Monday, August 22, 2011

Arsenal mbovumbovu yagaragazwa na Liverpool

Liverpool dakika za mwisho iliweza kupata mabao mawili ya haraka haraka na kupata ushindi wa kwanza kwenye uwanja wa Arsenal kwa miaka 11 iliyopita, hali ilnayozidi kumtia matatani meneja wa Arsenal, Arsene Wenger.
Suarez na Meireles wakishangilia bao la pili
Suarez na Meireles wakishangilia bao la pili

Arsenal - ikimchezesha Samir Nasri wakati huu mipango ya uhamisho wake kwenda Manchester City ikiwa imesita, iliweza kuwabana Liverpool hadi kiungo wao wa kutumainiwa Emmanuel Frimpong alipotolewa nje kwa kadi nyekundu zikiwa zimesalia dakika 20 kabla mchezo kumalizika.
Meneja wa Liverpool Kenny Dalglish haraka akamuingiza Luis Suarez na Raul Meireles uamuzi ulioonekana kuwa wa maana na wachezaji hao wawili walikuwemo katika mchakato wa kupatikana mabao hayo mawili.
Walishirikiana vizuri langoni mwa Arsenal hadi kijana chipukizi Ignasi Miquel, aliyechukua nafasi ya Laurent Koscielny aliyeumia, aliokoa mpira ambao ulimgonga Aaron Ramsey na kujaa wavuni na muda mfupi baadae Suarez alifunga bao la pili rahisi baada ya kupata pasi kutoka kwa Meireles katika sekunde za mwisho na kukamilisha ushindi wa kwanza wa Liverpool msimu huu.
Nayo klabu ya Newcastle iliendelea kufanya vizuri na kupata ushindi wa ugenini wa bao 1-0 dhidi ya Sunderland kwa bao lililofungwa na Ryan Taylor.
Alan Pardew meneja wa Newcastle
Alan Pardew meneja wa Newcastle

Wenyeji Sunderland walimiliki mpira kwa kiwango kikubwa kipindi cha kwanza, lakini Joey Barton wa Newcastle alikosa bao baada ya mpira wake wa kichwa alioupiga kumgonga Sebastian Larsson mkononi.
Stephane Sessegnon na Asamoah Gyan walikosa nafasi za kuipatia mabao Sunderland, wakati beki wao Phil Bardsley alitolewa nje kwa kadi ya pili ya manjano.
Ushindi huo wa Newcastle ina maana Newcastle imepoteza mechi moja tu kati katika michezo 13 iliyopita dhidi ya wapinzani wao hao wa jadi na ulikuwa ni ushindi wa kwanza kwa meneja Pardew tangu alipochukua hatamu za kuiongoza msimu uliopita.
Nayo Queens Park Rangers ama QPR wamefanikiwa kupata ushindi wao wa kwanza wa Ligi Kuu ya Soka ya England tangu mwaka 1996 baada ya mkongwe Tommy Smith kufunga bao lililoihakikishia ushindi huo wa kwanza wa ugenini dhidi ya Everton.
Adel Taraabt
Adel Taraabt

Eberton inayokabiliwa na matatizo ya fedha imekuwa ni mechi yao ya kwanza ya ligi kupoteza msimu huu.
Mabao yaliyofungwa na Gabriel Agbonlahor, Emile Heskey na Darren Bent yameipa ushindi Aston Villa katika mechi ya kwanza uwanja wa nyumbani wa Ligi kwa meneja Alex McLeish katika uwanja wa Villa Park.
Aston Villa na Blackburn
Aston Villa na Blackburn

Villa ilipata bao la kuongoza lililofungwa na Agbonlahor. Lilikuwa ni bao murua sana kwa mkwaju uliochongwa kwa ustadi na kujaa wavuni.
Heskey alifunga bao la pili kwa mkwaju wa chini chini kwa mkwaju wa yadi 20, lakini Morten Gamst Pedersen alifanikiwa kuifungia bao la kwanza Blackburn baada ya krosi ya Hoilett.
Lakini Bent aliihakikishia ushindi Aston Villa kwa bao la tatu rahisi baada ya mkwaju karibu na lango na kumpita mlinda mlango Paul Robinson.
Swansea City nayo ilifanikiwa kupata pointi ya kwanza katika kwanza Ligi Kuu ya England lakini mkwaju wa penalti waliopatiwa Wigan katika kipindi cha pili uliokolewa na mlinda mlango wa Swansea Michel Vorm na kuinyima ushindi Wigan.
Mlinda mlango huyo mpya aliyesajiliwa msimu huu, Vorm aliokoa mkwaju wa chini chini wa Ben Watson baada ya Jordi Gomez kuangushwa na Ashley Williams.

