Friday, September 7, 2012

NYAAAUUUU...SIMBA YARARURIWA NA SOFAPAKA


Akuffor wa Simba akijaribu kufunga bila mafanikio

Mabingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Simba S.C wamejikuta wakipelekeshwa puta na kupata kipigo cha fedheha cha mabao 3-0 kutoka kwa Sofapaka inayoshiriki Ligi Kuu ya Kenya katika mechi yao ya kimataifa ya kirafiki kwenye dimba kuu la Taifa jijini Dar es Salaam leo.
Sofapaka walipata bao la kuongoza katika dakika ya 18 kwa njia ya penati baada ya beki mpya wa kimataifa wa Simba, raia wa Mali
Komalbil Keita kufanya madhambi  ndani ya eneo la boksi na mshambualiaji wa zamani wa Yanga, John Baraza akatupia mpira wavuni kwa shuti kali lililomshinda kipa Juma Kaseja.

Safu ya mabeki wa Simba iliendelea kuwapa hofu mashabiki wa klabu yao baada ya Pascal Ochieng na keita kujichanganya na kuwapa wageni bao la pili katika dakika ya 57 kupitia tena kwa Baraza.


Kikosi cha Simba kinachonolewa na Mserbia Milovan Cirkovic kiliwasononesha mashabiki wao waliofika  kuwashangilia baada ya mabeki wake kuruhusu bao la tatu katika dakika ya 66 kwa shuti la Joseph Nyaga aliyemalizia vyema kazi nzuri iliyofanywa na mchezaji wa zamani wa klabu ya Azam, Osborne Monday.

Safu ya kiungo iliyotarajiwa kuwa 'kali' ya Salim Kinje na Mwinyi Kazimoto ilishindwa kuonyesha makali mbele ya Sofapaka, kama ilivyokuwa kwa viungo-washambuliaji Haruna Moshi 'Boban', Mrisho Ngassa aliyetua kwa kishindo katika timu hiyo akitokea Azam na mshambuliaji wao Christopher Edward aliyeibuka kinara wa kupachika mabao katika michuano iliyomalizika hivi karibuni ya Ligi ya Super8 na kuisaidia Simba B kutwaa ubingwa.

Awali, katika dakika ya 35, Simba walipata pigo baada ya Straika wao tegemeo kwa sasa, Mghana Akuffor kuumia vibaya baada ya kuchezewa faulo na Antony Kimani.


Alianguka uwanjani na kushindwa kupumua kwa muda, lakini alipozinduka alitaka kuendelea kucheza kabla daktari wa Simba, Cosmas Kapinga kumkataza na hivyo kutolewa uwanjani.


Kipigo cha leo kimemuacha kocha Milovan katika wakati mgumu wa kukiboresha kikosi chake kwani zimebaki siku chache kabla ya kushuka dimbani kuvaana na Azam wiki ijayo katika mechi ya kuwania Ngao ya Jamii kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


Kabla ya kuivaa Sofapaka leo, Milovan aliahidi soka safi na kusema kwamba mechi hiyo ndio kipimo chao kabla ya kucheza dhidi ya Azam kwani wameshajifua vya kutosha, hasa walipokuwa katika kambi yao jijini Arusha.


Licha ya ubutu wa safu yao ya ushambuliaji, rekodi ya mabeki wa Simba pia haionyeshi kuwa wako 'ngangari' vya kutosha tangu aondoke Kevin Yondan aliyejiunga na Yanga, kwani penati waliyoruhusu leo dhidi ya Sofapaka ni ya pili katika mechi zao nne za kirafiki za hivi karibuni.


Penati nyingine ilishasababishwa na Pascal Ochieng. Mabeki hao vilevile wana rekodi ya kujifunga mara mbili katika mechi hizo nne za kujipima nguvu, mabeki hao ni mabeki Juma Nyosso na Keita.




