Thursday, May 17, 2012

DEDICATION TO ALL PATRICK MAFISANGO,RWANDESE & SIMBA SPORTS CLUB SUPPORTERS-CANDLE IN THE WIND (ELTON JOHN)

LIVERPOOL WAMTIMUA KENNY DAGLISH

Kocha aliyetimuliwa Liverpool Kenny Daglish

Kocha Mkuu wa Liverpool Kenny Dalglish ametimuliwa kuifundisha klabu hiyo.

Taarifa iliyotolewa na klabu hiyo inasema uamuzi huo umefikiwa baada ya tathmini ya kina iliyofanywa.

"Baada ya kutathmini kwa makini klabu imefikia uamuzi na kuona mabadiliko ni ya muhimu" Imesema taarifa hiyo

"Matokeo ya ligi kuu ya Premia yametusikitisha na katika kulinda maendeleo yaliyopatikana ni lazima kufanya mabadiliko"


Dalglish kuondoka kwake kwenye klabu ''kumefanywa kwa utu na heshima kubwa''.

Kocha Mkuu wa Wigan Roberto Martinez na Kocha wa zamani wa Liverpool Rafael Benitez wanatajwa kuwa huenda wakachukua nafasi ya Dalglish.

Dalglish anaelezwa kutokuwa na matokeo mazuri katika ligi kuu ya England.

Kuondoka kwake kumekuja baada ya mazungumzo na wamiliki wa Klabu hiyo John Henry na Tom Werner mjini Boston,Marekani siku ya Jumatatu.

Zaidi ya Liverpool kufika fainali ya FA na kuchukua Kombe la Carling, timu hiyo imemaliza ligi kuu ya England ikiwa nafasi ya nane huku ikipoteza michezo mingi.


BREAKING NEWS...PATRICK "MUTESA" MAFISANGO AFARIKI DUNIA


Kiungo wa zamani wa Simba s.c Marehemu Patrick Mafisango"Mutesa"


Kiungo mashuhuri wa Simba sports club Patrick Mafisango amefariki ghafla katika ajali ya gari iliyotokea maeneo ya Tazara amabapo ni kituo cha gari moshi linalounganisha nchi ya Tanzania na Zambia,wilaya ya Temeke jijini Dar es salaam.

Chanzo cha ajali hiyo ni kitendo cha Marehemu Mafisango akiwa katika gari yake na mdogo wake alipojaribu kumkwepa muendesha pikipiki na katika harakati za kuokoa maisha ya muendesha pikipiki huyo hatimae gari la Mafisango liliacha njia na kuingia kwenye mtaro na kupinduka na kusababisha kifo cha mchezaji huyo wa Simba, katika ajali hiyo pia mdogo wake Mafisango alijeruhiwa vibaya na kukimbizwa hospitalini.

"Kifo cha Patrick mafisango kimetusikitisha sana hasa kipindi hiki ambachio alikuwa katika kiwango cha juu sana ametuachia pengo wanasimba" Alisema mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage alipohojiwa na kituo kimoja cha radiop nchini Tanzania.

Patrick Mafisango enzi za uhai wake akilisakata kabumbu

Mafisango akiwa amebebwa juujuu na wachezaji wenzake wakishangilia ushindi enzi za uhai wake

Mafisango kulia enzi za uhai wake akishangilia goli pamoja na mwenzake Emmanuel Okwi

Mafisango wa tatu kushoto waliosimama akiwa na kikosi cha Simba enzi za uhai wake

Mafisango akiwa amejipumzisha baada ya mazoezi na timu yake ya Simba

Mafisango katika swaga za kitaa enzi za uhai wake