Monday, February 20, 2012

R.I.P Mohammed Wardi


Mohammed Wardi

Mwimbaji maarufu wa Sudan, Mohammed Osman Wardi, amefariki mjini Khartoum akiwa na umri wa miaka 80.
Alivutia watu kupenda ala za asili za kabila lake, la WaNubi.
Kwa sababu ya maoni yake ya mrengo wa kushoto, Mohammed Osman Wardi alifungwa na Rais Jaafar Numeri katika miaka ya '80, na akahamia uhamishoni wakati rais wa sasa, Omar al-Bashir, aliponyakua madaraka mwaka wa 1989.
Mohammed Wardi kwenye concert Addis Ababa

No comments:

Post a Comment