Monday, July 25, 2011

AMY WINEHOUSE AFARIKI DUNIA

Mwimbaji maarufu mwanamke wa Uingereza, Amy Winehouse, amekutwa amekufa katika fleti yake mjini London.


Amy amefariki akiwa na umri wa mika 27 tu.
Amy Winehouse alishinda tuzo kadha kwa albamu yake ya pili, Back to Black, ambayo ilitolewa mwaka 2006.

Sababu ya kifo chake haijajulikana.

Lakini mwimbaji huyo amekuwa akipambana na uraibu wa ulevi na mihadarati kwa muda.

Mara nyingi alitokeza kwenye tamasha akiwa amelewa.

1 comment: