Thursday, December 6, 2012

WIMBO WA LEO- Nataka Kulewa (Diamond )


PATA COVER ZA UKURASA WAKO WA FACEBOOK (Timeline cover) ZA MWAKA 2013




Coundown New Year 2013 Facebook FB Timeline Covers








































happy new year 7







MAKALA YA KUUKARIBISHA MWAKA 2013


Zikiwa zimesalia siku 25 kumaliza mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka 2013 hatuna budi kumshukuru mwenyezi mungu muumba wa mbingu na ardhi na kila kitu kilichomo ndani yake kwa kutuwezesha kufikia mpaka hapa tulipo leo hii na tumuombe atujaalie kuuona mwaka mpya wa 2013.

Tutumie wakati huu ambao bado tuna baraka zake kwa kutuwezesha kupumua mpaka hivi sasa katika maombi, yatupasa kumuabudu kila mtu kwa wakati wake na kwa dini yake pasipo kumkwaza mtu mwingine. Tutumie muda huu kuomba msamaha kwa wale wote ambao kwa namna moja au nyingine umewakosea na vivyo hivyo usipokee tu msamaha nawe pia uwasamehe wote waliokukosea kwa namna moja au nyingine na hata kama hawajakusamehe kwa yale uliowakosea.

Ni muda mzuri wa kuwa karibu na familia na kujadili masuala yanayohusu familia yako na jamii inayokuzunguka, Kutafakari nini kimefanyika katika mwaka huu 2012 ambao kwa unyenyekevu tuna uaga na kuukaribisha mwaka mpya wa 2013 na nini kitafanyika katika mwaka mpya 2013.

Mimi binafsi napenda kumshukuru mwenyezi mungu kwa kuniwezesha kuwa hai mpaka dakika hii ninayoitumia kuandika makala hii,Kumshukuru kwa kuniwezesha kutimiza malengo fulanifulani katika mwaka wa 2012 na kunipa uwezo wa kuwa na mipango mipya kwa mwaka ujao wa 2013 na ninamuomba anisimamie na kuniongoza kufanikisha mipango yangu  ya siku za usoni.

Napenda nitumie fursa hii nikiwa kama binadamu wa kawaida ninaamini kuwa katika maisha yangu ya kila siku ninafanya mema na pia ninayo mabaya ninayoyafanya aidha kwa kujua au kutokujua na kuna watu wanaokwazika na mabaya hayo,nina imani kama nimekukosea aidha kwa makusudi au kwa bahati mbaya ni kwasababu mimi ni binadamu na sio mkamilifu na kwa kulitambua hilo ninaomba MSAMAHA kwa wale wote niliowakosea mpaka kufikia leo hii tukijiandaa na kuupokea mwaka mpya wa 2013. Kwa moyo mkunjufu bila kumung'unya maneno wala bila kupepesa macho na bila kukunjakunja vidole ninasema kwamba wale wote walionikosea NIMEWASAMEHE.

SISI sote hapa duniani ni ndugu na binaadamu wote tuko sawa tofauti yetu ni katika rangi ya ngozi,dini,Utaifa,Makabila,Maumbo na haiba. Hapa duniani tunapita safari yetu ni moja na njia ya kufanikisha safari hiyo ni KIFO. Hatuna budi kupendana,kuthaminiana na kusaidiana katika nyakati zote za shida na raha.

Kama mtanzania ninawaomba watanzania wote tutumie fursa hii pia kuiombea nchi yetu iweze kuwa katika UTULIVU tulio nao nasi kwa pamoja tudumishe AMANI na UPENDO tulionao. Akhsante kwa muda wako ulioutumia kusoma makala hii Mungu akubariki sana na akulinde na mabaya, akutangulie uweze kufika 2013.

Khalid Japhary Gomeka,
jiffjeff@yahoo.com
www.facebook.com/KhaledDeGomeka
www.twitter.com/KhaledDeGomeka
+255 712 18 45 98
+255 688 29 27 27

NI KITIMTIM NUSU FAINALI TUSKER LEO, TANZANIA MACHO KWA USO NA UGANDA,ZANZIBAR USO KWA MACHO NA KENYA


MABINGWA watetezi, Uganda na jirani zao Kenya watakuwa na kibarua kizito mbele ya Tanzania Bara na Zanzibar kwenye nusu fainali itakayochezwa leo kwenye Uwanja wa Nambolee, Kampala.

