Tuesday, July 10, 2012
MPAMBANO WA SOKA WABUNGE WA SIMBA NA YANGA KATIKA PICHA
Timu za wabunge wa Simba na Yanga wakiimba wimbo wa Taifa kabla ya mpambano
Waamuzi wa mpambano huo wakipiga picha ya pamoja na manahodha wa timu zote mbili
Wabunge wa Simba katika Dua kabla ya mtanange kuanza
Wabunge wa Yanga nao wakipiga dua kabla ya mtanange kurindima
Mashabiki wakiwahi mpambano
Mtanange umeanza
Mwamuzi wa mtanange huo Athuman Kazi akifuatilia kwa karibu kuhakikisha haki inatendeka
Mh Zitto Kabwe wa Simba akitoa pasi murua kama Iniesta vile!
Mbunge wa Simba akitiririka na kabumbu
Katibu uenezi wa CCM Nape Nnauye akifuatilia mpambano wa Wabunge wa Simba na wale wa Yanga katika dimba kuu la Taifa jijini Dar es salaam
Benchi la ufundi la Wabunge wa Simba wakifuatilia mpambano
Benchi la ufundi la Wabunge wa Yanga wakiongozwa na kocha mkuu mpya wa Yanga
Mbunge wa Yanga akiwa hoi bin taaban
Mbunge wa Yanga akijaribu kuihadaa ngome ya wabunge wa Simba
Hali tete mlinda mlango wa wabunge wa Yanga baada ya kichapo kwa njia ya matuta 3-2
Wera weraaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!! wabunge wa Simba hatimae waliwachapa wa Yanga katika matuta baada ya dakika 90 kumalizika kwa sare ya 0-0
Nani kama Simbaaaa woyooooo woyooooooooo
Hakunagaa zaidi ya Simba hakunagaa, hakunaaa hakunaaaa hakunaaaaaaaaaa!!!
Weraaaaa tupishe tupiteeee, tupisheeeee tupishe tupiteeeeeeee..Wabunge wa Simba wakiongozwa na Mh Zitto Kabwe na William Ngeleja kuserebuka baada ya kuwaangushia kisago wenzao wa Yanga kwa mikwaju ya penati 3-2
Mpambano Wabunge SIMBA Vs YANGA
Katika mtanange huo baada ya dakika 90 na kipyenga cha mwamuzi Athumani kazi kupulizwa matokeo yalikuwa ni 0-0. Mpambano huo wa kufurahisha na kusisimua uliopigwa katika dimba kuu la Taifa jijini Dar es salaam ikiwa ni katika mchezo wa hisani kukusanya pesa kuchangia ujenzi wa mabweni kwa shule za sekondari nchini!
shukrani za pekee kwa waandaaji wa tamasha hilo ambalo pia liliwakutanisha wasanii wa Bongo flava na Bongo Movie hali kadhalika mpambano wa Masumbwi kati ya wasanii maarufu nchini na wenye kutengeneza vichwa vya habari katika redio na magazeti mbalimbali hapa nchini, ni Wema Sepetu na Jaquiline Wolper ambapo katika mpambano mpambano huo uliodumu kwa raundi mbili matokeo yalikuwa ni droo hakukuwa na mshindi.
KEITA AONDOKA BARCELONA NA "NDOO"14 HUKU TITO AKIMRITHI PEP GUARDIOLA
Seydou Keita
kiungo wa Mali Seydou Keita amekihama klabu ya Barcelona baada ya kukipiga kwa miaka minne.
Katika muda huo wa miaka minne, Keita aliisaidia Barcelona kuzoa jumla ya vikombe 14.
Keita na Sanchez wakiwa wamebeba kombe wakikipiga Barcelona
Kwa wakati huu kuna fununu kwamba mchezaji huyo wa Mali huenda anahamia klabu moja ya Uchina, Dalian Aerbin
Tito Vilanova kocha alierithi mikoba ya Pep Guardiola
Tito Vilanova akiwa na Pep Guardiola
Monday, July 9, 2012
RATIBA KOMBE LA KAGAME 2012

