Monday, March 12, 2012

Chelsea yazinduka usingizini,Liverpool yapokea kichapo kutoksa kwa Sunderland


Didier Drogba akiwa katika harakati za kufunga na kufanikiwa kuipatia goli Chelsea


Drogba akishangilia goli dhidi ya Stoke City nyuma ni Sturridge na Juan Mata
Chelsea 1-0 Stoke City

Didier Drogba umaliziaji wake maridadi umeihakikishia ushindi ingawa mwembamba Chelsea dhidi ya Stoke City iliyokuwa ikicheza pungufu ya mchezaji mmoja katika pambano la kwanza la Roberto di Matteo kusimamia akiwa meneja wa muda Chelsea katika Ligi Kuu ya England.
Stoke walicheza karibu mchezo wote wakiwa na wachezaji 10 baada ya Ricardo Fuller kuoneshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja kwa kumtimba pajani Branislav Ivanovic.
Chelsea mipira yao iligonga mwamba mara mbili lakini iliwabidi wawe waangalifu kuikabili Stoke City iliyokuwa ikijihami vizuri.
Lakini Drogba hatimaye akamaliza kazi baada ya kumzunguka mlinda mlango Asmir Begovic baada ya kupokea pasi ya Juan Mata na kupachika bao lake la 100 tangu aanze kucheza Ligi Kuu ya England.
Hali ya kusua-sua kwa Liverpool kwenye ligi imeendelea tena baada ya kuchapwa na timu iliyoonesha ari ya kusaka ushindi ya Sunderland.
Baada ya kosakosa za kipindi cha kwanza, Sunderland walifanikiwa kuongoza kwa kupachika bao baada ya mkwaju wa Fraizer Campbell kuzuiwa na mlinda mlango Pepe Reina kabla ya Nicklas Bendtner kuuwahi na kuutumbukiza wavuni.
Liverpool waliwaingiza Steven Gerrard na Andy Carroll lakini mabadiliko hayo hayakuzaa matunda kwa upande wa wao.

Niclas Bendtner akishangilia goli alilofunga dhidi ya Liverpool

Sunderland 1-0 Liverpool

Sunderland walijihami vyema kulinda bao lao moja dhidi ya Liverpool ambao nusura wangesawazisha.
Junior Hoilett akifunga mabao mawili ameisaidia timu yake ya Blackburn kupanda juu kutoka eneo la hatari la kuteremka daraja na kuicha Wolves wakicheza uwanja wa nyumbani wakiendelea kusuasua eneo la kuteremka daraja wakiwa nafasi moja tu kutoka mkiani.
Mashabiki wa Wolves walifanya maandamano kabla ya mchezo dhidi ya Afisa Mtendaji Mkuu wa klabu yao ya Wolves Jez Moxey kwa kumteua Terry Connor kushikilia nafasi ya umeneja na hatimaye wakashuhudia timi yao ikiporomoka kwa kuonesha kiwango cha chini.
Hoilett alifunga bao lake la kwanza baada ya kumiliki mpira wa kimo cha mbuni na kuachia mkwaju kutoka upande wa kona na kuingia moja kwa moja wavuni.
Na baadae mshambuliaji huyo akafanikiwa kufunga bao lake la pili kwa mkwaju wa yadi 25 mara tu baada ya kuanza kipindi cha pili.
Kufungwa huko kumeicha Wolves nafasi ya 19, nafasi moja tu kutoka mkiani wakiwa wamepata ushindi wa mchezo mmoja tu katika mechi 14 za Ligi zilizopita.
Bao la kwanza la Andreas Weimann la Ligi Kuu ya England liliipatia ushindi Aston Villa dhidi ya Fulham waliokuwa wakicheza kwa kiwango cha juu na hatimaye wakamaliza kwa huzuni katika uwanja wa Villa Park.
Villa walimiliki mchezo katika kipindi cha kwanza huku Gabriel Agbonlahor nusura angepachika bao.
Marc Albrighton alipiga mkwaju uliogonga mwamba katika dakika za mwanzo za kipindi cha pili na baadae Damien Duff wa Fulham mkwaju wake nao ukagongwa mwamba. Hadi mwisho Aston Villa 1 Fulham 0.
Meneja wa QPR Mark Hughes aliachwa asifahamu la kufanya baada ya kushuhudia timu yake ikinyimwa ushindi baada ya bao la dakika za mwisho la Ivan Klasnic kuipatia ushindi wa mabao 2-1 Bolton.
QPR ilitakiwa kuwa mbele kwa bao moja kipindi cha kwanza lakini mpira wa kichwa aliochonga Clint Hill haukuhesabiwa bao licha ya mpira kuonekana umevuka mstari.
Bolton iliongoza kwa bao la kwanza lililofungwa kwa kichwa na Darren Pratley kabla Djibril Cisse kusawazisha kwa mkwaju wa karibu, ingawa baadae picha za televisheni zilizokuwa zikirudiwa zilionesha alikuwa ameotea.
Lakini bao la dakika za mwisho la Klasnic aliyepokea pasi murua kutoka kwa Ryo Miyaichi na kufanikiwa kumpita mlinda mlango Paddy Kenny, liliitoa Bolton kutoka eneo hatari la kuteremka daraja.