Mshambuliaji wa Simba Akuffor akitolewa baada ya kuumia

Christopher Edward wa Simba akijaribu kumhadaa mlinzi wa Sofapaka Antony Kimani aliemuumiza Akuffor

Rekodi katika mechi hizo zinaonyesha kuwa beki Ochieng aliyeondoka AFC Leopards ya Kenya kutokana na kukosa namba katika kikosi cha kwanza, alisababisha penalti moja wakati Keita ambaye ametua kutoka Mali, amejifunga goli moja na kusababisha penati moja huku Nyosso naye akijifunga moja katika mechi hizo nne ambazo Simba waliwafunga JKT Oljoro 2-1, wakawabwaga Mathare United 2-1 pia na kutoka sare ya 1-1 dhidi ya Sony Sugar ya Kenya.

Akuffor ndiye ambaye ameonekana kuwa mchezaji 'jembe' baada ya kufunga katika mechi zote tatu za kwanza kabla ya jana kuumia.

VIKOSI
Simba: Juma Kaseja, Shomari Kapombe, Amir Maftah, Pascal Ochieng, Komalbil Keita, Mwinyi Kazimoto, Salim Kinje, Haruna Moshi ‘Boban’, Edward Christopher, Daniel Auffor na Mrisho Ngassa.

Sofapaka: Duncan Ochieng, Antony Kimani, James Situma, Edgar Ochieng, George Owino, Collins Okoti, Osborne Monday, Humphrey Mieno, Kago Danson, Joseph Nyaga na John Baraza.

Monday, September 3, 2012

ROBIN VAN PERSIE APIGA "HAT TRICK"

Robin Van Persie Robin Van Persie of Manchester United celebrates the winning goal during the Barclays Premier League match between Southampton and Manchestrer United at St Mary's Stadium on September 2, 2012 in Southampton, England.
Van Persie
 
Robin van Persie amegeuka kuwa kipenzi cha mashabiki wa klabu yake mpya kwa kuiokoa Man.United alipofunga matatu mwenyewe kumuondolea maradhi ya moyo Sir Alex Ferguson kunako mechi yake ya 1,000th akiiongoza Manchester United kama meneja.

Mdachi huyo alitanguliza la kichwa kutokana na kona iliyochongwa na Nani katika mda wa ziada kuokoa jahazi.

Southampton ilipata bao la kuongoza kupitia Rickie Lambert kabla ya Morgan Schneiderlin kupata la pili pia la kichwa katikati ya magoli ya Van Persie ya kusawazisha.

Uhodari wa Van Persie uliwekwa kwenya mizani alipokosa mkwaju wa peneti mnamo dakika 88 wakati United ikidorora 2-1.

Kwa menejawa Southampton Nigel Adkins dakika za majeruhi zilikua kama mwaka wenye machungu kutokana na jinsi vijana wake walivyoweza kuidhibiti United na mabao ya haraka haraka mawili bila shaka yalimuumiza.

Kwa mashabiki wa United, matokeo haya ni sehemu ya malipo ya kitita cha milioni 24 za pauni za Uingereza zilizomleta United kutoka Arsenal.
Robin Van Persie Robin Van Persie of Manchester United scores the winning goal during the Barclays Premier League match between Southampton and Manchestrer United at St Mary's Stadium on September 2, 2012 in Southampton, England.
Van Persie akitupia goli la kwanza
Robin Van Persie Robin Van Persie of Manchester United scores his second goal during the Barclays Premier League match between Southampton and Manchestrer United at St Mary's Stadium on September 2, 2012 in Southampton, England.
Van Persie akitupia goli la pili
Robin Van Persie Robin Van Persie of Manchester United celebrates the winning goal during the Barclays Premier League match between Southampton and Manchestrer United at St Mary's Stadium on September 2, 2012 in Southampton, England.
Van Persie akishangilia bao
Robin Van Persie Robin Van Persie of Manchester United scores the winning goal during the Barclays Premier League match between Southampton and Manchestrer United at St Mary's Stadium on September 2, 2012 in Southampton, England.
Mpira uliopigwa na Van Persie ukitinga wavuni kuandika goli la tatu "Hat Trick" na la mwisho la Man United
Southampton vs Man United

ARSENAL YAANZA LIGI YAIDUNGUA LIVERPOOL 2 KAVU


Kocha wa Arsenal Arsene Wenger akizungumza na waandishi wa habari baada ya mechi.

