Saturday, March 31, 2012

WEMA AMWAGA CHOZI KWA KUTOLEWA NISHAI NA DIAMOND UKUMBINI KATIKA SHOW KALI MLIMANI CITY











Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya, Diamond Platinum akiwarusha mashabiki waliohudhuria katika tamasha lake la Diamond Are Forever lililofanyika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.











Diamond akitema cheche katika tamasha hilo














Diamond akitia mbwembwe mbele ya mashabiki wake














Dancers wakimpa support Diamond kufanya makamuzi










Sehemu ya umati wa mashabiki waliohudhuria show hiyo













Diamond akiendeleza makamuzi mbele ya mashabiki











Diamond anazidi kuwapagawisha mashabiki











Songombingo lilianzia pale Dimond aliposhuka stejini na kwenda kwenye meza waliyokaa wakina  Steve Nyerere na Mboni Masimba na ndipo walipompa t-shirt ambayo kwa mujibu wa udadisi na uchunguzi wa udadavuzi wa mambo wa Kajuna Blog, ilisemekana kuwa t-shirt hiyo ilikuwa inapicha ya mwanadada ambaye alikuwa akitoa na Diamond kwa sasa. Na ilikuwa ni maalum kwa ajili ya kumrusha roho Wema Sepetu.













Kazi ikaanza Mboni Masimba anamvalisha T'shirt yenye picha ya mpenzi mpya wa Diamond Steve Nyerere anatunza














Mhh........shabiki huyu akimtunza Diamond Dola za kimarekani watu vinywa wazi kulikoni?












Baada ya kutunza dolare za kutosha akaachia tabasamu nene














Wema nae akanyanyuka kwenda kutunza na pesa zikakataliwa














Wema kaganda akilazimisha Diamond apokee zile pesa bila mafanikio..ndio kwanzaaa kidume kiko bizeeeee!!!!!












Baada ya Diamond kugoma kutunzwa na Wema,Wema aliondoka stejini kwa hasira mithili ya Simba aliejeruhiwa









'Michuzi' aliyoikataa Diamond ikiwa stejini haijui iende wapi....













Hapo sasa 'Nimpende nani' uwanjani














Mlimbwende Jokate Mwegelo akijiachia na mashostito zake.














Diamond akimwaga mauno katika meza aliyokaa Jokate
















Mwanadadafada Mboni Masimba akiwa ametinga T'shirt yenye picha ya kifaa kipya cha Diamond














Baadhi ya wadau walimuita mshereheshaji wa show hiyo Taji Liundi akambembeleze Diamond aende kumuomba msamaha Wema lakini Diamond akasema 'nope'













Diamond akijiachia na warembo













Mashosti wakijaribu kumbembeleza Wema aache kulia kwani hayo yote ni ya dunia














Duuuh..Wema akizidi kumwaga chozi!
"sitakiiiiiiiiiiiii aaaaaaaaaaaaaaaaah aaaaaaaaaaaaaaaaaaaahhhh wakunifanyia hivi mimi jamani aaaaaaaaaaaaaaaaah aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaah diamond diamond aaaaahhh aaaaaahhhhhh!!















Ommy Dimpoz akitoa ushuhuda walipotokea na Diamond














Ushuhuda ulimgusa Diamond na kumwaga chozi "mhmhhmmmmmm"














Amini na Barnaba wakimpa shavu Diamond katika show hiyo.
















Hatimae Wema atuliza machungu kwa kumtunza Barnaba! "chukuaaa si anajifanya mjanja ataona akinitaka tena simtaki"


JOHN BOKO"ADEBAYOR" ACHOKA KUZOMEWA ASEMA 'STARS SASA BAAAAAAAASSSS'


JOHN BOKO 'ADEBAYOR'

Kinara wa mabao katika historia ya klabu ya Azam FC na kinara wa mabao katika ligi kuu ya Vodacom inayoendelea, John Raphael Boko 'Adebayor' ameliandikia barua shirikisho la soka nchini TFF ya kustaafu kuichezea timu ya Taifa 'Taifa Stars'. Huku akimuacha njia panda kocha wa kikosi hicho Jan Poulsen.

