Tuesday, August 7, 2012

ARSENAL YAMNASA SANTI CAZORLA


Santi Cazorla akiwa katika uzi wa timu ya taifa ya Spain

Klabu ya Soka ya Arsenal siku ya jumatatu imetangaza kumnasa Kiungo hodari wa Spain Santi Cazorla(27) na kumpa mkataba wa muda mrefu.

Mfahamu zaidi Santi Cazorla

Biography
Full name: Santi Cazorla
Position: Midfield
Date of birth: December 13, 1984
Place of birth: Llanera, Spain
Height: 5ft 6in
Honours
European Championship 2008, 2012
Spanish Player of the Year, 2007

International: 45 appearances (six goals)
Debut: v Peru - May 31, 2008

Previous clubs
YearTeamAppearancesGoals
2011-12Malaga389
2007-11Villarreal12723
2006-07     (loan)
Recreativo345
2003-06Villarreal542
Total25339

SANTI CAZORLA career stats
Season TeamAppearancesGoals
2011/12 Malaga 389
2010/11 Villarreal 375
2009/10 Villarreal 245
2008/09 Villarreal 308
2007/08 Villarreal 365
2006/07 Recreativo 345
2005/06 Villarreal 230
2004/05 Villarreal 292
2003/04 Villarreal 10

BORIS ARITHI KITI CHA STEWART AZAM F.C


Viongozi wa Azam FC wakimtambulisha kocha mpya Boris Bunjak(katikati)

Timu ya Soka ya Azam F.C ya jijini Dar es salaam hatimae imefanikiwa kupata kocha wa kukinoa kikosi chao baada ya kumtimua kocha Stewart aliekipatia mafanikio makubwa kikosi hicho ikiwa ni pamoja na kuiwezesha timu hiyo kushika nafasi ya pili ligi kuu Tanzania bara na nafasi ya pili katika kombe la Urafiki na pia aliiwezesha Azam kutinga katika hatua ya nusu fainali ya Kombe la Kagame lililokwisha hivi karibuni.

Azam F.C imemnasa kocha kutoka Serbia na kumpa majukumu ya kukinoa kikosi hicho kwa miaka miwili, namzungumzia Boris Bunjak. Boris amecheza soka na amezinoa timu mbalimbali za Uarabuni,Urusi na Serbia.

CV YA BORIS BUNJAK

FUDBALSKI SAVEZ SRBIJE FA PRO COACHING AWARD
FOOTBALL ASSOCIATION OF SERBIA UEFA PRO DIPLOMA
Adressa: Terazije 35 – Belgrade
Phone : +381 11 3246208



BORIS BUNJAK
Born : 17.11.1954.
Nationality : Serbian
Position : Coach
Languages : English , Rusian , Serbian
Current address : Kraljevo 36000 Veljka Vlahovica 33/15
Serbia
Contact : Serbian mob : +38163 776 44 88
Home number + fax : +38136 322 735
E-mail : bbunjak@yahoo.com
Facebook : Boris Bunjak
www.borisbunjakcoach.com
Education : Higher coach of football
UEFA – PRO LICENCE

Coaching career : 2011 FC „DAMAC“ SAUDI ARABIA- HEAD COACH
2011- FC „ AL NASER“ OMAN – HEAD COACH
2009-10 FC „ AL OROUBA“ OMAN – HEAD COACH
2008-09 FC „ ALL SHAAB“ UNITED ARAB EMIRATES –
TECHNICAL SUPERVISOR
2007-08 FC „ ALL SHAAB“ UNITED ARAB EMIRATES – HEAD
COACH
2006-07 FC „ AL NASER“ OMAN – HEAD COACH
2005-06 FK „ HAJDUK“ Kula – HEAD COACH
2004-05 FC „ALL SHAAB“ UNITED ARAB EMIRATES – FIRST

