Monday, August 6, 2012

YANAYOJIRI LONDON OLYMPIC 2012

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Mkimbiaji wa Uingereza Tiffany Potter katika mbio za mita 100 kuruka viunzi wanawake

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Usain Bolt akipiga dua kwa staili yake kabla ya kuanza kutoka nduki katika mbio za mita 100 kwa wanaume

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Juliana Silva wa Brazil akishangilia ushindi katika mchezo wa Beach Volleyball huku Sara Goller na Laura wakiwa wamelowa kwa kichapo

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Benjamin Kleibrink wa Ujerumani akizichapa na Alexander Massialas wa Marekani

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Juliana Silva wa Brazil akirudisha mchomo katika mchezo wa Beach Volleyball dhidi ya Ujerumani

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Tonje Nostvold wa Norway mwenye mpira akikabiliana na Andrea Barno San Martin wa Uhispania katika mpira wa mikono(Handball)

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Mchuano wa Mpira wa mikono (Handball) ukikutanisha Urusi(Nyeupe) na Montenegro(Nyeusi)

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Tulia weweeee!!! Mtanange mkali kati ya Karoline Dyhre wa Norway na Mata Manguez Gonzalez wa Spain katika mchezo wa mpira wa mikono katika dimba la Copper Box

Tiffany Porter of Great Britain competes in the Women's 100m Hurdles heat
Ezekiel Kiomboi wa Kenya mshindi wa medali ya dhahabu akisherehekea pamoja na Mehiedine Mekhissi-Benabad wa Ufaransa mshindi wa medali ya fedha baada ya kumaliza mbio za mita 3000 wanaume katika dimba la Olympic(Olympic Stadium)

SIMBA KUTEMBELEA YATIMA NA WAGONJWA KUELEKEA SIMBA DAY

Simba Sports Club
KIKOSI kizima cha wachezaji wa Simba SC, leo kinatarajiwa kutembelea kituo cha watoto yatima cha Maungu Orphanage Center, kilichopo Kinondoni Mkwajuni, Dar es Salaam katika mfululizo wa Wiki ya Simba na Jamii, kuelekea tamasha la kuazimisha kuzaliwa kwa klabu hiyo, Simba Day, Agosti 8, mwaka huu.

Wachezaji wa Simba, wanatarajiwa kujumuika na watoto hao, wanaoishi katika mazingira magumu na kuwafariji sambamba na kuwapa zawadi mbalimbali.

Ratiba inaonyesha kesho Simba watatembelea wagonjwa katika hospitali ya Mwananyamala mjini Dar es Salaam na keshokutwa ndipo litafanyika Tamasha la Simba Day, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika tamasha hilo, litakalotanguliwa na burudani mbalimbali, litafuatiwa na utambulisho wa wachezaji wote wa kikosi cha msimu ujao cha Simba SC wakiwemo Mrisho Khalfan Ngassa aliyesajiliwa kutoka Azam FC, Mbuyu Twite kutoka APR ya Rwanda na wengineo.

Baada ya utambulisho, Simba itacheza mechi ya kirafiki na timu ambayo hadi sasa haijatajwa ingawa wachunguzi wa mambo wamefunguka kuwa klabu ya Simba ipo kwenye mawasiliano na Nairobi City Stars ya Kenya.

Siku inayofuata, yaani Agosti 9, Simba watatembelea shule ya msingi Mgulani,ili kuhamasisha michezo mashuleni na Agosti 10, mabingwa hao wa Tanzania, watahitimisha wiki ya Simba na Jamii, kwa kutembelea kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kilichopo Ilala, Dar es Salaam.