Boko amefikia uwamuzi huo kutokana na kuchoshwa na tabia za mashabiki wanao hudhuria mechi za Timu ya Taifa kumzomea kila anapopagwa.

Kwa mujibu wa Taarifa iliyowekwa kwenye ukurasa wa Azam FC ndani ya Facebook unasema kuwa Boko amewaomba TFF walikemee suala la wachezaji kuzomewa wakiwa na jezi ya Taifa.

"John Boko astaafu kuchezea timu ya taifa na sasa anaelekeza nguvu zake kwa timu yake ya Azam FC, kwa mujibu wa barua yake kwa TFF Boko amewaomba viongozi wa soka nchini kukemea tabia ya zomea zomea Kama walivyokemea uharibifu wa Mali za uwanja," ili eleza taarifa hiyo.

Katika blog ya Shaffih Sports imemnukuu Boko akisema; "Nimefikia maamuzi haya baada ya kufikiria sana, nimekuwa nikijitoa kwa hali na mali kulitumikia taifa langu lakini mashabiki wa timu yetu wanaona sifai, hivyo ni bora nijitoe au nistaafu kuichezea timu hiyo ili kuepekana na dhahama zao. Naitakia kila kheri timu yangu ya taifa naipenda na nitaendelea kuipenda siku zote."

Boko ni miongoni mwa washambuliaji bora nchini kwa kizazi hiki, na amekuwa chaguo la Poulsein toka aachane na washambuliaji wa TP Mazembe, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu kwa madai ya kwamba hawajitumi wakiwa na timu ya Taifa.

Kama Poulsein akiendelea na uwamuzi wake wakutowajumuisha washambuliaji hao wa TP Mazembe, ni wazi kuwa atakuwa na wakati mgumu katika kusaka washambuliaji watakao ziba mwanya huo.

LIGI KUU TANZANIA BARA NYASI KUTOA 'JASHO' LEO SIMBA Vs LYON, YANGA Vs COASTAL UNION


Kocha wa Simba S.C Milovan Cirkovic.

Mbilingembilenge za ligi kuu Tanzania bara zinaendelea leo ambapo kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, mabingwa watetezi Yanga watakakuwa wageni wa Coastal Union, huku vinara wa ligi Simba wakiwa na kazi mbele ya African Lyon kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo.

Mabingwa hao wa kihistoria wa Tanzania, timu za Simba na Yanga watashuka dimbani wakiwa na malengo tofauti kila mmoja, Yanga wenyewe wanajua kupoteza mchezo huo ni kupoteza ndoto yao ya kutetea ubingwa wao huku Simba wakitaka ushindi wajiimarishe kileleni kabla ya kuelekea Algeria kuivaa ES Setif.


Kocha wa Yanga Kostadin Papic.

Yanga hivi sasa inashikilia nafasi ya tatu ikiwa na pointi 43, hivyo ushindi dhidi ya Coastal utasaidia kupunguza pengo kati yake na kinara Simba inayoongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 47, pia kuiondoa Azam FC katika nafasi ya pili ambayo ina pointi 44 kabla ya mechi yake ya kesho dhidi ya Ruvu JKT.

Ukweli ni kwamba uzito wa mechi kati ya Yanga na Coastal Union unazidishwa na taswira tofauti za timu zote mbili hivi sasa pamoja na uwepo wa kocha Jamhuri Kihwelo 'Julio'.

Mabingwa hao wa mwaka 1988, Coastal Union waliojikusanyia pointi 29 baada ya kuzinduka na kushinda mechi sita mfululizo za raundi ya pili wenyewe wanatarajiwa kuendeleza rekodi hiyo kwa kusaka pointi tatu zitakazoipandisha juu kutoka katika nafasi ya sita iliyojiweka mpaka sasa.

