Saturday, March 31, 2012

WEMA AMWAGA CHOZI KWA KUTOLEWA NISHAI NA DIAMOND UKUMBINI KATIKA SHOW KALI MLIMANI CITY











Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya, Diamond Platinum akiwarusha mashabiki waliohudhuria katika tamasha lake la Diamond Are Forever lililofanyika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.











Diamond akitema cheche katika tamasha hilo














Diamond akitia mbwembwe mbele ya mashabiki wake














Dancers wakimpa support Diamond kufanya makamuzi










Sehemu ya umati wa mashabiki waliohudhuria show hiyo













Diamond akiendeleza makamuzi mbele ya mashabiki











Diamond anazidi kuwapagawisha mashabiki











Songombingo lilianzia pale Dimond aliposhuka stejini na kwenda kwenye meza waliyokaa wakina  Steve Nyerere na Mboni Masimba na ndipo walipompa t-shirt ambayo kwa mujibu wa udadisi na uchunguzi wa udadavuzi wa mambo wa Kajuna Blog, ilisemekana kuwa t-shirt hiyo ilikuwa inapicha ya mwanadada ambaye alikuwa akitoa na Diamond kwa sasa. Na ilikuwa ni maalum kwa ajili ya kumrusha roho Wema Sepetu.













Kazi ikaanza Mboni Masimba anamvalisha T'shirt yenye picha ya mpenzi mpya wa Diamond Steve Nyerere anatunza














Mhh........shabiki huyu akimtunza Diamond Dola za kimarekani watu vinywa wazi kulikoni?












Baada ya kutunza dolare za kutosha akaachia tabasamu nene














Wema nae akanyanyuka kwenda kutunza na pesa zikakataliwa














Wema kaganda akilazimisha Diamond apokee zile pesa bila mafanikio..ndio kwanzaaa kidume kiko bizeeeee!!!!!












Baada ya Diamond kugoma kutunzwa na Wema,Wema aliondoka stejini kwa hasira mithili ya Simba aliejeruhiwa









'Michuzi' aliyoikataa Diamond ikiwa stejini haijui iende wapi....













Hapo sasa 'Nimpende nani' uwanjani














Mlimbwende Jokate Mwegelo akijiachia na mashostito zake.














Diamond akimwaga mauno katika meza aliyokaa Jokate
















Mwanadadafada Mboni Masimba akiwa ametinga T'shirt yenye picha ya kifaa kipya cha Diamond














Baadhi ya wadau walimuita mshereheshaji wa show hiyo Taji Liundi akambembeleze Diamond aende kumuomba msamaha Wema lakini Diamond akasema 'nope'













Diamond akijiachia na warembo













Mashosti wakijaribu kumbembeleza Wema aache kulia kwani hayo yote ni ya dunia














Duuuh..Wema akizidi kumwaga chozi!
"sitakiiiiiiiiiiiii aaaaaaaaaaaaaaaaah aaaaaaaaaaaaaaaaaaaahhhh wakunifanyia hivi mimi jamani aaaaaaaaaaaaaaaaah aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaah diamond diamond aaaaahhh aaaaaahhhhhh!!















Ommy Dimpoz akitoa ushuhuda walipotokea na Diamond














Ushuhuda ulimgusa Diamond na kumwaga chozi "mhmhhmmmmmm"














Amini na Barnaba wakimpa shavu Diamond katika show hiyo.
















Hatimae Wema atuliza machungu kwa kumtunza Barnaba! "chukuaaa si anajifanya mjanja ataona akinitaka tena simtaki"


No comments:

Post a Comment