Monday, September 19, 2011

Man United Tottenham Blackburn Zafanya mauaji, Arsenal Liverpool Chelsea Hoi Ligi kuu Uingereza

Wayne Rooney alifunga bao lake la tisa msimu huu wa ligi kuu ya Premier ya England, na kuiwezesha Manchester United, ikicheza katika uwanja wa Old Trafford siku ya Jumapili, kuifunga Chelsea magoli 3-1.

Mchezaji huyo wa timu ya taifa ya England aliweza kufunga bao la tatu, baada ya wenzake Chris Smalling kufunga bao la kichwa kufuatia mpira alioupata kutoka kwa Ashley Young, na Nani alikuwa pia amefunga la pili kutoka yadi 25.

Magoli yote mechi ya Man United na Chelsea

Mara tu baada ya kipenga kuashiria kipindi cha pili kuanza, Fernando Torres aliweza kuandikisha haraka bao lake la pili akiichezea Chelsea na kuwapa mashabiki wengi matumaini ya kusawazisha mambo katika kipindi cha pili.

Torres akikosa goli la wazi

Chelsea walipata moyo zaidi wa mambo kubadilika, hasa Rooney alipokosa kufunga kupitia mkwaju wa penalti, walioipata Man U baada ya Jose Bosingwa kumwangusha Nani.

Wasiwasi wa pekee kwa Sir Alex Ferguson, meneja wa Man U, ilikuwa ni kumtizama Javier Hernandez akichehemea katika kipindi cha pili, kufuatia Ashley Cole kumpata mguu.

Kulikuwa na matumaini ya Torres kuhakikisha angalau mechi ilikwisha kwa Chelsea kufungwa magoli 3-2, lakini mguu wake ulithibitisha kabisa ulishindwa kutimiza wajibu wakati huu, kwani mpira ulielekea juu, huku lango likiwa wazi kabisa.

Katika mechi nyingine za Jumapili, mpira kweli hauna adabu, na usiwacheke wenzako kwa kufungwa.

Adebayor alifunga magoli mawili katika mechi yake ya kwanza uwanja wa nyumbani wa White Hart Lane

Liverpool waliaibika kwa kufungwa na Tottenham katika uwanja wa White Hart Lane magoli 4-0.

Matukio na magoli yote Tottenham na Liverpool

Msimu huu inaelekea kila timu inataka kuweka kibindoni magoli mengi, kwani Sunderland, katika ushindi wake wa kwanza msimu huu, pia iliizaba Stoke magoli 4-0, kufuatia kutambua wapinzani wao walikuwa dhaifu mno katika kuimarisha ngome yao.

Sunderland vs Stoke City

Emmanuel Adebayor, ikiwa ni mechi yake ya kwanza katika uwanja wa nyumbani tangu kusajiliwa na Tottenham, alifunga magoli mawili, na Luka Modric na Jermain Defoe pia wakifunga.

Majirani wa Man U, Man City, walishindwa kuwika katika uwanja wa Craven Cottage, kwani licha ya kuongoza kwa magoli 2-0, hatimaye mchezo ulimalizika kwa sare ya 2-2.

Fulham na Man City

Arsenal Hoi Bin Taaban
Blackburn imeweza kupata ushindi wake wa kwanza katika Ligi Kuu ya England msimu huu na kumpunguzia ugonjwa wa moyo meneja wao Steve Kean baada ya kuwa nyuma lakini wakafanikiwa kuilaza Arsenal mabao 4-3 katika uwabnja wa Ewood Park.
Wachezaji wa Blackburn
Wachezaji wa Blackburn

Gunners walikuwa ndio wa kwanza kupata bao lililofungwa na Gervinho kutoka umbali wa yadi 12 lakini Blackburn walisawazisha kwa bao rahisi lililowekwa wavuni na Yakubu.
Mikel Arteta akaifungia Arsenal bao la pili kwa mkwaju safi wa yadi 18 kabla Alex Song hajajifunga mwenyewe.
Matukio na magoli Arsenal na Blackburn 
Yakubu tena akaipatia Blacburn bao la tatu na kufanya ubao wa matokeo usomeke 3-2, na muda mfupi baadae Laurent Koscielny akajifunga mwenyewe kabla ya dakika za mwisho Marouane Chamakh kuipatia Arsenal bao la kufutia machozi.
Kabla ya mechi hiyo mashabiki wa Blackburn walifanya maandamano wakitaka meneja wao Kean atimuliwe.
Koscielny akijifunga

Song akijifunga katika mechi hiyo
Wiki nzima meneja huyo alikuwa akijigamba kwamba yeye ni meneja anayefaa kwa klabu hiyo ya Blackburn na matokeo ya mechi hiyo dhidi ya Arsenal yanaweza kumfariji na kumuweka mahali pazuri kulinda nafasi yake.

No comments:

Post a Comment