Kocha wa Coastal, Kihwelo 'Julio' ameapa kuwadharirisha wapinzani wake kwenye mchezo huo akitarajiwa kuwatumia nyota kama Benard Mwalala, Edwin Mukenya kufikia malengo yake ingawa pia yupo Aziz Gilla anayecheza hapo kwa mkopo akitokea Simba.

Naye kocha wa Yanga, Kostadin Papic bila shaka ataingiza timu uwanjani akiwa katika hali ya kujiamini baada ya nyota wake waliokuwa kifungoni kufunguliwa kwa muda hivyo itakuwa ni hiyari yake kuwatumia au la.

Silaha za Papic zinazoweza kuonekana leo baada ya kunasuliwa kwa muda kutoka katika kifungo cha Kamati ya Ligi kutokana na utovu wa nidhamu ni mabeki, Nadir Haroub na mwenzake Stephano Mwasika, pamoja na viungo Omega Seme, Nurdin Bakari na mshambuliaji Jerryson Tegete.

Mechi hiyo itachezeshwa na mwamuzi Rashid Msangi wa Dodoma ambaye atasaidiwa na Rashid Lwena (Ruvuma) na Issa Malimali (Ruvuma).

Vita nyingine itakuwa jijini Dar es Salaam, wakati vinara wa ligi Simba wakiwa kwenye kiwango bora zaidi watakapowakabili ndugu zao African Lyon.

Kocha Milovan Cirkovic amewasisitizia wachezaji wake kutofanya uzembe utakaotoa nafasi kwa wapinzani wao ili kujiweka vizuri kabla ya kuivaa ES Setif wiki ijayo.

Simba itashuka dimbani bila ya kiungo wake Patrick Mafisango aliyesimamishwa na uongozi kutokana na utovu wa nidhamu.

Hata hivyo, Cirkovic licha ya kuwa na akiba ya kutosha ya wachezaji mahiri pia atakuwa na furaha baada ya kurejea kwa beki aliyekuwa majeruhi Juma Jabu.

Kesho matajiri wa Chamazi, Azam watakuwa wenyeji wa Ruvu JKT timu iliyopoteza makali yake katika siku za hivi karibuni.

Friday, March 30, 2012

WABUNGE KWENDA KUISHANGILIA SIMBA S.C ALGERIA


Mh Zitto Kabwe ataongoza kikosi cha wabunge kwenda Algeria kuipa Support Simba S.C

WABUNGE watano wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamethibitisha kuambatana na Simba katika safari ya kuelekea Algeria tayari kwa kuivaa ES Setif katika pambano la marudiano lililopangwa kupigwa Aprili 6, nchini humo.

Pambano dhidi ya Waaarabu hao kutoka katika jiji la Setif nchini humo ni la marudiano baada ya pambano la awali lililofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuishuhudia Simba ikiondoka na ushindi wa 2-0.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Simba, Ismail Rage aliwataja wabunge hao kuwa ni pamoja na Zito Kabwe (Kigoma Kusini), Musa Hassani Zungu(Ilala), Asnein Murij, Murtaza Mangungu(Kilwa Kaskazini)na Khalifa Suleiman Khalifa(Gando).

Alisema kuwa wakati safari ya wabunge Mangungu, Murij na Khalifa itaanzia Dar es Salaam, Kambwe ataanzia safari yake ya kuelekea Algeria akitokea nchini Nigeria huku Zungu akitarajiwa kuungana nao akitokea nchini Morocco alikodai yupo kwa sasa.

Aliongeza kuwa mbali ya wabunge hao, mashabiki 18 wa klabu pia wamethibitisha kuwa watasafiri na kikosi cha timu yao kwa ajili ya kuwaunga mkono ikiwa ni baada ya kununua tiketi za ndege.

