Monday, June 25, 2012

EURO 2012 ITALIA YATINGA NUSU FAINALI WAKATI ASHLEY WAWILI WAKIIGHARIMU UINGEREZA


Barwuah Balotelli akipiga tik-tak ambayo ilipaa langoni mwa Uingereza

Gianluigi Buffon akiokoa mchomo wa Johnson ambao almanusra uzae bao kwa Uingereza

Timu ya soka ya Uingereza imetupwa nje katika mashindano ya Euro 2012, baada ya kunyukwa na Italia usiku wa Jumapili katika robo fainali, kwa changamoto ya mukwaju ya penalti 4-2 mjini Kiev, Ukraine, kufuatia muda wa kawaida na dakika 30 zaidi kumalizika kwa timu hizo mbili kutofungana.

Italia sasa itavaana na Ujerumani katika mechi ya nusu fainali.
Alessandro Diamanti alifunga bao la kuamua mshindi katika mikwaju hiyo ya penalti, baada ya Ashley Young na Ashley Cole kukosa kufunga mabao kupitia mikwaju waliyopiga.

Vijana wa meneja Roy Hodgson ilikuwa wazi walilemewa katika mchezo mzima, lakini ni hali ya imani na uvumilivu iliwafanya kuwa na matazamio ya kuishinda Italia.

Italia iliweza kugonga mwamba, na bao la Antonio Nocerino lilikataliwa baada ya mwamuzi kusema aliotea mpira.

Kadri mechi ilivyoendelea, ndivyo wachezaji wa England nao walionekana wachovu, na ikielekea walitazamia bahati zaidi kuliko kujitahidi kuimarisha kiwango cha mchezo wao, na penalti kwao bila shaka ikawa sio za kutegemewa tena.

Baada ya mechi, nahodha Steven Gerrard alisema: "Wachezaji walicheza kadri ya uwezo wao wote. Nilidhani tungelipata bahati katika mikwaju ya penalti, lakini mambo hayakuwa hivyo. Ukiongoza katika penalti, unashikilia matumaini kwamba mambo yatasalia hivyo, lakini Italia ndio waliokuwa na bahati. Vijana waliokuwa walinzi walifanya kazi nzuri mno, na kuiletea nchi fahari, lakini tunarudi nyumbani na mioyo ya huzuni, na hili ni jambo gumu kulikubali."

England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
Balotelli akijaribu kombora langozi mwa Uingereza bila matumaini
England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
Ngoma inogile Lescott na Balotelli
England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final

England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final

England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
Imooooo..Joe Hart akichumpa kuokoa penati bila mafanikio
England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
Wachezaji wa Uingereza waliokosa penati A.Cole na A.Young na wenzao wakiwa hawaamini kilichojiri katika dimba la Olympic mjini Kiev

England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
John Terry akimtuliza Ashley Cole na Jermain Defoe akimtuliza Ashley Young baada ya Ashley wawili kukosa mikwaju ya penati katika mtanange dhidi ya Italia

Mikwaju ya penati Uingereza na Italia

Friday, June 22, 2012

CHRISTIANO RONALDO AIPELEKA URENO NUSU FAINALI EURO 2012


Gooooooooo!! Christiano Ronaldo akitupia kambani kwa kichwa maridadi

Woyoooooo nimemaliza kaziiiiiii!!! Ronaldo akishangilia goli lililoipeleka Ureno nusu fainali

Mshambuliaji hodari Christiano Ronaldo aliwaridhisha mashabiki wa Ureno kwa kucheza vizuri sana usiku wa Alhamisi, na juhudi zake zimeiwezesha Ureno kuifumua Jamhuri ya Czech bao 1-0 na kufanikiwa kutinga katika hatua ya nusu fainali.

Ronaldo, ambaye alifunga magoli mawili wakati Ureno ilipocheza na Uholanzi, aliweza kuichachafya ngome ya Czeck na mashuti mawili kugonga mlingoti wa goli.

Hatimaye aliweza kutupia kambani kwa kichwa, huku zikiwa zimesalia dakika 12 kabla ya mechi kumalizika, na kipa Petr Cech akiweza kuufikia mpira, lakini hakuweza kuuzuia kutokana na nguvu nyingi zilizotumiwa na Ronaldo.


Peter Cech akikabiliana na Christiano Ronaldo

Ilikuwa dhahiri kwamba wachezaji wa Czech waliingia uwanjani wakiwa na nia ya kuimarisha ngome yao, na wala sio kushambulia, na kamwe hawakumtisha kabisa kipa wa Ureno.

Ureno sasa itakutana aidha na Uhispania au Ufaransa katika juhudi za kufuzu kwa fainali.

