Thursday, August 25, 2011

ARSENAL YAIADHIBU UDINESE YATINGA HATUA YA MAKUNDI KLABU BINGWA ULAYA

Timu ya Arsenal ya Uingereza hatimae imefanikiwa kutinga katika hatua ya makundi ya michuano ya klabu bingwa ya ulaya baada ya kuilaza Udinese ya Italy 2-1, kwa matokeo hayo yaliiondosha Udinese kwa jumla ya mabao 3-1 kwani ikumbukwe mchezo wa kwanza uliochezwa Emirates Arsenal ilishinda
1-0.
Katika mesci hiyo Udinese ndio walikuwa wa kwanza kutia kambani kupitia mchezaji wake De Natali kabla ya Arsenal kusawazisha kupitia Mshambuliaji mahiri Van Persie baada ya kazi nzuri na ya kuridhisha iliyofanywa na Gervinho kwa kuwachambua mabeki wa Udinese na kumwagia majaro safi Van Persie nae bila ajizi akatia kambani, Goli la pili lilifungwa na Theo Walcott ambaye alionekana mwiba katika mechi hiyo akishirikiana vizuri na Gervinho.

Tazama magoli yalivyopatikana



No comments:

Post a Comment