Tuesday, June 19, 2012

EURO 2012 JESUS AIPELEKA SPAIN ROBO FAINALI


Jesus Navas akitupia kambani goli la pekee na la ushindi

Jesus Navas alikuwa ni mkombozi wa timu ya Uhispania, pale alipotupia kambani dakika za lala salama dhidi ya Croatia, na kuiwezesha nchi yake kufuzu katika hatua ya robo fainali za mashindano ya Euro 2012.


Nakuja kwako Modric.........Andre Iniesta"fundi" akiwa amekusanya kijiji cha wa-croatia

Ilielekea kana kwamba mabingwa watetezi Uhispania walikuwa wakicheza mechi hiyo ya Jumatatu usiku kwa wasiwasi.
Hata hivyo Jesus, ambaye ni mchezaji wa Seville ya Uhispania, aliweza kupenyezewa pande maridadi na Andres Iniesta, na zikiwa zimesalia dakika mbili kabla ya mechi kumalizika, alifanikiwa kuipatia Uhispania bao, na kuwahuzunisha mashabiki wa Croatia.

Bao hilo moja lilihakikisha Uhispania inaongoza kundi la C.
Uhispania walicheza karata yao vyema, kwani kwa kumtoa Fernando Torres na mahala pake kuingia Jesus Navas, ni mchezaji huyo wa zamu aliyeweza kutupia kambani.

Sasa mabingwa watetezi wanasubiri kujua kama watakutana na England au Ufaransa katika timu nane ambazo zitasalia kucheza robo fainali.
A Croatian Football Fan Reacts AFP/Getty Images
Mhh ishakuwa sooo!!! shabiki wa Croatia akiwa amelowa baada ya chama lake kuchapwa na Spain

Croatian Midfielder Ivan Perisic (L) Vies AFP/Getty Images
Iniesta akifanya udambwidambwi

Croatian Midfielder Luka Modric Controls AFP/Getty Images
Luka Modric akituliza ngozi mbele ya Xavi

Fans Of Croatia's National Football Team  React At The End Of The Euro 2012 Football Championships AFP/Getty Images
Kichapo ni noma asikuambie mtu, mashabiki wa Croatia wakisononeka kwa machungu kufuatia kamba ya Jesus dakika za lala salama

Fans Of Croatia's National Football Team  React At The End Of The Euro 2012 Football Championships AFP/Getty Images
Shabiki wa Croatia akimnyamazisha mwenzake alieangua kilio uwanjani baada ya kichapo cha bao 1 kwa 0 kutoka kwa Spain katika dimba la Gdansk Arena

Fans Of Croatia's National Football Team React At The End Of The Euro 2012 Football Championships AFP/Getty Images
Jikaze babaaa ndio mpira huoo

A Fan Of Croatia's National Football Team Reacts AFP/Getty Images
A Fan Of Croatia's National Football Team Reacts AFP/Getty Images
A Fan Of Croatia's National Football Team Reacts AFP/Getty Images
Croatian Defender Ivan Strinic Reacts AFP/Getty Images
Croatian Defender Vedran Corluka  Reacts AFP/Getty Images
Wachezaji na mashabiki wa Croatia wakiwa katika majonzi mazito baada ya kushindwa kutinga robo fainali ya mashindano ya EURO 2012

No comments:

Post a Comment