Tuesday, June 14, 2011

TOFAUTI YA PROFILE ZA WASICHANA/WANAWAKE NA WAVULANA/WANAUME KATIKA FACEBOOK

Mtandao wa kijamii wa Facebook maarufu kama FB umezidi kuchukua umaarufu siku hadi siku na katika hilo naweza kusema mtandao huu wa kijamii umeteka Dunia.
Katika mtandao huu watu hupata marafiki aidha kwa kujuana au kwa kujuana ki facebook facebook tu na kuombana urafiki kisha wanaendelea na mawasiliano. Kuna kitu kinaitwa Profile hapa ni pale ambapo habari binafsi za mwanachama hupatikana kama vile yeye ni nani,yupo wapi na anafanya shughuli gani vilevile unapata kuona picha zake ambazo amezihifadhi yeye.
Katika hizi PROFILE nimegundua kuwa za wasichana au wanawake zipo tofauti sana na za wale wa jinsia ya pili yaani wanaume, Tofauti hiyo ni hii;
Mwanamke akiandika kitu katika sehemu ya status kwa mfano; Najisikia vibaya......
Mwanaume nae aandike mfano; nimepata ajali nimeumia sana......
Sasa basi status ya mwanamke ina dakika moja tu tangu aandike, na mwanaume ina siku nne tokea aiandike lakini matokeo yatasomeka hivi;
Katika muda huo mfupi mwanamke atakuwa na likes 60, mwanaume atapata likes 1.
watakao comment kwa mwanamke watafikia 104 wakati mwanaume atapata comment 3.
Ukisoma walicho-comment kwa mwanamke kitasomeka hivi, Imekuwaje?
Sasa ninajiuliza mwanamke kaandika tu..najisikia vibaya lakini mwanaume kaandika kitu serious kwamba amepata ajali lakini duh..kila mtu anahitaji kuwasiliana na mwanamke,haya ndio yanayotokea katika mitandao mingi ya kijamii hasa FACEBOOK.

No comments:

Post a Comment