Thursday, June 28, 2012

URENO YATOLEWA KAMASI NA SPAIN, SPAIN YATINGA FAINALI EURO 2012


Andre Iniesta akijaribu kumtoka beki wa Ureno.

Mhhh sikio la kufa halisikii dawa.....C.Ronaldo akiwa ameduwaa baada ya kipigo

Mabingwa watetezi Uhispania wametinga fainali ya EURO 2012 baada ya kuifumua Ureno 4-2 katika changamoto za mikwaju ya penalti, baada ya dakika 90 na dakika 30 za ziaida kumalizika kwa timu hizo mbili kushindwa kufungana.

Bao la penati la mwisho lilitupiwa kambani kwa umaridadi mkubwa na Cesc Fabregas, na kuwapa wenzake matumaini ya kutetea ubingwa wa EURO 2012  na sasa wanasubiri mshindi katika nusu fainali nyingine  leo  kati ya Ujerumani na Italia katika fainali ya Jumapili.

Fabregas, ambaye ni kiungo wa  kati wa timu ya Barcelona, alipiga mkwaju ambao baada ya kugonga mwamba upande wa kushoto, ulitambaa wavuni, na ikawa ni tiketi ya Uhispania kufanya mipango ya kusafiri hadi Kiev, Ukraine, katika mchezo wa fainali.

Mchezaji wa Ureno, Bruno Alves, alielekea kuwa na wasiwasi, na kushindwa kufunga mkwaju wake, baada ya mpira kugonga mwamba, na Ronaldo, akiwa amepangwa na timu yake katika nafasi ya tano kwa wapigaji penalti, hakupata hata nafasi ya kutimiza wajibu huo.

Wengine waliokosa kufunga kupitia mikwaju ya penalti ni mchezaji wa Ureno, Joao Moutinho, wakati kipa wa Uhispania, Casillas, alipoweza kuokoa kwa kuruka upande wa kkulia.

Awali mchezaji wa Uhsipania Xabi Alonso naye alikosa kutupia kambani  mkwaju wa penalti, licha ya kwamba ulikuwa ni mkwaju wa kasi na uliopigwa kwa nguvu, lakini kipa Rui Patricio akaunyaka.

C.Ronaldo akijiangusha katikati ya mabeki Pique na Silva


Luis Nani wa Ureno akijaribu kukukuruka katika mechi hiyo


Beki wa Ureno Contrao akitunishiana misuli na D.Silva wa Uhispania


Beki wa Spain Gerald Pique akimmudu ipasavyo Christiano Ronaldo wa Ureno

URENO Vs UHISPANIA

No comments:

Post a Comment