Wednesday, September 28, 2011

Arsenal,Chelsea kibaruani leo ligi ya mabingwa ulaya

WINGA wa Chelsea, Juan Mata atakutana na rafiki zake wakati atakaporudi kucheza mechi Ligi ya Mabingwa dhidi ya Valencia leo ikiwa ni miezi mwezi moja tangu alipoondoka.

Kocha Andre Villas-Boas alitumia karibu dola 40.4 milioni kumsajili nyota huyo mwenye miaka 23 na tayari ameonyesha uwezo wake kwa kufunga kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi E walioshinda 2-0 dhidi ya Bayer Leverkusen.“Nipo tayari kucheza dhidi yake na wote tunamsubili,” alisema winga Valencia, Pablo Hernandez aliyekuwa wakilala chumba kimoja na Mata.

“Itakuwa ni siku yake nzuri kurudi nyumbani, lakini hatutakuwa na urafiki uwanjani. Tutafanya kila kitu kuhakikisha tunawafunga pamoja na Juan, baada ya hapo tutamtakia mfanikio mema.”

Chelsea wapo ipo kwenye kiwango cha juu baada ya kushinda 4-1 dhidi ya Swansea City pale Jumamosi na kuwafanya wapande hadi nafasi ya tatu katika Ligi Kuu, nyuma kwa pointi tatu kwa vinara Manchester United na Manchester City.Mshambuliaji wa Hispania, Fernando Torres alitolewa nje kwa kadi nyekundu dakika 39 pale Jumamosi, lakini anaonekana kurudi kwenye kiwango chake akiwa ameshafunga mabao mawili katika mechi mbili mfululizo.

Safu ya ushambuliaji wa Chelsea imeimarika na kurejea kwa nyota wa Ivory Coast, Didier Drogba aliyeingia kuingia akitokea benchi na kufunga baada ya wiki nne za kuwa nje kwa sababu ya kuumia.

LONDON, Robin van Persie ameanza kuthibisha kwamba anaweza kuiongoza Arsenal anategemewa kuibeba klabu hiyo leo kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Olympiakos.Van Persie alichukua unahodha huo baada ya Cesc Fabregas kutimikia Barcelona, Robin alifunga mabao mawili waliposhinda 3-0 dhidi ya Bolton Wanderers Jumamosi.

Olympiakos wenyewe wamepoteza mechi tisa walizocheza dhidi ya timu za England kwenye mashindano ya Ulaya, wakiwa wamefungwa mabao 29 na wao kufunga moja tu.

Van Persie, 28, ameshafunga mabao matano msimu huu na Wenger anaamini Mdachi huyo aliyeripotiwa na vyombo vya habari vya England, Jumatatu hataki kuharakisha kuongeza mkataba wake wake unamalizika 2013, kuwa kwa sasa amekuwa na anaweza kuongoza kwenye ufungaji na kuwatia moyo wenzake.

“Robin amekuwa kutoka mvulana anayesumbuliwa na presha za jamii wakati anakuja hapa na leo ni mtu mzima,” Wenger aliimbia tovuti ya Arsenal.Hilo alitakuwa vumbi pekee kutimka wiki hii Ulaya mashariki wakati BATE Borisov watakapowakaribisha mabingwa wa Ulaya, Barcelona katika mchezo wa Kundi H hapo leo.

BATE walitoka sare1-1 na Belshina Bobruisk pale Ijumaa, Barca walituma salamu kwa kuisambaratisha Atletico Madrid 5-0 Jumamosi huku mchezaji bora wa Dunia, Lionel Messi alifunga mabao matatu peke yake.

No comments:

Post a Comment