Thursday, May 17, 2012

BREAKING NEWS...PATRICK "MUTESA" MAFISANGO AFARIKI DUNIA


Kiungo wa zamani wa Simba s.c Marehemu Patrick Mafisango"Mutesa"


Kiungo mashuhuri wa Simba sports club Patrick Mafisango amefariki ghafla katika ajali ya gari iliyotokea maeneo ya Tazara amabapo ni kituo cha gari moshi linalounganisha nchi ya Tanzania na Zambia,wilaya ya Temeke jijini Dar es salaam.

Chanzo cha ajali hiyo ni kitendo cha Marehemu Mafisango akiwa katika gari yake na mdogo wake alipojaribu kumkwepa muendesha pikipiki na katika harakati za kuokoa maisha ya muendesha pikipiki huyo hatimae gari la Mafisango liliacha njia na kuingia kwenye mtaro na kupinduka na kusababisha kifo cha mchezaji huyo wa Simba, katika ajali hiyo pia mdogo wake Mafisango alijeruhiwa vibaya na kukimbizwa hospitalini.

"Kifo cha Patrick mafisango kimetusikitisha sana hasa kipindi hiki ambachio alikuwa katika kiwango cha juu sana ametuachia pengo wanasimba" Alisema mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage alipohojiwa na kituo kimoja cha radiop nchini Tanzania.

Patrick Mafisango enzi za uhai wake akilisakata kabumbu

Mafisango akiwa amebebwa juujuu na wachezaji wenzake wakishangilia ushindi enzi za uhai wake

Mafisango kulia enzi za uhai wake akishangilia goli pamoja na mwenzake Emmanuel Okwi

Mafisango wa tatu kushoto waliosimama akiwa na kikosi cha Simba enzi za uhai wake

Mafisango akiwa amejipumzisha baada ya mazoezi na timu yake ya Simba

Mafisango katika swaga za kitaa enzi za uhai wake

No comments:

Post a Comment