TBL ndio wadhamini wakuu wa Simba SC, kupitia bia yao ya Kilimanjaro Premium Lager, ambayo pia ndio imedhamini Wiki nzima ya Simba na Jamii, kuanzia kwenye Mkutano Mkuu wa mwaka wa klabu hiyo, jana Bwalo la Maofisa wa jeshi la Polisi, Oysterbay, Dar es Salaam,



RATIBA YA WIKI YA SIMBA KWA JAMII:

Agosti 5, 2012: Mkutano Mkuu wa mwaka Simba SC (Polisi Oystrebay)

Agosti 6, 2012: Kutembelea watoto yatima Maungu Orphanage Center, K’ndoni Mkwajuni

Agosti 7, 2012: Kutembelea wagonjwa Mwananyamala hospitali

Agosti 8, 2012: Simba Day (Uwanja wa Taifa, burudani na mechi)

Agosti 9, 2012: Kutembelea shule ya msingi Mgulani kuhamasisha michezo mashuleni

Agosti 10, 2012: Kutembelea kiwanda cha TBL Ilala

RAGE AWAFUNGUKIA YANGA DAU LA OKWI NI BILIONI 3,AUSTRIA KULIPWA MIL 57 KWA MWEZI


Emmanuel Okwi

KATIKA kile kinachoonekana kuwa ni kutaka kuwakomoa mahasimu wao wa jadi, Yanga, klabu ya Simba imetangaza kuwa tayari kumuuza straika wao Emmanuel Okwi kwa dau kufuru la dola za Marekani milioni 2, ambazo ni sawa na Sh. bilioni 3.

Bei hiyo ya Okwi kwa Yanga inazidi mara 13 ya kiasi cha pesa walichokihitaji Simba wakati wakimuuza straika wao Mbwana Samatta kwenda klabu tajiri ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambayo ilikuwa ni dola za Marekani 150,000 tu, sawa na Sh. milioni 230!

Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, ndiye aliyetangaza dau hilo linaloonekana wazi kuwa na dhamira ya kufuta ndoto za Yanga kumtwaa Okwi wakati akizungumza kwenye mkutano wa klabu hiyo ya Msimbazi uliofanyika leo kwenye ukumbi wa Bwalo la Mafisa wa Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage akizungumza katika mkutano uliofanyika kwenye bwalo la Polisi Oysterbay jijini Dar.
 
Aidha, dau hilo la Okwi pia linazidi takriban mara mbili ya bajeti ya Simba kwa mwaka ujao wa fedha ambayo ilisomwa jana kwenye mkutano huo na kukadiriwa kuwa haitazidi Sh. bilioni 1.6.

Rage alisema kuwa Okwi bado ni mchezaji halali wa klabu yao na kama Yanga wanamuhitaji kweli, basi watoe fedha taslim kiasi cha dola za Marekani milioni 2 (Sh. bilioni 3).

Hata hivyo, inakumbukwa kwamba ni wiki iliyopita tu, Simba ilisema kuwa inatarajia kumuuza Okwi kwa euro 600,000 (sawa na Sh. bilioni 1.1) kwa mabingwa wa Austria, klabu ya Redbull Salzburg ambayo ilishiriki hivi karibuni ilitoka kushiriki hatua ya awali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Viwango tofauti vya bei ya mchezaji huyo, vinamaanisha kwamba Simba iko tayari kumuuza Okwi kwa bei poa Ulaya kuliko kumuona anajiunga na Yanga; na kwamba thamani ya straika huyo wa kimataifa wa Uganda ni mara 13 ya Mbwana Samatta waliyemuuza kwa TP Mazembe.

Akieleza zaidi kwenye mkutano huo uliohudhuriwa na wanachama zaidi ya 700, Rage alisema kuwa kwa vyovyote vile, Okwi hawezi kukataa ofa ya mshahara wa euro 30,000 (sawa na Sh. milioni 57) kwa mwezi nchini Austria na kujiunga na watani zao, Yanga ambao wanasemekana wako tayari kumlipa mshahara wa Sh. milioni 2.5 kwa mwezi endapo atakubali kujiunga nao.
 

Friday, August 3, 2012

NGASSA AANZA MAZOEZI SIMBA, AKABIDHIWA TOYOTA VEROSSA ATIINGA NALO COCO BEACH


Ndinga alilokabidhiwa Ngassa na klabu yake mpa ya Simba S.C ya jijini Dar es salaam.
Club ya soka ya Azam ilitangaza kwamba Mchezaji wao Mrisho Ngasa tayari amepelekwa Simba kwa mkopo ambapo Simba walipewa sharti la kuhakikisha wanamlipa Ngasa mshahara wake kamili (TZsh 2,000,000) kwa mwezi pamoja na stahiki zake nyingine zote za kimkataba.


