Tuesday, April 3, 2012

DIVA AMCHANA WEMA, AFAGILIA DIAMOND KUWA NA JOKATE


LOVENESS LOVE "DIVA"

Mtangazaji wa kipindi cha ala za roho kupitia kituo cha redio cha Clouds FM 88.4 Loveness Love 'Diva' amefunguka na kumchana 'live' Msanii maarufu wa filamu za bongo Wema Sepetu kwa kile kilichoonekana kukerwa na tabia 'chafu' za msanii huyo.
Kupitia kipindi cha ala za roho ambacho huendeshwa mida ya usiku kupitia kituo cha Clouds FM Diva alikitumia kipindi hicho ipasavyo kumchana Wema baada ya kupatwa na mkasa wa kuachwa solemba katika show baada ya kuwekeana makubaliano kuwa Wema afanyiwe mahojiano 'interview' lakini hakutokea.

Loveness Love "DIVA" na mpenzi wake Mo Racka

Diva alifunguka huku akimshutumu Wema kwa kutojali kazi za wenzake"Yeye ni kazi yake na wenzake tupo kazini lazima abadilike aheshimu kazi za wenzake"Alisema Diva.
Diva alielezea kuwa baada ya Wema kutotimiza makubaliano alijaribu kumtafuta katika simu ya mkononi lakini Wema alikuwa hapokei ndipo alipompigia Meneja wa Wema ajulikanae kama Martin.
Diva anasema kuwa alichojibu Meneja huyo ni kuwa Wema ni mtu anaependa 'Drama na atention' akiwa na maana Wema ni mtu wa kupenda michezo ya kuigiza na kuwafanya watu wawe makini na nini kilichotokea ni kama aina ya mtu anaependa skendo hivi ili watu waweze kumfuatilia mara kwa mara.


Wema Sepetu

Diva alikasirishwa na tabia hiyo na kusema kuwa kama Wema ni mtu wa kupenda drama ndio maana Diamond amemmwaga,'kama ni kweli Diamond anatoka na Jokate namuunga mkono kwasababu hakuna mwanaume anaependa 'drama na attention' " alisema Diva.'
'Kama unapenda penda mtu kama Jokate' aliongeza Diva kwa kile kilichoonekana kumfagilia Jokate kuwa na Diamond na kumkejeli Wema kwa kupigwa chini.
Katika kuweka msisitizo Loveness Love Diva akaweka wimbo wa Dioamond "Nimpende nani?" na akaendelea kupiga vijembe akisema mpende Jokate. Hapa alinikumbusha show ya Diamonds are forever iliyofanyika pale Mlimani City ambapo baada ya kupigwa wimbo wa Diamond Nimpende nani,ukumbi ulilipika kwa shangwe na kila mtu akimtupia jicho Wema nahisi ndio kitu kinachoitwa drama na attention anachokipenda Wema,mwisho katika Wimbo wa nimpende nani mwisho kuna kibwagizo kinachosema "nani amenuuuna?" basi Diamond alipofika katika kibwagizo hicho watu ukumbini walikuwa wakiitikia "Wemaaaaa","nani amenuuna?"..."Wemaaaaaaa".


Diamond "rais wa wasafi"

Jokate Mwegelo

Diva hakuishia hapo ndipo alipoanza kuuchambua wimbo wa Barnaba "Magubegube". ikumbukwe Barnaba pia alikuwepo katika show ya Diamonds are forever,show ambayo Diva aliifagilia ile mbaya akisema hakika ni next level,"Elfu hamsini(50,000) na tiketi zimeisha watu wamejaa show baab kubwa" alisema Diva.

Diamond akimlisha Wema keki enzi za mapenzi yao

Diva alipoweka wimbo wa magubegube akasema" Usiombe ukutane na magubegube,Diamond amekutana nayo na sasa yanamsumbua lakini amesimama imara na wanaume wengi wamekutana nayo" Hii ni dhahiri kuwa ni vijembe kwa Wema na kumfananisha na Gubegube.
Jamani show ya Diamonds are forever ilikuwa ni baab kubwa elfu hamsini na tiketi zimeisha watu kibao show ya nguvu ni maneno ambayo Diva aliyarudia mara kwa mara akimfagilia Diamond na kusema kuwa amefungua milango kwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya hapa bongo.

No comments:

Post a Comment