Thursday, February 9, 2012

Ivory Coast yaichapa Mali yaifuata Zambia fainali kombe la mataifa ya Afrika

Ivory Coast itakutana na Zambia kwenye fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya timu hizo mbili kushinda mechi zao za nusu fainali.
Ivory Coast imefuzu baada ya kuishinda Mali 1-0 katika nusu fainali yao mjini Libreville, nchini Gabon.
Ivory coast 1-0 Mali

Bao la ushindi la Ivory Coast lilifungwa na mchezaji wa Arsenal Gervinho katika kipindi cha pili.
Awali katika mji wa Bata nchini Gabon Zambia iliibandua Ghana kutoka mashindano hayo kwa kuifunga 1-0.
Bao la Zambia lilifungwa katika dakika ya 78 na mshambuliaji Emmanuel Mayuka.
Katika kipindi cha kwanza mshambuliaji wa Ghana Asamoah Gyan alikosa kufunga penalti, mlinda mlango wa Zambia akautema nje mpira.
Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika itachezwa siku ya Jumapili mjini Libreville, nchini Gabon, mechi ambayo itatangazwa moja kwa moja kupitia Idhaa ya Kiswahili ya BBC.

No comments:

Post a Comment