Bila shaka timu ambayo itakutana na Ureno itakuwa na wasiwasi ni vipi itaweza kumzuia Ronaldo, ambaye baadhi ya wadau wa soka wanasema kwa sasa ndiye mchezaji bora zaidi barani Ulaya.

Kiungo Miguel Veloso akimrukia Ronaldo kwa furaha

Portuguese Football Fans AFP/Getty Images
Mashabiki wa Soka wa Ureno wakiwa katika viwanja vya Campo Pequeno Square jijini Lisbon,Ureno wakiangalia mechi ya nusu fainali kati ya chama lao na Jamhuri ya Czech mechi iliyokuwa ikipigwa katika dimba la Warsaw nchini Poland. 

PORTUGAL  1-0  CZECH REPUBLIC

Thursday, June 21, 2012

MREMBO WA SIKU

Mena Suvari

On Saturday evening, Mena Suvari put a sexy spin on the little black dress when she showed up at the Motion Picture & Television Fund gala in a barely-there Maria Lucia Hohan cocktail frock

WALIOONGOZA KWA KUTUPIA KAMBANI KATIKA HATUA YA MAKUNDI EURO 2012


1-(3)  Alan Dzagoev wa Urusi ameshatupia kambani mara mpaka kumalizika kwa hatua ya makundi, amekwishapoteza matumaini ya kunyakua daruga la dhahabu kwani Urusi haikufanikiwa kufuzu katika hatua ya robo fainali katika kundi A.


2-(3) Mario Gomez wa Ujerumani amekwisha kutupia kambani mara tatu na ana matumaini makubwa ya kuibuka kidedea kwa kutupia kambani katika michuano ya EURO 2012 baada ya Ujerumani kufuzu katika hatua ya robo fainali baada ya kuibuka namba moja katika kundi B ikijikusanyia pointi zote 9 ikifuatiwa na Ureno iliyomaliza kwa pointi 6.


3-(2) Andriy Shevchenko nahodha wa Ukraine ambao ndio wenyeji wenza wa michuano ya EURO 2012 ametupia kambani mara 2 na kwa bahati mbaya wenyeji hao wametupwa nje ya michuano hiyo baada ya kumaliza katika nafasi ya 3 katika kundi D, Uingereza na Ufaransa zikipenya kwa hatua ya robo fainali. 


4-(2) Christian Ronaldo wa Ureno amekwisha tupia mara 2 na ana matumaini makubwa ya kuwa kinara wa mabao katika mashindano hayo baada ya Ureno kufuzu robo fainali baada ya kushika nafasi ya pili katika kundi B nyuma ya Ujerumani.


5-(2) Fernando Torres wa Uhispania ametupia mara 2 na anaweza kuendelea kutupia baada ya timu yake ya Uhispania kufuzu kwa hatua ya robo fainali baada ya kuongoza kundi C.


6-(2) Francesc Fabregas wa Uhispania amekwishatupia kambani mara 2 matumaini ya kuendelea kutupia yanabaki baada ya timu yake kutinga katika hatua ya robo fainali ikiongoza kundi C na sasa atachuana na mhispania mwenzake Fernando Torres katika mbio za kuvaa daluga la dhahabu.


7-(2) Mario Mandzukic wa Croatia ametupia mara 2 na ndio mwisho baada ya Croatia kushindwa kuvuka hatua ya makundi kuelekea robo fainali za michuano ya EURO 2012 ikimaliza katika nafasi ya 3 kundi C


8-(2) Michael Krohn-Dehli wa Denmark ametupia kambani mara 2 na matumaini ya kuvaa daluga la dhahabu yaliyeyuka pale Denmark waliposhindwa kufuzu kwa hatua ya robo fainali baada ya kushika nafasi ya 3 kundi B


9-(2) Nicklas Bendtner wa Denmark ametupia mara 2 na ndio amemaliza hapo baada ya Denmark kuburuzwa nje ya michuano hiyo katika kundi B


10-(2) Olof Mellberg wa Sweden nae amefanikiwa kutupia kambani mara 2 na kutokana na ukweli kwamba Sweden haijafuzu kwa hatua za robo fainali matumaini yake ya kunyakua kiatu cha dhahabu yamezikwa rasmi.


11-(2) Petr Jiracek wa Jamhuri ya Czech ametupia mara mbili na itambidi asubiri miaka minne ijayo ili aendelee kuwania ufungaji bora kwasababu Timu yake imeshindwa kufuzu kwa hatua ya robo fainali za EURO 2012.


12-(2) Vaclav Pilar wa Jamhuri ya Czech nae ametupia kambani mara 2 lakini kutokana na timu yake kushindwa kufuzu kwa hatua ya robo fainali sasa matumaini yake ya kutwaa daluga la dhahabu yameishia hapo.