TEAM COACH
2002-04 FK „CRVENA ZVEZDA“ Beograd – FIRST TEAM COACH
2000-02 FK „ MLADI RADNIK“ Pozarevac - HEAD COACH
1999-00 FK „ URALAN“ Russia - HEAD COACH
1998-99 FK „ RADNICKI“ Nis - HEAD COACH
1996-97 FK „ CRVENA ZVEZDA“ Gnjilane - HEAD COACH
1995-96 FK „JAVOR“ Ivanjica - HEAD COACH
1993-94 INSTRUCTOR IN FA of Yugoslavia
1990-93 FK „ SLOGA“ Kraljevo – HEAD COACH

Playing career :
1967-75 FK „SLOGA“ Kraljevo
1975-78 FK „VOZDOVAC“ Beograd
1978-79 FK „RADNICKI“ Kragujevac
1979-80 FK „ OLIMPIA“ Ljubljana
1980-81 FK „ SUMADIJA“ Arandjelovac
1981-85 FK „SLOGA“ Kraljevo
1985-86 FK „BORAC“ Cacak
1986-90 FK „ SLOGA“ Kraljevo

NDUGAI AFUNGUKA WABUNGE HUINGIA MJENGONI WAMEPIGA "VYOMBO"

Wakati Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania likiwa bado kwenye kashfa ya rushwa mapya yameibuka kama "movie" vile tunatoa picha hii tunaweka picha ile na uzuri wa Watanzania huwa hatumalizii picha tunaishia katikati na hii ni nafuu kwa Mafisadi.

Naibu Spika na mbunge wa Kongwa,Dodoma(CCM) amefunguka na kutoa shutuma nzito kwa waheshimiwa kuwa na tabia ya kuingia mjengoni na kuhudhuria vikao vya Bunge wakiwa wamepiga "vyombo" kama vile Sigara kubwa(Bangi),Maji ya Mende(Bia) na nyeupe(madawa ya kulevya),
Amewashutumu Baadhi ya waheshimiwa ambao huonekana kupitia kamera za Mjengoni wakiwa wamelala na kusingizia uchovu.

Hivi ndivyo Mh Job Ndugai alivyofunguka “Kuna wabunge ninavyohisi wanaingia bungeni wakiwa wamevuta sigara fulani kubwa, kulamba vitu fulani au hata kupata bia mbili tatu,” alisema Ndugai akihojiwa jana asubuhi katika kipindi cha medani za siasa na uchumi cha Star tv.
Ndugai alifunguka kuwa madudu hayo hubainika mida ya kuanzia mchana na akalaumu kuwa hakuna hatua zozote zinazochukuliwa pindi "kipande" kinapobainika kimeingia mjengoni huku kikiwa kimepiga "vyombo". “Wabunge ni watu kama watu wengine, wana tabia kama walivyo wanadamu wengine, wapo ambao kwa namna ninavyohisi wanaingia bungeni hasa vikao vya kuanzia mchana wakiwa wamepiga bia,” alisisitiza
Ndugai

Monday, August 6, 2012

YANAYOJIRI LONDON OLYMPIC 2012

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Mkimbiaji wa Uingereza Tiffany Potter katika mbio za mita 100 kuruka viunzi wanawake

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Usain Bolt akipiga dua kwa staili yake kabla ya kuanza kutoka nduki katika mbio za mita 100 kwa wanaume

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Juliana Silva wa Brazil akishangilia ushindi katika mchezo wa Beach Volleyball huku Sara Goller na Laura wakiwa wamelowa kwa kichapo

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Benjamin Kleibrink wa Ujerumani akizichapa na Alexander Massialas wa Marekani

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Juliana Silva wa Brazil akirudisha mchomo katika mchezo wa Beach Volleyball dhidi ya Ujerumani

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Tonje Nostvold wa Norway mwenye mpira akikabiliana na Andrea Barno San Martin wa Uhispania katika mpira wa mikono(Handball)

