alielezea Williams.

"Sina muda wa kujisikitikia. Hilo sio jambo zuri. Nitautumia muda wangu katika mawazo yanayonipa nguvu. Ninaupenda mchezo huu."

Mara ya kwanza Williams kushindwa katika raundi ya kwanza ilitokea mwaka 1997, wakati alipoingia pambano lake la kwanza la Wimbledon, na wakati huo alikuwa hata hayumo miongoni mwa wale waliopangwa katika mashindano hayo kama wachezaji bora.

Ni wanawake wawili tu ulimwenguni ambao wameshawahi kupata ubingwa wa Wimbledon mara nyingi kumshinda Williams, lakini tangu mwaka 2008, hajawahi kuibuka bingwa wa mashindano hayo.

Mara tu baada ya ushindi wake wa mwisho, iligunduliwa kwamba anaugua ugonjwa wa Sjogren's Syndrome, na ambao humfanya mgonjwa kujihisi ni mchovu mno, na katika sehemu mifupa inaungana, maumivu.

Ayaaaaaaaa nimechapwa!!!!!


Kudadekii leo Venus hutoki hapa!!

Venus Williams baada ya kupokea kichapo kitakatifu kutoka kwa Mrusi Elena Vesnina


Monday, June 25, 2012

EURO 2012 ITALIA YATINGA NUSU FAINALI WAKATI ASHLEY WAWILI WAKIIGHARIMU UINGEREZA


Barwuah Balotelli akipiga tik-tak ambayo ilipaa langoni mwa Uingereza

Gianluigi Buffon akiokoa mchomo wa Johnson ambao almanusra uzae bao kwa Uingereza

Timu ya soka ya Uingereza imetupwa nje katika mashindano ya Euro 2012, baada ya kunyukwa na Italia usiku wa Jumapili katika robo fainali, kwa changamoto ya mukwaju ya penalti 4-2 mjini Kiev, Ukraine, kufuatia muda wa kawaida na dakika 30 zaidi kumalizika kwa timu hizo mbili kutofungana.

Italia sasa itavaana na Ujerumani katika mechi ya nusu fainali.
Alessandro Diamanti alifunga bao la kuamua mshindi katika mikwaju hiyo ya penalti, baada ya Ashley Young na Ashley Cole kukosa kufunga mabao kupitia mikwaju waliyopiga.

Vijana wa meneja Roy Hodgson ilikuwa wazi walilemewa katika mchezo mzima, lakini ni hali ya imani na uvumilivu iliwafanya kuwa na matazamio ya kuishinda Italia.

Italia iliweza kugonga mwamba, na bao la Antonio Nocerino lilikataliwa baada ya mwamuzi kusema aliotea mpira.

Kadri mechi ilivyoendelea, ndivyo wachezaji wa England nao walionekana wachovu, na ikielekea walitazamia bahati zaidi kuliko kujitahidi kuimarisha kiwango cha mchezo wao, na penalti kwao bila shaka ikawa sio za kutegemewa tena.

Baada ya mechi, nahodha Steven Gerrard alisema: "Wachezaji walicheza kadri ya uwezo wao wote. Nilidhani tungelipata bahati katika mikwaju ya penalti, lakini mambo hayakuwa hivyo. Ukiongoza katika penalti, unashikilia matumaini kwamba mambo yatasalia hivyo, lakini Italia ndio waliokuwa na bahati. Vijana waliokuwa walinzi walifanya kazi nzuri mno, na kuiletea nchi fahari, lakini tunarudi nyumbani na mioyo ya huzuni, na hili ni jambo gumu kulikubali."

England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
Balotelli akijaribu kombora langozi mwa Uingereza bila matumaini
England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
Ngoma inogile Lescott na Balotelli
England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final

England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final

England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
Imooooo..Joe Hart akichumpa kuokoa penati bila mafanikio
England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
Wachezaji wa Uingereza waliokosa penati A.Cole na A.Young na wenzao wakiwa hawaamini kilichojiri katika dimba la Olympic mjini Kiev

England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
John Terry akimtuliza Ashley Cole na Jermain Defoe akimtuliza Ashley Young baada ya Ashley wawili kukosa mikwaju ya penati katika mtanange dhidi ya Italia

Mikwaju ya penati Uingereza na Italia

Friday, June 22, 2012

CHRISTIANO RONALDO AIPELEKA URENO NUSU FAINALI EURO 2012


Gooooooooo!! Christiano Ronaldo akitupia kambani kwa kichwa maridadi

Woyoooooo nimemaliza kaziiiiiii!!! Ronaldo akishangilia goli lililoipeleka Ureno nusu fainali

Mshambuliaji hodari Christiano Ronaldo aliwaridhisha mashabiki wa Ureno kwa kucheza vizuri sana usiku wa Alhamisi, na juhudi zake zimeiwezesha Ureno kuifumua Jamhuri ya Czech bao 1-0 na kufanikiwa kutinga katika hatua ya nusu fainali.

Ronaldo, ambaye alifunga magoli mawili wakati Ureno ilipocheza na Uholanzi, aliweza kuichachafya ngome ya Czeck na mashuti mawili kugonga mlingoti wa goli.

Hatimaye aliweza kutupia kambani kwa kichwa, huku zikiwa zimesalia dakika 12 kabla ya mechi kumalizika, na kipa Petr Cech akiweza kuufikia mpira, lakini hakuweza kuuzuia kutokana na nguvu nyingi zilizotumiwa na Ronaldo.


