Tuesday, April 24, 2012

EVERTON YAIBANA MBAVU MAN UNITED


Nani akipigilia msumari huku kipa wa Everton akichumpachumpa bila mafanikio

Matumaini ya Manchester United kunyakua taji la ubingwa wa Ligi ya Kandanda ya England yalitiwa doa wakati Everton ilipopigana kiume wakiwa nyuma ya mabao 4-2 na kumaliza mchezo kwa sare ya mabao 4-4 katika mpambano wa kusisimua hasa dakika za mwisho kwenye uwanja wa Old Trafford.
Wayne Rooney aliisawazishia Manchester United baada ya kuunganisha kwa kichwa pasi kutoka kwa Nani baada ya bao la kuongoza la Everton lililofungwa kwa na Nikica Jelavi.


Rooney akitupia kambani katika mechi hiyo

Danny Welbeck na Nani waliipatia Manchester United mabao mawili kabla Marouane Fellaini kufunga bao moja jingine kwa Everton.

Rooney alionekana kuipatia ushindi Man United alipopachika bao la nne na muda mfupi baadae Everton wakacharuka na kupachika mabao mawili katika muda wa dakika tatu kupitia kwa Jelavic na Steven Pienaar.


Fellaini akipiga kichwa mbele ya Ferdinand na kuipatia bao la kusawazisha Everton

Katika dakika za mwisho, Patrice Evra alipiga mpira wa kichwa uliogonga mlingoti wa lango la Everton akiwa karibu kabisa na baadae mlinda mlango wa Everton Tim Howard aliokoa kwa ustadi mkubwa mkwaju wa Rio Ferdinand na kuinyima ushindi Manchester United.

Manchester United hata hivyo bado wanaongoza Ligi Kuu ya England wakiwa na pointi 83.

Dah hawa watoto vipi wametumwa?

No comments:

Post a Comment