13-(2) Zlatan Ibrahimovic mshambuliaji wa Sweden ametupia kambani mara 2 na ki ukweli kabisa kama Sweden ingesonga katika hatua ya robo fainali basi huenda angetupia mara nyingi zaidi kutokana na uwezo alionao, lakini sasa ndio basi tena Sweden wameshatupwa nje baada ya kushika mkia katika kundi D.

RATIBA YA MECHI ROBO FAINALI EURO 2012

Uefa Euro 2012 | FIXTURES

Thursday 21 June 2012
25 Czech Republic v   Portugal

Friday 22 June 2012
26    Germany v    Greece Arena Gdansk

Saturday 23 June 2012
27    Spain v    France Donbass Arena

Sunday 24 June 2012
28     England v   Italy     NSC Olimpiyskiy

Wednesday 27 June 2012
29  Winner Q/F 1 v Winner Q/F 3 Donbass Arena

Thursday 28 June 2012
30 Winner Q/F 2 v Winner Q/F 4    Warsaw National Stadium

Sunday 01 July 2012      FINAL
31 Winner SF1 v Winner SF2 Olympic Stadium

FAHAMU ZILIZOINGIA ROBO FAINALI EURO 2012 BAADA YA HATUA YA MAKUNDI

Uefa Euro 2012 | LOGS


Group A

Pos Team P W D L GF GA GD Pts
1 Czech Republic 3 2 0 1 4 5 -1 6
2 Greece 3 1 1 1 3 3 0 4
3 Russia 3 1 1 1 5 3 2 4
4 Poland 3 0 2 1 2 3 -1 2

Group B

Pos Team P W D L GF GA GD Pts
1 Germany 3 3 0 0 5 2 3 9
2 Portugal 3 2 0 1 5 4 1 6
3 Denmark 3 1 0 2 4 5 -1 3
4 Netherlands 3 0 0 3 2 5 -3 0

Group C

Pos Team P W D L GF GA GD Pts
1 Spain 3 2 1 0 6 1 5 7
2 Italy 3 1 2 0 4 2 2 5
3 Croatia 3 1 1 1 4 3 1 4
4 Ireland 3 0 0 3 1 9 -8 0

Group D

Pos Team P W D L GF GA GD Pts
1 England 3 2 1 0 5 3 2 7
2 France 3 1 1 1 3 3 0 4
3 Ukraine 3 1 0 2 2 4 -2 3
4 Sweden 3 1 0 2 5 5 0 3

RUNGU LA UEFA LAIANGUKIA ENGLAND KUFUATIA VURUGU ZA MASHABIKI EURO 2012



Mashabiki wa soka wa Uingereza wakilipuka kwa mayowe ya ushindi

Chama cha soka cha England, FA, kimelimwa faini ya Euro 5,000 (sawa na pauni 4000), kutokana na utovu wa nidhamu wa mashabiki wake ambao Ijumaa iliyopita walijaribu kuuvamia uwanja baada ya England kuichabanga Sweden.

Faini hiyo ni kufuatia mashabiki kujaribu kuingia uwanjani baada ya England kuiangushia kipigo Sweden cha 3-2 katika mechi ya kundi D mjini Kiev.
Chama cha FA kimeamua hakitakata rufaa kuhusiana na faini hiyo, na kwa kuwa UEFA haijaitoza FA pesa nyingi, inaashiria kwamba shirikisho hilo la soka ya Ulaya linalichukua tukio hilo kama jambo dogo.

"Tunakubali hatua iliyochukuliwa, na tunalifikiria tukio hili kama jambo ambalo limetatuliwa," taarifa ya FA ilielezea.

Baada ya magoli ya England yaliyotiwa wavuni na Theo Walcott na Danny Welbeck, mashabiki kati ya 20 hadi 30 walivikaribia vizuizi uwanjani, na kutaka kuingia ndani ya uwanja wa Olympic, lakini walifanikiwa kuifikia sehemu ya riadha tu.


Chama cha FA, kikijitetea, kiliweza kutoa ushahidi thabiti wa video mbele ya UEFA na kuonyesha kwamba “uvamizi” huo ulikuwa ni jambo ambalo lilitokea ghafula, na wala mashabiki hao hawakuwa wamepanga kutekeleza kitendo hicho.

Tukio hilo lilichukuliwa kama jambo dogo, na hata afisa wa UEFA katika mechi hiyo hakulitaja katika ripoti yake kuhusiana na mechi.

Chama cha FA pia kimethibitisha kwamba hakuna mashabiki wa England waliokamatwa aidha nchini Poland au Ukraine katika mashindano ya mwaka huu.