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Mchuano wa Mpira wa mikono (Handball) ukikutanisha Urusi(Nyeupe) na Montenegro(Nyeusi)

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Tulia weweeee!!! Mtanange mkali kati ya Karoline Dyhre wa Norway na Mata Manguez Gonzalez wa Spain katika mchezo wa mpira wa mikono katika dimba la Copper Box

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Ezekiel Kiomboi wa Kenya mshindi wa medali ya dhahabu akisherehekea pamoja na Mehiedine Mekhissi-Benabad wa Ufaransa mshindi wa medali ya fedha baada ya kumaliza mbio za mita 3000 wanaume katika dimba la Olympic(Olympic Stadium)

SIMBA KUTEMBELEA YATIMA NA WAGONJWA KUELEKEA SIMBA DAY

Simba Sports Club
KIKOSI kizima cha wachezaji wa Simba SC, leo kinatarajiwa kutembelea kituo cha watoto yatima cha Maungu Orphanage Center, kilichopo Kinondoni Mkwajuni, Dar es Salaam katika mfululizo wa Wiki ya Simba na Jamii, kuelekea tamasha la kuazimisha kuzaliwa kwa klabu hiyo, Simba Day, Agosti 8, mwaka huu.

Wachezaji wa Simba, wanatarajiwa kujumuika na watoto hao, wanaoishi katika mazingira magumu na kuwafariji sambamba na kuwapa zawadi mbalimbali.

Ratiba inaonyesha kesho Simba watatembelea wagonjwa katika hospitali ya Mwananyamala mjini Dar es Salaam na keshokutwa ndipo litafanyika Tamasha la Simba Day, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika tamasha hilo, litakalotanguliwa na burudani mbalimbali, litafuatiwa na utambulisho wa wachezaji wote wa kikosi cha msimu ujao cha Simba SC wakiwemo Mrisho Khalfan Ngassa aliyesajiliwa kutoka Azam FC, Mbuyu Twite kutoka APR ya Rwanda na wengineo.

Baada ya utambulisho, Simba itacheza mechi ya kirafiki na timu ambayo hadi sasa haijatajwa ingawa wachunguzi wa mambo wamefunguka kuwa klabu ya Simba ipo kwenye mawasiliano na Nairobi City Stars ya Kenya.

Siku inayofuata, yaani Agosti 9, Simba watatembelea shule ya msingi Mgulani,ili kuhamasisha michezo mashuleni na Agosti 10, mabingwa hao wa Tanzania, watahitimisha wiki ya Simba na Jamii, kwa kutembelea kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kilichopo Ilala, Dar es Salaam.

TBL ndio wadhamini wakuu wa Simba SC, kupitia bia yao ya Kilimanjaro Premium Lager, ambayo pia ndio imedhamini Wiki nzima ya Simba na Jamii, kuanzia kwenye Mkutano Mkuu wa mwaka wa klabu hiyo, jana Bwalo la Maofisa wa jeshi la Polisi, Oysterbay, Dar es Salaam,



RATIBA YA WIKI YA SIMBA KWA JAMII:

Agosti 5, 2012: Mkutano Mkuu wa mwaka Simba SC (Polisi Oystrebay)

Agosti 6, 2012: Kutembelea watoto yatima Maungu Orphanage Center, K’ndoni Mkwajuni

Agosti 7, 2012: Kutembelea wagonjwa Mwananyamala hospitali

Agosti 8, 2012: Simba Day (Uwanja wa Taifa, burudani na mechi)

Agosti 9, 2012: Kutembelea shule ya msingi Mgulani kuhamasisha michezo mashuleni

Agosti 10, 2012: Kutembelea kiwanda cha TBL Ilala

RAGE AWAFUNGUKIA YANGA DAU LA OKWI NI BILIONI 3,AUSTRIA KULIPWA MIL 57 KWA MWEZI


Emmanuel Okwi

KATIKA kile kinachoonekana kuwa ni kutaka kuwakomoa mahasimu wao wa jadi, Yanga, klabu ya Simba imetangaza kuwa tayari kumuuza straika wao Emmanuel Okwi kwa dau kufuru la dola za Marekani milioni 2, ambazo ni sawa na Sh. bilioni 3.