"Kimsingi maandalizi ya safari ya Algeria yanaendelea vizuri na hapa tunapoongea tayari wabunge watano akiwemo mheshimiwa Zitto, Zungu, Murij, Mangungu na Klalifa wamethibitisha kuungana nasi kule Algeria."

Kuhusu mapokezi pindi watakapotua nchini Algeria, Rage alisema mpaka wakati huu uongozi wake umekuwa ukiwasiliana mara kwa mara na wanafunzi wanaosoma nchini humo kwa ajili ya kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa.

"Hatuna ofisi ya ubalozi Algeria, lakini tunashukuru Wizara ya Mambo ya Nje inatupa msaada mkubwa, pia tuna mawasiliano na wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma kule ambapo tayari wamejipanga kutupokea na kutupa msaada utakaohitajikika,"alisema Rage

Thursday, March 29, 2012

FABRICE MUAMBA "AFUFUKA" WACHEZAJI NA FAMILIA ZAO WAMIMINIKA HOSPITALINI KUMJULIA HALI


FABRICE MUAMBA

Habari kutoka London Uingereza zinasema kiungo wa Bolton, Fabrice Muamba ameweza kuamka kitandani na kuzungumza na wachezaji wenzake waliokwenda kumuona hospitali.


Reo Cooker,Pratley na Davies wakitoka Hospitalini kumtembelea Muamba

"Anatia moyo na hali yake inazidi kuimarika," ilisema taarifa ya pamoja ya klabu na hospitali.

Kocha wake, Owen Coyle alisema Muamba alikuwa akiangalia mechi za ligi za mwishoni mwa wiki ikiwemo timu yake ilipoibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Blackburn.


Defoe na mama yake (Sandra) na nyuma ni dada yake (Chonte) walipomtembelea Muamba Hospitalini

"Nilikuwa nasikia raha, nilikuwa sijisikii hata kulala wakati tunaongoza kwa mabao 2-0," alisema Muamba.

Kocha huyo alikuwa katika mipango ya mechi ya marejeo ya Kombe la FA na aliwashukuru mashabiki wa Tottenham Hotspur kwa msaada wao.


Benoit Assou-Ekotto akiwatilia saini mashabiki wake alipokwenda kumjulia hali Muamba hospitalini

Bolton inarudi kwenye Uwanja wa White Hart Lane kwa ajili ya mechi hiyo iliyovunjika baada ya mchezaji huyo kupatwa na shambulio la moyo na kuanguka uwanjani.

"Tutakuwa tukikuwaza, Fabrice." Wachezaji wa Bolton walisema walipomtembelea mwenzao ikiwa ni siku chache kabla ya kurudiana na Spurs.


Essien akizungumza na waandishi wa habari nje ya hospitali alipoenda kumtembelea Muamba

Wakati wanajiandaa kwenda kumtembelea mchezaji mwenzao, Zat Knight, David Wheater na Jussi Jasskelainen walikuwa wanashindwa hata kutoka hotelini kwenda London Chest Hospital.


Shaun Wright Philips na Ashley Cole nao walijumuika Hospitalini kumjulia hali Muamba

Wachezaji wa timu hiyo walikuwa wamevalia suti za michezo, na walipanda teksi kwenda hospitali kumwona.


Nahodha wa Bolton Davie na mkewe(Emma) na mtoto wao walipomtembelea Muamba

Bolton pia walirudia kuipongeza Tottenham hasa kitengo chake cha huduma pamoja na shabiki wa Spurs, Dk. Andrew Deaner.


Shabiki akiweka mdoli nje ya Chest Hospital jijini London alikokuwa akitibiwa Muamba.

Taarifa iliishukuru Tottenham waliokuwa wakimtakia kila la kheri Muamba, waliwashukuru London Ambulance Service na wale wote waliojitolea kutoka taasisi za moyo kumsaidia Muamba.

CCM HAINA JIPYA KATIKA MAENDELEO YA TANZANIA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dk Jakaya Mrisho Kikwete akitafakari jambo katika moja ya mikutano ya Chama Cha Mapinduzi.