Arsenal imepata ushindi wake wa kwanza katika ligi ya Premier ya nchini Uingereza msimu huu baada ya kuidungua Liverpool 2-0 nyumbani kwao.
Hii ndio mara ya kwanza kabisa kwa Liverpool kuanza msimu kwa kichapo cha mabao 2-0 katika uwanja wao katika kipindi cha miaka 50,Magoli yote mawili ya Arsenal yalitupia kambani na wachezaji wapya Santi Cazorla na Lukas Podolski .

Mshambuliaji wa Ujerumani Podolski ndiye alikuwa wa kwanza kuipatia Arsenal bao katika dakika ya 31. Na katika dakika ya 68 Cazorla alipeleka kilio na kubadili ubao wa matangazo kuwa 2-0.
pod_2326586c.jpg
Podolski akitupia goli la kwanza

Podolsi akishangilia goli

Magoli hayo pia ndio yalikuwa ya kwanza kwa Arsenal tangu msimu huu uanze kwani katika mechi zao mbili za awali walitoka sare ya 0-0 na wapinzani wao.

Kufuatia ushindi huo Kocha wa Arsenal alisema kuwa uimara wa vijana wake unaongezeka katika kila mechi na kuwa amefurahishwa na matokeo ya timu yake.

Baada ya kucheza mechi tatu, Liverpool ambayo iko nchini ya mkufunzi mpya Brendan Rodgers ina pointi moja peke yake.

Hii inaweza kufananishwa na matokeo mabaya ya timu hiyo katika msimu wa mwaka 1962-63 chini ya Bill Shankly.

Katika mechi hii washambulizi Luis Suarez na Fabio Borini hawakuwa na kubwa uwanjani.

Nae mchezaji mpya wa kiungo Nuri Sahin wa Liverpool pia hakuonyesha makeke yake uwanjani.

Santiago Carzola akishangilia baada ya kutupia goli la pili


Golikipa wa Arsenal Manone akishangilia ushindi


Patashika Steven Gerrard na Abou Diaby

Liverpool 0-2 Arsenal

Thursday, August 30, 2012

REAL MADRID YATIA KIBINDONI KOMBE LA SUPERCOPA


Wachezaji wa Real Madrid wakishangilia na kombe la SUPERCOPA
 
Timu ya soka ya Real Madrid ya Uhispania imeanza kuweka kabatini makombe ya nchini Uhispania baada ya kuichabanga Barcelona magoli 2-1 katika dimba lao la nyumbani,Santiago Bernerbeu ambao pia ni mji mkuu wa Uhispania.

Ushindi wa Real Madrid wa mabao 2-1 ulifanya matokeo ya jumla kuwa 4-4 baada ya mechi ya kwanza iliyopigwa Nou Camp Barcelona kuilaza Rea Madrid kwa kamba 3-2, Na sasa Real Madrid imepata ushindi kutokana na kufanikiwa kutupia kambani magoli mengi ugenini.
Hi-res-150649730_crop_exact
Kazi moja tu Pique na Pedro

Katika mchezo huo wa jana Barcelona iliyoonekana kutokuwa imara sehemu ya Ulinzi na kuwaruhusu Real Madrid kutupia kambani goli 2 za fastafasta, Real Madrid walianza mchezo huo kama kwamba waliambiwa waingie kuharibu mipango na utulivu wa mtindo wa uchezaji wa Barcelona na walifanikiwa kwa 100%, na kwa kutumia udhaifu wa Safu ya Ulinzi ya Barcelona iliyokuwa chini ya Pique na Mascherano mafundi Christiano Ronaldo na Higuain walifanikiwa kuipatia Real Madrid magoli muhimu katika mchezo huo ingawa Higuain mchezo ulionekana kutokumkubali kwa sana.

