Wednesday, April 3, 2013

BALAA LA KHANGA MOKO HILI HAPA





Balaa linaanza mtu anamwagiwa Kinywaji kwenye makalio ooo maaamaaa
  
Sasa ni ndembendembe

Balaa hilo mie simoooo

Twende kazi..asie na mwana aeleke jiwe

PSG YAIKOMALIA BARCELONA, BAYERN YAITUNGUA JUVENTUS



Messi akitupia kambani goli la kwanza Katika dakika ya 37 kabla Zlatan Ibrahimovic hajaisawazishia PSG katika dk 78. Na Barcelona waliongeza bao la pili likitupiwa kambani na Xavi kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 88 lakini PSG walikomaa na kusawazisha katika dakika ya 90 bao la nduki kali ya Matuidi. Mpambano huo ulihudhuriwa na mashabiki wapatao 45,000.

Ibrahimovic akishangilia goli la kwanza la kusawazisha


Iniesta chini ya ulinzi mkali


Goli la pili na la kusawazisha la PSG likitinga wavuni

Mfungaji wa goli la kusawazisha la PSG Matuidi akishangilia


Messi na Beckham shughuli pevu

Messi baada ya kuumia akijiandaa kutoka nje
 
PSG 2-2 BARCELONA


 Katika robo fainali nyingine ya kwanza timu ngumu ya Ujerumani Bayern Munich waliiadabisha Bibi kizee wa Turin,Juventus kwa bao 2-0. Goli la kwanza likifungwa na Alaba dakika ya 0, Na sio mwingine alietupia msumari wa pili bali ni Thomas Muller katika dakika ya 62.

  
 
Nimetupiaaa..Alba akishangilia baada ya kufunga goli la mapema mno katika dakika ya 0.
  
Robben chini ya ulinzi
 
BAYERN 2-0 JUVENTUS