Ngassa akijiandaa "kutekenya ndinga yake"


Mashabiki wa Simba wakimkaribisha Ngassa klabuni maeneo ya Msimbazi


Ngassa akiingia coco beach ambako klabu yake mpya ilikuwa ikifanya mazoezi.



Ngassa akitiririka mazoezini katika ufukwe wa Coco Beach


Mrisho Ngassa na Uhuru Selemani




YAKWANGU BAADA YA KAULI YA Dk MWAKYEMBE KUZUIA "UCHIMBAJI DAWA"


Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe.

Waziri wa uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe kupitia bunge amepiga marufuku mabasi ya abiria yaendayo mikoani kusimama njiani ili kutoa fursa ya abiria kujisaidia(Kuchimba Dawa).Na kuahidi kuwachukulia hatua wenye mabasi watakaosimamisha mabasi njiani na abiria kwenda kujisaidia.
Binafsi nina haya ya kujiuliza, Swala la mtu kwenda haja ni la hiari au sio la hiari?
Pia anaposema kuwachukulia hatua wenye mabasi, shida ya kwenda haja ndogo ni ya wenye mabasi au ni ya abiria?
Na je amechukua hatua gani za makusudi kuwasaidia wasafiri jinsi ya kujisaidia wawapo safarini baada ya kupiga kupiga marufuku mabasi ya abiria kusimama njiani?


Nijuavyo mimi swala la mtu kwenda haja sio la kupanga ila ni swala la kibiolojia. Mtu huhitaji kwenda haja ndogo baada ya matumizi ya Vyakula na vinywaji na baada ya mwili kufanya kazi na kuchukua virutubisho muhimu huhitaji kutoa vile visivyohitajika mwilini. Na pindi mwili unapohitaji kutoa masalia ya chakula na vinywaji yasiyohitajika mwilini ni kitendo kisichokuwa cha hiari, ambacho kwa lugha ya kitaalamu hujulikana kama "Involuntary action".


Unaweza kumshauri mtu asitumie vinywaji au apunguze matumizi ya chakula awapo safarini, lakini ikumbukwe kuwa hali ya hewa,mshtuko na aina ya vyakula huweza kusababisha mabadiliko ya ghafla katika mwili wa binadamu na kusababisha mtu kuhitaji kutoa haja. Mara nyingi hutegemea na maumbile ya mtu na matumizi ya vyakula ama vinywaji,wakati mwingine vyakula au vinywaji mtu awapo safarini ndio huwa chanzo kikubwa cha kuleta mabadiliko ya ghafla katika mwili wa binadamu na kusababisha aidha kwenda haja ya kawaida au haja itokanayo na ugonjwa kutokana na chakula au kinywaji alichotumia mtu.


Sababu kubwa aliyoitoa Mh Mwakyembe ni kuwa kitendo cha mabasi ya abiria kusimama njiani na watu kujisaidia ni udhalilishaji kwa kile alichosema kwamba abiria wa rika tofauti huchanganyika wakati wa kujisaidia"kuchimba dawa". Binafsi pia naona huo ni udhalilishaji lakini sio busara kupiga marufuku mabasi ya abiria kusimama na watu kwenda kujisaidia kwasababu kitendo cha kujisaidia sio cha hiari ni cha kibiolojia.
Nafikiri ingekuwa busara kama Mh Mwakyembe kupitia bunge wangejadili ni jinsi gani ya kuwasaidia abiria wanaohitaji kujisaidia wawapo safarini ili kuwaepusha na udhalilishaji, Kitu ambacho kingefanyika Ni kuangalia jinsi gani utaratibu wa kujisaidia njiani"kuchimba dawa' ungeratibiwa ili kuondoa muingiliano wa rika na jinsia pindi mabasi yanaposimama njiani na abiria kujisaidia.
Hili lingewezekana kwa kuwashirikisha madereva na makondakta wa mabasi ya abiria, Kwa pamoja wakajadili utaratibu wa abiria kujisaidia njiani uwe wa namna gani ili kuondoa udhalilishaji uliozungumziwa.
Ingekuwa ni busara zaidi kupitia bunge wangepitisha Sheria ya kila basi la abiria la kwenda mikoani ni lazima liwe na choo,sheria au utaratibu huu ungeondoa madhila yote yanayotokea pindi abiria wanapojisaidia njiani.