Friday, March 9, 2012

WENGER AOPOA "JEMBE" KUTOKA F.C COLOGNE

Lukas Podolski
Kifaa kipya kitakachotua Arsenal Lukas Podolski

Klabu ya Arsenal imeafikiana na mshambuliaji wa Ujerumani Lukas Podolski kutoka klabu ya Cologne, BBC Michezo imefahamu.
Kwa mujibu wa taarifa Arsenal italipa pauni za Uingereza £10.9m kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 kwa mkataba wa miaka minne akilipwa pauni £100,000 kila wiki.

Thursday, March 8, 2012

HAPPY WOMENS DAY

MBWANA SAMATTA YUKO JUU ATIKISA NYAVU HUKO MBUJI-MAYI


Mbwana Samatta mfungaji wa goli pekee na la ushindi la TP Mazembe dhidi ya S.M Sanga Balende

MBWANA Samatta ameendelea kudhihirisha kuwa ni moto wa kuotea mbali katika kuzifumania nyavu, baada ya kuifungia timu TP Mazembe bao pekee katika ushindi wa 1-0 dhidi ya timu ya S.M Sanga Balende.
Mechi hiyo ya Ligi Kuu ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (Super League) ilichezwa mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Kumbuji- Mayi, kilomita 1000 kutoka jiji la Lubumbashi.

Mbwana alifunga bao hilo dakika 48, kutokana na krosi ya Kilitcho Kasusula aliyeingia kipindi cha pili dakika ya 46 kuchukua nafasi ya Ngandu Kasongo.
Muda huo ndiyo aliingia Mtanzania mwingine, Thomas Ulimwengu kuchukua nafasi ya Yannick Tusilu.
Baada ya mchezo huo, rais wa klabu hiyo, Moise Katumbi aliwapongeza wachezaji wake kwa ushindi huo mgumu.
Haya ni mafanikio mengine kwa Samatta akiwa na TP Mazembe na ndiye anaongoza kwa ubora kwenye timu hiyo tangu msimu mpya wa ligi uanze.

Hivi karibuni, Kocha wa timu ya Taifa (Taifa Stars, Jan Poulsen alimtema nyota huyo chipukizi kwenye kikosi cha Stars kwa maelezo kwamba hajitumi anapoitwa kuchezea timu hiyo.

Tuesday, March 6, 2012

Balanced Diet For Maintain Balanced Weight

There are several different diets around currently which can allow it to be quite difficult to decide which one is suitable for you. Some diet plans target reduced fat, some insist lower calorie consumption will be your best option. You can also find others that require that you reduce carbohydrates. A certain diet plan appears to mix aspects of at least two other popular weight loss plans and states to generate the best fat reduction weight loss system around. However, do any of these diets actually work, and they’re any of these fad diets?

Learning about a balanced diet growing up was easy. The food pyramid was standard, and also you knew to have a diet a whole lot of grains, some fruits and veggies, a little meat and dairy, and avoid the sugars and fats. However, as science and medicine have evolved, the concept of a balanced diet has changed. Why can it matter? Why should you care? These are also fair questions. This article will explain why a balanced diet is important, and ways for anyone to accomplish one.

First, you have to realize that a balanced diet is incredibly important. A primary reason that everybody thinks of first when thinking about balanced diet is your weight. If executed properly, particularly with exercise, well balanced diet can assist you maintain a healthy weight. Should you need to lose weight, well balanced diet may help.

However, the benefits of the balanced diet extend far beyond weight. Eating the right amounts of the right types of food can also develop your energy. The correct blend of nutrition can give you vitamins and minerals that will reduce your possibilities of suffering from cardio disease, diabetes and cancer. It has even been suggested that a balanced diet can improve your mood! All of these life is huge benefits to eating well balanced diet, regardless of how obnoxious you may get the idea or execution.

BALANCED DIET
Depending on balanced diets is the best and the most natural way to maintain good shape and also have direct control on weight. You need not spend extra bucks on weight loss or weight loss plans and also have to apply techniques for reducing calories if you shape your way of life with a balanced diet.

FORMULATING THE BALANCED DIET CHART
You might be tuned in to the basic nutrients the body requires. The chart is a ready-made one. But the proportion of each nutrient to make a balanced diet for an adult is important. What’s the key source of energy? Of course the carbohydrates leading to fat and then you require some proteins for growth. Vitamins and minerals are available the next category but they are essential on your well being.
More or less this is possibly the division pattern of your nutrients. You can consume a diet where the amount of carbohydrates can be up to 60%. The proportion of fats should be 50 % the carbohydrates. Somewhat lower than that will be better. You could have protein in between 12 to 15 percent.