KAGAME CUP 2012 FIXTURE
1-Sat. 14th July 1 APR vs WAU SALAAM Uwanja wa Taifa 2pm
2-YANGA vs ATLETICO Uwanja wa Taifa 4pm
3-Sun. 15th July 3 AZAM vs MAFUNZO Chamazi 4pm
4-Mon. 16th July 4 VITA CLUB vs PORTS Uwanja wa Taifa 2pm
5-SIMBA vs URA Uwanja wa Taifa 4pm
6-Tue. 17th July 6 ATLETICO vs APR Uwanja wa Taifa 2pm
7-WAU SALAAM vs YANGA Uwanja wa Taifa 4pm
8-Wed. 18th July 8 VITA CLUB vs URA Uwanja wa Taifa 2pm
9-PORTS vs SIMBA Uwanja wa Taifa 4pm
10-Thu. 19th July 10 ATLETICO vs WAU SALAAM Uwanja wa Taifa 2pm
11-MAFUNZO vs TUSKER Uwanja wa Taifa 4pm
12-Fri. 20th July 12 PORTS vs URA Uwanja wa Taifa 2pm
13-YANGA vs APR Uwanja wa Taifa 4pm
14-Sat. 21st July 14 AZAM vs TUSKER Uwanja wa Taifa 2pm
15-SIMBA vs VITA CLUB Uwanja wa Taifa 4pm
16-Sun. 22nd July REST DAY
QUARTER FINALS
Mon. 23rd July 16 B2 vs C2
17 A1 vs C3
Tue. 24th July 18 C1 vs A2
19 B1 vs A3
Wed. 25th July REST DAY
SEMI FINALS
Thu. 26th July 20 Winner 16 vs Winner 17
Thu. 26th July 21 Winner 18 vs Winner 19
Fri. 27th July REST DAY
FINALS AND 3rd PLACE PLAY OFFS
Sat. 28th July 22 Loser 20 vs Loser 21
23 Winner 20 vs Winner 21
DIVA AFUNGUKA ANAETAKA KUMUOA AWE NA MILIONI 500 TASLIMU
Loveness Love "Diva"
Mtangazaji maarufu wa radio moja ya jijini Diva Loveness Love,Clouds Fm amefunguka na kusema kuwa anaetaka kumtoa katika geti la Mzee Malinzi ambaye ni baba yake pale msasani basi kidume huyo atahitajika kuwa na Milioni 500 Taslimu.
Mtangazaji huyo wa kipindi cha ala za roho cha Clouds FM kinachoanza saa nne za usiku alikuwa akifanya mazungumzo na mtangazaji mwenzake Adam Mchomvu katika kipindi cha XXL mida ya saa 9:30 mchana Diva alifunguka kwa kujiamini kuwa mwanaume anaetaka kumuoa ni lazima awe na milioni 500 taslimu,ndipo atamng'oa kwa Mzee Malinzi, katika mazungumzo hayo Diva alisisitiza na alipoulizwa kama hatotokea akaema basi...tungoje mimi na wewe hatujui yetu macho na masikio. Dunia hii.
Diva katika possssssssssssss

LIL WAYNE AHUDHURIA NDOA YA MAMA YAKE MZAZI
Lil Wayne na Birdman wakiwa kanisani wakati mama yake Lil wayne akifunga ndoa
Lil Wayne a.k.a Lil Wiz akiwa na kidume chake Sarah kanisani
Binti yake Lil Wiz aitwae Reginae akiwa na mtoto wa kiume wa Birdman katika shughuli hiyo ya kukata na mundu
Padri akimfungisha ndoa mama yake Lil Wayne na baba yake mpya.
Birdman akimuongoza mama yake Lil Wayne Ms Jacinta
Lil Wayne akiwa na mama yake aitwae Jacinta katika ndoa ya Ms Jacinta na Avery
Binti yake Lil Wayne Reginae akiwaongoza wenzake kwenda kusimamia harusi ya bibi yake
Vijidume vya Lil Wayne,Sarah na Nivea vikitinga kanisani kusimamia harusi ya bibi yao
Burudani kabambe iliporomoshwa kanisani utaaaaaaaaaaaaaamu
Thursday, July 5, 2012
HASHEEM THABEET AULA OKC KUVUNA DOLA 880,000
Hasheem akifanya majamboooozz!!!
Nyota wa kikapu Mtanzania Hasheem Thabeet ameula baada ya kupata dili murua la kuhamia timu ya mpira wa Kikapu ya Oklahoma City Thunder (OKC) akitokea Portland Trail blazers ambapo kabla ya Portland alitokea Memphis Zote za nchini Marekani.
Habari zinasema Hasheem amesaini mkataba wa 'nyundo' mbili na anatarajiwa kuvuna umatemate wa kiasi cha dola za kimarekani 880,000 kwa mwaka a.k.a Nyundo.
Haya sasa vijana waliopo katika mchezo wa kikapu fuateni nyayo hizo.

Basketball sio lelemama lazima uwe umeshiba


Hasheem akiwa na rais wa Tanzania Mh Jakaya Mrisho Kikwete alipotembelea Ikulu jijini Dar es salaam
Menu time!!!!
Subscribe to:
Posts (Atom)