Makosa ya kizembe yaliyofanywa na Adriano ya kupewa kadi nyekundu yaliigharimu Barcelona kucheza pungufu kwa dakika za mwisho za kipindi cha kwanza na zote za kipindi cha pili.

Real walikuwa wa kwanza kutupia kambani kupitia Higuian katika dakika ya 11 na dakika 9 baadae Christiano Ronaldo aliipatia Real goli la pili kabla ya Leonel Messi kutupia kambani kwa "free kick" ya umbali wa mita 30 dakika chache kabla ya kwenda mapumziko.

Christiano Ronaldo akijiandaa kuachia "fataki" na kufunga goli la pili.
 
Christiano Ronaldo akishangilia baada ya kutupia kambani goli la pili dhidi ya Barcelona

Higuain Akishangilia goli la kwanza


Luka Modric akiangalia kombe la kwanza kulitwaa akiwa Real Madrid limeshikiliwa na Pepe na Ronaldo.

Hi-res-150521084_crop_exact
Mambo magumu..nisepe mie" ndivyo anavyoonekana kuwaza Leonel Messi

Katika mchezo wa jana timu zote ziliingiza majembe waliyoyasajili kutoka Ligi kuu ya Uingereza, Barcelona wakimuingiza Alexander Song aliesajiliwa kutoka Arsenal na Real Madrid wakimuingiza Luca Modric aliesajiliwa kutoka Tottenham Hotspurs zote za Uingereza.

Wednesday, August 29, 2012

RATIBA LIGI KUU UINGEREZA(BARCLAYS PREMIER LEAGUE)

Barclays Premier League | RATIBA


Kwa saa za A.Mashariki (EA, GMT+3)

Saturday 01 September 2012
West Ham v Fulham Upton Park 14:45
Tottenham v Norwich White Hart Lane 17:00
Swansea v Sunderland Liberty Stadium 17:00
West Brom v Everton The Hawthorns 17:00
Wigan v Stoke The DW Stadium 17:00
Man City v QPR Etihad Stadium 19:30

Sunday 02 September 2012
Liverpool v Arsenal Anfield 15:30
Southampton v Man Utd St. Mary's Stadium 18:00
Newcastle v Aston Villa Sports Direct Arena 18:00

Saturday 15 September 2012
Norwich v West Ham Carrow Road 14:45
Man Utd v Wigan Old Trafford 17:00
QPR v Chelsea Loftus Road Stadium 17:00
Stoke v Man City Britannia Stadium 17:00
Aston Villa v Swansea Villa Park 17:00
Arsenal v Southampton Emirates Stadium 17:00
Fulham v West Brom Craven Cottage 17:00
Sunderland v Liverpool Stadium of Light 19:30

Sunday 16 September 2012
Reading v Tottenham Madejski Stadium 18:00

Monday 17 September 2012
Everton v Newcastle Goodison Park 22:00

Saturday 22 September 2012
Swansea v Everton Liberty Stadium 14:45
West Ham v Sunderland Upton Park 17:00
Newcastle v Norwich Sports Direct Arena 17:00
Wigan v Fulham The DW Stadium 17:00
Chelsea v Stoke Stamford Bridge 17:00
West Brom v Reading The Hawthorns 17:00
Southampton v Aston Villa St. Mary's Stadium 17:00

Sunday 23 September 2012
Liverpool v Man Utd Anfield 15:30
Man City v Arsenal Etihad Stadium 18:00
Tottenham v QPR White Hart Lane 18:00

