Thursday, July 21, 2011

MAN UNITED YAICHAKAZA SEATTLE SOUNDERS 7-0 NGASSA NDANI

Rio Ferdinand akiondosha mpira mbele ya Mrisho Ngassa

Mshambuliaji wa Man United Wyne Rooney amepiga Hat-Trick katika mechi yao dhidi ya Seattle Sounders wakiwa ziarani nchini Marekani, Rooney alipiga mabao matatu akitokea benchi. Goli la kwanza la Man lilifungwa na Michael Owen Dk 14 baada ya kazi nzuri ya kupasiana mpira kati ya Ashley Young na Evra.Goli la pili lilipatikana Dk 29 mfungaji akiwa ni Macheda kabla ya Rooney kupiga goli Dk 51 na Park akapiga lingine Dk52  na Rooney kuchomeka lingine.
Rooney alipiga goli lake la tatu Dk 71 na la sita kwa Man kabla ya Gabrieol Orbertan kuhitimisha karamu hiyo kwa goli la saba katika Dk 88.
Katika mechi hiyo mtanzania Mrisho Khalfan Ngassa alicheza upande wa Seattle Sounders ikiwa ni mechi yake ya majaribio. mpaka gmechi inakwisha kina Ngassa walikuwa wameloa goli 7 kwa buyu.
 Zifuatazo ni picha katika mechi hiyo


Rooney na Nani

Giggs akichuana vikali

Van Der Sar akipangua mchomo

Umati wa mashabiki

Uwanja wa Seattle Sounders

No comments:

Post a Comment