Wednesday, November 9, 2011

Adebayor kutua Real Madrid

EPL,Emmanuel Adebayor,Wolverhampton Wanderers v Tottenham Hotspur
Emmanuel Adebayoy ndani ya swaga za kiduku

Mchezaji wa zamani wa Arsenal Adebayor anahusishwa na kuhamia Real Madrid. Adebayor kwa sasa anakipiga Tottenham kwa mkopo akiwa ametokea Man City ambako alidumu kwa miezi sita tu.
Kuhusiana na sakata la kuhamia Real Madrid Adebayor alikuwa na haya ya kusema......
"Harry Redknapp is a top manager.
“I would put him closer to Mourinho because of the way he treats players.
“He gives you full confidence.
“He too knows how to talk to players and that makes him special as well. I have huge respect for Mourinho.
I learned a lot at Real Madrid. Even after my goal at Wolves I woke up the next morning and had a message from him.
“That is what he is like and it is appreciated."

Taifa Stars kuelekea Chad leo,serikali yaipatia milioni 10


Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, inaondoka leo kuelekea nchini Chad, huku serikali ikitoa kiasi cha sh10 milioni kama hamasa ya ushindi katika mechi ya kuwania kufuzu kucheza hatua ya makundi tayari kwa fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil.
Awali safari ya Stars ilikuwa ifanyike jana, lakini ilikwama kutokana na kuchelewa kupatikana kwa viza kuingia nchini Chad, na sasa itapaa mchana huu kwa ndege ya Shirika la Ndege la Kenya.
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi fedha hizo juzi usiku kwenye hoteli ya New Africa, Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema fedha hizo ni motisha kwa wachezaji ili waweze kufanya vizuri.
"Naamini wengi mnafahamu timu yetu ina mtihani mkubwa wa kucheza na Chad Ijumaa wiki hii, na marudiano Novemba 15. Nimeona na mimi nitoe motisha kwa wachezaji ili wafanye vizuri," alisema Pinda.
"Naomba makampuni, taasisi, watu binafsi, na mashirika mbalimbali waisapoti timu yetu kwa hali na mali kwa wale wote wanaitakia heri Tannzania.
"Nimempa jukumu Waziri mwenye dhamana ya michezo Emmanuel Nchimbi kuhakikisha michango yote inapita kwake na inawafikia walengwa," alisisitiza.
Kocha wa Stars Jan Poulsen alisema wanakwenda kupambana kiume kwenye mchezo huo na kuwataka Watanzania kuwaunga mkono.

"Tumefanya maandalizi mazuri, sijaona mapungufu. Kwenye ushindani kuna kushinda, kushindwa au kwenda sare. Tumejiandaa kushinda mechi hii," alisema Poulsen.Naye Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodgar Tenga alimshukuru Waziri mkuu kwa kutoa mchango huo na kuahidi kuwapa wachezaji fedha hizo ikiwa ni motisha kwao.
Wakati huo huo, Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Bonifas Wambura, amesema jana kuwa msafara wa Stars utakuwa na watu 40 na utaongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya shirikisho hilo Eliud Mvella.
Pia wamo wajumbe wawili wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na baadhi ya mashabiki wa soka.
Msafara huo unatarajia kuwasili mjini N’Djamena, mji mkuu wa Chad leo saa 1.15 usiku saa za huko, sawa na saa 3.15 kwa muda wa nyumbani.

Aspirini ni kinga ya saratani

Wataalamu wa tiba wameshauri kua watu ambao afya yao inakabiliwa na uwezekano wa kukumbwa na saratani ya kibofu, wapewe dozi ya aspirini.
Jarida linalochapisha habari za utafiti wa wataalamu ''The Lancet'' limearifu kua tembe mbili kwa kila siku zilipunguza saratani ya kibofu kwa asili mia 63% kati ya kundi la wagonjwa 861.
Wataalamu wengine wamesema kua utafiti huo umetoa mwangaza mpya kwamba aspirini inaweza kutumika katika kutibu saratani kwa ujumla.
Utafiti huu ulifanywa kwa kutumia wagonjwa 861 waliorithi maradhi haya ya saratani ya kibofu, ambayo huathiri mtu mmoja kati ya watu 1,000.
Kuna tatizo la kugundua wagonjwa kama hawa waliorithi magonjwa kama haya na tiba ya viini vya urathi huwa kazi kubwa, ikimaanisha kwamba kuna uwezekano kwao kukumbwa na maradhi kama saratani ya kibofu, kizazi na tumbo.
Uchunguzi wa wagonjwa wote wakati wa majaribio, wale waliokua katika kundi lililopewa miligramu 600 ya vidonge vya aspirini kwa kila siku, 19 kati yao walipatikana na uvimbe ikilinganishwa na uvimbe uliopatikana miongoni mwa wagonjwa ambao walikua wakitazamwa kwa karibu sana, ambao kiwango cha uvimbe kilipungua kwa asili mia 44.

Wataalamu hawa walipochunguza wagonjwa pekee waliotumia dawa hii kwa kipindi cha miaka miwili wakakuta kuna upungufu wa asili mia 63%.

