Wednesday, August 29, 2012

SUPER CUP LEO MADRID Vs BARCA PUYOL KUVAA "MASK"

Carlos Puyol
 
Nahodha wa Barcelona Carlos Puyol anatarajiwa kukipiga katika mechi ya Super Cup pale Barcelona itakapomenyana na Real Madrid katika mchezo wa marudiano katika dimba la Santiago Bernabeu ambalo ni Dimba la Real Madrid baada ya mchezo wa kwanza uliopigwa katika dimba la Nou Camp,ambapo wenyeji Barcelona waliibuka na ushindi wa 3-2 Dhidi ya Real Madrid.
 
Puyol anatarajiwa kukipiga katika mechi hiyo ya leo lakini atahitajika kuvaa kofia ya kuzuia taya"MASK" kutokana na kusumbuliwa na mifupa ya taya aliyoumia hivi karibuni,Alisema kocha wa Barcelona Tito Vilanova. Puyol aliumia katika mechi ya ligi dhidi ya Osasuna siku ya jumapili na Barca walishinda 3-2, Ingawaje alifanya mazoezi na wenzake siku ya jumanne lakini kocha amesema kucheza au kutocheza itajulikana Jumatano(leo).
 
"Kesho(leo) asubuhi tutaangalia anaendeleaje, na tutamsikiliza Daktari anasemaje hatuwezi kuhatarisha hali ya Puyol"Alisema Vilanova.
 
Taarifa kutoka Barca zinasema Kiungo Mholanzi Ibrahim Affelay aliomba kuondolewa katika safari ya mechi hiyo ili aweze kuangalia maendeleo yake, Affelay aliefanyiwa oparation mwezi Oktoba 2011 kabla ya kujiunga na Timu ya taifa ya Spain katika michuano ya EURO 2012 amesema atahakikisha anapata namba ya kudumu katika kikosi cha Barcelona.
 
Afellay mwenye miaka 26 amehusishwa na uwezekano wa kuhamia Liverpool katika ligi kuu ya Uingereza"Barclays Premier League".

No comments:

Post a Comment