Monday, April 16, 2012

MAN U YAIFUMUA ASTON VILLA 4-0, CHELSEA YAIZABUA SPURS 5-1

Chelsea thrash Spurs to reach FA Cup final
Drogba na wachezaji wenzake wakishangilia goli

Chelsea iliwachapa Tottenham mabao 5-1 nakuingia katika fainali za kombe la FA ambapo watakutana na Liverpool.
Hata hivyo ushindi huyo haukukosa manung'uniko baada ya refa kuipa Chelsea goli ambalo ilidaiwa kuwa mpira ulikuwa haujavuja mstari wa goli.
Utata huo sasa umeibua mjada kwamba kuna haja ya kuanzishwa mara moja kwa utaalam wa kuangalia kama mpira umevuka mstari wa goli au la.

Goooooooooooooooal!!!

Ushindi huo mnono umempa raha mkufunzi wa Chelsea Roberto di Matteo kwani umeiweka katika hali nzuri ya kupambana na Barcelona watakapowatembelea siku ya Jumatano.
Wakati Chelsea wakifurahia ushindi wao Spurs walikua na malalamiko chungu nzima kwani walidai kuwa walikuwa wanaonewa pale mpuliza kipenga ,Martin Atkinson alipowapa Chelsea bao la utata.

MAN UNITED YAUA

Manchester United imeongeza wigo wa pointi hadi tano dhidi ya Manchester City kileleni mwa Ligi Kuu ya Kandanda ya England lakin i ushindi wao dhidi ya Aston Villa uligubikwa kwa mara nyingine na penalti iliyoonekana ni ya utata.

Wayne Rooney - Manchester United v Aston Villa - Premier League
Rooney akitupia kambani kwa mkwaju wa penati

Ashley Young, ambaye alifanikiwa kupata penalti wakati Manchester United walipocheza na QPR, kwa mara nyingine alifanikiwa kupata penalti baada ya kutegewa na Ciaran Clark.
Kuguswa huko kwa Young kulikuwa kudogo sana lakini Wayne Rooney alifanikiwa kufunga mkwaju huo wa penalti kabla Danny Welbeck kuipatia Manchester United bao la pili.
Villa iliimarika kidogo baada ya kipindi cha pili lakini walikuwa Rooney na Nani walioandika mabao mengine mawili yaliyohitimisha karamu ya mabao 4-0.
Wayne Rooney - Manchester United v Aston Villa - Premier League
Rooney katikati na Young mgongoni pamoja na Carrick wakishangilia goli la Rooney

Manchester United walionekana kikosi bora zaidi katika kipindi cha kwanza na ushindi huo umepunguza pia deni la mabao ya kufunga na Manchester City na sasa kuwa manne.
Lakini bado swali litaendelea kubakia kwa wapenzi wa kandanda juu ya Young anavyojiangusha na aliposhutumiwa alipofanya hivyo dhidi ya QPR, ambapo Shaun Derry aliadhibiwa kwa kumsukuma mshambuliaji huyo wa pembeni na alioneshwa kadi nyekundu.
Rufaa iliyokatwa na Rangers ilitupiliwa mbali na Chama cha Kandanda cha England na shutuma zitaendelea kumuandama Young kutokana na alivyofanya kwa mara nyingine.
Na kubwa zaidi Young alifanya hivyo kwa timu aliyowahi kuichezea na itaongeza zaidi chumvi kwenye jeraha kwa timu ya Aston Villa.
Wayne Rooney - Manchester United v Aston Villa - Premier League
Rooney akishangilia bao

Villa walishindwa kuivunja rekodi dhidi yao wanapopambana na Manchester United, ambapo wamewahi kushinda mara moja tu katika mechi 31.
Jambo muhimu ni kwamba wapo pointi sita juu ya msatari wa kuteremka daraja na sasa wanajiandaa kwa pambano dhidi ya Sunderland, Bolton na West Brom ambapo lazima watafute pointi kujihakikishia hawateremki daraja.

No comments:

Post a Comment