Mutharika afukuza kazi mawaziri wote

Rais wa Malawi, Bingu wa Mutharika, amelifuta kazi baraza lake lote la mawaziri baada ya majuma kadha ya maandamano ya ghasia, ambapo watu karibu 20 wamekufa.
Maandamano ya Malawi

Bwana Mutharika sasa ameshika wizara zote 42; na hakutoa sababu ya kufanya hivo.
Mataifa kadha ya magharibi, yamesimamisha msaada kwa Malawi baada ya waandamanaji kuuwawa mwezi uliopita, ambao wakilalamika juu ya kupanda kwa gharama za maisha na kama walivosema, serikali mbovu.

Friday, August 19, 2011

MNARA UNAOTAJWA KUWA MREFU KULIKO YOTE DUNIANI WAANZA KUJENGWA

Ujenzi wa mnara unaotarajiwa kuwa mrefu kuliko yote ambayo imepata kutokea duniani umeanza, Unatarajiwa kupewa jina la KINGDOM TOWER. Mnara huo unajengwa nchini Saudi Arabia na unatarajiwa kuwa na urefu wa zaidi ya futi 3000 na unatarajiwa kugharimu zaidi ya dola bilioni moja.
Mnara utakapokamilika muonekano uwapo mnarani utakuwa wa ajabu sana, ambapo ni zaidi ya 2/3 ya maili moja, utakuwa na maeneo ya biashara,maduka na sehemu za starehe.
Zifuatazo ni picha zitakazotokana na mnara huo pindi utakapokamilika.


 Tallest-tower
Manjonjo ya mnara huo sehemu ya juu na jinsi utakavyoonekan kwa mbele ukiwa Bahari ya Hindi.

Kingdom Tower
Taswira halisi ya mnara huo itakavyokuwa.


Tall Tower
Mandhari ya Kingdom Tower yatakavyokuwa sehemu ya chini.

JUKWAA LAANGUKA WAKATI WA TAMASHA LA MUZIKI NA KUUA

Nchini Ubelgiji jukwaa limeanguka na kuua watu kadhaa, Jukwaa hilo lilianguka katka tamasha la muziki linalojulikana kama Pukkelpop Music Festival jijini Hasselt, watu wanne wameripotiwa mapema kufariki dunia katika tukio hilo.

Belgium-Pukkelpop
Watu wakiwa wamepigwa na butwaa katika tukio hilo.

Msanii Cullen Omori amekaririwa mapema leo hii akisema "Ndio kwanza tulikuwa tumemaliza kuimba wimbo wetu wa kwanza katika nyimbo zetu hapa Pukkelpop, ndipo jukwaa na hema vikaanza kutingishika na tukafikiri labda ni kimbunga tu kinapita, ndipo nikaamrisha tuendelee na wimbo wa pili ndipo meneja wa msafara alisikika akipiga yowe kuwa tuteremke kutoka jukwaani, mara ghafla upande mmoja ukaanguka futi moja kwenda chini, tukafikiri kuwa ni jukwaa tu ndio limeanguka na sio hema ghafla vilio na kelele vilitosha kutueleza kilichotokea, lakini mpaka wanauja waokoaji na kututaarifu kuwa kuna watu waliopoteza maisha wapatao wanne na kadhaa wamejeruhiwa, huruma na mawazo yetu yakawa kwa wale waliowapoteza wapendwa wao katika janga hili."

Tazama jinsi ilivyokuwa

FAHAMU WATU MAARUFU WAMESEMA NINI WIKI HII

 photo | Jennifer Hudson
Jennifer Hudson "Najivunia kupungua uzito kuliko tuzo yangu ya Oscar"


 photo | Emma Stone, Jimmy Kimmel
Emma Stone amefunguka na kusema "It's a fake farm, but it doesn't feel fake, Jimmy. I was leaving dinners to harvest." Na kwa maneno hayo anasema ndio maana alijitoa Facebook.




 photo | Amber Heard
Amber Heard amefunguka na kusema "To say I came out implies that I was once in. Let me be straight about that – no pun intended [laughs] – I never came out from anywhere." Nyota huyo wa klabu ya Play Boy ameyasema hayo huku akitanabaisha kuwa huwa hafichi mahusiano yake lakini anapenda kuyafanya maisha yake binafsi kuwa ya siri.




 photo | Nicole Polizzi
Nae Nicole "snooki" Pollizi amefunguka na kushare na mashabiki wake mambo yake ya faragha kwa kusema "When I'm really excited about something, I poop."




 photo | Jimmy Kimmel, Kate Gosselin
Kate nae anafunguka hivi kuhusiana na suala la watoto "[Kate said] she will now devote more time to motivational speaking. Why not? She's already motivated millions of people to not have kids.