Vilevile tiba hii ina athari juu ya saratani nyingine za uruthi, ambazo pia zilishuka kwa kadiri ya nusu kwa wagonjwa wanaochunguzwa kwa makini.
Profesa Sir John Burn, kutoka Chuo kikuu cha Newcastle alisema kua watu wazima 30,000 nchini Uingereza walirithi saratani ya kibofu.
Profesa Burn aliongezea kusema kua ikiwa watu hao watapewa matibabu basi tutapunguza saratani elfu kumi katika kipindi cha miaka 30 na kuonelea kua hilo linaweza kuepusha vifo takriban 1,000 kutokana na maradhi haya.
Hata hivyo, kuna athari zake pia.
"tukiweza kupunguza saratani 10,000 na kuzusha madonda ya tumbo 1,000 pamoja na kuondoa mishtuko ya moyo 100, kwa fikra za watu wengi ni bora kuliko kusubiri vifo, alisema Profesa Burns.
"watu wenye asili ya familia ambayo huathiriwa na magonjwa ya aina hii, hususan saratani ya kibofu ingefaa wajaribu dozi ndogo ya asipirini kama tabia."
Tangu hapo Aspirini ina sifa ya kupunguza maradhi ya mshituko wa moyo na kiharusi.
Utafiti mwingine katika kipindi cha miongo miwili iliyopita umeonyesha kua dawa aspirini hupunguza hatari ya saratani, ingawa utafiti huu wa sasa ndio wa kwanza kwa kutumia wagonjwa katika majaribio na kuhakiki aspirini katika kutibu saratani.
Moja ya maswali yaliyoulizwa kuhusu utafiti huu ni kama watu ambao hawana matatizo ya afya wala familia zenye historia ya ugonjwa huo wanaweza kutumia dawa hii.
Jibu likawa kua matumizi ya aspirini yanapunguza uwezekano wa saratani na maradhi ya moyo, kwa hiyo ni vizuri lakini kuna athari zake pia. Kwa Profesa Sir John, ni hoja nzuri hio kwa sababu yeye binafsi anaonelea kua athari za dawa hio ikilinganishwa na kiwango cha kuepuka saratani na maradhi ya moyo ni ndogo.
Hata hivyo anaonya kua atakayeamua kutumia aspirini kuepusha balaa la saratani, kiharusi au maradhi mengine ya moyo lazima achukue tahadhari. Matumizi ya dawa hio huongeza uwezekano wa madonda tumboni, kutokwa damu ndani ya tumbo ingawa wataepuka kiharusi kwa kutumia aspirini."

KIBOKO YA MUHAMMAD ALI, JOE FRAZIER AFARIKI DUNIA

Bingwa zamani wa ndondi za uzito wa juu duniani Joe Frazier amefariki baada ya kuugua saratani ya ini.
Joe Frazier ni mgonjwa sana
Joe Frazier wakati alipokuwa mgonjwa sana

Kulingana na familia yake, Frazier - anayejulikana pia kwa jina la Smokin' Joe - aligunduliwa anaugua saratani wiki kadha zilizopita na alikuwa anapokea matibabu.
Frazier mwenye umri wa miaka 67 alishikilia mkanda wa ubingwa wa dunia miaka kati ya 1970 na 1973.
Alikuwa ndiye mtu wa kwanza kumchapa Muhammad Ali mwaka 1971. Baadae akachapwa na Ali katika mapambano mawili yaliyofuatia.
Meneja wake Leslie Wolf amesema Frazier aligunduliwa na maradhi ya saratani ya ini mwezi uliopita na alikuwa anatibiwa katika nyumba maalum inayotunza wagonjwa mahututi huko Philadelphia.
Hapo jumamosi, Bw Wolf alisema hali yake haikuwa nzuri lakini madaktari wak walikuwa wanafanya kila juhudi kumsaidia.
Frazier alishinda taji la ubingwa wa dunia kwa uzito wa juu mwaka 1970 baada ya kumtwanga Jimmy Ellis mjini New York.
Aliendelea kushikilia taji hilo hadi mwaka 1973, ambapo alipigwa na George Foreman.
Lakini mwanamasumbwi huyo huenda anafahamika zaidi kwa mapambano makubwa na Ali, likiwemo lile la kukata na shoka la Phillipines lililopewa jina la Thriller in Manila mwaka 1975.

WAZIRI MKUU ITALIA KUJIUZULU

Waziri Mkuu wa Italia Silvio Berlusconi
Waziri mkuu wa Italia Silvio Berlusconi

Waziri Mkuu wa Italia, Silvio Berlusconi, amethibitisha kwamba atajiuzulu wadhifa huo.

Hata hivyo, amesema hataondoka hadi pale bunge litakapoidhinisha mpango wa marekebisho ya kufufua uchumi wa nchi hiyo.

Uchumi wa Italia umeathirika vibaya kutokana na mzozo wa madeni unaokumba mataifa yanayotumia sarafu ya Euro.

Mapendekezo hayo yatawasilishwa bungeni katika wiki mbili zijazo.

Bwana Berlusconi alitangaza mpango wa kujiuzulu baada ya kura iliyobainisha kuwa umaarufu wake bungeni umepungua.

Kiwango cha riba katika hawala ya serikali ya Italia ilishuka Jumatano iliyopita, kumaanisha kuwa sasa bei za hawala hizo zimeshuka kwa nchi hiyo kukopa kutoka kwa masoko ya kifedha.

Kulikuwa na fununu kuwa iwapo Bwana Berlusconi angejiuzulu, utawala ambao ungechukua nafasi hiyo ungeundwa na kundi la watalaam, ambao jukumu lao kuu lingekuwa ni kuinua uchumi wa nchi hiyo.

Lakini bwana Berlusconi amepinga hilo. Amesema kwa maoni yake,'' kufanyika kwa uchaguzi ndio njia pekee ya nchi hiyo kupiga hatua''.

Bwana Berlusconi ametawala siasa za Italia kwa kipindi cha miaka 17.

Ameponea kura 50 za kutokuwa na imani naye, lakini hivi karibuni amezongwa na misururu ya sakata za kisheria na ngono, pamoja na migororo ya kisiasa na kiuchumi.