Thursday, May 17, 2012

LIVERPOOL WAMTIMUA KENNY DAGLISH

Kocha aliyetimuliwa Liverpool Kenny Daglish

Kocha Mkuu wa Liverpool Kenny Dalglish ametimuliwa kuifundisha klabu hiyo.

Taarifa iliyotolewa na klabu hiyo inasema uamuzi huo umefikiwa baada ya tathmini ya kina iliyofanywa.

"Baada ya kutathmini kwa makini klabu imefikia uamuzi na kuona mabadiliko ni ya muhimu" Imesema taarifa hiyo

"Matokeo ya ligi kuu ya Premia yametusikitisha na katika kulinda maendeleo yaliyopatikana ni lazima kufanya mabadiliko"


Dalglish kuondoka kwake kwenye klabu ''kumefanywa kwa utu na heshima kubwa''.

Kocha Mkuu wa Wigan Roberto Martinez na Kocha wa zamani wa Liverpool Rafael Benitez wanatajwa kuwa huenda wakachukua nafasi ya Dalglish.

Dalglish anaelezwa kutokuwa na matokeo mazuri katika ligi kuu ya England.

Kuondoka kwake kumekuja baada ya mazungumzo na wamiliki wa Klabu hiyo John Henry na Tom Werner mjini Boston,Marekani siku ya Jumatatu.

Zaidi ya Liverpool kufika fainali ya FA na kuchukua Kombe la Carling, timu hiyo imemaliza ligi kuu ya England ikiwa nafasi ya nane huku ikipoteza michezo mingi.


No comments:

Post a Comment