Caroline Gonzalez msichana mwenye umri wa nyundo 11 anafunguka na kusema "I like his music and I like him. And I thought, why not have a street in my hometown named after my favorite singer?"  Aliyasema hayo wakati akiupatia mtaa jina katika kitongoji cha Forney jijini Texas, alipochaguliwa kuwa meya wa siku moja.




 photo | Kim Kardashian, Tyra Banks
Tyra Banks nae anafunguka kuhusiana na harusi ya Kim Kardashian inayotarajiwa hivi karibuni "Nothing! A kiss and a congratulations."




BOB JUNIOR SIO SHOGA NI SANAA

Hivi karibuni katika vyombo vya habari vingi kumekuwa na habari ambayo imebamba vilivyo, nayo ni kumhusu mtayarishaji na msanii wa muziki wa kizazi kipya Bongo flava,huyu si mwingine ni Rais wa Masharobaro Raheem Nanji a.k.a Bob Junior, ikisemekana kwamba kukatika kwake viuno katika kazi yake ya muziki kuna uhuziano na yeye kuwa shoga, Nimeshindwa kujizuia nikiwa shabiki wake namba moja na shabiki wa sanaa ya muziki huu wa bongo flava kusikia mtu akisingiziwa vitu ambavyo havipo kwasababu ya sanaa.

Raheem Nanji a.k.a Bob Junior

Huu ni ushamba kumtafsiri mtu tofauti na vile alivyo, kukata viuno ni kazi ya sanaa kwani wacheza show za muziki huwa wanafanya nini? hata hivyo wasanii wangapi duniani wanakata viuno? mbona hata Mr Nice enzi hizo alikuwa viuno kwa kwenda mbele,je ni shoga? H Baba nae hivyohivyo,je ni shoga? Fally Ipupa nae,je ni SHOGA? Acheni kufuatilia maisha ya mtu kama mnapenda muziki pendeni muziki kama hampendi kazi zake mpotezeeni acheni kumfuatafuata katika maisha binafsi. Hata kama ni shoga yanawahusu? kuweni basi na nyinyi mashoga kama mnamuonea wivu.

Elton John na wengine maarufu ni mashoga na wapo juu ile mbaya mbona hamsemi? acheni hizo kwanza nafikiri hamjui nini maana ya sanaa au nini maana ya msanii ndio maaana mnakurupuka na kumpakazia Bob Junior. Bob Junior kama unisoma hii mzee nakushauri makamuzi ya viuno kwa kwenda mbele asiependa kazi zako na akupotezee sio lazima awe fan wako, hiyo ni sanaa na lazima msanii aheshimiwe kulingana na hisia na mawazo yake, Bob Junior be more concerned with your character than reputation, because a character is what really you are and reputation is what people think you are...wapotezeeeeeee.
Labda kwa faida ya wasiojua nini maana ya msanii au sanaa,
Kwanza Sanaa ni dhima ya upangaji wa dhana kulingana na hisia na mawazo ya msanii,
Pili Msanii sasa ndio mtu anaepanga dhana kulingana na hisia na mawazo yake.

Sasa basi Bob Junior anahaki ya kufanya kazi vile hisia na mawazo yake yanavyomtuma ili kukamilisha kazi yake ya usanii na kazi hiyo isitafsiriwe kuwa ni ushoga kwani sanaa itabaki kuwa sanaa na ushoga utabaki kuwa ushoga na ndio maana nikasema Bob Junior ameona staili ya viuno ndio inaendana na hisia zake,basi tumheshimu kama kuna mengine hayahusu katika kazi zake, au mmepandikizwa na wasanii wanaomuonea wivu kwa kazi zake naweza kuwaelewa lakini sio kiivyo.

SONGI LA LEO

Linex na wimbo wa moyo wa subira