Thursday, August 2, 2012

Artist-RICH MAVOKO Song-SILALI

MRISHO NGASSA...PWAAAAH MSIMBAZI


Mrisho Ngassa

Mabingwa wa kabumbu nchini, Simba wamewabwaga watani wao Yanga katika vita ya kumwania winga wa Azam FC, Mrisho Ngassa, na sasa nyota huyo anatarajia kutinga kwa mara ya kwanza uzi wa rangi nyekundu na nyeupe msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara.Ngassa aliyekuwa pia akiwania na klabu yake iliyompa chati, mabingwa wa Kombe la Kagame, Yanga ya Dar es Salaam, amejiunga na Wekundu hao wa Msimbazi kwa mkopo.

Awali ilitegemewa kuwa, Ngasa aliyechoka kuendelea kukosa namba kikosi cha kwanza cha Uwanja wa Chamazi, angejiunga na timu yake ya zamani ya Yanga.

Azam ilitangaza kupitia tovuti yao mwanzoni mwa wiki hii, kwamba iko tayari kumuuza Ngasa kwa timu yoyote itakayofika dau la dola 50,000.

Taarifa hiyo ya kwenye tovuti ilikuja siku chache tangu Ngasa aonekana akiibusu nembo ya klabu ya Yanga wakati akishangilia bao kwenye mechi ya Kombe Kagame.

Katika ofa yao, Yanga ilisema ingekuwa tayari kumtwaa mchezaji huyo kwa dau la Sh20 milioni, huku wapinzani wao Simba wakija na dau la Sh25 milioni.

Lakini mwenyewe Ngasa alipoulizwa kuhusu kupelekwa kwa mkopo Simba, alionekana kushangazwa na habari hizo na kusema hafahamu lolote.

"Na mimi nimesikia watu wanasema kwamba natakiwa kwenda Simba kwa mkopo. Naloweza kukuambia ni kwamba, mimi naheshimu mkataba wangu," alisema Ngasa.

"Sijaambiwa lolote na viongozi wangu, kwa maana hiyo basi mimi bado mchezaji halali wa Azam mpaka itakapotangazwa tofauti."

Meneja wa Azam, Patrick Kahemela aliithibitishia Mwananchi jana kuwa, klabu yao imeamua kumpeleka kwa mkopo Ngasa klabu ya Simba.

"Kwa sasa bado ana mkataba na Azam, tumeamua kumtoa kwa mkopo kwenda Simba mpaka mkataba wake utakapomalizika mwishoni mwa msimu," alisema Kahemela.

Kahemela alisema ameshangazwa na hatua ya Yanga kushindwa kufika kwenye mazungumzo ya kumsajili mchezaji huyo kama walivyokuwa wamepanga.

"Yanga walikuwa wa kwanza kuleta ofa yao, na sisi tuliwapa wao zaidi nafasi kuliko Simba, lakini walipopaswa kuja kwa ajili ya mazungumzo ya mwisho hawakutokea," alisema.

Aliongeza: "Yanga walifanya mzaha katika suala hili. Tulimtafuta Katibu Mkuu [Mwesigwa Celestine] lakini hakuonyesha kujali."

Taarifa za Ngasa kutua kwa mkopo Simba pia zilithibitishwa na Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo, Godfrey Nyange.

"Tumemalizana na Azam kuhusu suala la Ngasa. Huyu sasa ni mchezaji wetu, atasaidia kuimarisha safu ya ushambuliaji," alisema Kaburu.