Tuesday, July 19, 2011

MFALME ANAPOCHAGUA KIFAA SWAZILAND MAMBO HUWA HIVI

Agosti 31, nchi ndogo ya Swaziland iliyopo katikati ya Afrika ya kusini hufanya sherehe ya mwaka kumtafuta malkia. Wasichana 50,000 hukusanyika karibu na ikulu, wasichana hawa huwa watupu kama walivyozaliwa isipokuwa baadhi tu ya sehemu za mwili huwa zimezibwa huku wakiimba na kupigiza miguu kwa kishindo katika ardhi yenye vumbi jekundu, wakati huo mfalme wa Zulu akiwa amekaa kivulini kwenye hema akiangalia wasichana hao kwa tabasamu la kuopoa kifaa kipya. Sherehe hizi zimejizolea umaarufu kwa wasichana wa kizulu ambao baadhi hutoka mile kadhaa,mfano Durban ili kuja kucheza katika sherehe hiyo ya heshima. Zifuatazo ni picha za sherehe hizo zinavyokuwa.

Wasichana wa kizulu wakipita mbele ya mfalme

Wakiimba na kucheza kwa furaha



Wakipita kwa mbwembwe

Hatime wamesimama mfalme apate kuchagua kifaa chake



FASHION MPYA KWA VIATU VYA KIKE








UAE’s Awana Diab attempts insane penalty kick (and it works)