Uganda 'The Cranes' ilikata tiketi hiyo baada ya kuwafunga Ethiopia mabao 2-0, huku Harambee Stars ikiwalaza Malawi kwa bao 1-0.

Awali katika mechi ya robo fainali iliyochezwa mwanzoni, kiungo wa zamani ya Yanga na Simba, Mike Baraza aliiyeingia akitokea benchi aliifungia Kenya 'Harambee Stars' bao pekee katika dakika ya 57 baada ya kuunganisha kwa kichwa shuti la mbali mita 25 la Abdalla Juma na kumpoteza kipa wa Malawi, Charles Swini.

Kwa ushindi huo sasa Harambee Stars watakuwa na kibarua kigumu mbele ya Zanzibar Heroes inayosaka ubingwa wa pili wa michuano hiyo tangu walipofanya hivyo mwaka 1995 hapo Uganda.

Wakati huo huo;Kocha wa Kilimanjaro Stars, Kim Poulsen amemsifia kiungo wake Mwinyi Kazimoto kwa kusema ni mchezaji mwenye akili nyingi na mchezeshaji bora kabisa.

Kauli hiyo ya Poulsen imekuja baada ya Mwinyi kutoa pasi zote mbili zilizozaa mabao mawili yaliyoipa Stars ushindi wa mabao 2-0 katika pambano la robo fainali dhidi ya Rwanda.

Kim alisema kuwa Kazimoto ni kiungo kikuu cha matokeo mazuri ya timu yake kutokana na aina ya uchezaji wake aliodai ni wa kutumia akili zaidi.

Wednesday, December 5, 2012

SOMA BARUA YA WENGER ALIYOWAANDIKIA MASHABIKI WA ARSENAL




Wenger: 'We have to find a solution'
Dear Arsenal supporter,

We were not creative or sharp on Saturday.

Swansea had a lot of possession so we tried to change things and took a lot of risks. In the end it turned against us and looking back maybe we should have been more cautious and at least secured a 0-0 draw.

Overall the quality of our game was not there. It was frustrating because we lacked decisiveness and creativity. It is true that Swansea deserved to win the game.

I knew Swansea were a good side and before the game I was concerned that we could be a bit jaded because we had many players who had played a lot of hard games recently. But we were guilty of losing the game at the moment when we should not have lost it.

It is a challenging time but we are in this job to turn things around, and I am confident we will because of the quality of the players and the spirit we have in the team. It is a good time to stick together.

Away from home we are quite consistent and our results are mainly positive. But at home we have not produced the performances since the beginning of the season that you would expect from us, and that is where we have to find a solution.

I am often asked about the January transfer window and the support from the board is there to spend the money if we find the players. But we have a lot of important games coming up. We'll decide on our targets in January but we have to find solutions before then.

At the moment there is uncertainty among the fans, they do not have complete confidence that we will win the games. But the results show that it is difficult for everybody at the moment - even those who invested a lot of money.

We have to keep the focus, the desire and the ambition, and turn it on. That's how it works during the season. You cannot always jump to definitive conclusions from one game.

Saturday's defeat affects the thinking for Olympiacos. There are many players who need a rest, because they are on the verge of getting injured. Some played with knocks against Swansea.

It's important that we do well in Greece but, away from home, I'm not too concerned. We look like we play a little bit with the handbrake on at home. It's not fluent. There might be a psychological component in there as well.

Finally, I would like to wish Peter Hill-Wood a speedy recovery after he was admitted to hospital on Friday. I hear he is recovering well and my thoughts, along with those of everyone at the Club, are with Peter and his family at this time.



Thanks for your support.

Arsene Wenger's signature
Arsène Wenger

KEEP FIGURE DO EXERCISE



Wanawake wengi wanapenda kuwa na miili "shape" kama hizi lakini wao hukimbilia kufanya diet ya vyakula bila kuzingatia mazoezi yanayojenga mwili.
Unatakiwa ufanye Diet ukiwa katika mazoezi maalum ya kujenga mwili, Ni hatari kufanya diet ya vyakula kwa kujinyima na mwisho wa siku unausababishia mwili maradhi yatokanayo na ukosefu wa aina fulani ya virutubisho vinavyopatikana katika vyakula.
FANYA MAZOEZI+DIET(MLO SAHIHI)= GOOD FIGURE(SHAPE)