Tuesday, August 21, 2012

EVERTON YAIDUNGA MAN UNITED KIMOKO


Fellaini akipiga kichwa kilichozama moja kwa moja kambani kuandika goli la pekee la Everton

Kimuhemuhe cha ligi kuu ya Uingereza kimendelea jana jumatatu huku mamilioni ya mashabiki wa soka duniani wakishuhudia Timu ya Everton ikichabanga Manchester united kwa bakora moja kwa yai katika dimba la Goodison Park, mchezo huo ulishuhudiwa na watazamaji wapatao 38,415.

Katika mtanange huo goli la pekee la Everton lilitupiwa kambani na Fellaini katika dakika ya 56 na kuwaacha hoi Man United.


Cleverley wa Man U akioneshana umwamba na Pienaar wa Everton

Fellaini akishangilia goli

Hapa kazi tuu..Welbeck akiwa chini ya ulinzi mkali


Van Persie akitia mchomo katika mpambano huo

Ngoma ngumu..Rooney na Kagawa wakiwa wameloa baada ya kuchapwa goli la kwanza
 


Daah hivi kweli tumechapwa?

No comments:

Post a Comment