Peter Cech akikabiliana na Christiano Ronaldo

Ilikuwa dhahiri kwamba wachezaji wa Czech waliingia uwanjani wakiwa na nia ya kuimarisha ngome yao, na wala sio kushambulia, na kamwe hawakumtisha kabisa kipa wa Ureno.

Ureno sasa itakutana aidha na Uhispania au Ufaransa katika juhudi za kufuzu kwa fainali.

Bila shaka timu ambayo itakutana na Ureno itakuwa na wasiwasi ni vipi itaweza kumzuia Ronaldo, ambaye baadhi ya wadau wa soka wanasema kwa sasa ndiye mchezaji bora zaidi barani Ulaya.

Kiungo Miguel Veloso akimrukia Ronaldo kwa furaha

Portuguese Football Fans AFP/Getty Images
Mashabiki wa Soka wa Ureno wakiwa katika viwanja vya Campo Pequeno Square jijini Lisbon,Ureno wakiangalia mechi ya nusu fainali kati ya chama lao na Jamhuri ya Czech mechi iliyokuwa ikipigwa katika dimba la Warsaw nchini Poland. 

PORTUGAL  1-0  CZECH REPUBLIC

Thursday, June 21, 2012

MREMBO WA SIKU

Mena Suvari

On Saturday evening, Mena Suvari put a sexy spin on the little black dress when she showed up at the Motion Picture & Television Fund gala in a barely-there Maria Lucia Hohan cocktail frock

WALIOONGOZA KWA KUTUPIA KAMBANI KATIKA HATUA YA MAKUNDI EURO 2012


1-(3)  Alan Dzagoev wa Urusi ameshatupia kambani mara mpaka kumalizika kwa hatua ya makundi, amekwishapoteza matumaini ya kunyakua daruga la dhahabu kwani Urusi haikufanikiwa kufuzu katika hatua ya robo fainali katika kundi A.


2-(3) Mario Gomez wa Ujerumani amekwisha kutupia kambani mara tatu na ana matumaini makubwa ya kuibuka kidedea kwa kutupia kambani katika michuano ya EURO 2012 baada ya Ujerumani kufuzu katika hatua ya robo fainali baada ya kuibuka namba moja katika kundi B ikijikusanyia pointi zote 9 ikifuatiwa na Ureno iliyomaliza kwa pointi 6.


3-(2) Andriy Shevchenko nahodha wa Ukraine ambao ndio wenyeji wenza wa michuano ya EURO 2012 ametupia kambani mara 2 na kwa bahati mbaya wenyeji hao wametupwa nje ya michuano hiyo baada ya kumaliza katika nafasi ya 3 katika kundi D, Uingereza na Ufaransa zikipenya kwa hatua ya robo fainali. 


4-(2) Christian Ronaldo wa Ureno amekwisha tupia mara 2 na ana matumaini makubwa ya kuwa kinara wa mabao katika mashindano hayo baada ya Ureno kufuzu robo fainali baada ya kushika nafasi ya pili katika kundi B nyuma ya Ujerumani.


5-(2) Fernando Torres wa Uhispania ametupia mara 2 na anaweza kuendelea kutupia baada ya timu yake ya Uhispania kufuzu kwa hatua ya robo fainali baada ya kuongoza kundi C.


6-(2) Francesc Fabregas wa Uhispania amekwishatupia kambani mara 2 matumaini ya kuendelea kutupia yanabaki baada ya timu yake kutinga katika hatua ya robo fainali ikiongoza kundi C na sasa atachuana na mhispania mwenzake Fernando Torres katika mbio za kuvaa daluga la dhahabu.


7-(2) Mario Mandzukic wa Croatia ametupia mara 2 na ndio mwisho baada ya Croatia kushindwa kuvuka hatua ya makundi kuelekea robo fainali za michuano ya EURO 2012 ikimaliza katika nafasi ya 3 kundi C


8-(2) Michael Krohn-Dehli wa Denmark ametupia kambani mara 2 na matumaini ya kuvaa daluga la dhahabu yaliyeyuka pale Denmark waliposhindwa kufuzu kwa hatua ya robo fainali baada ya kushika nafasi ya 3 kundi B


9-(2) Nicklas Bendtner wa Denmark ametupia mara 2 na ndio amemaliza hapo baada ya Denmark kuburuzwa nje ya michuano hiyo katika kundi B


10-(2) Olof Mellberg wa Sweden nae amefanikiwa kutupia kambani mara 2 na kutokana na ukweli kwamba Sweden haijafuzu kwa hatua za robo fainali matumaini yake ya kunyakua kiatu cha dhahabu yamezikwa rasmi.


11-(2) Petr Jiracek wa Jamhuri ya Czech ametupia mara mbili na itambidi asubiri miaka minne ijayo ili aendelee kuwania ufungaji bora kwasababu Timu yake imeshindwa kufuzu kwa hatua ya robo fainali za EURO 2012.


12-(2) Vaclav Pilar wa Jamhuri ya Czech nae ametupia kambani mara 2 lakini kutokana na timu yake kushindwa kufuzu kwa hatua ya robo fainali sasa matumaini yake ya kutwaa daluga la dhahabu yameishia hapo.


13-(2) Zlatan Ibrahimovic mshambuliaji wa Sweden ametupia kambani mara 2 na ki ukweli kabisa kama Sweden ingesonga katika hatua ya robo fainali basi huenda angetupia mara nyingi zaidi kutokana na uwezo alionao, lakini sasa ndio basi tena Sweden wameshatupwa nje baada ya kushika mkia katika kundi D.