Bei hiyo ya Okwi kwa Yanga inazidi mara 13 ya kiasi cha pesa walichokihitaji Simba wakati wakimuuza straika wao Mbwana Samatta kwenda klabu tajiri ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambayo ilikuwa ni dola za Marekani 150,000 tu, sawa na Sh. milioni 230!

Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, ndiye aliyetangaza dau hilo linaloonekana wazi kuwa na dhamira ya kufuta ndoto za Yanga kumtwaa Okwi wakati akizungumza kwenye mkutano wa klabu hiyo ya Msimbazi uliofanyika leo kwenye ukumbi wa Bwalo la Mafisa wa Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage akizungumza katika mkutano uliofanyika kwenye bwalo la Polisi Oysterbay jijini Dar.
 
Aidha, dau hilo la Okwi pia linazidi takriban mara mbili ya bajeti ya Simba kwa mwaka ujao wa fedha ambayo ilisomwa jana kwenye mkutano huo na kukadiriwa kuwa haitazidi Sh. bilioni 1.6.

Rage alisema kuwa Okwi bado ni mchezaji halali wa klabu yao na kama Yanga wanamuhitaji kweli, basi watoe fedha taslim kiasi cha dola za Marekani milioni 2 (Sh. bilioni 3).

Hata hivyo, inakumbukwa kwamba ni wiki iliyopita tu, Simba ilisema kuwa inatarajia kumuuza Okwi kwa euro 600,000 (sawa na Sh. bilioni 1.1) kwa mabingwa wa Austria, klabu ya Redbull Salzburg ambayo ilishiriki hivi karibuni ilitoka kushiriki hatua ya awali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Viwango tofauti vya bei ya mchezaji huyo, vinamaanisha kwamba Simba iko tayari kumuuza Okwi kwa bei poa Ulaya kuliko kumuona anajiunga na Yanga; na kwamba thamani ya straika huyo wa kimataifa wa Uganda ni mara 13 ya Mbwana Samatta waliyemuuza kwa TP Mazembe.

Akieleza zaidi kwenye mkutano huo uliohudhuriwa na wanachama zaidi ya 700, Rage alisema kuwa kwa vyovyote vile, Okwi hawezi kukataa ofa ya mshahara wa euro 30,000 (sawa na Sh. milioni 57) kwa mwezi nchini Austria na kujiunga na watani zao, Yanga ambao wanasemekana wako tayari kumlipa mshahara wa Sh. milioni 2.5 kwa mwezi endapo atakubali kujiunga nao.
 

Friday, August 3, 2012

NGASSA AANZA MAZOEZI SIMBA, AKABIDHIWA TOYOTA VEROSSA ATIINGA NALO COCO BEACH


Ndinga alilokabidhiwa Ngassa na klabu yake mpa ya Simba S.C ya jijini Dar es salaam.
Club ya soka ya Azam ilitangaza kwamba Mchezaji wao Mrisho Ngasa tayari amepelekwa Simba kwa mkopo ambapo Simba walipewa sharti la kuhakikisha wanamlipa Ngasa mshahara wake kamili (TZsh 2,000,000) kwa mwezi pamoja na stahiki zake nyingine zote za kimkataba.


Ngassa akijiandaa "kutekenya ndinga yake"


Mashabiki wa Simba wakimkaribisha Ngassa klabuni maeneo ya Msimbazi


Ngassa akiingia coco beach ambako klabu yake mpya ilikuwa ikifanya mazoezi.



Ngassa akitiririka mazoezini katika ufukwe wa Coco Beach


Mrisho Ngassa na Uhuru Selemani