Saturday 29 September 2012
Arsenal v Chelsea Emirates Stadium 14:45
Sunderland v Wigan Stadium of Light 17:00
Stoke v Swansea Britannia Stadium 17:00
Reading v Newcastle Madejski Stadium 17:00
Norwich v Liverpool Carrow Road 17:00
Fulham v Man City Craven Cottage 17:00
Everton v Southampton Goodison Park 17:00
Man Utd v Tottenham Old Trafford 19:30

Sunday 30 September 2012
Aston Villa v West Brom Villa Park 18:00

SUPER CUP LEO MADRID Vs BARCA PUYOL KUVAA "MASK"

Carlos Puyol
 
Nahodha wa Barcelona Carlos Puyol anatarajiwa kukipiga katika mechi ya Super Cup pale Barcelona itakapomenyana na Real Madrid katika mchezo wa marudiano katika dimba la Santiago Bernabeu ambalo ni Dimba la Real Madrid baada ya mchezo wa kwanza uliopigwa katika dimba la Nou Camp,ambapo wenyeji Barcelona waliibuka na ushindi wa 3-2 Dhidi ya Real Madrid.
 
Puyol anatarajiwa kukipiga katika mechi hiyo ya leo lakini atahitajika kuvaa kofia ya kuzuia taya"MASK" kutokana na kusumbuliwa na mifupa ya taya aliyoumia hivi karibuni,Alisema kocha wa Barcelona Tito Vilanova. Puyol aliumia katika mechi ya ligi dhidi ya Osasuna siku ya jumapili na Barca walishinda 3-2, Ingawaje alifanya mazoezi na wenzake siku ya jumanne lakini kocha amesema kucheza au kutocheza itajulikana Jumatano(leo).
 
"Kesho(leo) asubuhi tutaangalia anaendeleaje, na tutamsikiliza Daktari anasemaje hatuwezi kuhatarisha hali ya Puyol"Alisema Vilanova.
 
Taarifa kutoka Barca zinasema Kiungo Mholanzi Ibrahim Affelay aliomba kuondolewa katika safari ya mechi hiyo ili aweze kuangalia maendeleo yake, Affelay aliefanyiwa oparation mwezi Oktoba 2011 kabla ya kujiunga na Timu ya taifa ya Spain katika michuano ya EURO 2012 amesema atahakikisha anapata namba ya kudumu katika kikosi cha Barcelona.
 
Afellay mwenye miaka 26 amehusishwa na uwezekano wa kuhamia Liverpool katika ligi kuu ya Uingereza"Barclays Premier League".

FULHAM YAMRUHUSU DEMBELE KUKIPIGA TOTTENHAM

Moussa Dembele
 
Klabu ya Tottenham Hotspurs imepata idhini ya kuendelea mbele na mchakato wa kumnasa kiungo wa kati wa klabu ya Fulham, Moussa Dembele, kufuatia vilabu hivyo kuafikiana juu ya malipo ya kumnunua mchezaji huyo.

Mchezaji huyo wa Ubelgiji yuko katika mwaka wake wa mwisho katika mkataba wa kukipiga Fulham inayochezea uwanja wa Craven Cottage, na hakushiriki katika mechi ya kombe la Capital One dhidi ya Sheffield Wednesday, wakati timu yake ilipochapwa.

Meneja wa Fulham, Martin Jol, amesema Dembele, mwenye umri wa miaka 25, yumo katika vipimo vya afya yake ndani ya klabu ya Tottenham.

Dembele alijiunga na Fulham kutoka klabu ya Uholanzi ya AZ Alkmaar, kwa gharama ya pauni milioni 5, mwaka 2010.

Hayo yakiendelea, Fulham imekuwa katika hali ya kushauriana na Kieran Richardson, baada ya kuelewana na Sunderland kuhusu kitita kinachohitajika kumpata mlinzi huyo.

Meneja wa Sunderland, Martin O'Neill alithibitisha kwamba tayari wamekubaliana juu ya kiwango cha pesa ambazo Fulham watatoa kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27.