Monday, September 3, 2012

ROBIN VAN PERSIE APIGA "HAT TRICK"

Robin Van Persie Robin Van Persie of Manchester United celebrates the winning goal during the Barclays Premier League match between Southampton and Manchestrer United at St Mary's Stadium on September 2, 2012 in Southampton, England.
Van Persie
 
Robin van Persie amegeuka kuwa kipenzi cha mashabiki wa klabu yake mpya kwa kuiokoa Man.United alipofunga matatu mwenyewe kumuondolea maradhi ya moyo Sir Alex Ferguson kunako mechi yake ya 1,000th akiiongoza Manchester United kama meneja.

Mdachi huyo alitanguliza la kichwa kutokana na kona iliyochongwa na Nani katika mda wa ziada kuokoa jahazi.

Southampton ilipata bao la kuongoza kupitia Rickie Lambert kabla ya Morgan Schneiderlin kupata la pili pia la kichwa katikati ya magoli ya Van Persie ya kusawazisha.

Uhodari wa Van Persie uliwekwa kwenya mizani alipokosa mkwaju wa peneti mnamo dakika 88 wakati United ikidorora 2-1.

Kwa menejawa Southampton Nigel Adkins dakika za majeruhi zilikua kama mwaka wenye machungu kutokana na jinsi vijana wake walivyoweza kuidhibiti United na mabao ya haraka haraka mawili bila shaka yalimuumiza.

Kwa mashabiki wa United, matokeo haya ni sehemu ya malipo ya kitita cha milioni 24 za pauni za Uingereza zilizomleta United kutoka Arsenal.
Robin Van Persie Robin Van Persie of Manchester United scores the winning goal during the Barclays Premier League match between Southampton and Manchestrer United at St Mary's Stadium on September 2, 2012 in Southampton, England.
Van Persie akitupia goli la kwanza
Robin Van Persie Robin Van Persie of Manchester United scores his second goal during the Barclays Premier League match between Southampton and Manchestrer United at St Mary's Stadium on September 2, 2012 in Southampton, England.
Van Persie akitupia goli la pili
Robin Van Persie Robin Van Persie of Manchester United celebrates the winning goal during the Barclays Premier League match between Southampton and Manchestrer United at St Mary's Stadium on September 2, 2012 in Southampton, England.
Van Persie akishangilia bao
Robin Van Persie Robin Van Persie of Manchester United scores the winning goal during the Barclays Premier League match between Southampton and Manchestrer United at St Mary's Stadium on September 2, 2012 in Southampton, England.
Mpira uliopigwa na Van Persie ukitinga wavuni kuandika goli la tatu "Hat Trick" na la mwisho la Man United
Southampton vs Man United

No comments:

Post a Comment