Thursday, September 19, 2013

LIGI YA MABINGWA ULAYA CHELSEA YACHAPWA BARCELONA, ARSENAL KAMA KAWA KAMA DAWA



Ligi ya mabingwa barani ulaya imeendelea tena hapo jana huku wapenda soka ulimwenguni wakishuhudia Vijana wa Mourinho Chelsea wakitandikwa na FC Basel palepale darajani kwa bao 2-1.
Huku nako ikishuhudiwa timu mbili zenye soka safi na la kuridhisha yaani FC Barcelona ya Uhispania na Arsenal ya Uingereza zikifanya mauaji, Barcelona wakiiadabisha Ajax ya Uholanzi nayo Arsenal ikiitandika Marseille ya Ufaransa.

Oscar akishangilia goli la kwanza la Chelsea
 
Marco Streller akishangilia goli lililoizamisha Chelsea darajani


Wachezaji wa FC Basle wakishangilia ushindi dhidi ya Chelsea
 
CHELSEA 1-2 FC BASLE

Katika mpambano kati ya Chelsea waliokuwa wenyeji wa mchezo huo pale darajani mabao ya timu zote mbili yalitupiwa kambani na Oscar (44) na yale ya Basle yalitupiwa kambani na M Salah (70) na Steller (81).

Katika mtanange baina ya Arsenal na Marseille mabao yalitupiwa kambani na Walcott (64) na Ramsey (83) na la kufutia machozi lilitupiwa kambani kwa mkwaju wa penati na Jordan Ayew (90).
 
Theo Walcott Walcott akitupia kambani bao la kwanza

Walcott akishangilia
 
Ramsey akishangilia baada ya kutupia kambani bao la pili

Giroud na Ozil wakimpongeza Ramsey
 
Ozil kibaruani
 
MARSEILLE 1-2 ARSENAL

Barcelona na Ajax mabao yalitupiwa kambani na Leonel Messi (21,54 na 74) na Pique (68).

Messi akifanya mauaji


Zuia hiyooooooooooooooooooooooo
 
Messi akipiga faulo iliyoenda moja kwa zote kambani




Iniesta akifanya udambwidambwi

Messi akitoka na mpira wake baada ya kutupia kambani mabao matatu ''Hat Trick''
 
BARCELONA 4-0 AJAX

Matokeo ya mechi zote

AC Milan 2-0 Celtic
Chelsea 1-2 FC Basle
Marseille 1-2 Arsenal
Atletico Madrid 3-1 Zenit St Petersburg
Austria Vienna 0-1 Porto
Barcelona 4-0 Ajax
Napoli 2-1 Borussia Dortmund
Schalke 04 3-0 Steaua Bucharest

































































No comments:

Post a Comment