Thursday, July 28, 2011

WANIGERIA WAZICHAPA NDANI YA JUMBA LA BIG BROTHER AFRICA

Asubuhi ya leo Karen alimshambulia Vina kwa maneno akimshutumu na kumpasha kwa kujipendekeza kwa Lomwe wakati hamtaki hali iliyozua tafaruku kati ya mabinti hao ndani ya jumba la Big Brother africa, Karen na Vina wote wanatoka Nigeria.

Karen (kushoto) na Vina (kulia)
Awali mabinti hao walishutumiana katika vitu fulanifulani na kuanza kushikana nguo hali iliyomfanya Hanni aingilie kati ili kunusuru amani baina ya mabinti hao wawili, "mmoja akiwa moto, lazima mmoja awe maji" alisikika Hanni akiwasihi mabinti hao waache ugomvi, Kitendo cha Hanni kumsihi Vina aachane na Karen na amzoee kwani ndivyo alivyo kilionekana kumjaza ghadhabu zaidi Karen, ambapo ugomvi huo ulianza 26 julai, siku ambayo ilikuwa ni birthday ya Vina, siku hiyo Vina alibainisha kuwa Karen utani wake umezidi mipaka na sasa sio utani tena bali ni kusambaza uongo. Zikiwa zimebaki siku mbili.je wanigeria hao wataweza kushinda?

No comments:

Post a Comment