GAIN BALANCE WITH SELF CONTROL
The best assistance is self-help. This can be much good for your diets. Unless you are able to moderate your food cravings and feel the importance of controlling your weight loss ambitions from within it is very difficult to abide by the set norms of the balanced form of diet.

Proper meals should be broken into 4 to 5 parts each day and also you must eat during these parts. Break your day’s diet into breakfast, lunch, evening snacks and dinner. At the break of the day, you must consume the maximum and at going home time the diet should be minimum based upon very low calories. Don’t either keep your stomach empty or overeat a single time. They are very dangerous habits and increase your appetite.

WEIGHT LOSS-TRUTH ABOUT FAD DIETS
Many weight loss fat loss programs promise almost immediate results, in addition to a short time they could work. However, of course your reality takes hold. You start to realize there’s no way possible that you are able to remain on eating plans program during the course of your daily life. This can be something you are absolutely not forget, because preferably you need to be trying to find a balanced weight reduction and maintenance plan simply not only a fad diet.

Although a very low-calorie, a liquid diet plan or perhaps a diet program that only takes a short time may help you lose weight to start with, but you’ll certainly realize that your weight loss troubles revisit at a later stage. Rather than looking to find a miraculous cure, choose a fat reduction plan that may help you to accomplish your aims on a long term basis.

When contemplating participating in any weight loss system or diet program, constantly think about these questions. Am I Gonna learn a balanced, nutritionally sound diet regime through this diet? Is this a diet plan I’m able to follow long-term? And does this eating habits mix sensible eating with some physical exercise?

Once you discover a diet plan or weight loss system which fits all three of these questions, you may be aware you may have discovered the most effective diet plan to suit your needs. When it comes to all diet program, it is usually recommended that you simply see a medical professional previous to participating in any weight loss routine.

LIGI YA MABINGWA ULAYA ARSENAL KUPENYA KWENYE TUNDU LA SINDANO LEO?


AC Milan na Barcelona zina dalili kubwa ya kusonga mbele katika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya wiki hii, huku Zenit St Petersburg na Olympique Lyon zikiwa mashakani na zitajaribu kutetea ushindi mwembamba zilizopata katika mechi za awali.
AC Milan ambayo bado inasaka ubingwa wa Serie A, Kombe la Italia na Ligi ya Mabingwa Ulaya, inakwenda kuitembelea Arsenal katika Uwanja wa Emirates leo Jumanne ikiwa na akiba ya mabao 4-0 iliyoyafunga katika mechi ya kwanza ya hatua ya 16 bora.
Nao mabingwa watetezi, Barcelona, walishinda mabao 3-1 dhidi ya Bayer Leverkusen na hawana wasiwasi mkubwa kwa kuwa watawakaribisha wapinzani wao katika uwanja wa nyumbani.  

Kikosi cha AC Milan

Kikosi cha Arsenal

Huenda kukawa na stori tofauti leo Jumanne kwa kuwa Zenit ilishinda mabao 3-2 dhidi ya Benfica na huenda kibao kikageuka.
Vile vile Olympique Lyon ilipata ushindi mwembamba wa bao 1-0 katika mechi ya kwanza dhidi ya APOEL Nicosia, na kibaya ni kwamba safari hii itakuwa ugenini.
Kama APOEL itaingia robo fainali itakuwa ni timu ya kwanza ya Cyprus kufikia hatua hiyo na kama ikisonga mbele itazipiku klabu za Ufaransa ambazo zimejikuta zikianguka katika hatua hiyo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa misimu minne.
AC Milan na Zenit ni klabu ambazo zitasaka nafasi muhimu wiki hii huku zikiwa zinaongoza ligi.
Katika hatua nyingine, Arsene Wenger ana wasiwasi kama wanaweza kubadilisha mambo yaliyotokea katika Uwanja wa San Siro.

“Hatuishi katika dunia ya ndoto, ukiangalia kwa makini utaona ni kama tumeshatolewa,” alisema kocha huyo.
Kama AC Milan itafunga bao katika Uwanja wa Emirates maana yake ni kwamba Arsenal itatakiwa kufunga mabao sita ili kusonga mbele.

Habari mbaya kwa Arsenal ni kuwa AC Milan imekuwa ikifunga angalau bao moja katika kila mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu huu.
Katika hatua nyingine, kama Leverkusen ikitolewa itatoa wasiwasi kwa mashabiki wa Ujerumani ambao wanaweza kukosa wawakilishi katika hatua ya robo fainali kwa kuwa Bayern Munich ambayo nayo ipo katika hatua ya 16 bora ilifungwa na FC Basel bao 1-0 katika mechi ya awali.
Wasiwasi mkubwa upo kwa Leverkusen, ambayo itacheza na Barcelona kesho Jumatano kwa kuwa wapinzani wao ni balaa.
Kikosi cha Pep Guardiola hakijafungwa na vikosi vya Ujerumani katika mechi 16 walizokutana karibuni.
Benfica ilikuwa ikienda vizuri, ghafla ilianza kufanya vibaya baada ya kufungwa mabao 3-2 na St Petersburg wiki tatu zilizopita.