Thursday, May 14, 2015

BURUNDI "KIMENUKA"



Makundi hasimu ya askari yanakabiliana katikati mwa mji mkuu wa Burundi- Bunjumbura, mahala ambapo tangazo lilitolewa jana Jumatano kuwa Rais Pierre Nkurunziza, amepinduliwa.
Makabiliano ya risasi yanaendelea kwa sasa, huku milipuko kadhaa ikisikika.
Radio na runinga ya taifa inang'ang'aniwa kwa sasa huku wanajeshi waaminifu kwa rais Nkurunziza ndio wanaoidhibiti.

Wednesday, May 13, 2015

WATCH LIIVEEEE REAL MADRID Vs JUVENTUS


21:45 - 23:45
Spain
The UEFA Champions LeagueReal Madrid vs Juventus

HALI ILIVYO BURUNDI BAADA YA NKURUNZINZA KUPINDULIWA


Wananchi wakishangilia Baada ya Nkurunzinza kupinduliwa


Waandamanaji wakijimwayamwaya mitaani









Wananchi wakishangilia Burundi




Raia wakikumbatiana katika bustani la uhuru Bujumbura 

 
Raia wakiwazoma maafisa wapolisi ambao awali walikuwa wakikabiliana nao 

Tuesday, May 12, 2015

WATCH BAYERN MUNICH Vs BARCELONA LIVEEEE


21:45 - 23:45
Germany
The UEFA Champions LeagueBayern Munchen vs FC Barcelona

BUNGE LA BAJETI KUANZA LEO, WASOMI WALIKOSOA

Bunge la Bajeti ya Serikali ya 2015/16 linaanza leo mjini Dodoma kwa mwendo wa mchakamchaka kutokana na kuongezwa saa mbili kila siku ili limalizike Juni 27.
Saa za mjadala katika vikao zimeongezwa ili kuziba pengo la siku 12 zinazopungua na kutoa fursa kwa wabunge kuchangia bajeti za wizara na Bajeti Kuu ya Serikali ndani ya siku 44 ikilinganishwa na siku 56 zilizotumika kupitisha bajeti ya mwaka 2014/15 na miaka ya nyuma.
Kutokana na hali hiyo, wachambuzi wa bajeti, wachumi na wanasiasa wamesema hawatarajii kuona jipya isipokuwa mipasho inayolenga Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.
Serikali imepanga kukusanya na kutumia Sh22.4 trilioni katika mwaka wa fedha 2015/16 ikiwa ni nyongeza ya Sh2.6 trilioni ikilinganishwa na Bajeti ya mwaka 2014/15 ambayo ilikuwa Sh19.8 trilioni.
Kwa miaka iliyopita, baadhi ya wizara zenye majukumu mengi zilikuwa zinatengewa siku mbili au tatu, lakini safari hii hali itakuwa tofauti kwa kuwa zitajadiliwa kwa siku moja tu au mbili kulingana na mjadala utakavyokuwa na mapumziko yatakuwa Jumapili pekee.
Mkurugenzi wa Habari, Elimu kwa Umma na Uhusiano wa Kimataifa wa Bunge, Jossey Mwakasyuka alisema badala ya Bunge kuanza saa 3.00 asubuhi hadi saa 7.00 mchana na baadaye saa 11 jioni hadi saa 1.45 usiku; sasa litaanza 3.00 asubuhi hadi saa 8.00 mchana na kuendelea saa 10.00 jioni hadi saa 2.00 usiku.
“Ili kuendana na muda, tumeongeza saa kadhaa ili kumaliza shughuli zote zilizopangwa. Siku za Jumamosi zitahesabika kama siku za kazi kama kawaida.” alisema.
Alisema Bunge hilo litamalizika Juni 27 lakini akaongeza: “Tumeacha siku tatu za dharura, kuanzia Juni 28 hadi 30 ili kama kuna jambo lolote la muhimu litajitokeza Bunge linaweza kuendelea kwa muda huo wa siku tatu.”
Alisema kutokana na mabadiliko ya uwasilishaji, ni lazima bajeti iwe imesomwa kabla ya kuanza utekelezaji wa bajeti ya mwaka unaofuata Julai Mosi.
“Inawezekana tukapata kiongozi wa kulihutubia Bunge au katika upitishaji wa bajeti za wizara akidi isitimie na kulazimika shughuli husika kuendelea siku inayofuata. Zamani Bunge la Bajeti lilikuwa likianza Juni hadi Agosti, lakini kwa mabadiliko haya sasa lazima limalizike Juni,” alisema.
Alisema bajeti zote za wizara hadi kufikia Juni 10 zitakuwa zimeshasomwa, Juni 11 itasomwa Bajeti Kuu ya Serikali na kuanza kujadiliwa.
Alisema ratiba hiyo pia inaweza kuvurugika utakapoanza mfungo wa Ramadhani.

Friday, May 8, 2015

TASWIRA YA JIJI LA DAR NA MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA












Maeneo ya Jangwani jijini Dar



Gari limetumbukia kwenye daraja lililobomoka maeneo ya Mbezi Makondeni kwa Mahita








Mmoja ya wakazi walioathirika na mafuriko







Mtaa wa Azikiwe jijini Dar









Lori la kokoto likiwa limezama Mto Msimbazi jijini Dar


Thursday, May 7, 2015

LIGI KUU SPAIN YAPIGWA "STOP"



Wapenda soka ulimwenguni hususani wanaopenda kuangalia ligi kuu ya Uhispania wale mashabiki wa Barcelona na Real Madrid bila kusahau wazee wa mikeka wataimiss ligi hiyo baada ya kusimamishwa,Hatua hii inafuatia mtafaruku baina ya shirikisho la ligi kuu la Uhispania na serikali ya taifa kuhusiana na ugavi wa mapato ya haki miliki ya kupeperusha mechi.
Pande zote zimeshindwa kukubaliana kuhusu ugavi wa mapato ya matangazo ya mechi za ligi hiyo maarufu duniani.

Agizo hilo liitaanza kutekelezwa kuanzia tarehe 16 mei.
Maamuzi  hayo yataathiri zaidi ya wachezaji laki sita (600,000) na mechi elfu thelathini (30,000).
Kufikia hizi sasa Barcelona inaongoza jedwali la La Liga,wakiwa na alama mbili pekee zaidi ya wapinzani wao wakuu Real Madrid huku zikiwa zimesalia mechi tatu tu msimu ukamilike.
Serikali kuu imepitisha mswada mpya ambao utasimamia ugavi wa fedha zinazotokana na hati miliki ya matangazo ya mechi hizo za la Liga.

Mswada huo unaungwa mkono na muungano wa wachezaji wa kulipwa LFP.
Mkataba uliopa sasa inaziruhusu vilabu viwili vikuu nchini humo yaani , Barcelona na Real Madrid kukubaliana kivyao kuhusu nani atapeperusha mechi zao.
Kuna madai kuwa timu hizo mbili zinatia kibindoni nusu ya mapato yanayotokana na mechi zao.
Shirikisho lenyewe limesema kuwa linafahamu hasara itakayotokea lakini halijafunga mlango wa majadiliano.