CCM Kweli ni chama kilichotuletea Uhuru na kutulea lakini sasa kimepitwa na wakati linapokuja swala la teknolojia kwani karne hii inabidi tuwe na Vitu vya karne hii.
Sasa ukiiangalia CCM ni ya zamani na sera za kizamani ndio maana Viongozi wa CCM wanashindwa kuleta mabadiliko katika nchi yetu.Kwa mtazamo wa kawaida wa umasikini uliokithiri wa watanzania,migogoro na ukosefu wa huduma bora za jamii ni dhahiri CCM imeelemewa na inaonekana kushindwa kutatua ama kuleta nafuu kwa watanzania kupitia serikali yake.

Nimesikitika sana kusikia Rais wetu Dk Kikwete akikosolewa na wataalamu wa Uchumi kutoka China na Vietnam mbele ya jamii na kadamnasi,Wakosoaji  Wameshangazwa sana na mfumuko wa bei na ubinafsishwaji wa viwanda.
Ni dhahiri kuwa ubinafsishaji wa Viwanda umetupandishia gharama za maisha kwani viwanda ndio kitu pekee kingeweza kumkomboa mkulima kwa kuongeza thamani ya mazao ya kilimo ambacho asilimia 80 ya watanzania wanakitegemea, na ajira za watanzania zingeongezeka kutokana na viwanda lakini leo hii tumebinafsisha kila kitu.

Mfano mzuri ameutoa Profesa Do DucDinh wa Taasisi ya kimataifa ya uchumi ya Vietnam kuwa Vietnam hawalimi kabisa zao la korosho lakini wana Viwanda vya kubangua korosho sasa iweje Tanzania ikose viwanda vya kubanguaimesheheni hapa nchini?
Suala la mfumuko wa bei Profesa Do Ducnh anasema mwaka jana alikuja akakuta kilo ya mchele 1,200/= leo hii kilo ya mchele 2,500/= ameshangazwa sana na mfumuko huo wa bei, Kama ugali ndio chakula kikuu halafu bei ya unga ipo juu unategemea maisha yatakuwaje? lazima yawe magumu nchi zote duniani chakula kikuu huuzwa kwa bei ya chini tofauti na vyakula vingine.

Wednesday, March 28, 2012

VICHUPI VYAPIGWA 'STOP' MASHINDANO YA OLIMPIKI 2012


Vichupi vilivyopigwa "stop"olimpiki

Wanawake sasa hawatohitajika kuvaa vichupi'bikini"katika mchezo wa volleyball ya ufukweni katika mashindano ya olimpiki yatakayofanyika katika jiji la London nchini Uingereza mwaka huu.
Utaratibu huo mpya umetangaza siku ya jumanne 27 March 2012 na kamati ya maandalizi ya Olimpiki ukisema kuwa katika mashindano ya Olimpiki ya kipindi cha kiangazi kwa upande wa mchezo wa Volleyball wanawake watatakiwa kuvaa kaptula fupi ama sketi fupi"vibwaya".
Tangu mashindano ya Olimpiki yalipoanzishwa mwaka 1996 huko Atlanta wanawake wamekuwa wakivaa vichupi"Bikini" na sasa hawatoruhusiwa tena kuvaa vichupi wanaruhusiwa kuvaa kaptlula ama sketi fupi pia "body suit".
Mabadiliko hayo yamefanyika ili kuweza kuenda sambamba na tamaduni za nchi mbalimbali zinazoshiriki michezo ya olimpiki. Kaptula ama sketi fupi zenye urefu wa nchi 1.18 juu ya magoti au bodysuit ndio mavazi yatakayoruhusiwa kwa mujibu wa utaratibu mpya wa kamati ya maandalizi ya olimpiki.
Kamati hiyo imesema utaratibu huu mpya utasaidia kushawishi nchi zenye tamaduni tofauti kukutana pamoja bila migongano.